TAKUKURU inamshikilia meneja wa Bandari ya Kipumbwi kwa kuomba na kushawishi rushwa ya sh. 900,000

Nyendo

JF-Expert Member
Jun 4, 2017
1,174
4,062
TAKUKURU inamshikilia Meneja wa Bandari ya Kipumbwi, Stephen Elly Mbakweni kwa kuomba na kushawishi Hongo ya Tsh. 900,000 kutoka kwa mteja wake ili aweze kumruhusu kusafirisha mzigo kutoka Handeni kwenda Zanzibar kupitia Bandari hiyo.

Uchunguzi wa TAKUKURU umebaini kuwa Meneja huyo aliomba na kushawishi hongo hiyo baada ya mteja wake kumpatia nyaraka zote za malipo zilizohitajika na zinazoonesha alitekeleza taratibu zote kwa mujibu wa Sheria ili asafirishe mzigo wake.

Nyaraka hizo zilikataliwa na Meneja Stephen kwa madai kwamba hazitambui, huku akiwa na lengo la kushawishi apewe hongo ya Tsh. 900,000 ili aweze kuruhusu mzigo huo upite katika bandari hiyo.

Baada ya TAKUKURU kupokea taarifa hizo ilianza kumfuatilia Meneja huyo na kumuwekea mtego ambapo ilifanikiwa kumkamata kwa kupokea Tsh. 270,000 kutoka kwa mteja huyo aliyemuomba ashushe kutoka Tsh. 900,000. Atafikishwa Mahakamani baada ya Uchunguzi.
1593169264780.png

1593168982392.png

1593169034016.png
 

Attachments

  • 1593168957472.png
    1593168957472.png
    150.9 KB · Views: 3
  • 1593168999617.png
    1593168999617.png
    133.8 KB · Views: 3
  • 1593169020723.png
    1593169020723.png
    133.8 KB · Views: 2
TAKUKURU inamshikilia Meneja wa Bandari ya Kipumbwi, Stephen Elly Mbakweni kwa kuomba na kushawishi Hongo ya Tsh. 900,000 kutoka kwa mteja wake ili aweze kumruhusu kusafirisha mzigo kutoka Handeni kwenda Zanzibar kupitia Bandari hiyo

Uchunguzi wa TAKUKURU umebaini kuwa Meneja huyo aliomba na kushawishi hongo hiyo baada ya mteja wake kumpatia nyaraka zote za malipo zilizohitajika na zinazoonesha alitekeleza taratibu zote kwa mujibu wa Sheria ili asafirishe mzigo wake

Nyaraka hizo zilikataliwa na Meneja Stephen kwa madai kwamba hazitambui, huku akiwa na lengo la kushawishi apewe hongo ya Tsh. 900,000 ili aweze kuruhusu mzigo huo upite katika bandari hiyo

Baada ya TAKUKURU kupokea taarifa hizo ilianza kumfuatilia Meneja huyo na kumuwekea mtego ambapo ilifanikiwa kumkamata kwa kupokea Tsh. 270,000 kutoka kwa mteja huyo aliyemuomba ashushe kutoka Tsh. 900,000. Atafikishwa Mahakamani baada ya Uchunguzi kukamilika

1.jpg

2.jpg

3.jpg
 
Akome,

Binafsi huwa nafurahi pale mtu anashughulikiwa kama hivi kwa kutaka hongo ili atimize majukumu yake
 
MENEJA pengine mshahara ni TZS 4,000,000 plus unanaswa na rushwa ya TSHS 270,000. Kwanini maofisa wenye mishahara mikubwa msitumie hiyo mishahara yenu kama mitaji kulima au kufanya biashara?
 
Nitapambana Na Rushwa Bila Kigugumizi Chochote Na Dawa Ya Jipu Ni Kulitumbua
Rais Wa Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania
 
takukuru bado hamjafanya kazi... trafiki inamaana hamuwaoni? ..mbona wanakamatika kirahisi mnoo...kuna wale wa asubuhi mida ya saa1 mpaka saa3 asubuhi. wakiona pick up, dala dala na malori ya mchanga lazima yasimamishwe. ila gari binafsi zinaenda.. kila kona wapo wengi.

nakumbuka kipindi cha awamu ya MkAPA, Takukuru iliwadaka sana mapolisi na mahakimu. yeye alijua unyeti wa hizo sehemu
 
takukuru bado hamjafanya kazi... trafiki inamaana hamuwaoni? ..mbona wanakamatika kirahisi mnoo...kuna wale wa asubuhi mida ya saa1 mpaka saa3 asubuhi. wakiona pick up, dala dala na malori ya mchanga lazima yasimamishwe. ila gari binafsi zinaenda.. kila kona wapo wengi.

nakumbuka kipindi cha awamu ya MkAPA, Takukuru iliwadaka sana mapolisi na mahakimu. yeye alijua unyeti wa hizo sehemu
Takukuru wanakuwa na kigugumizi kuwakamata trafic,wakirejea kauli ya Jiwe.Kwamba hizo 5000 ni za kubrashia viatu.
 
takukuru bado hamjafanya kazi... trafiki inamaana hamuwaoni? ..mbona wanakamatika kirahisi mnoo...kuna wale wa asubuhi mida ya saa1 mpaka saa3 asubuhi. wakiona pick up, dala dala na malori ya mchanga lazima yasimamishwe. ila gari binafsi zinaenda.. kila kona wapo wengi.

nakumbuka kipindi cha awamu ya MkAPA, Takukuru iliwadaka sana mapolisi na mahakimu. yeye alijua unyeti wa hizo sehemu
Trafiki hawachukui rushwa, kwa muujibu wa mkuu ile ni pesa ya kung'arishia viatu vyao vinavyopigwa vumbi mchana kutwa wanaposimama barabarani.
 
Mleta maada nadhani umepata taarifa juu kwa juu bila kutafuta tarifa kwa kina, huyo mzee anae tuhumiwa kupokea rushwa ya 270000, sio kweli bali TAKUKURU Pangani ndo walipokea rushwa ili kuja kumzalilisha huyo meneja wa bandari Kipumbwi wakishirikiana na Umoja wa wenye Madau Kipumbwi ambao wanaukiritimba ulio kithiri kijiji hapo, pamoja na serikali ya kijiji walikuwa wanaingilia majukumu ya meneja huyo. Meneja huyo baada ya kuona anaingiliwa majukumu yake alimuandikia Mkuruhenzi Mtendaji(W) Pangani juu ya sitogahamu hiyo. Mkurugenzi baada ya kupata barua hiyo alitoa mwongozo kwa wa majukumu kwa Mtendaji kijiji na Mwenyekiti kijiji Kipumnwi, kuto muingilia meneja bandari kipumbwi. Kitu kilicho firahisha sasa baada TAKUKURU Pangani kumtia nguvuni meneja bandari Kipumbwi, M/kiti kijiji alipika biriani siku ya tarehe 22/06/2020 Kujipongeza kwa kazi alioifanya pamoja na mjumbe wake Alfan Subeti pamoja na Issa Farahani bila kumsahau mmiliki wa dau la SURA SI ROHO Sabri Abdi Omary wote hawa wakazi wa kijiji cha Kipumbwi. Pia TAKUKURU Pangani baada ya kumshikilia meneja bandari Kipumbwi walishinikiza mzigo uliokamatwa na tuhuma udafirishwe mara moja kwenda Unguja, huku mamlaka ya bandari walitaka mzigo huo isitoke kwani ni sehemu ya ushahidi zidi ya tuhuma za rushwa ya Kiasi cha fedha za kitanzania shilingi 270000, pia TAKUKURU Pangani walishinikiza kama mzigo wenye tuhuma hautaruhusiwa kitoka basi meneja wa bandari kipumbwi hato pewa dhamana.

Kwa kifupi MARWA, TAKUKURU Pangani ulizingua sana.
 
Mleta maada nadhani umepata taarifa juu kwa juu bila kutafuta tarifa kwa kina, huyo mzee anae tuhumiwa kupokea rushwa ya 270000, sio kweli bali TAKUKURU Pangani ndo walipokea rushwa ili kuja kumzalilisha huyo meneja wa bandari Kipumbwi wakishirikiana na Umoja wa wenye Madau Kipumbwi ambao wanaukiritimba ulio kithiri kijiji hapo, pamoja na serikali ya kijiji walikuwa wanaingilia majukumu ya meneja huyo. Meneja huyo baada ya kuona anaingiliwa majukumu yake alimuandikia Mkuruhenzi Mtendaji(W) Pangani juu ya sitogahamu hiyo. Mkurugenzi baada ya kupata barua hiyo alitoa mwongozo kwa wa majukumu kwa Mtendaji kijiji na Mwenyekiti kijiji Kipumnwi, kuto muingilia meneja bandari kipumbwi. Kitu kilicho firahisha sasa baada TAKUKURU Pangani kumtia nguvuni meneja bandari Kipumbwi, M/kiti kijiji alipika biriani siku ya tarehe 22/06/2020 Kujipongeza kwa kazi alioifanya pamoja na mjumbe wake Alfan Subeti pamoja na Issa Farahani bila kumsahau mmiliki wa dau la SURA SI ROHO Sabri Abdi Omary wote hawa wakazi wa kijiji cha Kipumbwi. Pia TAKUKURU Pangani baada ya kumshikilia meneja bandari Kipumbwi walishinikiza mzigo uliokamatwa na tuhuma udafirishwe mara moja kwenda Unguja, huku mamlaka ya bandari walitaka mzigo huo isitoke kwani ni sehemu ya ushahidi zidi ya tuhuma za rushwa ya Kiasi cha fedha za kitanzania shilingi 270000, pia TAKUKURU Pangani walishinikiza kama mzigo wenye tuhuma hautaruhusiwa kitoka basi meneja wa bandari kipumbwi hato pewa dhamana.

Kwa kifupi MARWA, TAKUKURU Pangani ulizingua sana.

Kweli kwenye fitna hakuna majungu mkuu.
Hiyo bandari ya Kipumbwi iko busy sana na majahazi, boti za uvuvi lakini serikali ya kijiji na wilaya haiweki mkazo wa kujengewa hata maboya ya kuelea ya kushushia abiria (Floating Buoy Bridge).

Abiria kushuka au kupanda maji yakiwa yamejaa mpaka abebwe na mtu au apande boti ndogo.Wakati wangeweka boya wangeweza kutoza jahazi kupakia au kushusha mtu shilingi elfu 1.

Hata kupambania gati lijengwe ili waongeze chanzo cha mapato ya wilaya serikali ya kijiji ipo kimya.

Kipumbwi ni bandari inayojiweza sana wajanja wachache wanairudisha nyuma.Bandari haiendi mbele hairudi nyuma.
 
Haiwatoshi kwakua wanawaza harrier matako ya nyani
Kwa meneja wa bandari kuwaza Harrier ni jambo la ajabu, mshahara anakula wa maana,hela ya pango na posho kibao.

Pia kama ana connection hiyo gari anapata kule Dar port zinazopigwa mnada bandarini kwa bei chee. Hiyo bandari ina loop kubwa za hela za hapa na pale ila sio za kula rushwa.
 
Takukuru wanakuwa na kigugumizi kuwakamata trafic,wakirejea kauli ya Jiwe.Kwamba hizo 5000 ni za kubrashia viatu.
sasa nimeelewa, ila ni tofauti kabisa na kipindi cha Mzee Mkapa. mzee Mkapa alijitahidi sana kupiga vita rushwa hasa zile zinazokandamiza wanyonge ambao ndio wengi
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom