Bila bila
JF-Expert Member
- Dec 20, 2016
- 21,472
- 37,735
Katika maelezo "mazuri" ya Mheshimiwa Lijualikali bungeni alieleza jinsi alivyopata ubunge kwa njia isiyo sahihi. Pia alieleza matumizi mabaya ya fedha za michango ya wabunge, jambo ambalo nasikia TAKUKURU wameanza kufanyia kazi maneno mazuri ya Lijualikali.
Lakini kuna jambo la pili ambalo sijasikia TAKUKURU wakilifanyia kazi, nalo ni hilo la kupata Ubunge kwa njia haramu na hivyo mapato yote ya Ubunge wake tangu 2015 hadi 2020 ni fedha haramu na hivyo ni utakatishaji wa fedha halali zilizotokana na ajira haramu.
Tuanze na mnufaika, halafu tuwapate wawezeshaji, Yaani DED, OCD, Mwenyekiti wa CCM na mratibu wa uchaguzi.
Lakini kuna jambo la pili ambalo sijasikia TAKUKURU wakilifanyia kazi, nalo ni hilo la kupata Ubunge kwa njia haramu na hivyo mapato yote ya Ubunge wake tangu 2015 hadi 2020 ni fedha haramu na hivyo ni utakatishaji wa fedha halali zilizotokana na ajira haramu.
Tuanze na mnufaika, halafu tuwapate wawezeshaji, Yaani DED, OCD, Mwenyekiti wa CCM na mratibu wa uchaguzi.