TAKUKURU: Chenge hahusiki na tuhuma za RADA

nickname

JF-Expert Member
Dec 20, 2009
544
147
edward-hosea-mkuu-wa-takukuru-229x300.jpg

Bosi wa TAKUKURU Dk. Edward Hosea


TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
YAH: UCHUNGUZI KUHUSU TUHUMA ZA RADA

Tunapenda kuujulisha umma kuwa uchunguzi na ushahidi uliokusanywa na Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) pamoja na Shirika la Upelelezi - SFO la Uingereza kuhusu tuhuma za Rushwa katika ununuzi wa Rada, umeshindwa kumhusisha Bw. Andrew Chenge katika tuhuma hizo.

TAKUKURU inawaomba wananchi waendelee kutoa ushirikiano kwa chombo hiki kwa kutoa taarifa za kuwafichua wale wote wanaojihusisha na Rushwa kwani jukumu hili ni la kila mmoja wetu.

Imetolewa na
Doreen J. Kapwani,
Afisa Uhusiano-TAKUKURU
Novemba 08 , 2010
S. L.P. 4865,
Dares Salaam.


Simu: 2150043-6/2150360
Nukushi: (022) 2150047
Baruapepe:dgeneral@pccb.go.tz
Mtandao Prevention and Combating of Corruption Bureau
 
Niidhani uchunguzi ulikuwa unafanywa na SFO peke yao sijawahi sikia kuwa PCCB walikuwa wanachunguza hii kitu. That aside kwani uchunguzi ulikwisha lini jana au vinginevyo na kama ilikuwa kabla ya hapo kwa nini wasiseme siku zote hizo kuhusu hili, why today.

Tuna uhakika gani kama tukitoa taarifa za kufichua wala rushwa zitapuuzwa kama mlivyofanya arusha wakati wa kugombea ubunge????
 
Washaanza kumsafishia njia ya USPIKA mafisadi hawa.Nchi imeshauzwa hii lol!!!
 
Kwa kweli nina hasira!!!
Isitoshe huu upuuzi wao ndiyo umenisabishia pressure kupanda bila kutegemea..OMG!!
 
Chenge.jpg


Waziri wa Miundombinu, Bw. Andrew Chenge, amegeuka bubu, hataki kuzungumza na waandishi, sasa anawakimbia.

Bw. Chenge maarufu kwa jina la `bilionea wa vijisenti`, alifanya kioja hicho jana jijini Dar es Salaam baada ya kufunga Mkutano wa Kimataifa wa masuala ya Usalama wa Vyombo vya Usafiri Baharini (IMO).

Mkutano huo ulioshirikisha mashirika mbalimbali ya kupambana na uhalifu wa aina mbalimbali duniani, wadau walitiliana saini Mkataba wa Makubaliano ya Usalama wa Vyombo vya Usafiri Magharibi mwa Bahari ya Hindi.

Bw. Chenge ambaye alionekana mpole mno muda wote wa hotuba yake, alipomaliza alitoka nje tofauti na kawaida yake kuzungumza na waandishi nje ya ukumbi, jana aliwaona waandishi hao kama adui zake.

Waandishi wakiwa nje ya ukumbi huo jijini Dar es Salaam, walimzonga Waziri Chenge huku wengine wakimuwekea vipaza sauti, lakini aliamsha mdomo wake mara moja tu na kusema ``sizungumzi chochote`` huku akishuka kwa kasi ngazi za ghorofa ya kwanza ulipo ukumbi huo, akisindikizwa na wasaidizi wake. Hata hivyo, waandishi wa habari huku wakiendelea kuwa na matumaini kwamba huenda Waziri huyo atajibu maswali yao akiwa nje, hali ilikuwa tofauti, kwani alifunguliwa mlango wa gari lake na kuingia haraka haraka na kuondoka. Aprili 12, mwaka huu, gazeti la The Guardian la Uingereza, liliandika habari kuwa, Waziri Chenge amejilimbikizia dola zaidi ya milioni moja (zaidi ya Shilingi bilioni moja) kwenye benki moja iliyopo kisiwa cha Jersey, Uingereza.

Gazeti hilo lilieleza kuwa, inasadikiwa fedha hizo ni sehemu ya mgawo wa rushwa iliyotokana na ununuzi wa rada ya serikali ya Tanzania, wakati huo Bw. Chenge akiwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali. Wakati huo huo, Mwenyekiti DP, Mchungaji Christopher Mtikila, amemshauri Bw. Chenge, kujiuzulu. Aidha, Mchungaji Mtikila amesema ameanza kukusanya mikataba mibovu aliyodai ilisababisha hasara ya mabilioni ya fedha kwa serikali kwa nyakati tofauti. Aliyasema hayo jana jijini Dar es Salaam wakati wa mkutano na waandishi wa habari.

Alisema pamoja na kumshauri Bw. Chenge ajiuzulu, ni vyema akarudisha fedha anazotuhumiwa kumiliki ili kulinda heshima ya taifa.

Akizungumzia mikataba inayokusanywa na kupitiwa kutoka kwenye taasisi na wizara, alisema ni pamoja na ile ya umeme ya Richmond, Dowans, IPTL, Songas, Aggreko na Net Group Solutions.

Mingine alisema ni ya madini iliyosainiwa kati ya Benki Kuu (BoT) na Hazina ile ya Kampuni ya Simu Nchini (TTCL) pamoja na ya ununuzi wa rada na ndege ya Rais, vyakula feki vyote vikigharimu mabilioni ya fedha.

Alisema mikataba hiyo itapitiwa kwa umakini na kamati maalumu pamoja na wanasheria alioafikiana nao ili kuiweka wazi kwa wananchi.

Alisema wanasheria zaidi ya 40 wanahitajika kufanya kazi hiyo. ``Tunahitaji wanasheria wasiopungua 20 ili kukamilisha idadi ya 40 tunayohitaji ambao wako tayari kwa ukombozi,`` alisema.
 
... I said so three weks ago. Nlipishana naye kwenye corridors flani UK akitafuta kusafishwa na hilo. yanayoendele sasa ni implementation. Kwa nini ni lazima yeye awe spika???

Panapofuka moshi iko MOTO!!!
 
Nawasikitikia Wa-Tz wezangu waliochagua hiki chama..ndo watajua ufisadi madhara yake ni kitu gani...
 
Bado tunazo kumbukumbu:

Following the uproar over its halted Saudi investigation, the Serious Fraud Office is expected to decide whether to bring fresh corruption charges against arms manufacturer BAE within six weeks, over a second arms deal, this time with Tanzania.


A minister from the east African state has denied that more than $1m (£507,500) in his offshore accounts came from BAE.


Investigators involved in a three-year inquiry after the controversial deal to sell Tanzania a £28m radar system identified the money in Jersey accounts controlled by the poverty-striken country's infrastructure minister, Andrew Chenge.


Tanzania's anti-corruption bureau, which has been working with authorities in the UK, Switzerland and Jersey, wants to establish if the money is linked to multi-million pound secret commission payments made by BAE.


Chenge does not dispute the money in his Jersey accounts. But he told the Guardian: "The obvious inference [of the investigations] is that I have received for my benefit 'corrupt payments' from BAE. This is untrue."


He said he was only involved in minor aspects of the radar deal, which was promoted by other ministries and approved by the Tanzanian cabinet. His bank records, he said, would show investigators that "there is no connection to the BAE Tanzanian radar deal".


His US lawyer from Cleveland, Ohio, J Lewis Madorsky, added: "While the matters in question took place a number of years ago, we can state ... that any and all allegations of illegality, impropriety, misconduct and unethical behaviour made against our client are categorically and vigorously denied".


Investigators say Chenge could be a valuable witness. The target of their investigation is not him but BAE. The arms company made the commission payments to a local agent in Tanzania to promote the £28m radar sale, through an elaborate chain of offshore companies and a Swiss bank.


The agent has now left the country and is wanted by Interpol.


These developments come at a key moment in the BAE saga. A landmark high court ruling on Thursday said that the decision to drop the SFO's Saudi inquiry was wrong.


In a huge embarrassment for the British and Saudi governments, the court rejected the claims that the inquiry had to be closed down for reasons of national security and because lives would be at risk.


And it took the extraordinary step of naming Prince Bandar, the crown prince's son, as the man behind what it said could be characterised as an attempt to pervert the course of justice.


Former prime minister Tony Blair caused uproar by personally forcing a halt to investigations into the Saudi deal. The Guardian subsequently disclosed that £1bn had been paid into accounts controlled by Prince Bandar during the deal. Bandar says the payments were not improper.


Inspectors from the Organisation for Economic Co-operation and Development (OECD) grilled British officials in London last week about their failure to get results from any of their BAE investigations. Britain signed up to an international treaty to outlaw bribery, but there have never been any prosecutions.


The Tanzania deal, although smaller in cash terms than the Saudi deals, is equally controversial: Tanzania is one of the world's poorest countries, and the UK government is paying more than £100m this year to help the heavily-indebted country's budget.


It was Blair again who forced the radar deal through the British cabinet, despite protests from the then international development secretary, Clare Short. She said the sale, for which Tanzania had to borrow yet more from a commercial bank, was corrupt and "stank".


A lengthy SFO investigation in the UK subsequently discovered that 31% of the deal's contract price had been diverted via Switzerland.


BAE transferred the money to a subsidiary, Red Diamond Trading, registered anonymously in the British Virgin Islands.


Red Diamond then moved the cash to a Swiss account in the name of a Panama company, Envers Trading Corporation. This entity had two Panamanian nominee directors. But it was secretly controlled by a Tanzanian middleman, Shailesh Vithlani, according to Dar es Salaam court papers.


Investigators are now checking whether Vithlani arranged to pass any money in turn to Tanzanian politicians and officials.


Sources said the bank in Jersey had promptly frozen transactions and filed a suspicious activity report when the Tanzanian inquiries began.


Vithlani, who is of Indian extraction but holds a British passport, is listed as wanted by Interpol.


He has been charged by the Tanzanian anti-corruption bureau with lying to investigators, but has left the country. His whereabouts are unknown.


According to the charges, Vithlani falsely denied he was the owner of the Panama company, and falsely claimed he had only handled a separate commission of 1% on the deal.


The SFO's new director, Richard Alderman, former head of UK tax investigations, is due to take over this month. The SFO refused to comment yesterday.


BAE, which has previously denied wrongdoing, also declined to comment, or to explain its chain of offshore payments, other than to say "BAE Systems continues to fully co-operate with the SFO investigation".


The company has recently launched an extensive public relations campaign and last week unveiled a report commissioned from a commercial consultancy, Oxford Economics, which claimed BAE was of key value to the UK economy.
 
kuanzia leo ninatangaza kuwa kirefu cha TAKUKURU ni "Taasisi ya KUENDELEZA na KUSAFISHA WALA rushwa". Hawa jamaa hawana hata aibu, wanafikiri tumesahau walivyowasafisha Mafisadi wa RICHMOND! Shame on you TAKUKURU!
 
Hivi "vijisenti" vyake aliwahi hata siku moja kuvitolea maelezo kwenye kamati ya maadili au fomu za wapi sijui ambazo viongozi wanapaswa kujaza? Safi sana ngoma ya Uspika inanoga sasa, mwishoe itapasuka tu!
 
kuanzia leo ninatangaza kuwa kirefu cha takukuru ni "taasisi ya kuendeleza na kusafisha wala rushwa". Hawa jamaa hawana hata aibu, wanafikiri tumesahau walivyowasafisha mafisadi wa richmond! Shame on you takukuru!

"taasisi ya kuzua na kupamba rushwa"
 
... I said so three weks ago. Nlipishana naye kwenye corridors flani UK akitafuta kusafishwa na hilo. yanayoendele sasa ni implementation. Kwa nini ni lazima yeye awe spika??? Panapofuka moshi iko MOTO!!!

You are right panapofuka moshi kuna moto. Hawa TAKAKURU hawaeleki kabisa. Sijui kwanini isifutwe iko kisiasa zaidi.
 
Interesting coincidence....alikuwa wapi siku zote kumsafisha? Yaani kaamua kuongea mara baada ya Chenge kutangaza anagombea uspika???

Ee Mwenyezi Mungu tunusuru na laana hii!!!
 
"taasisi ya kuzua na kupamba rushwa"

Nafikiri kirefu hiki kimetulia zaidi, ingawa hakionyeshi kama kupamba rushwa ndiyo kusafisha wala rushwa!! je wana JF twaweza kukubaliana na kirefu rasmi cha taasisi hii?
Hii mijamaa ya ovyo kweli kweli, haina hata utu wala mishipa ya huruma kwa Watanganyika wanyonge wanaoibibiwa rasilimali za nchi yao kila siku! Hivi huyu hosea alizaliwa na mwanamke kweli? mbona mi namuona mtu feki sana? Hiyo Doctorate imepatikana je? au ametunukiwa na Mamet kile chuo cha Rostam na Salva Rweyemamu
 
Hii taarifa wangetoa SFO ningeamini. Lakini siyo taasisi hii ya kulinda mafisadi ndani ya CCM! By the way si PCCB ndiyo ilikuja na kitu cha namna hii kumsafisha Lowassa?
 
Back
Top Bottom