Taja vyote, vita dhidi ya rushwa na ufisadi imefanikiwa!

wandamba

JF-Expert Member
Apr 29, 2014
510
839
Na Emmanuel J. Shilatu

Tukiwa tunaelekea maadhimisho ya miaka mitatu tangu utawala wa Serikali ya awamu ya tano unaoongozwa na Rais John Pombe Magufuli uingie madarakani hauwezi kuacha kutaja suala la rushwa na ufisadi.

Vipindi vya awali suala la rushwa na ufisadi vilijaa wingu zito vikipambwa na misamiati mbalimbali ya sakata ya matukio yaliyoonyeshwa kukubuhu kwa himaya ya Mafisadi nchini pasipo hatua za kuridhisha kupambana nayo.

Ilifika wakati Watanzania wakawa wanamkumbuka Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere ambaye katika kipindi chake wala rushwa na ufisadi walikuwa wakifungwa miaka 2 jela pamoja na kuchapwa viboko 24. Hii ilitia hofu na kupunguza matukio ya rushwa na ufisadi kipindi hicho.

Tukiwa tunaadhimisha miaka 3 tangu Rais Magufuli aingie madarakani, Serikali yake imeitendea haki ibara ya 11, 12 na 13 iliyopo ukurasa wa 6 katika ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2015 - 2020 inayoelezea namna itakavyopigia vita dhidi ya rushwa nchini.

Leo hii tunaona mapambano ya dhati ya kutokomeza rushwa na ufisadi nchini tukishuhudia "Mapapa" ya rushwa na ufisadi wakipandishwa Mahakamani, kitu ambacho hakikutarajiwa na wengi.

Hata upande wa Watumishi wa umma, suala la uadilifu na uwajibikaji limeimarika zaidi kutokana na kupungua kwa matukio ya rushwa na ufisadi miongoni mwao.

Hayo yamepelekea leo hii Tanzania kupanda kwa nafasi 13 katika mwaka 2016 na 2017 na pia ikishika nafasi ya pili (2) katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mapambano haya ya rushwa na ufisadi nchini yamepelekea zaidi ya Tsh. Bilioni 127 kuweza kuokolewa tangu Serikali ya awamu ya 5 iingie madarakani.

Katika hili, Watanzania tunasema *Ahsante sana Rais Magufuli*, Serikali unayoiongoza imetekeleza vyema Mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi nchini.

*Shilatu E.J*
 
hujataja yule aliyeingiza makontena kwa jina binafsi bwana BASHITE ile haikuwa rushwa! hujataja ile ya CAG 1.5 trilion ! pitia kwenye hizi halmashauri ukajionee mwenyewe. nakushauri ujue kwa upana maana halisi Y rushwa kwa upana wake. hata kutompandisha mtu cheo kwa zaid ya miaka mitatu bila sababu za msingi ni rushwa hiyo, watumishi hawajPandishwa nakuhakikishia!
 
Imefanikiwa wapi? Makontena,Ujenzi usioheshimu bajeti ( Chato miradi yote) Kutokuonekana kwa 1.5 trillions (hazikuibiwa ila hazionekani) ....Kuna madudu mengi Mlichofanikiwa ni kuzuia watu kuyasema kwa kuwapiga risasi,kuzuia mikutano na kubambikia kesi. KIBAYA ZAIDI SAIVI ANAKULA MTU MMOJA NA NCHI JIRANI.....acha unafki kuwa mzalendo kwa taifa lako kwa faida ya vizazi vijavyo.
 
Na Emmanuel J. Shilatu

Tukiwa tunaelekea maadhimisho ya miaka mitatu tangu utawala wa Serikali ya awamu ya tano unaoongozwa na Rais John Pombe Magufuli uingie madarakani hauwezi kuacha kutaja suala la rushwa na ufisadi.

Vipindi vya awali suala la rushwa na ufisadi vilijaa wingu zito vikipambwa na misamiati mbalimbali ya sakata ya matukio yaliyoonyeshwa kukubuhu kwa himaya ya Mafisadi nchini pasipo hatua za kuridhisha kupambana nayo.

Ilifika wakati Watanzania wakawa wanamkumbuka Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere ambaye katika kipindi chake wala rushwa na ufisadi walikuwa wakifungwa miaka 2 jela pamoja na kuchapwa viboko 24. Hii ilitia hofu na kupunguza matukio ya rushwa na ufisadi kipindi hicho.

Tukiwa tunaadhimisha miaka 3 tangu Rais Magufuli aingie madarakani, Serikali yake imeitendea haki ibara ya 11, 12 na 13 iliyopo ukurasa wa 6 katika ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2015 - 2020 inayoelezea namna itakavyopigia vita dhidi ya rushwa nchini.

Leo hii tunaona mapambano ya dhati ya kutokomeza rushwa na ufisadi nchini tukishuhudia "Mapapa" ya rushwa na ufisadi wakipandishwa Mahakamani, kitu ambacho hakikutarajiwa na wengi.

Hata upande wa Watumishi wa umma, suala la uadilifu na uwajibikaji limeimarika zaidi kutokana na kupungua kwa matukio ya rushwa na ufisadi miongoni mwao.

Hayo yamepelekea leo hii Tanzania kupanda kwa nafasi 13 katika mwaka 2016 na 2017 na pia ikishika nafasi ya pili (2) katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mapambano haya ya rushwa na ufisadi nchini yamepelekea zaidi ya Tsh. Bilioni 127 kuweza kuokolewa tangu Serikali ya awamu ya 5 iingie madarakani.

Katika hili, Watanzania tunasema *Ahsante sana Rais Magufuli*, Serikali unayoiongoza imetekeleza vyema Mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi nchini.

*Shilatu E.J*
Nilitegemea utatupa angalau mrejesho wa wapi zilipo tillioni 1.5 za walalahoi wa nchi hii unakuja na porojo za kuunga mkono juhudi....
 
..hawa wanaodai wameokota VICHWA VYA TRENI bandarini na baadaye wanavinunua ndiyo unawaamini wanapambana na rushwa?

..pale tulishuhudia jinsi waongo, na mafisadi, walivyojipanga kuuhadaa umma.

..rushwa na ufisadi bado vipo.

..Kilichobadilika ni hatari ya kufichua rushwa, au majanga yanayoweza kukutokea ukifichua vitendo vya rushwa na ufusadi.

..inabidi uwe tayari KUFA au kupata kilema cha maisha.

Cc tindo
 
kamuulize Lema aliyefukuzwa na ushahidi dhidi ya wahonga kodi, a k a team mnyeti..
kuna fisadi moja lililamba 1.5 trilioni yeye na mpwa wake..
sasa hivi kuna fisadi la kura..
hilo unaambiwa mpinzani huna namna ya kupata haki..
kihistoria fisadi hili lilikuwa linapaki hadi matrekta barabarani ili mpinzani asirudishe fomu..
UMEONA WAPI FEDHA ZOTE KUSHIKILIWA NA MTU NA MPWA WAKE ?
 
Tofauti na awamu zilizopita tulichofanikiwa ni kudhibiti habari ili taarifa za upigaji zisijulikane,subiria awamu nyingine yatakavofukuliwa makaburi. Rushwa ya nafasi za kugombea tena ubunge, ripoti chafu karibu halmashauri zote ni upigaji kwenye miradi, kupungua kwa tija ya uzalishaji kwa Watumishi wasio na motisha,1.5,chatu airport, kiongozi ajae atapata tabu sana kuiweka sawa nchi.Atengeneze umoja wa kitaifa,kuongeza tija kwa Watumishi, kuondoa chuki kwa matajiri, kurudisha uzalendo, kujenga diplomacy ya kimataifa, nk.
 
Mafisadi wakajaribu kuunda zengwe la upotevu wa trilioni 1.5 ili wampunguze kasi lakini ndo kwanza raisi anazidi kuwawashia moto.
 
..hawa wanaodai wameokota VICHWA VYA TRENI bandarini na baadaye wanavinunua ndiyo unawaamini wanapambana na rushwa?

..pale tulishuhudia jinsi waongo, na mafisadi, walivyojipanga kuuhadaa umma.

..rushwa na ufisadi bado vipo.

..Kilichobadilika ni hatari ya kufichua rushwa, au majanga yanayoweza kukutokea ukifichua vitendo vya rushwa na ufusadi.

..inabidi uwe tayari KUFA au kupata kilema cha maisha.

Cc tindo


Kula tano mkuu, Sasa hivi mapambano makubwa ni dhidi ya matumizi ya neno fisadi na wale wanaofichua rushwa. Ni hatari sana sasa kwenda kutoa taarifa ya rushwa kwani inaonekana kusema ulaji wa rushwa ni kuichafua serekali. Kwa hiyo sio kwamba hakuna rushwa, bali haitakiwi kutangazwa.
 
Ni mpumbavu pekee ndiye anayeweza kusema ufisadi na Rushwa vimepungua.Ni ushamba wa ndani ndani huko.NIDA, na akina makonda na mahuni wenzie ni wala rushwa wakubwa.Makonda mwaka 1 baada ya uRC akamiki Range Rover ya 300+mil.Halafu mshahara hata mil 7 haufiki.Ni nini hii?
 
Na Emmanuel J. Shilatu...Katika hili, Watanzania tunasema *Ahsante sana Rais Magufuli*, Serikali unayoiongoza imetekeleza vyema Mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi nchini.
Katika hili, Wana CCM tunasema *Ahsante sana Rais Magufuli*, Serikali unayoiongoza imefanikiwa kubinafsisha rushwa na ufisadi na sasa ni viongozi wa CCM na serikali pekee wanaoruhusiwa kupokea rushwa na kufaidi matunda ya ufisadi.
 
Na Emmanuel J. Shilatu

Tukiwa tunaelekea maadhimisho ya miaka mitatu tangu utawala wa Serikali ya awamu ya tano unaoongozwa na Rais John Pombe Magufuli uingie madarakani hauwezi kuacha kutaja suala la rushwa na ufisadi.

Vipindi vya awali suala la rushwa na ufisadi vilijaa wingu zito vikipambwa na misamiati mbalimbali ya sakata ya matukio yaliyoonyeshwa kukubuhu kwa himaya ya Mafisadi nchini pasipo hatua za kuridhisha kupambana nayo.

Ilifika wakati Watanzania wakawa wanamkumbuka Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere ambaye katika kipindi chake wala rushwa na ufisadi walikuwa wakifungwa miaka 2 jela pamoja na kuchapwa viboko 24. Hii ilitia hofu na kupunguza matukio ya rushwa na ufisadi kipindi hicho.

Tukiwa tunaadhimisha miaka 3 tangu Rais Magufuli aingie madarakani, Serikali yake imeitendea haki ibara ya 11, 12 na 13 iliyopo ukurasa wa 6 katika ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2015 - 2020 inayoelezea namna itakavyopigia vita dhidi ya rushwa nchini.

Leo hii tunaona mapambano ya dhati ya kutokomeza rushwa na ufisadi nchini tukishuhudia "Mapapa" ya rushwa na ufisadi wakipandishwa Mahakamani, kitu ambacho hakikutarajiwa na wengi.

Hata upande wa Watumishi wa umma, suala la uadilifu na uwajibikaji limeimarika zaidi kutokana na kupungua kwa matukio ya rushwa na ufisadi miongoni mwao.

Hayo yamepelekea leo hii Tanzania kupanda kwa nafasi 13 katika mwaka 2016 na 2017 na pia ikishika nafasi ya pili (2) katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mapambano haya ya rushwa na ufisadi nchini yamepelekea zaidi ya Tsh. Bilioni 127 kuweza kuokolewa tangu Serikali ya awamu ya 5 iingie madarakani.

Katika hili, Watanzania tunasema *Ahsante sana Rais Magufuli*, Serikali unayoiongoza imetekeleza vyema Mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi nchini.

*Shilatu E.J*
Shillatu kuwa msukuma kusikufanye ujivue akili. Sasa hivi ndio ufisadi na rushwa umetamalaki muulize mtendaji yeyote wa umma wa ngazi ya juu akuambie
 
Hakika
Katika hili, Wana CCM tunasema *Ahsante sana Rais Magufuli*, Serikali unayoiongoza imefanikiwa kubinafsisha rushwa na ufisadi na sasa ni viongozi wa CCM na serikali pekee wanaoruhusiwa kupokea rushwa na kufaidi matunda ya ufisadi.
 
Na Emmanuel J. Shilatu

Tukiwa tunaelekea maadhimisho ya miaka mitatu tangu utawala wa Serikali ya awamu ya tano unaoongozwa na Rais John Pombe Magufuli uingie madarakani hauwezi kuacha kutaja suala la rushwa na ufisadi.

Vipindi vya awali suala la rushwa na ufisadi vilijaa wingu zito vikipambwa na misamiati mbalimbali ya sakata ya matukio yaliyoonyeshwa kukubuhu kwa himaya ya Mafisadi nchini pasipo hatua za kuridhisha kupambana nayo.

Ilifika wakati Watanzania wakawa wanamkumbuka Hayati Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere ambaye katika kipindi chake wala rushwa na ufisadi walikuwa wakifungwa miaka 2 jela pamoja na kuchapwa viboko 24. Hii ilitia hofu na kupunguza matukio ya rushwa na ufisadi kipindi hicho.

Tukiwa tunaadhimisha miaka 3 tangu Rais Magufuli aingie madarakani, Serikali yake imeitendea haki ibara ya 11, 12 na 13 iliyopo ukurasa wa 6 katika ilani ya uchaguzi ya Chama Cha Mapinduzi ya mwaka 2015 - 2020 inayoelezea namna itakavyopigia vita dhidi ya rushwa nchini.

Leo hii tunaona mapambano ya dhati ya kutokomeza rushwa na ufisadi nchini tukishuhudia "Mapapa" ya rushwa na ufisadi wakipandishwa Mahakamani, kitu ambacho hakikutarajiwa na wengi.

Hata upande wa Watumishi wa umma, suala la uadilifu na uwajibikaji limeimarika zaidi kutokana na kupungua kwa matukio ya rushwa na ufisadi miongoni mwao.

Hayo yamepelekea leo hii Tanzania kupanda kwa nafasi 13 katika mwaka 2016 na 2017 na pia ikishika nafasi ya pili (2) katika nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki.

Mapambano haya ya rushwa na ufisadi nchini yamepelekea zaidi ya Tsh. Bilioni 127 kuweza kuokolewa tangu Serikali ya awamu ya 5 iingie madarakani.

Katika hili, Watanzania tunasema *Ahsante sana Rais Magufuli*, Serikali unayoiongoza imetekeleza vyema Mapambano dhidi ya rushwa na ufisadi nchini.

*Shilatu E.J*
Anaelewa maana ya "Rushwa" na "Ufisadi". Tuanzie hapo kwanza!
 
Eti nini? Rushwa ipo sana tuu....sema sasa hivi mbinu zimebadilika ....hawako careless kama awamu ya nne
 
Back
Top Bottom