General Galadudu
JF-Expert Member
- Nov 7, 2015
- 1,837
- 2,119
Enzi zile kila inapokaribia mwaka mpya tunatengeneza baruti kwenye vichwa vya spoku za baiskeli/pikipiki, ili kuitest unasubiri sehemu walipokaa watu wamejisahau basi unaenda kuifyatua pale, wakistuka wewe ni burudaaaaaani moyoni.
Mwaka wa 1993 ndio sintokuja kuusahau, nilitaka mwaka huo niweke historia kubwa zaidi, na kweli......nilitengeneza baruti, lakin ya safari hii lilikuwa ni BOMU, nilitumia bomba la pampu ya baiskeli (hawa watoto wa siku hizi sidhani kama wanayajua), ilinichukua muda mrefu kidogo hadi kukamilisha utengenezaji wake, siku limekamilika sikwenda kulitega mimi, kuna rafiki yangu nilimpa maelekezo yote ya namna ya kulitega lakini yule NYUMBU KICHWA MAJI akakosea maelekezo.
Dude likalipuka wakati bado yupo kwenye harakati za kulitega, likaporomosha kibanda cha kufugia mbuzi huku likiondoka na uhai wa ndama mmoja wa mbuzi, likimuacha na ulemavu wa kukatika vidole vitatu vya mkono wa kushoto na majereha mabaya sana usoni.
Kila nikiendaga Tabora huwa sikasahau kale ka mtaa tulikokuwa tunaishi aisee
Mwaka wa 1993 ndio sintokuja kuusahau, nilitaka mwaka huo niweke historia kubwa zaidi, na kweli......nilitengeneza baruti, lakin ya safari hii lilikuwa ni BOMU, nilitumia bomba la pampu ya baiskeli (hawa watoto wa siku hizi sidhani kama wanayajua), ilinichukua muda mrefu kidogo hadi kukamilisha utengenezaji wake, siku limekamilika sikwenda kulitega mimi, kuna rafiki yangu nilimpa maelekezo yote ya namna ya kulitega lakini yule NYUMBU KICHWA MAJI akakosea maelekezo.
Dude likalipuka wakati bado yupo kwenye harakati za kulitega, likaporomosha kibanda cha kufugia mbuzi huku likiondoka na uhai wa ndama mmoja wa mbuzi, likimuacha na ulemavu wa kukatika vidole vitatu vya mkono wa kushoto na majereha mabaya sana usoni.
Kila nikiendaga Tabora huwa sikasahau kale ka mtaa tulikokuwa tunaishi aisee