Taja jambo lolote lililotamba enzi hizo na unahisi vijana wa leo hawajashuhudia zaid ya kusikia tu!

Ha ha ha haaah Babaubaya umenikumbusha kijiji kimoja huku kwetu alienda mchungaji kuhubiri injili, gari yake ilikuwa imechorwa msalaba kwa rangi nyekundu, alijikuta yuko peke yake wenyeji wamekimbilia mashambani.

we unafikiri kuna mtu anapenda kufa kizembe??
 
Last edited by a moderator:
Maviatu yenye soli kubwa kama inchi 3-5...!

umesahau na vle viatu vya chakacha,na raba za solo,unavaa ukienda church 2!ukirudi utamsikia maza vua haraka viatu na hzo nguo za kwendea kanisa!duh jaman maisha yanabdilika kweli!
 
umesahau na vle viatu vya chakacha,na raba za solo,unavaa ukienda church 2!ukirudi utamsikia maza vua haraka viatu na hzo nguo za kwendea kanisa!duh jaman maisha yanabdilika kweli!

kupiga picha ni mpaka sikukuu tena ukipiga picha yenyewe unaonyesha dole gumba!
 
Maeneo ya vijijini ukiona gari jekundu ni wanyonya damu!
Ilinitokea live nilipokwenda kumsalimia babu, hiyo siku tulikwenda kusanya kuni habla hatujaingia porini gari lenye rangi nyekundu likawa linakuja kwa mbele yetu, wale ndugu zangu walikimbia wote porini huku wakiambia kwa kilugha "bee mkwamisi kimbile avanyonya damu ivo vakusa na mtuka si wiona ilangi dung'u iyoo!"

Tena mnyonya damu huyo alikuwa ni mwanamke akiitwa Msekwa
 
Ukikutana Na mtu usiku, unamwambia "usiku" asipokujibu unatoka nduki ukijua ni ndondocha.
 
umesahau na vle viatu vya chakacha,na raba za solo,unavaa ukienda church 2!ukirudi utamsikia maza vua haraka viatu na hzo nguo za kwendea kanisa!duh jaman maisha yanabdilika kweli!
...hehehe...umenikumbusha "saa sita utanikoma"...vile viatu flani hivi vilikuwa vya plastic....ikifika mida ya mchana jua kali unabeba mkononi mwenyewe...!!!
 
Zamani ukikutana na police ghafla.. Unamsalimia mara nne nne! Lakini cku hz,unaweza hata kumchapa!
 
Jeans za wakati huo zikiitwa Lee.
Kulikuwa na Lee West halafu Lee Major.
Viatu vya platform lazima viwe vyekundu au brown.
Halafu ukiwa nazo lazima uvae saa.
 
Zamani ukikutana na police ghafla.. Unamsalimia mara nne nne! Lakini cku hz,unaweza hata kumchapa!

kipindi hiyo polisi wenyewe ni vipande vya watu yaan hadi full respect.. Siku hizi polisi unaeza ukamchapa hata kofi
 
Mabasi ya UDA (Usafiri Dar es Salaam). Mabasi aina ya Leyland Albion.

Umenikumbusha mbali mkuu. Ukipanda mabasi hayo lazima upandie mlango wa nyuma kisha unakutana na konda na kimashine chake cha kukatia tiketi then unateremkia thr mlango wa mbele.
 
1 Reactions
Reply
Back
Top Bottom