Taifa Stars yafungwa 1 - 0

Nemesis

JF-Expert Member
Feb 13, 2008
5,457
4,351
Mwendo wa kuelekea kombe la dunia umezidi kuwa mgumu baada ya timu ya Taifa kufungwa na visiwa dhaifu kisoka. Bao la wenyeji limefungwa dakika ya 73. Hata hivyo tusikate tamaa, tunaweza kuifunga Cameroon wiki ijayo.
 
hivi ni kwa nini tunatumia njia ndefu kupata jibu la 1 + 1 na ilhali tuna maswali magumu yanatukabili.

timu yetu ya taifa kwa kweli haina mwamko wa kimapinduzi... hawa vijana wanatakiwa fahamu kwamba wawapo uwanjani ni bendera ya taifa wanayoiwakilisha!

Somo la Uraia liongezwe katika ratiba za mazoezi yao!
 
Minimo (Maximo) ni kocha wa gwaride, hivi aliwahi kufundisha klabu ipi duniani au timu ya Taifa na kuwa na mafanikio yaliyostahili apewe mkataba na kulipwa mabilioni ya fedha na sirikali?
 
Hivi tatizo ni kocha, wachezaji au mfumo??????
Nasikitika kufungwa fungwa hivi la sivyo nitahama nchi ohoooo
 
ovyoooooooooooooooooo wanakera hadi basiiii wanatupa kimuhe muhe hadi twaamini na sisi tuna ka manchester united ketu ka taifa lakini ovyooo
 
yan nimekereka kama mie ndo mwenye timuu...looh so kwa mahesabu ya haraka haraka if cape verde walifungwa na cameroon,na sie tukafungwa na cape verde basi hata huko camerun tusije enda maana tutabebeshwa migoliii
 
na nimesoma mahala imelalamikiwa kuwa goli tulilofungwa ni makosa ya kipa...nachoshindwa kuelewa iweje kocha akamwita ivo mapunda so mapema n haraka after kufungiwa wakati hajacheza match nyingi na kumwacha mtu kama juma kaseja??hivi kaseja alimfanyaga kosa gan maximo???sio bure aiseee
 
na nimesoma mahala imelalamikiwa kuwa goli tulilofungwa ni makosa ya kipa...nachoshindwa kuelewa iweje kocha akamwita ivo mapunda so mapema n haraka after kufungiwa wakati hajacheza match nyingi na kumwacha mtu kama juma kaseja??hivi kaseja alimfanyaga kosa gan maximo???sio bure aiseee

Tatizo si mtu mmoja,kosa linaweza kutokea kwa mtu yeyote awapo uwanjani.Kama timu ni nzuri ingesawazisha na kufunga la ushindi.Lakini kama walitolewa kamasi na Mauritius nyumbani leo hii unategemea muujiza?
Mimi siwalaumu wachezaji wala kocha hawa wanajua kuwa kila mtu anawatazama wao walete ushindi sasa wao wamefanya kila lilo ndani ya uwezo wao na hayo ndo mavuno yaani uwezo wao ndo umeishia hapo.

Tuwape moyo wakamilishe ratiba vizuri angalau wasitoke kwa aibu ya magoli sawa na idadi ya wachezaji uwanjani.
 
Mkuu Mtu mzima, ninakubaliana na wewe ni vema tukawapa moyo ili wakamilishe ratiba ndiyo maana nikasema huenda tukashinda Jmosi dhidi ya Cameroon uwanja wa Taifa Dar.

Mkuu Mtaalam, ni haki kukerwa pale matokeo yanapokuwa tofauti na matarajio na wewe ndiyo mwenye timu. Yaani ile ni timu yetu Watanzania ndiyo maana inaitwa Taifa stars (wachezaji nyota wa taifa).
 
taifa maradhi oooh samahanini wakuu taifa stars. poleni na tuwe pole sote maana ni aibu kwa kweli.

maana hatujui ni lipi ambalo sisi tunaliweza
 
kwa utabiri wangu wa chap chap kampeni hizi za sasa tutavurunda kuliko hata zile za ghana ambazo mpaka dakika za mwisho tulikua hai hai....kwa aibuu hatukawii shika mkia alafu sijui tutaambiwa nini ndo ndege yetu idara ya mpira yaanza kupaa nako???maana kila siku maximo keep on saying ndo kwanza twaanza,inakua kama benitez anavyowapaga moyo wana wa bwawa la maini,tuko kati kati ya msimu wemsahaachwa kama point 9 au kumi utasikia ndo msimu wetu umeanza
 
taifa maradhi oooh samahanini wakuu taifa stars. poleni na tuwe pole sote maana ni aibu kwa kweli.

maana hatujui ni lipi ambalo sisi tunaliweza

...Mkuu ukija idara ya Ngoma na wizi wa sanaa za wengine ndo fani pekee tunayoimudu kuliko nchi nyingi duniani.... Sijui kwa nini hakuna mashindano ya ngoma ya dunia....lol

Tumeombwa na tunaendelea kuombwa tumpe nafasi Maximo ambaye hata simtofautishi na makocha wa simba au yanga ambao wakiwa na biff na mcehzaji watamuotesha kutu benchi. Kuna golikipa kama Kaseja ambaye sidhani kama kashuka chat na huyu maximo ameapa kutomuita stars (Ndolanga style) labda awe ameondoka....

Naulizaaaa.... kama hakuna faida na mpaka sasa soka halijakua as we promised then what????? basi hata mie naweza kuwa kocha wa stars kama ndo hivyo
 
Tatizo la Taifa stars siyo mlanda mlango, Ivo Mapunda bado anaonyesha uwezo mkubwa sana, sioni tunachokikosa kutoka kwa Kaseja. Tatizo ni washambuliaji, tena tunaviongo wazuri kama vile Nizar Khalfani na Athman Idd. Kwa mfano hiyo mechi ya jana, tulitaka tutoke 0 - 0? kwanini wafungaji walishidwa kupata bao dakika zote 90? tulitaka Ivo azuie mpaka mwisho ili tutoke nao sare sare, sare zingetufikisha wapi? Siuoni sababu ya kumlaumu Ivo kwa kagoli hako kamoja. Lets find strikers hata kama ni kwa kuanzisha chuo cha kufundisha namna ya kufunga magoli.
 
I want to say something ambacho wadau wengi wa soka humu JF na Tz kwa ujumla hawatapenda kukisikia?

Hivi team ya taifa hukusanya wachezaji (asilimia kubwa) toka wapi?, si klabu zetu hizi hizi?, si SIMBA NA YANGA?, asa let me say this; kwa mfumo huu DUME wa kuona SIMBA NA YANGA ni alfa na omega ktk soka la bongo, na kwa system ambayo hizi klabu zinajiendesha na kutafuta wachezaji na ikibidi kuwaendeleza..then TZ we will be lagging behind FOREVER!!!!

Wengi hatupendi kukubali ukweli lakini twende mbele turudi nyuma soka ya Bongo kwa system hii tuliyonayo itabakia kuwa nyuma siku zote, i mean tutakuwa TUNABAHATISHA!!

Kwa wewe mpenzi wa soka unayesoma hapa sikia hii;

Kazi ya Fellipe Scorali, Van Basten, Cappello etc kimsingi, kazi yao sio kumfundisha Ronaldo au Robben au Rooney jinsi ya kucheza mpira, ila tu kuangalia the way atakavyo pair mastaa wake, atumie tactics gani etc ili kushinda, kazi ya kumfundisha mpira unavyochezwa, kumjenga mchezaji etc ni kazi ya SAF, AW, Ancelloti, au Rikaard, sio kazi za national coach.

Binafsi naona still kama soka yetu ya klabu za ndani itaendelea kuwa ya kubahatisha kama hivi ilivyo then we should not labour ourselves alot to expect makubwa from our national team...!

Kwa mfumo huu dume tukionao, wakuu nawambia hata akija Guss Hiddink au Scorali still we will be far from being better!!, tutamlaumu Maximo mzee wa watu bure!!

Kama unabisha jiulize hili: Ivi kweli ni kazi ya Maximo kumfundisha Emmanuel Gabriel kufunga ni hvi unapiga, hivi, mguu unaweka hivi, unainama hivi kidogo, panalti unapiga hiviii, etc??

Not really bro!!!
 
Soka la Tanzania lina matatizo mengi mno
1.Wachezaji hawaandaliwi mapema
Wachezaji wetu wamekosa basics za uchezaji soka vitu kama ball control,nguvu na ufungaji ni vitu ambavyo inatakiwa mchezaji avijue tangu mdogo kama ni mfungaji aanze kufunga magoli tangu akiwa mdogo

2.Kocha hatufai
Sina maana kwamba ni mbovu but Tanzania bado ni changa sana kwenye soka nafikiri tunatakiwa tupate kocha toka SERBIA,YUGOSLAVIA,ROMANIA,CZECH,GERMANY&FRANCE
Hawa jamaa wana experience na soka la africa

3.Timu ya Taifa
Naona timu ya taifa yote hutoka DSM,kuna umuhimu wa kujenga timu za vijana mikoani ili baadae tupate wachezaji kwa sasa ni usa nii mkubwa sijaona kazi anayofanya huyo TINOCO anakula hela za bure
 
kwa kweli tuna matatizo kila idara.

mawazo yako ni mazuri ila watanzania tunapenda maendeleo ya haraka haraka.

tokea kwenye siasa mpaka ngazi nyengine.


hata kusoma mwananfunzi anahangaika kwa kutafuta kuiba mitihani, ni shem lkn ndio ukweli tena mpaka chuo kikuu.


ukweli tunahitaji kubadilika sana tena sana


tuache tabia ya zima moto
 
Tunahitaji mabadiliko ya benchi la ufundi; anfikiri matokeo ya mechi na Cameroun wiki ijayo yanatosha kumfungia virago huyu kocha Mbrazil 'koko'

Kwanza mkataba wa MAximo unaisha mwezi huu, bora asijaribu hata kufikiria extension aondoke kimyakimya tutaanza upya raundi za marudiano.
 
Sifa Moja Kubwa Ya Sisi Watanzania Ni Mafundi Wa Maneno! Ni Nchi Gani Duniani Iliyowahi Kuwa Na Wachezaji Wazuri Bila Kuandaliwa Tangu Wakiwa Wadogo! Sasa Ni Miaka Zaidi Ya 30 Tunafungwa Na Kila Tukifungwa Tunarudi Kujadili... Tukibahatisha Mechi Moja Tumetosheka... Utafikiria Manyani Na Kesho Tutajenga Nyumba Yanaponyeshewa. Hebu Tuanze Kuwafunza Watoto Tangu Wakiwa Na Miaka 7........baada Ya Miaka 10 Tutayaona Matokeo
 
jamani huko sio kwetu!Raisi avipe vitu vingine kipaumbele na sio mpira!Tanzania kichwa cha mwendawazimu!hivi wanashindwa nini kumsuck kocha?
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom