Taifa Stars waliwatoroka polisi Abidjan kimya kimya

BAK

JF-Expert Member
Feb 11, 2007
124,792
287,994
Date::2/26/2009
Taifa Stars waliwatoroka polisi Abidjan kimya kimya
Na Saleh Ally, Abidjan
Mwananchi

UAMUZI wa kikosi cha Taifa Stars kuamua kutokula chakula kwenye hoteli ya Golf ya mjini hapa ili kukwepa hujuma, kulizua tafrani kubwa baada ya askari Polisi aliyepewa dhamana ya kuwalinda kutaka kuwalazimisha kupanda kwenye basi kwa nguvu.

Stars juzi iliibuka na ushindi wake wa kwanza wa mashindano ya CHAN kwa kuwachapa wenyeji Ivory Coast kwa bao 1-0 lililofungwa na Mrisho Ngassa kwa kichwa cha kuchupa.

Kamati maalum iliyo jijini hapa ilichukua uamuzi wa kuhakikisha Stars hawali chakula cha hotelini hapo na maandalizi yakafanyika kwenda kula mafichoni ili kuepuka hujuma hasa suala la kuwekewa 'vitu' mbalimbali kwenye chakula.

Lakini ilibidi ifanyike kazi ya ziada kuwatoroka walinzi ambao wamekuwa wakitembea na timu hiyo tangu imewasili jijini hapa, wakiwamo askari Polisi wawili wa usalama barabarani wenye mbwembwe za kila namna.

Wachezaji Stars walitoroka kimya kimya kutoka hoteli ya Golf ndani ya Taxi sita kwenda kula huko walikopangiwa, baada ya hapo walinzi hao walianza kuwasaka kila kona ya jiji na mwisho walifanikiwa kuwapata pale walipokuwa kitu ambacho kilimshangaza kila mmoja.

'Kila mtu alishangaa jamaa wamepajua vipi, tulibaki tumepigwa na butwaa na mara moja wakaanza kutulazimisha kupanda kwenye gari, lile basi tunalotumia lakini viongozi pamoja na (Crescentius ) Magori na Teddy Mapunda wakazuia. Hatukupanda.

'Walitaka kuanza kutumia nguvu na sisi tukagoma, ikawa mshike mshike, lakini mwisho jamaa wakakubali kufuatana na sisi. Tukaingia kwenye zile taxi na kuanza kurudi hotelini huku wakitusindikiza kwa ving'ora na basi likiwa tupu,' anaeleza mmoja wa wachezaji wa Stars.

Lakini hali ya kuwalazimisha wachezaji kupanda kwenye basi hilo tayari ilionyesha kulikuwa na walakini na askari mmoja aliiambia Mwananchi kwamba ule ni utaratibu ingawa mmoja alikiri kwamba ilikuwa ni amri kutoka ngazi za juu zinazoshughulikia masuala ya usalama katika michuano ya CHAN ambao walitaka kuona lazima wachezaji wa Stars wapande basi hilo.

Kumekuwa na hujuma katika mechi nyingi hasa katika nchi za Afrika kitu ambacho kimeifanya Stars kuongeza umakini hasa inapokua mbali na nyumbani.

Hali hiyo pia ilijitokeza wakati wa mechi yake ya mwisho kufuzu katika michuano ya CHAN dhidi ya Sudan mjini Kharthoum ambako wenyeji walilala kwa mabao 2-1.

Imeelezwa kumekua na tabia ya kupulizia dawa kwenye vyumba au kwenye chakula na wachezaji baada ya muda mfupi wanachoka hivyo kuwafanya washindwe kucheza kwenye viwango vyao. Ingawa Caf imeshindwa kuthibitisha hilo hadharani lakini imekua hali inayojitokeza mara kwa mara.
 
Date::2/26/2009
Taifa Stars waliwatoroka polisi Abidjan kimya kimya
Na Saleh Ally, Abidjan
Mwananchi

UAMUZI wa kikosi cha Taifa Stars kuamua kutokula chakula kwenye hoteli ya Golf ya mjini hapa ili kukwepa hujuma, kulizua tafrani kubwa baada ya askari Polisi aliyepewa dhamana ya kuwalinda kutaka kuwalazimisha kupanda kwenye basi kwa nguvu.

Stars juzi iliibuka na ushindi wake wa kwanza wa mashindano ya CHAN kwa kuwachapa wenyeji Ivory Coast kwa bao 1-0 lililofungwa na Mrisho Ngassa kwa kichwa cha kuchupa.

Kamati maalum iliyo jijini hapa ilichukua uamuzi wa kuhakikisha Stars hawali chakula cha hotelini hapo na maandalizi yakafanyika kwenda kula mafichoni ili kuepuka hujuma hasa suala la kuwekewa 'vitu' mbalimbali kwenye chakula.

Lakini ilibidi ifanyike kazi ya ziada kuwatoroka walinzi ambao wamekuwa wakitembea na timu hiyo tangu imewasili jijini hapa, wakiwamo askari Polisi wawili wa usalama barabarani wenye mbwembwe za kila namna.

Wachezaji Stars walitoroka kimya kimya kutoka hoteli ya Golf ndani ya Taxi sita kwenda kula huko walikopangiwa, baada ya hapo walinzi hao walianza kuwasaka kila kona ya jiji na mwisho walifanikiwa kuwapata pale walipokuwa kitu ambacho kilimshangaza kila mmoja.

'Kila mtu alishangaa jamaa wamepajua vipi, tulibaki tumepigwa na butwaa na mara moja wakaanza kutulazimisha kupanda kwenye gari, lile basi tunalotumia lakini viongozi pamoja na (Crescentius ) Magori na Teddy Mapunda wakazuia. Hatukupanda.

'Walitaka kuanza kutumia nguvu na sisi tukagoma, ikawa mshike mshike, lakini mwisho jamaa wakakubali kufuatana na sisi. Tukaingia kwenye zile taxi na kuanza kurudi hotelini huku wakitusindikiza kwa ving'ora na basi likiwa tupu,' anaeleza mmoja wa wachezaji wa Stars.

Lakini hali ya kuwalazimisha wachezaji kupanda kwenye basi hilo tayari ilionyesha kulikuwa na walakini na askari mmoja aliiambia Mwananchi kwamba ule ni utaratibu ingawa mmoja alikiri kwamba ilikuwa ni amri kutoka ngazi za juu zinazoshughulikia masuala ya usalama katika michuano ya CHAN ambao walitaka kuona lazima wachezaji wa Stars wapande basi hilo.

Kumekuwa na hujuma katika mechi nyingi hasa katika nchi za Afrika kitu ambacho kimeifanya Stars kuongeza umakini hasa inapokua mbali na nyumbani.

Hali hiyo pia ilijitokeza wakati wa mechi yake ya mwisho kufuzu katika michuano ya CHAN dhidi ya Sudan mjini Kharthoum ambako wenyeji walilala kwa mabao 2-1.

Imeelezwa kumekua na tabia ya kupulizia dawa kwenye vyumba au kwenye chakula na wachezaji baada ya muda mfupi wanachoka hivyo kuwafanya washindwe kucheza kwenye viwango vyao. Ingawa Caf imeshindwa kuthibitisha hilo hadharani lakini imekua hali inayojitokeza mara kwa mara.
"Ingawa Caf imeshindwa kuthibitisha hilo hadharani lakini imekua hali inayojitokeza mara kwa mara..." sasa mbona ulitaka uthibitisho wa CAF kama unajua hilo tatizo lipo mara kwa mara?

"Hali hiyo pia ilijitokeza.. dhidi ya Sudan mjini Kharthoum..." Nini kilitokea Kharthoum, hebu taja kimoja!

"Kamati maalum iliyo jijini hapa ilichukua uamuzi wa kuhakikisha Stars hawali..." kamati maalum ya nani, CAF, UMISHUMTA au kamati maalum ya bunge la Jamhuri?

"Kumekuwa na hujuma katika mechi nyingi..nchi za Afrika..." Taja timu moja iliyojumiwa, ilihujumiwa vipi!

"...ilibidi ifanyike kazi ya ziada kuwatoroka walinzi..." Ungewauliza CAF halafu ukaripoti ni utaratibu gani huo unaosema wageni hawatakiwi kukanyaga nje ya hoteli kwenda wanapotaka kula mpaka watoroke.

Eti mwandishi anaenda kuuliza wahusika kama tatizo lipo, hapati uthibitisho, anaamua kutangaza tatizo lipo!

Udaku!
 
Hizi ndio mbinu za Medani, nawatakia kila la heri katika kutupatia ushindi. Sijui mechi ijayo wale jamaa wa Senegal wanaoonesha TVyao online watatufanyia tena kama siku ya TZ na Ivory Coast, manake walionesha tu kpindi cha kwanza.
 
"Ingawa Caf imeshindwa kuthibitisha hilo hadharani lakini imekua hali inayojitokeza mara kwa mara..." sasa mbona ulitaka uthibitisho wa CAF kama unajua hilo tatizo lipo mara kwa mara?

"Hali hiyo pia ilijitokeza.. dhidi ya Sudan mjini Kharthoum..." Nini kilitokea Kharthoum, hebu taja kimoja!

"Kamati maalum iliyo jijini hapa ilichukua uamuzi wa kuhakikisha Stars hawali..." kamati maalum ya nani, CAF, UMISHUMTA au kamati maalum ya bunge la Jamhuri?

"Kumekuwa na hujuma katika mechi nyingi..nchi za Afrika..." Taja timu moja iliyojumiwa, ilihujumiwa vipi!

"...ilibidi ifanyike kazi ya ziada kuwatoroka walinzi..." Ungewauliza CAF halafu ukaripoti ni utaratibu gani huo unaosema wageni hawatakiwi kukanyaga nje ya hoteli kwenda wanapotaka kula mpaka watoroke.

Eti mwandishi anaenda kuuliza wahusika kama tatizo lipo, hapati uthibitisho, anaamua kutangaza tatizo lipo!

Udaku!


,,,,Mzee inaonesha umekua mkali sana kwa huyu REPORTER,lakini kama wewe ni mpenzi wa soka la KIAFRIKA,mbona hizi ni habari za kweli tu ingawa FACTS zake ni vigumu sana kuzianika.:rolleyes::rolleyes:
 
Ndio twajua wanawewkewa dawa wanachoka haraka sana...na kuishiwa nguvu kabisa.maji na chakula ndio vibaya zaidi ya vyumba kubadilishia nguo
 
mimi hapa ndio huwa nawakubali watu kama akina Mhe. Magori
huwezi kupelekwa pelekwa tu na wenyeji wakati huo huo unatakiwa
kucheza nao game jioni.
Nimekipenda kitendo hiki 100%
BIG UP TO BRAZA MAGORI NA JOPO LAKE...
 
Fitna ya mpira ipo sana Afrika na hasa Afrika magharibi. Hongereni sana kwa kuwa makini na fitna hizo. Nakutakieni kila la kheri na mafanikio. Tujitahidi Kombe lije Tz.
 
Hongera kwa meza ya ufundi kung'amua mbinu hizo mapema, Enzi za mwalimu wangeliondoka na Mwanamalundi/shekhe Yahaya.

Endeleeni kususia misosi yao ili mrudi na ushindi kwani watu wa magharibi ni hatari sana kwa mazingaobwe.
 
Mkuu Amwamba, ratiba ni hiyo chini utaona na muda, nikiipaste haikai vizuri, lakini utaipata hapa Fixtures: CHAN 22/02-08/03/09 - African Nations Championship 2009 - CAF

No Match Gp Date time Venue:
16H00
1. Cote D’Ivoire V Zambia A 22.02.09 Abidjan
19H00
2. Senegal V Tanzania A 22.02.09 Abidjan
15H00
3. Ghana V Zimbabwe B 23.02.09 Bouake
18H00
4. RD Congo V Libya B 23.02.09 Bouake
16H00
5. Zambia V Senegal A 25.02.09 Abidjan
19H00
6. Tanzania V Cote D’Ivoire A 25.02.09 Abidjan
15H00
7. Zimbabwe V RD Congo B 26.02.09 Bouake
18H00
8. Libya V Ghana B 26.02.09 Bouake
16H00
9. Cote D’Ivoire V Senegal A 28.02.09 Abidjan
16H00
10. Zambia V Tanzania A 28.02.09 Bouake
16H00

11. Ghana V RD Congo B 01.03.09 Bouake
16H00
12. Zimbabwe V Libya B 01.03.09 Abidjan

Semi-Finals/½ Finale

13. 1st B V 2nd A 04.03.09 15H00 Bouake

14. 1st A V 2nd B 04.03.09 19H00 Abidjan

3rd Place match/Match de classement

15. Loser-Perdant: 13 V Loser-Perdant: 14 07.03.09 16H00 Abidjan


Final match/Match final

16. Win./Vainq.:13 V Win./Vainq.: 14 08.03.09 16H00 Abidjan
 
VIJANA TUPENI RAHA WATANZANIA, waTanzania sote tuko nyuma yenu.

Mungu Ibariki Taifa Stars, Mungu Ibariki Tanzania.
 
Kweli nakumbuka tulienda kule shinyanga kwenye mashindano ya shule za Sekondari basi unajua mchana watu wakishakula wanalala basi walitumwagia upupu si kawaida ndani ya vyumba ,ilibidi tushindwe maana ni kujikuna tu hakuna kutliza mpira.
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom