Taifa lipo njiapanda, wananchi ndiyo tutakaoliokoa au kuliangamiza

Mystery

JF-Expert Member
Mar 8, 2012
15,480
30,152
Naanza kwa kunukuu Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Ibara ya 18(1) ambayo inasema hivi " Kila mtu yuko huru kuwa na maoni yake na kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana zozote kupitia chombo chochote bila ya kujali mipaka ya nchi na pia Uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa kati na chombo chochote" mwisho wa kunukuu.

Nimeanza kwa kunukuu Ibara hiyo ya Katiba ya nchi yetu, ambayo ndiyo sheria mama nchini mwetu, ambayo pia Katiba hiyo viongozi wetu wakuu akiwemo Rais wetu wa nchi aliapa kuilinda na kuitii kabla ya kukabidhiwa madaraka ya kuliongoza Taifa letu.

Kwa bahati mbaya sana Taifa letu linaloongozwa na serikali hii ya CCM ya awamu ya tano imeintroduce kitu cha hatari sana kwenye nchi yetu ambacho kama kisipokemewa na kila mwananchi mwenye kuitakia mema nchi hii, hakika nchi hii inaelekea kuangamia.

Kitu hicho si kingine Bali ni kuwa Taifa letu hivi sasa linatakiwa liimbe mwimbo mmoja tu wa kuisifu serikali yetu ya awamu ya 5 hususani Rais wetu kwa kila jambo wanalolifanya na kwa yeyote anayeikosoa serikali hii ametengenezewa msamiati mpya wa kuitwa mchochezi na mtetezi wa mafisadi wanaopora rasilimali zetu!

Kutokana na hali hiyo Taifa letu hivi sasa wananchi wake almost wote wamejazwa hofu kuanzia viongozi na wanachama wa CCM, viongozi na wanachama wa vyama vya upinzani, wanaharakati, viongozi wa dini, vyombo vya habari vya Umma pamoja na vya binafsi na wananchi wote kwa ujumla wake wametengenezewa mazingira ya kuzibwa midomo yao kwa yeyote anayetaka kuikosoa serikali ya awamu ya 5.

Lakini wakati huo huo metolewa RUKSA isiyo na mipaka kwa yeyote anayeimba wimbo wa kuisifia serikali ya awamu ya 5!

Tumeshuhudia wale wanaoandamana na kutoa maoni yao kuwa Katiba ya nchi ibadilishwe na kumfanya Rais wetu JPM awe Life President wetu ingawa ni maoni ya hatari sana yanayoweza kulitumbikiza Taifa letu kwenye machafuko, lakini watu hao wamekuwa wakiachwa huru bila kuguswa na chombo chochote cha dola.

Lakini wakati huo huo kwa yeyote mwenye kutoa maoni ya kuikosoa serikali hii ya awamu ya 5, ingawa ni haki yake ya kikatiba tumekuwa tukishuhudia watu wa aina hiyo wakishughulikiwa kikamilifu kwa kuwekwa ndani kwa kile kinachoitwa masaa 'yao' 48 ya wateule wa Rais!

Tunawaomba hao wateule wa Rais watufafanulie ni Ibara ipi ndani ya Katiba yetu inayotoa katazo kwa mwananchi yoyote kumkosoa Rais wetu?

Hebu tujiulize kitu kimoja iwapo ndani ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, Ibara ya 3(1) inatamka wazi kuwa nchi yetu itakuwa na mfumo wa vyama vingi vya kisiasa na vyama hivyo vitatakiwa kuwa huru katika uendeshaji wa shughuli zake za kisiasa, sasa tunapaswa kumuuliza Rais wetu amepata wapi mamlaka ya kupiga marufuku mikutano yote ya kisiasa ya vyama vya upinzani hadi mwaka 2020 wakati akiruhusu chama chake cha CCM kiendelee kufanya shughuli zake za kisiasa bila kubughuziwa na vyombo vya usalama?

Baba wa Taifa Mwalimu Nyerere katika moja ya hotuba zake amewahi kutamka kuwa wananchi hatupaswi kukaa kimya tunapoona Rais wetu ana elements za kuendesha nchi yetu kidikteta na tunapaswa kupaza sauti zetu bila woga kumkenea Rais wa aina hiyo na Mwalimu Nyerere alikwenda mbali zaidi na kumuelezea Rais wa aina hiyo asiyetaka kuendesha nchi kwa misingi ya Katiba yetu kuwa HATUFAI.

Kwa hiyo hivi sasa siyo wajibu wa vyama vya siasa vya upinzani peke yao kukemea mfumo wa uendeshaji wa serikali ya awamu ya 5 wa kukandamiza waziwazi demokrasia yetu bali ni wajibu wa kila mwananchi, kila Kiongozi wa dini na kwa taasisi za haki za kibinadamu pamoha na vyombo vya habari vyote kukemea kwa nguvu zetu zote kuiambia serikali yetu ya awamu ya 5 kuwa ijirekebishe na kurudi kwenye mfumo wa utawala wa sheria wa Kuifuata Katiba ya nchi ambapo Rais wetu kabla hajaingia madarakani aliapa kuilinda na kuitii Katiba yetu.

Iwapo wananchi tutaamua kukaa kimya kwa hofu ya kiviogopa vyombo vya dola kutulaza ndani kwa zile saa 'zao' 48 za wateule wa Rais kwa kile walichokibatiza jina la uchochezi, hakika tutakuwa tumeamua kuliangamiza Taifa letu na historia haitatuacha salama kwa maana itatuhukumu.

Mungu libariki Taifa letu la Tanzania na uliepushe lisiangamie.
 
Na mbaya zaidi baadhi ya wa-Tanzania wakiwemo viongozi wa mihimili ya ''dola'' kama Spika, kaimu Jaji Mkuu, viongozi wa CCM, media na wananchi wa kawaida wameshaingiwa na hali ya kisaikolojia inayojulikana ''Stockholm Syndrome'', yaani wameshaanza kukubali hali na kuizoea na kuiona ni hali safi kabisa na ya kawaida kabisa kiasi maandamano yanafanyika kupongeza hali hii ya ukiukwaji wa uhuru wao kama wenye nchi na badala yake kuwa mateka.
 
Na mbaya zaidi baadhi ya wa-Tanzania wakiwemo viongozi wa mihimili ya ''dola'' kama Spika, kaimu Jaji Mkuu, viongozi wa CCM, media na wananchi wa kawaida wameshaingiwa na hali ya kisaikolojia inayojulikana ''Stockholm Syndrome'', yaani wameshaanza kukubali hali na kuizoea na kuiona ni hali safi kabisa na ya kawaida kabisa kiasi maandamano yanafanyika kupongeza hali hii ya ukiukwaji wa uhuru wao kama wenye nchi na badala yake kuwa mateka.
Very true Mkuu.

Ni wajibu wa kila mtanzania popote alipo kukemea kwa nguvu zote hii hali ya serikali yetu ya awamu ya 5 kuamua kuisigina Katiba ya nchi waziwazi huku wananchi walio wengi wakiendeleza unafiki wao kwa kuamua kukaa kimya, bila kuiona hatari ambayo Taifa letu itakabiliana nayo huko mbele kwa wananchi kutoikemea hali hiyo mapema kadri iwezekanavyo.
 
Ni kweli kabisa Mkuu BAK.

Kwa bahati mbaya sana nchi yetu kwenye awamu hii ya 5 tumepata Mkuu wa nchi ambaye anaamini kila kitu anachoongea yeye ni 100% perfect na kwa yeyote anayeamua kumkosoa, ingawa ni haki yake ya kikatiba, anamwita analeta chokochoko na anaviagiza vyombo 'vyake' vya dola vimshughulikie!

Kama Taifa hakika safari hii tumeuingia mkenge.....
 
Ni mtu hatari sana huyu Mkuu. Nahofia sana kuhusu nchi yetu inapoelekea Mkuu.



Ni kweli kabisa Mkuu BAK.

Kwa bahati mbaya sana nchi yetu kwenye awamu hii ya 5 tumepata Mkuu wa nchi ambaye anaamini kila kitu anachoongea yeye ni 100% perfect na kwa yeyote anayeamua kumkosoa, ingawa ni haki yake ya kikatiba, anamwita analeta chokochoko na anaviagiza vyombo 'vyake' vya dola vimshughulikie!

Kama Taifa hakika safari hii tumeuingia mkenge.....
 
Viongozi wetu wa dini ndiyo wanao tukwamisha kama wao wangeli kuwa mstari wa mbele kutoa matamko ya misimamo sahihi nina imani huu UKOLONI ungeli ondoka bahati mbaya wanaogopa JELA kuliko MUNGU
 
Ni mtu hatari sana huyu Mkuu. Nahofia sana kuhusu nchi yetu inapoelekea Mkuu.

Wenye macho tunaona kabisa kuwa nchi yetu inaelekea shimoni.....

Lakini as usual ile Lumumba buku 7 team wanaendeleza 'mapambio' ya kumsifu Mkulu na kumwita mzalendo na mwenye uchungu na rasilimali zetu!

Sasa la kumuuliza huyo mlinzi wa rasilimali zetu, hivi ni nani yule aliyeuza nyumba zetu za serikali enzi zile kwa bei ya kutupa?

Hebu tena tuwaulize hivi ni nani aliyenunua ile boti ya mwendokasi ya kwenda Bagamoyo, ambayo haijafanya kazi zaidi ya muezi 2 na hivi sasa ipo juu ya mawe?
 
Inashangaza sana Mkuu kuona maovu yote aliyofanya huyu huyu akiwa Waziri leo wanajifanya wameyasahau na anaendelea kufanya maovu mengine ambayo ni tishio kubwa sana kwa nchi yetu kwa mfano kulidharau Bunge, kudharau katiba na sheria za nchi, kufuja pesa za umma kwa kuzitumia bila idhini ya Bunge na wala kufuata taratibu za manunuzi za Serikalini. Kitu cha kushangaza sana watu ndani ya Serikali kumuogopa huyu kiasi hiki hata kumwambia tu unavyofanya si sawa wanahofia! Na yeye kadri anavyoona anaogopwa ndivyo atazidi kufanya maovu ya kustaajabisha sana. Angalia hili la Bashite kwa mfano, kavunja sheria mara mbili mchana kweupe lakini hakuna wa kumgusa kisa ni mkolomije mwenzie!

Wenye macho tunaona kabisa kuwa nchi yetu inaelekea shimoni.....

Lakini as usual ile Lumumba buku 7 team wanaendeleza 'mapambio' ya kumsifu Mkulu na kumwita mzalendo na mwenye uchungu na rasilimali zetu!

Sasa la kumuuliza huyo mlinzi wa rasilimali zetu, hivi ni nani yule aliyeuza nyumba zetu za serikali enzi zile kwa bei ya kutupa?

Hebu tena tuwaulize hivi ni nani aliyenunua kile kivuko cha kwenda Bagamoyo, ambacho hakijafanya kazi zaidi ya muezi 2 na hivi sasa kipindi juu ya mawe?
 
Viongozi wetu wa dini ndiyo wanao tukwamisha kama wao wangeli kuwa mstari wa mbele kutoa matamko ya misimamo sahihi nina imani huu UKOLONI ungeli ondoka bahati mbaya wanaogopa JELA kuliko MUNGU
It is very true.

Hivi ni kweli mafundisho ya dini zetu ndivyo yanavyowaelekeza watumishi wetu wa Mungu wawe 'mabubu' wanapoona waumini wao wananyanyasika kama ambavyo hii serikali ya awamu ya 5 inavyofanya badala ya kujenga viwanda kama ilivyojinadi, badala yake imegeukia kujenga 'viwanda' vya kupambana na kutaka kuua upinzani nchini kwa kutumia vyombo vya dola ambavyo sisi walipa kodi ndiyo tunaovifanya viendelee kuwepo kupitia kodi zetu
 
Inashangaza sana Mkuu kuona maovu yote aliyofanya huyu huyu akiwa Waziri leo wanajifanya wameyasahau na anaendelea kufanya maovu mengine ambayo ni tishio kubwa sana kwa nchi yetu kwa mfano kulidharau Bunge, kudharau katiba na sheria za nchi, kufuja pesa za umma kwa kuzitumia bila idhini ya Bunge na wala kufuata taratibu za manunuzi za Serikalini. Kitu cha kushangaza sana watu ndani ya Serikali kumuogopa huyu kiasi hiki hata kumwambia tu unavyofanya si sawa wanahofia! Na yeye kadri anavyoona anaogopwa ndivyo atazidi kufanya maovu ya kustaajabisha sana. Angalia hili la Bashite kwa mfano, kavunja sheria mara mbili mchana kweupe lakini hakuna wa kumgusa kisa ni mkolomije mwenzie!
Yaani ameamua kumbeba kwa mbeleko huyo Bashite, ambapo hivi sasa hata kipofu hivi sasa anaona namna Mkulu anavyotumia kufavour hao makolomojie wenzie......

Hakuna hivi sasa mwananchi yeyote ambaye hajui kuwa Bashite kafoji vyeti.....

Hakuna asiyejua kuwa huyo Bashite aliingia na askari wenye silaha kwenye studio za Clouds na kuwatisha watangazaji wa studio hiyo kuwa atawabambikia makosa ya uuzaji wa madawa ya kulevya kama watagoma kumrushia clip yake ya Askofu Gwajima!

Lakini pamoja na madudu yote hayo Mkulu anamkingia kifua Bashite na anawakejeli watanzania kuwa eti yeye hapangiwi la kufanya kwa kuwa ni yeye mwenyewe aliyeenda Dodoma kuchukua fomu za kugombea Urais na hakushauriwa na mtu yeyote!

Sasa kwa kauli hiyo aliyotukejeli watanzania na sisi tunamsubiri 2020 tuone sisi aliyetukejeli kuwa hazitaki kura zetu, tuone kama kura yake moja na ya mama Jesca kama ndiyo zitatosha kumrejesha Ikulu!
 
  • Thanks
Reactions: BAK
Rais kula kiapo cha kulinda katiba ni taratibu tu, kwani asipotekeleza hashitakiwi leo wala kesho. Kinga kwa watawala ni maangamizi kwa nchi yoyote.
 
Rais kula kiapo cha kulinda katiba ni taratibu tu, kwani asipotekeleza hashitakiwi leo wala kesho. Kinga kwa watawala ni maangamizi kwa nchi yoyote.
Sass kama Rais anaapishwa kuilinda na kuitii Katiba ya nchi kama formality na haina ulazima wa kiasi hiko....

Kama ndiyo hivyo kuna haja gani kwa nchi kuwa na Katiba ambayo inatambulika kuwa ndiyo sheria mama iwapo unasema haina umuhimu wa kiasi hicho?
 
Na mbaya zaidi baadhi ya wa-Tanzania wakiwemo viongozi wa mihimili ya ''dola'' kama Spika, kaimu Jaji Mkuu, viongozi wa CCM, media na wananchi wa kawaida wameshaingiwa na hali ya kisaikolojia inayojulikana ''Stockholm Syndrome'', yaani wameshaanza kukubali hali na kuizoea na kuiona ni hali safi kabisa na ya kawaida kabisa kiasi maandamano yanafanyika kupongeza hali hii ya ukiukwaji wa uhuru wao kama wenye nchi na badala yake kuwa mateka.
It is true.

Yaani watu wanashangilia hao wanaoitwa waandamanaji wanaopendekeza JPM awe Life President wetu.....

Wakati Katiba yetu ya nchi inatoa ukomo wa miaka 10 kwa Rais yeyote hapa nchini kuwa hapaswi kuongoza nchi yetu kwa zaidi ya miaka 10
 
Rais kula kiapo cha kulinda katiba ni taratibu tu, kwani asipotekeleza hashitakiwi leo wala kesho. Kinga kwa watawala ni maangamizi kwa nchi yoyote.
This will never stay forever. There will come a time when everything will change and that time in the spiritual world is more sooner than later. Let's just wait and see

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mimi nadhani unataka huruma ya kisiasa tu! unachokitaka wewe ni kile unachokiita uhuru wa habari na mawasiliano kwa kuitumia katiba vibaya, ili upate fursa ya kuupotosha umma.
Unasema kwamba taifa lipo njia panda, wewe mwenyewe unafahamu kwamba hii si sahihi, bali chama chako chadema ndiyo kipo njia panda.
Jitahidi kuleta threads ambazo zitawarudisha ktk mstari, vinginevyo tutawamisi sana chadema.
 
Back
Top Bottom