Taifa limejaa vijana wenye ufahamu mdogo sana. Tuombe kwaajili ya vijana

Bonde la Baraka

JF-Expert Member
Sep 22, 2016
4,580
7,938
Habari wanajukwaa.
Katika pitapita yangu huku na kule, mitandaoni na hata katika mazingira halisi nazidi kuona vijana wako katika wimbi la ujinga.

Nimeona vijana wakishare pages na picha za watu maarufu kwa kuahidiwa kupewa zawadi mbalimbali hasa simu za iphone zenye gharama ya juu.
Mtu anasema nina simu 1000 kesho jioni nazigawa kwa watu 1000, ukishare mara nyingi utajinyakulia zawadi hii.

Wanashindwa hata kujiuliza maswali kama haya;

1. Simu 10000 zenye thamani ipatayo kama milioni 2 kila moja zitakuwa na gharama ya jumla ya sh. ngapi na je, nani aitoe bilioni mbili kwa vijana kama zawadi kwa kushare page yake tu?

2. Kama yeye atatoa zawadi zenye gharama ya bil.2 atapata faida gani ya ziada na kwa namna gani?

Halafu cha ajabu ujumbe ukiuangalia kwenye source yake kabisa ulitumwa miezi miwili nyuma ukisema zawadi zinatoka kesho lakini wao wanasambaziana kila leo.

Kama kijana anamtukana mwenzake kisa Manchester United au Arsenal huku ameusahau undugu wa kitaifa utasemaje huyo kijana yuko timamu?
Tusipoomba kwa nguvu mapema taifa litazidi kuzalisha vijana wa ajabu.
 
vijana wanauana kisa tako la mwanamke aliepita mbele yao na hata kumsalimia wakaogopa..

huyu anasema tako kubwa mwingine tako dogo mwishowe wanauana

wanabishana kuhusu man utd na arsenal hadi wanaumwa vichwa...
 
Habari wanajukwaa.
Katika pitapita yangu huku na kule, mitandaoni na hata katika mazingira halisi nazidi kuona vijana wako katika wimbi la ujinga.

Nimeona vijana wakishare pages na picha za watu maarufu kwa kuahidiwa kupewa zawadi mbalimbali hasa simu za iphone zenye gharama ya juu.
Mtu anasema nina simu 1000 kesho jioni nazigawa kwa watu 1000, ukishare mara nyingi utajinyakulia zawadi hii.

Wanashindwa hata kujiuliza maswali kama haya;

1. Simu 10000 zenye thamani ipatayo kama milioni 2 kila moja zitakuwa na gharama ya jumla ya sh. ngapi na je, nani aitoe bilioni mbili kwa vijana kama zawadi kwa kushare page yake tu?

2. Kama yeye atatoa zawadi zenye gharama ya bil.2 atapata faida gani ya ziada na kwa namna gani?

Halafu cha ajabu ujumbe ukiuangalia kwenye source yake kabisa ulitumwa miezi miwili nyuma ukisema zawadi zinatoka kesho lakini wao wanasambaziana kila leo.

Kama kijana anamtukana mwenzake kisa Manchester United au Arsenal huku ameusahau undugu wa kitaifa utasemaje huyo kijana yuko timamu?
Tusipoomba kwa nguvu mapema taifa litazidi kuzalisha vijana wa ajabu.
Umenikumbusha kuku wa kisasa!!
 
vijana wanauana kisa tako la mwanamke aliepita mbele yao na hata kumsalimia wakaogopa..

huyu anasema tako kubwa mwingine tako dogo mwishowe wanauana

wanabishana kuhusu man utd na arsenal hadi wanaumwa vichwa...
Usinikumbushe kituko hicho.
Niliwahi kumsimulia wife wangu alicheka sana.
Halafu wale waliouana ujue ni ndugu wa damu kabisa.
 
Hapa co kusema tuwaombee vijana,me nakataa kata kata......mifumo yetu ya elimu mibovu ndo inatuzalishia mambugila wengi wanaolitia aibu na hasara kubwa Taifa letu. Hatuna budi kufumua mifumo yetu ya elimu kuanzia vidudu mpaka vyuo vikuu ili kijana akitoka uko au akiwa anasoma uko awe na hamu ya kutaka kujifunza kitu au kuvumbua kitu co akili za kushea picha ili apate zawadi. "Mifumo mibovu ya uongozi na elimu uzalisha watu wa wabovu, vieleele na wapumbafu"
 
Hakuna haja ya maombi hapo. Ni stress tu zamaisha. Ukiwa na stress hauwezi kufikiri vizuri.
Neno ufahamu lina maana kubwa kuliko ulivyo lieleza. Man u au arsenal, simba au yanga ni sehemu ya burudani tu. Kutukana ni tabia tu haina uhusiano na ufahamu kwa maana anaye tukana anajua alitendalo.
 
Vijana wa sahivi ni ma expert katika kubet na kuimba tu. Mengine acha tuendelee tu kuwasoma
 
Shida sana tumebakia kulalamika kwenye mitandao ya kijamii na kushinda vijiweni.
 
Dunia ya Leo hutakiwi utumie akili nyingi lasivyo kila siku iendayo kwa Mungu utakuwa unaumia nafsi yako!!!
 
Back
Top Bottom