The lost
JF-Expert Member
- Jul 3, 2017
- 2,695
- 8,208
Nimemuona Zito ametwiti kuwa iundwe tume ya kijaji kuhoji watu wote walioteswa, kuumiza na kuharibiwa mali zao wakati wa awamu ya tano.
Mimi naona nchi yetu inahitaji jambo kubwa kabisa kwa sasa nalo ni MSAMAHA KWA WOTE waliotenda maovu wakiwa katika utumishi wao.
Neno la Mungu linasema "Hakuna amri iliyo kuu zaidi ya upendo" tuwapende na kuwaombea wale wanaotuudhi maana kama tukiwachukia tunafanya kipi cha maana? ama kama tukiwapenda wale tu wanaotupenda tutakuwa tumetenda ziada gani?
Kwa maana hata waovu huwapenda wale wawapendao. Basi kama taifa tujiepushe na visasi kwa maana hiyo siyo kazi ya mwanadamu bali ya Mungu.
Ole Sabaya, Paul Makonda na wengine walifanya kazi ya utumishi wao kwa uwezo wao, mapungufu yao yameonekana kuwa makubwa basi wasamehe na taifa lipate baraka kwa toba hiyo.
Tukiweka visasi mbele basi taifa letu litaangamia maana hakuna aliye salama kuanzia kwa Spika, naibu spika, Jaji mkuu, Mwanasheria mkuu wa Serikali, Mwenyekiti tume ya uchaguzi, Mkurugenzi wa tume ya uchaguzi. etc
Mimi naona nchi yetu inahitaji jambo kubwa kabisa kwa sasa nalo ni MSAMAHA KWA WOTE waliotenda maovu wakiwa katika utumishi wao.
Neno la Mungu linasema "Hakuna amri iliyo kuu zaidi ya upendo" tuwapende na kuwaombea wale wanaotuudhi maana kama tukiwachukia tunafanya kipi cha maana? ama kama tukiwapenda wale tu wanaotupenda tutakuwa tumetenda ziada gani?
Kwa maana hata waovu huwapenda wale wawapendao. Basi kama taifa tujiepushe na visasi kwa maana hiyo siyo kazi ya mwanadamu bali ya Mungu.
Ole Sabaya, Paul Makonda na wengine walifanya kazi ya utumishi wao kwa uwezo wao, mapungufu yao yameonekana kuwa makubwa basi wasamehe na taifa lipate baraka kwa toba hiyo.
Tukiweka visasi mbele basi taifa letu litaangamia maana hakuna aliye salama kuanzia kwa Spika, naibu spika, Jaji mkuu, Mwanasheria mkuu wa Serikali, Mwenyekiti tume ya uchaguzi, Mkurugenzi wa tume ya uchaguzi. etc