Taifa au CCM- Kadi au Katiba?

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,988
Na. M. M. Mwanakijiji

Habari ambazo zimekuwa zikitiririka kwa muda wa masaa kadhaa yaliyopita zinatuthibitishia kuwa waoga wanaongoza CCM sasa hivi. Habari za kuwa Spika wa Bunge la Muungano alipewa kibano katika mojawapo ya vikao vya juu vya CCM ni habari za kuudhi, kukera, na kuchekesha; yote kwa kwa wakati mmoja. Vile vile tukio la kujadili mambo ya Bungeni na taratibu za Bungeni kuonesha kutoridhishwa kwa mwenendo wa Bunge kwenye vikao vya chama ni tukio la kulaaniwa na kukataliwa na kila mpenda demokrasia.

Kwa vile CCM wamelewa ugimbi wa madaraka inaonekana hawajui kuwa Bunge siyo tawi la CCM wala Jumuiya ya chama. Spika wa Jamhuri ya Muungano siyo Spika wa Bunge la CCM. Bunge la namna hiyo halipo.

Bunge linaendeshwa kwa taratibu zake na wakati wowote mbunge yoyote hafurahishwi au kuridhishwa na mwenendo wa Bunge taratibu zipo za kutoa malalamiko yake na kama ni kundi kubwa la wabunge basi wana nafasi ya kujadili na hata kumuondoa Spika kwa taratibu za Kibunge (Impeachment).

Lakini CCM imejinyanyua juu na kujiweka kwenye kiti cha enzi
ambapo kitu kinachoitwa Katiba hakiangaliwi tena isipokuwa kadi na sheria zilizotungwa na Bunge lenyewe haziangaliwi tena bali taratibu za chama. Imefika mahali watu wanapewa uchaguzi wa "Chama" au "Taifa".

Mjadala wa viongozi hao wa CCM wakiongozwa na Mwenyekiti wao na "vigogo" wengine wa chama hao kuhusu mwenendo wa Bunge au maamuzi ya "Spika" ni mjadala potofu, usio na msingi na kwa hakika ni wa kiwoga!

Kama kuna kundi la wabunge wa CCM ambao wanaamini kuwa Spika hawatendei haki na wao ndio wako wengi Bungeni kwanini wasilete malalamishi yao ndani ya Bunge na badala yake kutumia mbinu za kiviziaji nje ya Bunge? Kama kuna watu ambao wanaona Spika anawapendelea watu wengine kwanini watu hao wasifuate taratibu za Bunge kutoa malalamiko yao?

Hawawezi. Hawawezi kwa sababu wanajua kabisa kuwa Bunge ni mhimili mwingine wa dola na Spika ni Mkuu wa Mhimili huo. Hawawezi kwa sababu wanajua kabisa hawaungwi mkono ndani ya Bunge; Hawawezi kwa sababu wanajua wakizungumza Bungeni Taifa zima litajua nani kazungumza nini na ana hoja gani! Wanaogopa; wanawaogopa Watanzania! Wanaogopa kujulikana!


Ni waoga.

Alichofanya Spika Sitta ni kile vitani kinaitwa "strategic retreat" yaani kurudi nyuma kimkakati ili kujipanga upya. Kama nilivyoandika wiki iliyopita hii ni vita na siyo mapambano. Unaweza ukapoteza pambano moja au mawili lakini mwisho wa siku utashinda vita.

Wao wametumia vikao vya chama, Sitta anawasubiri tena Bungeni. Bunge haliongozwi na Katiba ya CCM au maoni ya wana CCM peke yake. Hivyo, badala ya kuwapa njia rahisi ya kutokea (kumvua uanachama - kitu ambacho nina uhakika hawawezi pamoja na mikwara yao yote!) Sitta ameamua kuwapa ushindi wa pambano moja.

Ndugu zangu mafisadi wanaweza kushinda kwa sababu nyingi lakini kubwa ni kwa sababu Watanzania tumewaachia hivyo. Kuna watu ambao wanatumia hoja ya kuwa "Sitta naye si safi" hoja hii haina msingi! Uchafu wa mtu haumfanyi ashindwe kuona usafi au kuutetea usafi! Mtu mchafu ambaye hataki kusafishika au kufuata usafi wala kuupigia usafi debe ni mchafu per exellence!

Tanzania haiitaji watu wakamilifu (kwani hawapo duniani); Tanzania haiitaji watu watakatifu (wako mbinguni); Tanzania haiitaji watu wasiokosea (hawapatikani); Tanzania inahitaji watu ambao wanajua mapungufu yao, wamesahihisha makosa yao na wanakubali kusahihishwa. Watu ambao wanatukuza uadilifu na wanautafuta sana. Tanzania inahitaji viongozi ambao wanatambua wito wao kuwa ni mkubwa zaidi kuliko makosa au udhaifu wao, watu ambao wako tayari kusahihissha walikokaribu siyo wanaoendelea kunyosha vidole kuwa "fulani naye si safi"!

Ninaamini kwa moyo wangu wote, hakuna kiongozi wa Tanzania sasa hivi ambaye amesimamia wito huu wakuliinua taifa zaidi kama Spika Sitta. Leo hii anasimama kama ngao peke kati ya mafisadi kuliteka Bunge letu na wananchi kulimiliki. Spika Sitta aidha kwa makusudi au kwa bahati mbaya amelipa Bunge letu kile ambacho kwa miaka mingi tumekuwa tukikilalamikia; meno.

Kuna viongozi watatu wa dola yetu; Rais (Utendaji), Jaji Mkuu (mahakama) na Spika (Utungaji wa Sheria na Usimamizi wa serikali). Mhimili hii mitatu katika nchi ya demokrasia haiwezi kuwa pamoja wakati wote. Urais, Mahakama, na Bunge vikikubaliana kwa kila kitu na wakati wote basi tujue kuwa tunaishi kwenye nchi ya Udikteta! Havipaswi kukubaliana kila kitu na wakati wote; ni lazima vigongane.

Hivyo sasa tunashuhudia kugongana kati ya Urais na Bunge na huko tunakokwenda tutashuhudia kugongana kati ya Urais na Mahakama au Mahakama na Bunge. Hii ni sehemu ya demokrasia.

Ni kwa sababu hiyo tunapoona kikundi cha wahuni wachache (namaanisha neno "wahuni" katika kila maana yake mbaya) kujaribu kuliteka Bunge letu na kulijadili pembeni na kutaka lifanye mambo kwa manufaa ya kikundi cha watu hao wachache kwa jina la "chama" ni lazima tuwapinge.

Tunawapinga kwa sababu siyo kazi yao (ni wabunge Bungeni); tunawapinga kwa sababu Bunge si la kwao (ni Bunge la Watanzania); tunawapinga kwa sababu wamefanya kwa woga (wangetaka kuwa majasiri wangesimama Bungeni mbele ya huyo Spika).

Nawataadharisha CCM, makuwadi wa ufisadi na vikaragosi vyao; Msiliteke Bunge wala kusababisha Bunge lisimame peke yake au Spika afanye mambo yamewahi kutokea sehemu nyingine ambako kumekuwepo na mvutano kati ya Bunge na Urais. Ninawahakikishia kuwa mkiendelea kulishambulia Bunge letu namna hii (kama walivyofanya wengine mwaka jana) tutawapinga kwa nguvu zaidi kwani sasa hivi ni Bunge tu linasimama kati yetu na mafisadi waliiokubuhu wanaoshirikiana na mafisadi wa kizungu (wanaitwa wawekezaji) kutugeuza vijakazi wa milele.

Kama mnafikiri mambo hayaendi vizuri, na mnafikiri mna hoja, Bunge lina watu wenu wengi, na Rais anatoka chama chenu; vunjeni Bunge mrudi kwa wananchi sasa! Kama Bunge halichezi ngoma mnayoipiga au kuitikia mlio wa sauti zetu, rudini kwa wananchi mtafute madaraka upya.

CCM mmeruhusu utajiri wetu utweke nyara na mafisadi na sasa mnataka kuteka na Bunge letu? Nyinyi mmechagua CCM ishikeni na ikumbatieni; nyinyi mmechagua kadi za chama chenu zibebeni na mlale nazo; tuachieni Taifa letu; iacheni Katiba yetu!

Mshindwe!

niandikie: mwanakijiji@jamiiforums.com

Makala hii inaweza kutumika na gazeti lolote lile bila ya kubadilisha mtunzi.
 
Last edited:
M.M,

Heshima mbele, well said and said it all. Swali, je wanamasikio yanayosikia na kama yanasikia, je wana political will ya kuyafanyia kazi haya?
 
Kazi nzuri mwanakijiji,

Naomba kila mtu kwa nafasi yake apinge kitendo cha CCM kutaka kuliteka Bunge,

Shame on CCM
 
Kuna watu huwa mnamwaga sifa hapa kwamba Kikwete ni mwana mapinduzi ana heshimu na kusikiliza maoni ya watu na ndiyo maana uhuru wa watu kujieleza umejaa ? Mimi nasema uhuru huu umejaa kwa kuwa ni muda wake they can no longer silence the mass .Lakino JK si mkweli na hapendi kuambiwa ukweli na kwa JK CCM kwanza Tanzania na haki za Nchi baadaye .Majuzi ameshutumiwa kwa kutoa go ahead Mbunge ambaye ni Mganda kule Bigaramulo na yeye ana injinia muda Tume kutangaza CCM wameshinda ni Tarime pekee alishdwa mara zote pamoja na majeshi yake kutumika .
 
Kama vile ninavyokataa mafisadi kuiteka nchi yetu; ndivyo ninavyokataa CCM kuliteka Bunge na kuigeuza jumuiya yao!
 
UTANZANIA AU UZANZIBARI UNA THAMANI GANI IKIWA KUPEWA KITAMBULISHO CHA URAIA MPAKA UWE CCM AU UTOWE KITU KIDOGO NA HILO BUNGE LIMESEMA NINI JUU WATANZANIA HAWA KUNYIMWA URAIA WAO WA KUZALIWA AU KOSA LAO NI KUJIUNGA NA CHAMA CHA UPINZANI ?

".
*He went on saying that some Zanzibar people living in Tanga wanted to be
registered, which according to the RC, was not possible because they were
not living in Zanzibar.
"I have a brother living in the mainland, Mwenge and has a Zanzibar birth
certificate, but he cannot be registered for the national ID or to vote
because he does not fulfil the condition that requires him to have stayed in
Zanzibar for 3 years," Mr Juma said.
"
*Coments*
* *
*If what Regional Commissioner Kassim Juma says is true; i.e. that a
Zanzibari cannot be issued with an ID and/or allowed to register for the
purpose of voting because he/she is not living in Zanzibar, then there is no
doubt that Zanzibar has a bigger problem than that. In fact, it is
unconstitutional to deny a citizen of his/her inalienable right to vote
simply because he/she is living outside Zanzibar. *
**
*I need to remind RC Kassim, in case he has forgotten, that there are so
many countries today that have deliberately opted to make special
arrangements aimed at enabling their citizens to exercise their right to
vote while they are outside their countries of citizenship. *
**
*What is incomprehensible is the fact that in Zanzibar; and may be only in
Zanzibar, is where a citizen can travel all the way from his country or
place of residence to his/her country of birth and citizenship only to be
systematically denied his/her inalienable right to register for the purpose
of vote by the Authorities of his/her own country; not because he/she is not
a citizen, but only because he/she has been living outside Zanzibar for
three years consecutively...*
* *
*In other words: In Zanzibar, a citizen can neither be issued with a
national ID; nor can he/she be allowed to register to vote (even if he/she
has a valid birth certificate to prove his/her citizenship). What an
outright misrepresentation of justice.*
 
Yaani CCM haifai hata kidogo, na style walioanza nayo ya kuwanunua wapinzani, jamani tunakoelekea ni kubaya
 
I salute you mwanakijiji, kwa kweli tunashukuru sana kwa kujitoa muhanga kwa ajili ya hili taifa lkenye kila aina ya utajiri lakini wenzetu wachache wanalifaidi na sisi wengine tunabakia kubanana kwenye madala dala kuwahi mwajiri asitufukuze kazi.... Mafisadi tyuoneeni huruma jamani mlichochukua kinatosha sasa tuachieni angalau wajukuu zetu wafaidike na rasilimali za nchi yao jamana maana sisi mmeshatuumiza tayari.
Ah inaboa lakini ah sawa tu
 
Hivi hii kaulimbio bado ipo kwenye ccm au wameitenga? " Nitasema kweli daima Fitina kwangu mwiko" Hii ilikuwa miongoni mwa sentensi za kiapoa cha mwanachama wa CCM.
 
Leo ni siku ambayo nimeumia sana kichwa kuliko siku nyingine yeyote, kwa mambo mawili ambayo nimeyasoma kwa kina kwenye magazeti. la Zombe kuachiwa huru na mahakama, na hili la spika. La zombe linaweza kuendelea, kama Serikali ina nia ya dhati kuliendeleza, wanaweza kukata rufaa.

Hili la Spika ni kubwa mno, linauma kwa kuwa CCM inataka kuteka nguvu ya Umma. CCM imesahau kwamba, wabunge ni wawakilishi wa wananchi, na maamuzi yao ni maamuzi ya nchi. Spika, kama Spika alichofanya pale bungeni ni kutekeleza majukumu yake. Ni kama mwalimu anayefundusha somo la hisabati, kisha akatoa maswali, wanafunzi wamejibu na wamepata, atakachofanya ni kutoa tiki tu, hana visingizio pale, huwezi kumkosesha wanafunzi kama amepata swali na njia ni sahihi. Utampa tiki na vema utamwandikia. hana Kosa mwalimu, na hana kosa Spika. kazi yote ile imefanyika chini ya usimamizi wake na waliowajibika ni wabunge wote.

CCM wao wanaona bora nchi isambaratike kwa ufisadi kuliko chama chao. Huu ni ubinafsi, uzandiki na umangimeza uliokithiri ambao sisi watanzania hatuuhitaji. kaeni na CCM yenu, fanyeni mambo yenu, lakini pale kwenye Bunge linaloongozwa na katiba ya nchi, tuachieni.

Wabunge wa Tanzania msiogope, fanyeni kazi yenu kwani ninyi ni wawakilishi wa wananchi hata kama wengi wenu mmeupata uwakilishi huo kupitia CCM.

Ole wenu mafisadi, vita hii hamtashinda!!! kwakuwa mnapigana na kundi kubwa la wananchi.
 
Leo ni siku ambayo nimeumia sana kichwa kuliko siku nyingine yeyote, kwa mambo mawili ambayo nimeyasoma kwa kina kwenye magazeti. la Zombe kuachiwa huru na mahakama, na hili la spika. La zombe linaweza kuendelea, kama Serikali ina nia ya dhati kuliendeleza, wanaweza kukata rufaa.

Hili la Spika ni kubwa mno, linauma kwa kuwa CCM inataka kuteka nguvu ya Umma. CCM imesahau kwamba, wabunge ni wawakilishi wa wananchi, na maamuzi yao ni maamuzi ya nchi. Spika, kama Spika alichofanya pale bungeni ni kutekeleza majukumu yake. Ni kama mwalimu anayefundusha somo la hisabati, kisha akatoa maswali, wanafunzi wamejibu na wamepata, atakachofanya ni kutoa tiki tu, hana visingizio pale, huwezi kumkosesha wanafunzi kama amepata swali na njia ni sahihi. Utampa tiki na vema utamwandikia. hana Kosa mwalimu, na hana kosa Spika. kazi yote ile imefanyika chini ya usimamizi wake na waliowajibika ni wabunge wote.

CCM wao wanaona bora nchi isambaratike kwa ufisadi kuliko chama chao. Huu ni ubinafsi, uzandiki na umangimeza uliokithiri ambao sisi watanzania hatuuhitaji. kaeni na CCM yenu, fanyeni mambo yenu, lakini pale kwenye Bunge linaloongozwa na katiba ya nchi, tuachieni.

Wabunge wa Tanzania msiogope, fanyeni kazi yenu kwani ninyi ni wawakilishi wa wananchi hata kama wengi wenu mmeupata uwakilishi huo kupitia CCM.

Ole wenu mafisadi, vita hii hamtashinda!!! kwakuwa mnapigana na kundi kubwa la wananchi.


JK na wenzake watakuwa na mambo ya kujibu siku za usoni .
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Ndugu zangu mafisadi wanaweza kushinda kwa sababu nyingi lakini kubwa ni kwa sababu Watanzania tumewaachia hivyo. Kuna watu ambao wanatumia hoja ya kuwa "Sitta naye si safi" hoja hii haina msingi! Uchafu wa mtu haumfanyi ashindwe kuona usafi au kuutetea usafi! Mtu mchafu ambaye hataki kusafishika au kufuata usafi wala kuupigia usafi debe ni mchafu per exellence!

Tanzania haiitaji watu wakamilifu (kwani hawapo duniani); Tanzania haiitaji watu watakatifu (wako mbinguni); Tanzania haiitaji watu wasiokosea (hawapatikani); Tanzania inahitaji watu ambao wanajua mapungufu yao, wamesahihisha makosa yao na wanakubali kusahihishwa. Watu ambao wanatukuza uadilifu na wanautafuta sana. Tanzania inahitaji viongozi ambao wanatambua wito wao kuwa ni mkubwa zaidi kuliko makosa au udhaifu wao, watu ambao wako tayari kusahihissha walikokaribu siyo wanaoendelea kunyosha vidole kuwa "fulani naye si safi"!
.

Mwanakijiji tunashukuru kwa uchambuzi mzuri

hii paragraph nyekundu ingeongezewa kule kwenye waraka wa Wakatoliki au wengine wanaofikiria kuandaa nyaraka. nimeipenda

Tuendelee kumpa moyo Spika Sitta aendelee kulipigania taifa hili. Mungu ambariki sana, na atamlipa.
 
Na. M. M. Mwanakijiji

Habari ambazo zimekuwa zikitiririka kwa muda wa masaa kadhaa yaliyopita zinatuthibitishia kuwa waoga wanaongoza CCM sasa hivi. Habari za kuwa Spika wa Bunge la Muungano alipewa kibano katika mojawapo ya vikao vya juu vya CCM ni habari za kuudhi, kukera, na kuchekesha; yote kwa kwa wakati mmoja. Vile vile tukio la kujadili mambo ya Bungeni na taratibu za Bungeni kuonesha kutoridhishwa kwa mwenendo wa Bunge kwenye vikao vya chama ni tukio la kulaaniwa na kukataliwa na kila mpenda demokrasia.

Kwa vile CCM wamelewa ugimbi wa madaraka inaonekana hawajui kuwa Bunge siyo tawi la CCM wala Jumuiya ya chama. Spika wa Jamhuri ya Muungano siyo Spika wa Bunge la CCM. Bunge la namna hiyo halipo.

Bunge linaendeshwa kwa taratibu zake na wakati wowote mbunge yoyote hafurahishwi au kuridhishwa na mwenendo wa Bunge taratibu zipo za kutoa malalamiko yake na kama ni kundi kubwa la wabunge basi wana nafasi ya kujadili na hata kumuondoa Spika kwa taratibu za Kibunge (Impeachment).

Lakini CCM imejinyanyua juu na kujiweka kwenye kiti cha enzi ambapo kitu kinachoitwa Katiba hakiangaliwi tena isipokuwa kadi na sheria zilizotungwa na Bunge lenyewe haziangaliwi tena bali taratibu za chama. Imefika mahali watu wanapewa uchaguzi wa "Chama" au "Taifa".

Mjadala wa viongozi hao wa CCM wakiongozwa na Mwenyekiti wao na "vigogo" wengine wa chama hao kuhusu mwenendo wa Bunge au maamuzi ya "Spika" ni mjadala potofu, usio na msingi na kwa hakika ni wa kiwoga!

Kama kuna kundi la wabunge wa CCM ambao wanaamini kuwa Spika hawatendei haki na wao ndio wako wengi Bungeni kwanini wasilete malalamishi yao ndani ya Bunge na badala yake kutumia mbinu za kiviziaji nje ya Bunge? Kama kuna watu ambao wanaona Spika anawapendelea watu wengine kwanini watu hao wasifuate taratibu za Bunge kutoa malalamiko yao?

Hawawezi. Hawawezi kwa sababu wanajua kabisa kuwa Bunge ni mhimili mwingine wa dola na Spika ni Mkuu wa Mhimili huo. Hawawezi kwa sababu wanajua kabisa hawaungwi mkono ndani ya Bunge; Hawawezi kwa sababu wanajua wakizungumza Bungeni Taifa zima litajua nani kazungumza nini na ana hoja gani! Wanaogopa; wanawaogopa Watanzania! Wanaogopa kujulikana!

Ni waoga.

Alichofanya Spika Sitta ni kile vitani kinaitwa "strategic retreat" yaani kurudi nyuma kimkakati ili kujipanga upya. Kama nilivyoandika wiki iliyopita hii ni vita na siyo mapambano. Unaweza ukapoteza pambano moja au mawili lakini mwisho wa siku utashinda vita.

Wao wametumia vikao vya chama, Sitta anawasubiri tena Bungeni. Bunge haliongozwi na Katiba ya CCM au maoni ya wana CCM peke yake. Hivyo, badala ya kuwapa njia rahisi ya kutokea (kumvua uanachama - kitu ambacho nina uhakika hawawezi pamoja na mikwara yao yote!) Sitta ameamua kuwapa ushindi wa pambano moja.

Ndugu zangu mafisadi wanaweza kushinda kwa sababu nyingi lakini kubwa ni kwa sababu Watanzania tumewaachia hivyo. Kuna watu ambao wanatumia hoja ya kuwa "Sitta naye si safi" hoja hii haina msingi! Uchafu wa mtu haumfanyi ashindwe kuona usafi au kuutetea usafi! Mtu mchafu ambaye hataki kusafishika au kufuata usafi wala kuupigia usafi debe ni mchafu per exellence!

Tanzania haiitaji watu wakamilifu (kwani hawapo duniani); Tanzania haiitaji watu watakatifu (wako mbinguni); Tanzania haiitaji watu wasiokosea (hawapatikani); Tanzania inahitaji watu ambao wanajua mapungufu yao, wamesahihisha makosa yao na wanakubali kusahihishwa. Watu ambao wanatukuza uadilifu na wanautafuta sana. Tanzania inahitaji viongozi ambao wanatambua wito wao kuwa ni mkubwa zaidi kuliko makosa au udhaifu wao, watu ambao wako tayari kusahihissha walikokaribu siyo wanaoendelea kunyosha vidole kuwa "fulani naye si safi"!

Ninaamini kwa moyo wangu wote, hakuna kiongozi wa Tanzania sasa hivi ambaye amesimamia wito huu wakuliinua taifa zaidi kama Spika Sitta. Leo hii anasimama kama ngao peke kati ya mafisadi kuliteka Bunge letu na wananchi kulimiliki. Spika Sitta aidha kwa makusudi au kwa bahati mbaya amelipa Bunge letu kile ambacho kwa miaka mingi tumekuwa tukikilalamikia; meno.

Kuna viongozi watatu wa dola yetu; Rais (Utendaji), Jaji Mkuu (mahakama) na Spika (Utungaji wa Sheria na Usimamizi wa serikali). Mhimili hii mitatu katika nchi ya demokrasia haiwezi kuwa pamoja wakati wote. Urais, Mahakama, na Bunge vikikubaliana kwa kila kitu na wakati wote basi tujue kuwa tunaishi kwenye nchi ya Udikteta! Havipaswi kukubaliana kila kitu na wakati wote; ni lazima vigongane.

Hivyo sasa tunashuhudia kugongana kati ya Urais na Bunge na huko tunakokwenda tutashuhudia kugongana kati ya Urais na Mahakama au Mahakama na Bunge. Hii ni sehemu ya demokrasia.

Ni kwa sababu hiyo tunapoona kikundi cha wahuni wachache (namaanisha neno "wahuni" katika kila maana yake mbaya) kujaribu kuliteka Bunge letu na kulijadili pembeni na kutaka lifanye mambo kwa manufaa ya kikundi cha watu hao wachache kwa jina la "chama" ni lazima tuwapinge.

Tunawapinga kwa sababu siyo kazi yao (ni wabunge Bungeni); tunawapinga kwa sababu Bunge si la kwao (ni Bunge la Watanzania); tunawapinga kwa sababu wamefanya kwa woga (wangetaka kuwa majasiri wangesimama Bungeni mbele ya huyo Spika).

Nawataadharisha CCM, makuwadi wa ufisadi na vikaragosi vyao; Msiliteke Bunge wala kusababisha Bunge lisimame peke yake au Spika afanye mambo yamewahi kutokea sehemu nyingine ambako kumekuwepo na mvutano kati ya Bunge na Urais. Ninawahakikishia kuwa mkiendelea kulishambulia Bunge letu namna hii (kama walivyofanya wengine mwaka jana) tutawapinga kwa nguvu zaidi kwani sasa hivi ni Bunge tu linasimama kati yetu na mafisadi waliiokubuhu wanaoshirikiana na mafisadi wa kizungu (wanaitwa wawekezaji) kutugeuza vijakazi wa milele.

Kama mnafikiri mambo hayaendi vizuri, na mnafikiri mna hoja, Bunge lina watu wenu wengi, na Rais anatoka chama chenu; vunjeni Bunge mrudi kwa wananchi sasa! Kama Bunge halichezi ngoma mnayoipiga au kuitikia mlio wa sauti zetu, rudini kwa wananchi mtafute madaraka upya.

CCM mmeruhusu utajiri wetu utweke nyara na mafisadi na sasa mnataka kuteka na Bunge letu? Nyinyi mmechagua CCM ishikeni na ikumbatieni; nyinyi mmechagua kadi za chama chenu zibebeni na mlale nazo; tuachieni Taifa letu; iacheni Katiba yetu!

Mshindwe!

niandikie: mwanakijiji@jamiiforums.com

Makala hii inaweza kutumika na gazeti lolote lile bila ya kubadilisha mtunzi.
CCM wameharibu nchi kabisa sasa kuna mambo mawili ya hatari nanayoyaaona mbele yetu ama wananchi wataamua kudharau CCM na wakiidharau watakata tamaa,wakikata tamaa watauamua cha kufanya ikiwamo pamoja na kukamata mwenyekiti wa CCM,Katibu Mkuu makamu mwenyekiti wakawabonda mawe mpaka wakatoweka ili kurejesha utawala wa kuheshimu katiba na mihimiri ya dola
La pili kama njia halali za uwakilishi ikiwemo bunge kupitia kwa wabunge wao hazitaheshimika japo wabunge wengi wa CCM wanapatikana kwa mizengwe wao wataamua kuunda Bunge lao kwa mfumo wowote.
Nadhani Mwenyekiti aache majungu na asimame imara kuhakikisha nchi hii anaicha kwa amani kama alivyoipokea,hivi huyu Jakaya anaelewa lakini anaoongeza vidonda kwenye mifumo inayostahili kulinda mfumo wa utendaji na uteteaji wa haki za watanzania,asipooangalia atakuja kuondoka madarakani akiwa ni Raisi aliyechukiwa mno kuliko yeyote tangia tupate uhuru
Nasema hivyo kwa sababu hasikii wala haambili alipopokea uenyekiti wa CCM watu walimuonya sana asimpe Makamba ukatibu mkuu kwa sababu atagawa wanachama,kwa sababu makamba maisha yake yote hakuwa mwanasiasa wa moja kwa moja alikuwa upande wa serikali kwa maana ya uanajeshi,ukuu wa wilaya na ukuu wa mkoa,ubishi wake anauona sasa,ana bip mambo ya kisiasa kwa mara ya kwanza aliweka safu mpya kabisa katika uongozi wa juu wa ccm kama vile mweka hazina makamu mwenyekiti katibu mwenezi mambo yamefikia mahala ameyakoroga chama chake kanamomonyoka kila siku,hakuna maelewano kati yake ni mihimiri mikuu ya dola kwa maana ya mahakama na bunge huyu jakaya ni raisi hatari sana watanzania tusipooangalia atatupeleka pabaya hatutakuja tujua tufanye nini
 
Kama kuna kundi la wabunge wa CCM ambao wanaamini kuwa Spika hawatendei haki na wao ndio wako wengi Bungeni kwanini wasilete malalamishi yao ndani ya Bunge na badala yake kutumia mbinu za kiviziaji nje ya Bunge?
Hawawezi kwa sababu wanajua wakizungumza Bungeni Taifa zima litajua nani kazungumza nini na ana hoja gani! Wanaogopa; wanawaogopa Watanzania!
Hahaa! Mwizi havunji nyumba kweupe, wala mbakaji habaki kweupe barabarani kwani watu wema watapita na kushuhudia na kisha kumshughulikia. Matendo ya kishetani hufanyika mafichoni au mahali watu wema wasipoweza kuyaona. Naogopa kuwaita mashetani, lakini wana kila sifa za shetani !!
 
Mkwere alikuja kwa umaarufu wa sura, sasa umeyeyuka kama barafu iliyoanikwa juani mchana wa saa sita. Anafanya jitihada za kujishikiza kwa kutumia kamba za migomba baada ya kuona ngoma imemshinda. Walizoea kuwatumia waliohemea njaa zao kama Msekwa, sasa wenye kuipenda nchi yao wanapowaambia ukweli hawautaki.

Hizi ni harakati, na kama ulivyo upepo wa kisulisuli hauzuiliwi kwa ungo. Laiti wangejua kuwa kukataa tamaa ni kubaya sana: matokeo yake ni kurushiwa mawe msafara wa rais na wananchi wasiojua kesho watakula nini, kuchoma vituo na kuwapiga polisi wanaojidai wanawalinda raia, kuwazomea mawaziri na huenda tuendako itakuwa kuwamwagia maji ya moto, pamoja na mengi yanayofanana na haya. Sisemi wala sipendi haya yafanyike, ila hii ni vita ya waliokata tamaa na wanaoamini kuwa hata wakiishi leo bado kesho hawatakuwa na faida.

Tukemee kwa nguvu zetu zote ikiwa ni pamoja na kuandamana kupinga umangimeza huu ambao ccm inataka kutudisha ndani ya chupa. Wamefanya juhudi siku zote kuiba kura, kufunga mfumo wa utawala usiwe wa kidemokrasia ili wao kwa wao waendeleze mirija yao. Hawana budi kufahamu kuwa sasa watanzania wamechoka, hatuwezi kuendelea kuvaa viroba na kushindia uji wa mtama, ilihali wao kwa wao wanavaa suti na kula kuku kwa mirija kwa jasho letu na utajiri tuliopewa na Muumba!
 
Hivi hii kaulimbio bado ipo kwenye ccm au wameitenga? " Nitasema kweli daima Fitina kwangu mwiko" Hii ilikuwa miongoni mwa sentensi za kiapoa cha mwanachama wa CCM.

Imekuwa hivi:

Nitasema Uongo Daima, Ukweli Kwangu Mwisho!
 
Back
Top Bottom