BAK
JF-Expert Member
- Feb 11, 2007
- 124,790
- 288,007
Wabunge msikubali hoja nzito kuzimwa bungeni
SPIKA wa Bunge, Samuel Sitta, juzi baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali na majibu, alitangaza uamuzi wa kuzuia kuwasilishwa bungeni hoja binafsi tatu zilizokuwa zimewasilishwa kwake na wabunge.
Hoja zilizozuiliwa ni pamoja na ya Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbrod Slaa (CHADEMA), iliyotaka maelezo ya serikali kuhusu madai ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha, kuingilia mchakato wa utengenezaji wa vitambulisho vya taifa.
Sitta alisema baada ya kuipeleka hoja hiyo katika Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, ambako ilijadiliwa na yeye kupewa ushauri, amekubaliana na ushauri wa kamati hiyo kuwa mchakato wa zabuni hiyo uendelee kwani umeshachelewa.
Kwamba, baada ya mchakato huo kukamilika na kama kutakuwa na malalamiko kuhusu zabuni hiyo ilivyoendeshwa, jambo hilo linaweza kurejeshwa bungeni na kujadiliwa ili kuona ni nani alikosea.
Hoja nyingine iliyozuiliwa ni ya Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed (CUF), iliyotaka kuwepo kwa mabadiliko ya vifungu katika Katiba vitakavyoweka ukomo wa ukubwa wa serikali.
Alisema hoja hiyo haiwezi kujadiliwa kwa vile inaingiliana na marekebisho ya Katiba, kwamba Ibara ya 98 ya Katiba inaeleza kuwa jambo kama hilo linahitaji kushughulikiwa kwa kuwasilisha muswada bungeni na si kuwasilishwa na mbunge mmoja kama hoja binafsi.
Aidha, alizuia kuwasilishwa kwa hoja binafsi ya Mbunge wa Viti Maalumu, Halima Mdee (CHADEMA), iliyohusu mgogoro katika eneo la Chasimba, mkoani Dar es Salaam, na kwa madai kuwa ameridhika kuwa shauri hilo liko mahakamani, hivyo haliwezi kujadiliwa bungeni.
Wakati huo huo, Spika Sitta alieleza kuwa kutojadiliwa kwa taarifa ya serikali kuhusu suala la Kampuni ya Richmond, uendeshaji usioridhisha wa Shirika la Reli Tanzania (TRL), na utendaji wa kazi usioridhisha wa Kampuni ya Tanzania International Container Terminal Services (TICTS) na taarifa kuhusu uendeshaji wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), kumetokana na taarifa hizo kuendelea kufanyiwa kazi.
Tunakukubaliana na maelezo ya Sitta kuhusu kuzuiliwa kwa baadhi ya hoja binafsi, lakini hatuungi mkono sababu alizotoa kuzima hoja binafsi ya Dk. Slaa, na kuzuia kutosomwa kwa taarifa za serikali kuhusu utekelezaji wa maazimio mbalimbali ya Bunge, hususan kuhusu Richmond, TRL, TICTS na ATCL.
Uamuzi wa Sitta kuruhusu kuendelea kwa mchakato wa vitambulisho vya taifa, wakati hoja ya Dk. Slaa ikiwa bado haijawasilishwa bungeni na kudai kukiwa na haja itarejeshwa bungeni, tunaamini kinalenga kuzima uzito na pengine kudhoofisha ushahidi wa hoja hiyo kama si kutoipa nafasi kabisa ya kuwasilishwa bungeni.
Haituingii akilini, hoja ihusuyo kuingiliwa kwa mchakato wa zabuni ya vitambulisho vya taifa, halafu mchakato huo uruhusiwe kuendelea kabla ya hoja hiyo kujadiliwa, hivi kutakuwa na ushahidi gani mzito wa kuthibitisha kuingiliwa kwa mchakato huo wakati tayari Spika amekwisha kutoa mwanya kwa waliofanya makosa kurekebisha kasoro zao na kufuata taratibu?
Kwetu sisi, kutojadiliwa kwa hoja hiyo, kutosomwa kwa taarifa za serikali na wabunge kutopewa fursa ya kujadili taarifa za Richmond, uendeshaji mbovu wa TRL, TICTS na ATCL, kunazidi kuahirisha utatuzi wake, ambapo wabunge kama wawakilishi wa wananchi walipaswa kuiona taarifa hiyo, kuijadili na kutoa ufumbuzi badala ya Spika kujiridhisha peke yake.
Tunawataka wabunge warejee jinsi mjadala wa hotuba ya Rais Jakaya Kikwete ulivyozimwa kwa sababu zisizo na mashiko, hivyo tunawataka bila kujali itikadi zao, kutumia mwanya mwingine wa kanuni za Bunge kumbana Spika, pale anapochukua maamuzi yasiyofaa.
- Msikubali uhuru wenu wa kikatiba kutekwa nyara na Sitta na Pinda
SPIKA wa Bunge, Samuel Sitta, juzi baada ya kumalizika kwa kipindi cha maswali na majibu, alitangaza uamuzi wa kuzuia kuwasilishwa bungeni hoja binafsi tatu zilizokuwa zimewasilishwa kwake na wabunge.
Hoja zilizozuiliwa ni pamoja na ya Mbunge wa Karatu, Dk. Wilbrod Slaa (CHADEMA), iliyotaka maelezo ya serikali kuhusu madai ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Lawrence Masha, kuingilia mchakato wa utengenezaji wa vitambulisho vya taifa.
Sitta alisema baada ya kuipeleka hoja hiyo katika Kamati ya Bunge ya Mambo ya Nje, Ulinzi na Usalama, ambako ilijadiliwa na yeye kupewa ushauri, amekubaliana na ushauri wa kamati hiyo kuwa mchakato wa zabuni hiyo uendelee kwani umeshachelewa.
Kwamba, baada ya mchakato huo kukamilika na kama kutakuwa na malalamiko kuhusu zabuni hiyo ilivyoendeshwa, jambo hilo linaweza kurejeshwa bungeni na kujadiliwa ili kuona ni nani alikosea.
Hoja nyingine iliyozuiliwa ni ya Mbunge wa Wawi, Hamad Rashid Mohamed (CUF), iliyotaka kuwepo kwa mabadiliko ya vifungu katika Katiba vitakavyoweka ukomo wa ukubwa wa serikali.
Alisema hoja hiyo haiwezi kujadiliwa kwa vile inaingiliana na marekebisho ya Katiba, kwamba Ibara ya 98 ya Katiba inaeleza kuwa jambo kama hilo linahitaji kushughulikiwa kwa kuwasilisha muswada bungeni na si kuwasilishwa na mbunge mmoja kama hoja binafsi.
Aidha, alizuia kuwasilishwa kwa hoja binafsi ya Mbunge wa Viti Maalumu, Halima Mdee (CHADEMA), iliyohusu mgogoro katika eneo la Chasimba, mkoani Dar es Salaam, na kwa madai kuwa ameridhika kuwa shauri hilo liko mahakamani, hivyo haliwezi kujadiliwa bungeni.
Wakati huo huo, Spika Sitta alieleza kuwa kutojadiliwa kwa taarifa ya serikali kuhusu suala la Kampuni ya Richmond, uendeshaji usioridhisha wa Shirika la Reli Tanzania (TRL), na utendaji wa kazi usioridhisha wa Kampuni ya Tanzania International Container Terminal Services (TICTS) na taarifa kuhusu uendeshaji wa Shirika la Ndege Tanzania (ATCL), kumetokana na taarifa hizo kuendelea kufanyiwa kazi.
Tunakukubaliana na maelezo ya Sitta kuhusu kuzuiliwa kwa baadhi ya hoja binafsi, lakini hatuungi mkono sababu alizotoa kuzima hoja binafsi ya Dk. Slaa, na kuzuia kutosomwa kwa taarifa za serikali kuhusu utekelezaji wa maazimio mbalimbali ya Bunge, hususan kuhusu Richmond, TRL, TICTS na ATCL.
Uamuzi wa Sitta kuruhusu kuendelea kwa mchakato wa vitambulisho vya taifa, wakati hoja ya Dk. Slaa ikiwa bado haijawasilishwa bungeni na kudai kukiwa na haja itarejeshwa bungeni, tunaamini kinalenga kuzima uzito na pengine kudhoofisha ushahidi wa hoja hiyo kama si kutoipa nafasi kabisa ya kuwasilishwa bungeni.
Haituingii akilini, hoja ihusuyo kuingiliwa kwa mchakato wa zabuni ya vitambulisho vya taifa, halafu mchakato huo uruhusiwe kuendelea kabla ya hoja hiyo kujadiliwa, hivi kutakuwa na ushahidi gani mzito wa kuthibitisha kuingiliwa kwa mchakato huo wakati tayari Spika amekwisha kutoa mwanya kwa waliofanya makosa kurekebisha kasoro zao na kufuata taratibu?
Kwetu sisi, kutojadiliwa kwa hoja hiyo, kutosomwa kwa taarifa za serikali na wabunge kutopewa fursa ya kujadili taarifa za Richmond, uendeshaji mbovu wa TRL, TICTS na ATCL, kunazidi kuahirisha utatuzi wake, ambapo wabunge kama wawakilishi wa wananchi walipaswa kuiona taarifa hiyo, kuijadili na kutoa ufumbuzi badala ya Spika kujiridhisha peke yake.
Tunawataka wabunge warejee jinsi mjadala wa hotuba ya Rais Jakaya Kikwete ulivyozimwa kwa sababu zisizo na mashiko, hivyo tunawataka bila kujali itikadi zao, kutumia mwanya mwingine wa kanuni za Bunge kumbana Spika, pale anapochukua maamuzi yasiyofaa.