TAHAJUDI (Meditation): Mbinu, faida, aina na mambo ya kuzingatia

" Mungu akasema, na tumfanye mtu kwa mfano wetu , kwa sura yetu, akatawale samaki wa baharini na vyote vitambaavyo ardhini " MWANZO 1:26

Tuna nguvu za kiungu ndani yetu, kwa kuwa tumeumbwa kwa mfano wake




Sent from my iPhone using JamiiForums

Una nguvu ipi ya Kiungu wewe ?
Usikimbie Swali na kujifanya hujaelewa.

Suala la Mungu kuumba binaadamu kwa mfano wake linahusika vipi na Nguvu za Mungu?

Mungu anaadhibu kwa Moto wa jahannamu Waovu na kuwalipa watu wema pepo.
Mungu anaumba Na Kutoa roho.
Nakuuliza Yesu km ana uwezo wa kuyafanya hayo?
Na km Jibu ni Ndio Nipe Andiko kuwa Yesu aliwahi kutamka kuwa yeye ni MUNGU.
Au wapi Yesu alisema ataadhibu waovu na kuwalipa Wema!
Acheni kumsingizi Yesu mambo ambayo yeye mwenyewe hakutamka
Mtapigwa laana ya milele.
 
Chimbuko/historia ya tahajudi:

Neno tahajudi limetokana na neno la kiingereza linaloitwa 'meditation' likiwa na maana ya kufikiri kwa uzingativu au kwa kujali. Neno meditation, nalo limetokana na neno la kilatini linaloitwa 'meditatio' likiwa na maana ya mazoezi ya mwili na akili.

Asili ya tahajudi ni dini za mashariki. Ilianzia huko Asia zaidi ya miaka 5,000 iliyopita. Kwa sasa tahajudi hufanywa zaidi huko magharibi (Ulaya na Marekani).

Tahajudi ya miaka hii (ya wakati huu), inazungumzia zaidi tahajudi ya kiyoga ambayo asili yake ni huko India.

Kwa ujumla, tahajudi inaelezwa kama njia za uzingativu katika jambo ambalo mawazo yamelinuia. Lakini pia inaweza kuelezwa kama ifuatavyo:

=> Ni hali ya uzingativu na utulivu katika hali halisi ya wakati wa sasa hivi.

=> Ni ile hali wakati mawazo yanapokuwa yameyeyushwa na kufikia mahali ambapo hakuna fikra yenye kuingia tena.

=> Ni ile hali ambayo, uzingativu, kwa makusudi kabisa umeachwa kuelekea kwenye nguvu kubwa zaidi ( Mungu? Nguvu kuu? ).

=> Ni ile hali ya kuweka mawazo na uzingativu katika kitu kimoja, mfano- sanamu ya kidini, pumzi au neno fulani unalotamka (mantra).

=> Wengine wanaielezea tahajudi kwamba, ni sala za usiku wa manane.

CouplePraying.jpg


Tahajudi na dini:

Kila dini ina aina yake ya uzingativu, ingawa ukiutazama kwa undani utagundua kwamba ni tahajudi halisi.

Dini ya kikristo wanatumia rozari, hii huwasaidia kujenga uzingativu. Waislamu wanatumia tasbihi ambayo huwasaidia kujenga uzingativu, lakini pia huwa wanakuwa na sala za usiku wa manane (tahajudi). Wabudha huwa wanafanya tahajudi kila siku kwani ndiyo nguzo yao kuu. Wabahai, hufanya tahajudi kila baada ya sala.

Faida za tahajudi:

Ili uweze kutambua faida za tahajudi, ni muhimu kuifanya kila siku, ikiwezekana asubuhi na jioni. Tahajudi ina faida nyingi sana, faida hizi utaziona tu kama utafanya tahajudi kila siku. Hivyo, tahajudi inahitaji nguvu kubwa sana ya kujituma (wheel power). Ina faida kubwa sana, hivyo ni vizuri ukajenga mazoea ya kuifanya kila siku. Nakushauri, kama huwezi kufanya tahajudi, basi ni afadhali ujifunze upendo ingawa, ni rahisi mara kumi kufanya tahajudi kuliko kuwa na upendo. baadhi ya faida hizo ni kama ifuatavyo:

1. Husaidia kuongeza ubora wetu kiakili, kimwili pamoja na uwezo wetu kwa ujumla. Husaidia kuuburudisha mwili, pia husaidia kupumzisha akili na mwili.

2. Husaidia kujenga uzingativu na kukuwezesha kumudu kupata suluhu ya matatizo kirahisi.

3. Husaidia kuratibu msukumo wa damu pamoja na usafirishwaji wa damu mwilini.

4. Husaidia pumzi pamoja na kurahisisha usagwaji wa chakula mwilini.

5. Husaidia kuimarisha mfumo wa kinga mwilini.

6. Husaidia kuleta furaha ya nafsi.

7. Husaidia kuimarisha nguvu yako ya machale pamoja na nguvu zako za ziada.

8. Husaidia kutibu matatizo mengi ya kisaikolojia kwani hubadili hali ya mfumo wa fahamu na mawazo (endapo itafanywa kila siku).

9. tahajudi pia inaweza kutumika kuomba kitu unachohitaji, kama vile kazi au mahitaji mbalimbali, ingawa inashauriwa uwe mwangalifu badala ya kufanya kazi unaweza ukawa mtegemezi wa tahajudi. Mfano, unaweza ukatumia tahajudi kuomba shilingi laki moja na ukapata bila kufanya kazi yoyote au kwa kufanya kazi kidogo sana ambayo hailingani na malipo ya laki moja.

Je, tahajudi huleta utajiri?

Ni swali gumu kwa sababu, utajiri ni dhana pana sana, inategemea tu unazungumzia utajiri upi, wa kitu gani na wapi. Hata ule utajiri wa kimazoea, nao bado ni mgumu kuuelezea. Mfano, tajiri wa kijijini, akihamia mjini anaonekana ni mtu wa kawaida kabisa kwani kuna matajiri wengi sana wanaomzidi.

Lakini, swali la kujiuliza ni hili, unataka utajiri ili iweje au upate nini? Kama unataka utajiri ili uwe maarufu kwa kuandikwa na magazeti, ukweli ni kwamba, kuna uwezekano mkubwa wa wewe kuandikwa na magazeti ingawa siyo kwa utajiri ila kwa kubaka mtoto. Lakini pia kama unataka utajiri ili ukupe furaha na amani, ukweli utabaki palepale kwamba, hata kama utaupata huo utajiri, furaha au amani haitapatikana kwani utakuwa umevunja kanuni ya maisha kwani hukuja duniani kutafuta utajiri, bali kuishi kwa kufanya kazi unayoipenda sana, inayokupa furaha na amani bila kujali maslahi, heshima au umaarufu kutoka kwenye kazi hiyo.

Kwakuwa kazi hii unaipenda, utaifanya kwa ufanisi mkubwa sana, na ndipo utajiri utakapokuja. Kanuni ya maisha kuhusu utajiri inaanza na kufanya kazi inayokupa furaha na amani na ndipo utajiri unafuata, haianzi na utajiri na ndipo furaha na amani vipatikane. Kama huamini, wachunguze matajiri unaowafahamu, ambao walipata utajiri ili uwape furaha na amani, utagundua kwamba, hawana furaha wala amani. Kwa upande wa pili wa shilingi, wale matajiri ambao, utajiri wao ulikuja kupitia kwa kufanya kazi inayowapa furaha na amani, utagundua kwamba wana furaha na amani kubwa sana.

Swali lililoulizwa hapo juu linasema, je, tahajudi huleta utajiri? Kama utajiri ni kupata furaha na amani ya nafsi, jibu ni ndiyo. Hii ni kwa sababu, tahajudi hukusaidia au kukufundisha namna bora kabisa ya kupumzisha akili na mwili na hivyo kuwa mtu mwenye furaha na amani. Kumbuka, ukishakuwa mwenye furaha na amani, wewe tayari ni tajiri wa mali pia.


Tahajudi ina madhara yoyote?

Kwa watu wenye matatizo ya kifafa, matatizo makubwa ya moyo au wenye matatizo ya akili, tahajudi inaweza kuwaumiza wasipokuwa waangalifu, ingawa kwa upande mwingine, tahajudi ni tiba/dawa kwao. Hivyo, wanashauriwa wachague tahajudi ambayo haitawaletea matatizo.

Ni vizuri wakajaribu aina tofauti tofauti ya tahajudi, halafu wakaangalia ni ipi inawasumbua na ni ipi inawapa nafuu. Wakishapata inayowapa nafuu, ni vizuri wakaendelea kuifanya mara kwa mara. Baada ya muda, watagundua kwamba, matatizo yao ya akili, moyo au kifafa yamepungua kwa kiwango kikubwa sana au yameisha kabisa.

meditation-techniques.jpg


Jinsi ya kufanya tahajudi:

Mbinu za kufanya tahajudi hutofautiana kutokana na kiwango cha uzingativu, uwezo wa kujenga taswira na namna mtu anavyoweza kukabili mawazo yanayomwingilia wakati anafanya tahajudi yake.

Baadhi ya mbinu hizi, humfanya mtu apotelee kwenye kile anachozingatia na kutoingiliwa kabisa na wazo lolote. Mbinu hizi ni rahisi mtu kujifunza mwenyewe, ingawa kuna baadhi zinahitaji awepo mwongozaji.


Hatua zinazotakiwa wakati unajiandaa kufanya tahajudi ni kama ifuatavyo:

1. Tafuta sehemu iliyotulia, isiyo na makelele. Kaa kwenye kiti au chini, au lala kitandani. Hakikisha huumii mahali popote. Legeza mwili wako pamoja na misuli yote ya mwili wako kwa kadri utakavyoweza.

2. Sahau matatizo yako yaliyopita, yaliyopo na yajayo. Sahau matatizo yako ya kazini au nyumbani. Jitahidi usifikirie chochote. kama kuna mawazo yataingia, usigombane nayo, usiyape muda na nafasi, wewe endelea na kile ulichoamua kukizingatia. Hakikisha uzingativu wako ni mkubwa. Pia kione hicho unachokizingatia kwa jicho lako la ndani, kijengee taswira kana kwamba unacho tayari au kana kwamba unakiona (unacho).

3. Ni muhimu sana kujali hisia zako wakati unafanya tahajudi. Kwa mfano, kama unafanya tahajudi ya kujenga nyumba. Hakikisha hiyo nyumba unaiona ilivyo, ingia ndani ya hiyo nyumba, sebuleni, chumbani, chooni, stoo, jikoni na sehemu ya kulia chakula (dining). Kila unapoingia, onyesha hisia zako, jione una furaha ndani mwako na ikiwezekana tabasamu, pia jione una amani ndani mwako. Ukweli ni kwamba, utakapokuja kujenga hiyo nyumba, zile hisia ulizokuwa unazionyesha wakati unafanya tahajudi, zitajitokeza au utaziona. Kama tahajudi yako ulikuwa unaifanya ukiwa na huzuni, hali hiyo itajitokeza baada ya kumaliza kujenga nyumba yako. Inaweza ikatokea baada tu ya kujenga nyumba yako, ndugu zako au wa mkeo wakajaa pale nyumbani, wakawa wanafanya vurugu ambazo zitakuletea huzuni na hivyo kuanza kujuta ni kwa nini umejenga hiyo nyumba.

Ukweli ni kwamba, tatizo siyo ndugu, tatizo ni wewe mwenyewe, ni hisia zako ulizokuwa unazionyesha wakati unafanya tahajudi yako ya kujenga nyumba. Na kama wakati unafanya tahajudi yako ulikuwa na hisia za furaha, hali hiyo pia itajitokeza baada ya kumaliza nyumba yako. Hata kama ndugu wa mkeo au mumeo watajaa pale nyumbani, vicheko, tabasamu na mambo mengine ambayo yatakupa furaha yatatamalaki pale nyumbani. Kwa hiyo, hisia ni muhimu sana wakati unafanya tahajudi.

4. Pumua kwa kuingiza pumzi ya kutosha mapafuni, halafu toa pumzi yote na kufanya kifua kiwe kama kitupu. Weka mawazo yako yote kwenye pumzi zako. Vuta pumzi kwa kina kiasi ili oksijeni iingie nyingi zaidi. Unapotoa pumzi unafanya msuli wa mapafu kujisafisha bila kukwazwa. Ni muhimu kuvuta na kutoa pumzi kwa kina angalau mara tatu kabla ya kuanza kufanya tahajudi yoyote.

5. Kila siku asubuhi baada tu ya kuamka na jioni au usiku baada ya watu wote kulala (au usiku wa manane), tenga dakika kumi na tano au zaidi kwa ajili ya kufanya tahajudi. Kuna wakati utakuta mwili hautaki, lakini jenga utashi mkubwa zaidi ya mwili hadi uzoee. Ukiahidiwa safari ya bure ya kwenda ulaya kutembea na ukaambiwa ndege itaondoka saa kumi usiku, nina uhakika ikifika saa saba utakuwa macho au yamkini unaweza usilale kabisa. Lakini pia ikitokea ukaahidiwa kutiwa au kumtia kila siku saa nane mchana na umpendaye sana, nina uhakika utafika kwenye eneo saa sita au saa saba mchana, hata chakula hutakumbuka. Ninakuomba ujenge utashi wa aina hii kwenye tahajudi.

6. Ukipata muda, kama huna kazi ya kufanya, ukiwa peke yako, ofisini, nyumbani, kwenye basi/daladala, kituoni, jaribu kufanya tahajudi. Mazoezi ya tahajudi hufanyika mahali popote.

7. kama ukifanya vizuri tahajudi, utahisi nafuu fulani kimwili au kiakili ama vyote. Utagundua kwamba, mwili hasa upande wa msukumo wa damu, utakuwa na mabadiliko.


Aina za tahajudi:

1. Tahajudi ya pumzi.

Ni kongwe zaidi. Ilianzia china na India. Ni tahajudi nzuri au muhimu kwa wale wanaoanza kujifunza.

Jinsi ya kuifanya: tafuta sehemu tulivu, kaa chini,kwenye kiti au lala kitandani (chali). Hakikisha mwili wako hauumii mahali popote, legeza misuli na viungo vyako vyote vya mwili, fumba macho yako. Vuta pumzi kwa kina halafu iruhusu itoke taratibu, wakati pumzi inatoka unaweza kutaja neno 'moja' au 'one' au neno lolote ambalo ni rahisi kwako. Usitaje neno hilo kwa mdomo, litaje kwa kulifikiri (kimoyomoyo) na baada ya muda utalizoea, litakuwa linakuja lenyewe.

Faida yake: husaidia kupumzisha mwili na akili.


2. Tahajudi ya mkono:

Hii inakuonyesha ni kwa jinsi gani mawazo yako yana nguvu zaidi kuliko mwili. Lakini pia inakuonyesha uhusiano uliopo kati ya mawazo yako na mwili wako.

Jinsi ya kuifanya: kaa kwenye kiti kisichokuwa na mkono. Miguu ikanyage chini na uweke mikono yako magotini (juu ya mapaja). Fumba macho, tulia, usiwaze kitu chochote, mawazo yakija usishindane nayo, usiyape nafasi wala muda, wewe endelea kutulia.

Ukiwa katika hali ya kupumzika na kufumba macho, chagua kati ya mkono wako wa kulia au kushoto na kupeleka mawazo (ufahamu) wako hapo. Peleka ufahamu wako kwenye mkono uliouchagua (mfano wa kulia). Fahamu kuwa sasa unaufahamu mkono wako wa kulia, yaani unauona kwa macho ya mawazo yako (kumbuka mawazo yetu yana macho, yanaweza kuona kitu hata kama hakipo mbele yetu).

Kwa kutumia macho ya mawazo yako, kitazame kiganja chako cha mkono wa kulia, kifahamu kabisa jinsi kilivyo huku ukiwa umefumba macho. Halafu kwa macho ya mawazo yako, itazame damu inavyozunguka kwenye mkono na kiganja chako, endelea kukitazama kiganja cha mkono huo wa kulia, kitazame kwa mbele na nyuma (ndani na nje). Halafu itazame damu inayotiririka ndani ya kiganja hicho. Wakati unaendelea kukitazama kiganja chako kwa macho ya mawazo yako, kuna mawazo yanapita kwenye ufahamu wako na kukuondoa kwenye uzingatifu wako. Usijaribu kushindana na mawazo hayo, yaache, bali endelea kuweka nguvu yako kwenye kiganja na damu inayotiririka ndani ya kiganja. Endelea kukitazama kiganja chako tena na tena na tena. Sasa hama kwenye kiganja na kitazame kidole gumba cha mkono wako, endelea kukitazama na baada ya muda, hamisha ufahamu wako na kukiona kidole cha pili, cha tatu, cha nne na cha tano yaani cha mwisho. Baada ya hapo, hamisha mawazo yako na kutazama katikati ya paji lako la uso, ni wazi unafahamu vizuri jinsi paji lako la uso lilivyo, endelea kulitazama kwa muda. Jaribu kukadiria umbali uliopo kati ya paji lako la uso na kiganja chako.

Baada ya hapo, endelea kukitazama kiganja chako kwa ndani, ione damu inayotiririka kwenye kiganja chako, tumia muda kidogo kuiangalia. Halafu angalia kiganja chako kwa juu(nje), kione vizuri jinsi kilivyo, peleka ufahamu wako kwenye kidole gumba, kidole kinachofuata, yaani cha pili, cha tatu, cha nne na cha tano. Peleka ufahamu wako kwenye paji lako la uso, endelea na zoezi hili kama ilivyoelezwa hapo juu. Baada ya muda, kama umejenga uzingativu wa kutosha kwa kufuata maelekezo, utaona mkono wako umeanza kupanda wenyewe. Na kama utaendelea kufanya zoezi hili, mkono wako utapanda na kugusa paji lako la uso. Na kama utaendelea kufanya, mkono utashuka wenyewe baada ya kugusa paji lako la uso na kutelemka chini mpaka kwenye paja lako na ukiendelea utapanda tena na kushuka tena.

Faida yake: husaidia kupumzisha mwili na akili, husaidia kutuliza maumivu ya mwili, husaidia kujenga uzingativu, n.k.

3. Tahajudi ya mshumaa.

Jinsi ya kuifanya:
Tayarisha mshumaa na kiberiti. Kaa chini au kwenye stuli. Weka mshumaa wako mbele yako kwenye stuli au kitu chochote ili mradi uwe usawa wa macho yako. Uwashe na uanze kuuangalia kwa kuukazia macho bila kupepesa kope. Ukishindwa, pepesa kidogo halafu endelea kuuangalia bila kupepesa tena. Endelea kuuangalia kwa muda usiopungua dakika 10 au 30.

Pia, unaweza kutumia moto huu wa mshumaa kuchoma mambo ambayo uliambiwa huwezi. Mfano, uliambiwa huna akili, hivyo, chukua hili neno na lichome kwenye moto huu wa mshumaa. Kama utakuwa umezingatia sana, utaona moto wa mshumaa ukiongezeka au ukibadilika rangi.

Tahadhari: wakati unachoma, usije ukachoma yale mambo mazuri uliyoambiwa.

4. Tahajudi ya mtoto wa ndani:

Hii ni kwa ajili ya kufuta mambo ambayo uliambiwa huwezi. Huwa tunasema, ongea na mtoto wako wa ndani.

Jinsi ya kufanya: kaa chini, kwenye kiti au lala kitandani (chali). Jenga taswira ya picha yako ulipokuwa mtoto. Jione mahali ulipokuwa kama ni nyumbani au shuleni. Angalia yale maeneo ambayo unayakumbuka na ambayo uliambiwa huwezi. Kila unapofanya chagua eneo moja moja ambalo unakumbuka uliambiwa hufai. Baada ya kutengeneza taswira ya mtoto huyo ambaye ni wewe, rudi kwako sasa ukiwa mtu mzima. Anza kuongea na huyo mtoto ambaye ni wewe pia. Mwambie kwamba, uliambiwa huna akili (kama uliambiwa huna akili) na wewe ukaamini kwa sababu ya utoto, lakini sasa umekua, fahamu ukweli huu kwamba wewe una akili sana sawa na mtu yoyote. Endelea kurudiarudia hayo maneno kwa muda wa dakika tano au zaidi.

Unapoongea na mtoto wako wa ndani mara kwa mara, pamoja na kukupa faida zingine za tahajudi, itakusaidia pia kukuwezesha kujiamini katika hayo maeneo ambayo uliambiwa huwezi au hufai.

5. Tahajudi ya namba:

Hapa, unatakiwa kuhesabu namba kinyumenyume huku ukiwa umefumba macho. Unaweza ukaanzia 100, 99, 98, 97, 96, mpaka 1, au unaweza kuanzia 200, 198, 196, 194, 192, mpaka 2. hakikisha wakati unahesabu namba hizi hukosei, na ikitokea ukakosea namba yoyote hata kama umekaribia kumaliza, itakulazimu kuanza upya. Tahajudi hii ni nzuri sana kwa kurejesha kumbukumbu, ingawa pia ina faida nyingine.
225px-Maharishi_Huntsville_Jan_1978A  .JPG


6. Tahajudi ya maua:

Tafuta ua la rangi nyekundu, kijani, njano au nyeupe. Hapa usifumbe macho. Liweke mbele yako na uliangalie kwa kulikazia macho bila kupepesa kope. Hakikisha mawazo, fikra na uzingativu wako wote unaupeleka kwenye ua hilo. Lakini kama una bustani ya maua, unaweza kwenda kukaa bustanini na kuanza kuyaangalia maua hayo kwa kuyakazia macho huku mawazo na uzingativu wako wote ukiwa kwenye ua ulilolichagua.

7. Tahajudi ya rangi:

Hii hutumika kwa ajili ya kujiponya kwani kila rangi inatibu magonjwa fulani kwenye mwili wako kama utaiangalia kwa muda mrefu au kama utavaa nguo ya rangi hiyo. Unaweza ukatumia tunda lenye rangi husika, mfano matunda damu au nyanya kuwakilisha rangi nyekundu.

8. Tahajudi ya sauti:

Hii inahusisha kutaja neno kimoyomoyo ambalo ukishalizoea neno hili itafika mahali huhitaji kulitaja ila utalisikia neno hilo likijitaja lenyewe. Unaruhusiwa kuchagua neno lolote ambalo ndiyo litakuwa nguzo yako ya kujenga uzingativu. Mfano, amani, mungu, furaha n.k.

9. Tahajudi ya kusogea:

Hii huhusisha kuikabili ardhi kama kitovu cha nguvu, huhusisha kusogea kwa aina fulani. Watu wengi hupenda kuifanya usiku.

10. Tahajudi ya kujikagua:

Huhusisha kujikagua baadhi ya maeneo yako ya mwili kwa kutumia macho yako ya akili.

11. Tahajudi ya ukuaji:

Ni tahajudi ambayo imefanyiwa utafiti mwingi sana wa kisayansi na kuthibitishwa kwamba, tahajudi husaidia mwili, akili na hisia, pia ni rahisi kujifunza. Katika tahajudi hii, kila mmoja hupewa neno ambalo hatakiwi kumpa mtu mwingine. Neno unalifanyia kazi ili kujenga uzingativu.

Hizi ni baadhi tu ya tahajudi ambazo huwa zinatumika mara kwa mara. Unachotakiwa ni kuwa mbunifu ili na wewe ubuni tahajudi ya kwako (za kwako) na kuzipa majina yoyote unayotaka. Kwenye maisha hasahasa katika tahajudi, hutakiwi kuwa kasuku wa kutumia tahajudi zilizobuniwa na watu wengine, fanya kila uwezalo kubuni tahajudi yako hata kama ni ndogo kiasi gani ili mradi inakusaidia kukupa uzingativu. Kumbuka kwamba, tahajudi inaweza kufanywa muda wowote na mahali popote.

Usikubali mwili ukutawale kwa kukuambia umechoka na hivyo nenda kalale. Hivi, kuna kitu kinaitwa kuchoka ambako kutakufanya ushindwe kufanya tahajudi? Kama jibu ni ndiyo, jiulize swali hili: umetoka kazini, umechoka sana na unataka kwenda kulala hata kuoga huwezi, halafu kabla hujanyanyuka kwenda kulala, ukamuona nyoka anaingia ndani je, utaendelea kulala au utanyanyuka ili umpige nyoka huyo? Bila shaka, usingizi na uchovu wote utaisha. Unaonaje kama tahajudi itachukua nafasi ya nyoka? Inawezekana! Maelezo haya yanakuonyesha kwamba, hakuna kitu kinachoitwa kuchoka ila wewe unasemaje!

3 hours of Meditation Music




Kwa leo naishi hapa, kama kuna mwenye changamoto, namkaribisha ili tupate kuelimishana.....

Hizi mambo naweza kujifunza vip maana kwakusoma nikifatisha nitakosea
 
Una nguvu ipi ya Kiungu wewe ?
Usikimbie Swali na kujifanya hujaelewa.

Suala la Mungu kuumba binaadamu kwa mfano wake linahusika vipi na Nguvu za Mungu?

Mungu anaadhibu kwa Moto wa jahannamu Waovu na kuwalipa watu wema pepo.
Mungu anaumba Na Kutoa roho.
Nakuuliza Yesu km ana uwezo wa kuyafanya hayo?
Na km Jibu ni Ndio Nipe Andiko kuwa Yesu aliwahi kutamka kuwa yeye ni MUNGU.
Au wapi Yesu alisema ataadhibu waovu na kuwalipa Wema!
Acheni kumsingizi Yesu mambo ambayo yeye mwenyewe hakutamka
Mtapigwa laana ya milele.


 
Chimbuko/historia ya tahajudi:

Neno tahajudi limetokana na neno la kiingereza linaloitwa 'meditation' likiwa na maana ya kufikiri kwa uzingativu au kwa kujali. Neno meditation, nalo limetokana na neno la kilatini linaloitwa 'meditatio' likiwa na maana ya mazoezi ya mwili na akili.

Asili ya tahajudi ni dini za mashariki. Ilianzia huko Asia zaidi ya miaka 5,000 iliyopita. Kwa sasa tahajudi hufanywa zaidi huko magharibi (Ulaya na Marekani).

Tahajudi ya miaka hii (ya wakati huu), inazungumzia zaidi tahajudi ya kiyoga ambayo asili yake ni huko India.

Kwa ujumla, tahajudi inaelezwa kama njia za uzingativu katika jambo ambalo mawazo yamelinuia. Lakini pia inaweza kuelezwa kama ifuatavyo:

=> Ni hali ya uzingativu na utulivu katika hali halisi ya wakati wa sasa hivi.

=> Ni ile hali wakati mawazo yanapokuwa yameyeyushwa na kufikia mahali ambapo hakuna fikra yenye kuingia tena.

=> Ni ile hali ambayo, uzingativu, kwa makusudi kabisa umeachwa kuelekea kwenye nguvu kubwa zaidi ( Mungu? Nguvu kuu? ).

=> Ni ile hali ya kuweka mawazo na uzingativu katika kitu kimoja, mfano- sanamu ya kidini, pumzi au neno fulani unalotamka (mantra).

=> Wengine wanaielezea tahajudi kwamba, ni sala za usiku wa manane.

CouplePraying.jpg


Tahajudi na dini:

Kila dini ina aina yake ya uzingativu, ingawa ukiutazama kwa undani utagundua kwamba ni tahajudi halisi.

Dini ya kikristo wanatumia rozari, hii huwasaidia kujenga uzingativu. Waislamu wanatumia tasbihi ambayo huwasaidia kujenga uzingativu, lakini pia huwa wanakuwa na sala za usiku wa manane (tahajudi). Wabudha huwa wanafanya tahajudi kila siku kwani ndiyo nguzo yao kuu. Wabahai, hufanya tahajudi kila baada ya sala.

Faida za tahajudi:

Ili uweze kutambua faida za tahajudi, ni muhimu kuifanya kila siku, ikiwezekana asubuhi na jioni. Tahajudi ina faida nyingi sana, faida hizi utaziona tu kama utafanya tahajudi kila siku. Hivyo, tahajudi inahitaji nguvu kubwa sana ya kujituma (wheel power). Ina faida kubwa sana, hivyo ni vizuri ukajenga mazoea ya kuifanya kila siku. Nakushauri, kama huwezi kufanya tahajudi, basi ni afadhali ujifunze upendo ingawa, ni rahisi mara kumi kufanya tahajudi kuliko kuwa na upendo. baadhi ya faida hizo ni kama ifuatavyo:

1. Husaidia kuongeza ubora wetu kiakili, kimwili pamoja na uwezo wetu kwa ujumla. Husaidia kuuburudisha mwili, pia husaidia kupumzisha akili na mwili.

2. Husaidia kujenga uzingativu na kukuwezesha kumudu kupata suluhu ya matatizo kirahisi.

3. Husaidia kuratibu msukumo wa damu pamoja na usafirishwaji wa damu mwilini.

4. Husaidia pumzi pamoja na kurahisisha usagwaji wa chakula mwilini.

5. Husaidia kuimarisha mfumo wa kinga mwilini.

6. Husaidia kuleta furaha ya nafsi.

7. Husaidia kuimarisha nguvu yako ya machale pamoja na nguvu zako za ziada.

8. Husaidia kutibu matatizo mengi ya kisaikolojia kwani hubadili hali ya mfumo wa fahamu na mawazo (endapo itafanywa kila siku).

9. tahajudi pia inaweza kutumika kuomba kitu unachohitaji, kama vile kazi au mahitaji mbalimbali, ingawa inashauriwa uwe mwangalifu badala ya kufanya kazi unaweza ukawa mtegemezi wa tahajudi. Mfano, unaweza ukatumia tahajudi kuomba shilingi laki moja na ukapata bila kufanya kazi yoyote au kwa kufanya kazi kidogo sana ambayo hailingani na malipo ya laki moja.

Je, tahajudi huleta utajiri?

Ni swali gumu kwa sababu, utajiri ni dhana pana sana, inategemea tu unazungumzia utajiri upi, wa kitu gani na wapi. Hata ule utajiri wa kimazoea, nao bado ni mgumu kuuelezea. Mfano, tajiri wa kijijini, akihamia mjini anaonekana ni mtu wa kawaida kabisa kwani kuna matajiri wengi sana wanaomzidi.

Lakini, swali la kujiuliza ni hili, unataka utajiri ili iweje au upate nini? Kama unataka utajiri ili uwe maarufu kwa kuandikwa na magazeti, ukweli ni kwamba, kuna uwezekano mkubwa wa wewe kuandikwa na magazeti ingawa siyo kwa utajiri ila kwa kubaka mtoto. Lakini pia kama unataka utajiri ili ukupe furaha na amani, ukweli utabaki palepale kwamba, hata kama utaupata huo utajiri, furaha au amani haitapatikana kwani utakuwa umevunja kanuni ya maisha kwani hukuja duniani kutafuta utajiri, bali kuishi kwa kufanya kazi unayoipenda sana, inayokupa furaha na amani bila kujali maslahi, heshima au umaarufu kutoka kwenye kazi hiyo.

Kwakuwa kazi hii unaipenda, utaifanya kwa ufanisi mkubwa sana, na ndipo utajiri utakapokuja. Kanuni ya maisha kuhusu utajiri inaanza na kufanya kazi inayokupa furaha na amani na ndipo utajiri unafuata, haianzi na utajiri na ndipo furaha na amani vipatikane. Kama huamini, wachunguze matajiri unaowafahamu, ambao walipata utajiri ili uwape furaha na amani, utagundua kwamba, hawana furaha wala amani. Kwa upande wa pili wa shilingi, wale matajiri ambao, utajiri wao ulikuja kupitia kwa kufanya kazi inayowapa furaha na amani, utagundua kwamba wana furaha na amani kubwa sana.

Swali lililoulizwa hapo juu linasema, je, tahajudi huleta utajiri? Kama utajiri ni kupata furaha na amani ya nafsi, jibu ni ndiyo. Hii ni kwa sababu, tahajudi hukusaidia au kukufundisha namna bora kabisa ya kupumzisha akili na mwili na hivyo kuwa mtu mwenye furaha na amani. Kumbuka, ukishakuwa mwenye furaha na amani, wewe tayari ni tajiri wa mali pia.


Tahajudi ina madhara yoyote?

Kwa watu wenye matatizo ya kifafa, matatizo makubwa ya moyo au wenye matatizo ya akili, tahajudi inaweza kuwaumiza wasipokuwa waangalifu, ingawa kwa upande mwingine, tahajudi ni tiba/dawa kwao. Hivyo, wanashauriwa wachague tahajudi ambayo haitawaletea matatizo.

Ni vizuri wakajaribu aina tofauti tofauti ya tahajudi, halafu wakaangalia ni ipi inawasumbua na ni ipi inawapa nafuu. Wakishapata inayowapa nafuu, ni vizuri wakaendelea kuifanya mara kwa mara. Baada ya muda, watagundua kwamba, matatizo yao ya akili, moyo au kifafa yamepungua kwa kiwango kikubwa sana au yameisha kabisa.

meditation-techniques.jpg


Jinsi ya kufanya tahajudi:

Mbinu za kufanya tahajudi hutofautiana kutokana na kiwango cha uzingativu, uwezo wa kujenga taswira na namna mtu anavyoweza kukabili mawazo yanayomwingilia wakati anafanya tahajudi yake.

Baadhi ya mbinu hizi, humfanya mtu apotelee kwenye kile anachozingatia na kutoingiliwa kabisa na wazo lolote. Mbinu hizi ni rahisi mtu kujifunza mwenyewe, ingawa kuna baadhi zinahitaji awepo mwongozaji.


Hatua zinazotakiwa wakati unajiandaa kufanya tahajudi ni kama ifuatavyo:

1. Tafuta sehemu iliyotulia, isiyo na makelele. Kaa kwenye kiti au chini, au lala kitandani. Hakikisha huumii mahali popote. Legeza mwili wako pamoja na misuli yote ya mwili wako kwa kadri utakavyoweza.

2. Sahau matatizo yako yaliyopita, yaliyopo na yajayo. Sahau matatizo yako ya kazini au nyumbani. Jitahidi usifikirie chochote. kama kuna mawazo yataingia, usigombane nayo, usiyape muda na nafasi, wewe endelea na kile ulichoamua kukizingatia. Hakikisha uzingativu wako ni mkubwa. Pia kione hicho unachokizingatia kwa jicho lako la ndani, kijengee taswira kana kwamba unacho tayari au kana kwamba unakiona (unacho).

3. Ni muhimu sana kujali hisia zako wakati unafanya tahajudi. Kwa mfano, kama unafanya tahajudi ya kujenga nyumba. Hakikisha hiyo nyumba unaiona ilivyo, ingia ndani ya hiyo nyumba, sebuleni, chumbani, chooni, stoo, jikoni na sehemu ya kulia chakula (dining). Kila unapoingia, onyesha hisia zako, jione una furaha ndani mwako na ikiwezekana tabasamu, pia jione una amani ndani mwako. Ukweli ni kwamba, utakapokuja kujenga hiyo nyumba, zile hisia ulizokuwa unazionyesha wakati unafanya tahajudi, zitajitokeza au utaziona. Kama tahajudi yako ulikuwa unaifanya ukiwa na huzuni, hali hiyo itajitokeza baada ya kumaliza kujenga nyumba yako. Inaweza ikatokea baada tu ya kujenga nyumba yako, ndugu zako au wa mkeo wakajaa pale nyumbani, wakawa wanafanya vurugu ambazo zitakuletea huzuni na hivyo kuanza kujuta ni kwa nini umejenga hiyo nyumba.

Ukweli ni kwamba, tatizo siyo ndugu, tatizo ni wewe mwenyewe, ni hisia zako ulizokuwa unazionyesha wakati unafanya tahajudi yako ya kujenga nyumba. Na kama wakati unafanya tahajudi yako ulikuwa na hisia za furaha, hali hiyo pia itajitokeza baada ya kumaliza nyumba yako. Hata kama ndugu wa mkeo au mumeo watajaa pale nyumbani, vicheko, tabasamu na mambo mengine ambayo yatakupa furaha yatatamalaki pale nyumbani. Kwa hiyo, hisia ni muhimu sana wakati unafanya tahajudi.

4. Pumua kwa kuingiza pumzi ya kutosha mapafuni, halafu toa pumzi yote na kufanya kifua kiwe kama kitupu. Weka mawazo yako yote kwenye pumzi zako. Vuta pumzi kwa kina kiasi ili oksijeni iingie nyingi zaidi. Unapotoa pumzi unafanya msuli wa mapafu kujisafisha bila kukwazwa. Ni muhimu kuvuta na kutoa pumzi kwa kina angalau mara tatu kabla ya kuanza kufanya tahajudi yoyote.

5. Kila siku asubuhi baada tu ya kuamka na jioni au usiku baada ya watu wote kulala (au usiku wa manane), tenga dakika kumi na tano au zaidi kwa ajili ya kufanya tahajudi. Kuna wakati utakuta mwili hautaki, lakini jenga utashi mkubwa zaidi ya mwili hadi uzoee. Ukiahidiwa safari ya bure ya kwenda ulaya kutembea na ukaambiwa ndege itaondoka saa kumi usiku, nina uhakika ikifika saa saba utakuwa macho au yamkini unaweza usilale kabisa. Lakini pia ikitokea ukaahidiwa kutiwa au kumtia kila siku saa nane mchana na umpendaye sana, nina uhakika utafika kwenye eneo saa sita au saa saba mchana, hata chakula hutakumbuka. Ninakuomba ujenge utashi wa aina hii kwenye tahajudi.

6. Ukipata muda, kama huna kazi ya kufanya, ukiwa peke yako, ofisini, nyumbani, kwenye basi/daladala, kituoni, jaribu kufanya tahajudi. Mazoezi ya tahajudi hufanyika mahali popote.

7. kama ukifanya vizuri tahajudi, utahisi nafuu fulani kimwili au kiakili ama vyote. Utagundua kwamba, mwili hasa upande wa msukumo wa damu, utakuwa na mabadiliko.


Aina za tahajudi:

1. Tahajudi ya pumzi.

Ni kongwe zaidi. Ilianzia china na India. Ni tahajudi nzuri au muhimu kwa wale wanaoanza kujifunza.

Jinsi ya kuifanya: tafuta sehemu tulivu, kaa chini,kwenye kiti au lala kitandani (chali). Hakikisha mwili wako hauumii mahali popote, legeza misuli na viungo vyako vyote vya mwili, fumba macho yako. Vuta pumzi kwa kina halafu iruhusu itoke taratibu, wakati pumzi inatoka unaweza kutaja neno 'moja' au 'one' au neno lolote ambalo ni rahisi kwako. Usitaje neno hilo kwa mdomo, litaje kwa kulifikiri (kimoyomoyo) na baada ya muda utalizoea, litakuwa linakuja lenyewe.

Faida yake: husaidia kupumzisha mwili na akili.


2. Tahajudi ya mkono:

Hii inakuonyesha ni kwa jinsi gani mawazo yako yana nguvu zaidi kuliko mwili. Lakini pia inakuonyesha uhusiano uliopo kati ya mawazo yako na mwili wako.

Jinsi ya kuifanya: kaa kwenye kiti kisichokuwa na mkono. Miguu ikanyage chini na uweke mikono yako magotini (juu ya mapaja). Fumba macho, tulia, usiwaze kitu chochote, mawazo yakija usishindane nayo, usiyape nafasi wala muda, wewe endelea kutulia.

Ukiwa katika hali ya kupumzika na kufumba macho, chagua kati ya mkono wako wa kulia au kushoto na kupeleka mawazo (ufahamu) wako hapo. Peleka ufahamu wako kwenye mkono uliouchagua (mfano wa kulia). Fahamu kuwa sasa unaufahamu mkono wako wa kulia, yaani unauona kwa macho ya mawazo yako (kumbuka mawazo yetu yana macho, yanaweza kuona kitu hata kama hakipo mbele yetu).

Kwa kutumia macho ya mawazo yako, kitazame kiganja chako cha mkono wa kulia, kifahamu kabisa jinsi kilivyo huku ukiwa umefumba macho. Halafu kwa macho ya mawazo yako, itazame damu inavyozunguka kwenye mkono na kiganja chako, endelea kukitazama kiganja cha mkono huo wa kulia, kitazame kwa mbele na nyuma (ndani na nje). Halafu itazame damu inayotiririka ndani ya kiganja hicho. Wakati unaendelea kukitazama kiganja chako kwa macho ya mawazo yako, kuna mawazo yanapita kwenye ufahamu wako na kukuondoa kwenye uzingatifu wako. Usijaribu kushindana na mawazo hayo, yaache, bali endelea kuweka nguvu yako kwenye kiganja na damu inayotiririka ndani ya kiganja. Endelea kukitazama kiganja chako tena na tena na tena. Sasa hama kwenye kiganja na kitazame kidole gumba cha mkono wako, endelea kukitazama na baada ya muda, hamisha ufahamu wako na kukiona kidole cha pili, cha tatu, cha nne na cha tano yaani cha mwisho. Baada ya hapo, hamisha mawazo yako na kutazama katikati ya paji lako la uso, ni wazi unafahamu vizuri jinsi paji lako la uso lilivyo, endelea kulitazama kwa muda. Jaribu kukadiria umbali uliopo kati ya paji lako la uso na kiganja chako.

Baada ya hapo, endelea kukitazama kiganja chako kwa ndani, ione damu inayotiririka kwenye kiganja chako, tumia muda kidogo kuiangalia. Halafu angalia kiganja chako kwa juu(nje), kione vizuri jinsi kilivyo, peleka ufahamu wako kwenye kidole gumba, kidole kinachofuata, yaani cha pili, cha tatu, cha nne na cha tano. Peleka ufahamu wako kwenye paji lako la uso, endelea na zoezi hili kama ilivyoelezwa hapo juu. Baada ya muda, kama umejenga uzingativu wa kutosha kwa kufuata maelekezo, utaona mkono wako umeanza kupanda wenyewe. Na kama utaendelea kufanya zoezi hili, mkono wako utapanda na kugusa paji lako la uso. Na kama utaendelea kufanya, mkono utashuka wenyewe baada ya kugusa paji lako la uso na kutelemka chini mpaka kwenye paja lako na ukiendelea utapanda tena na kushuka tena.

Faida yake: husaidia kupumzisha mwili na akili, husaidia kutuliza maumivu ya mwili, husaidia kujenga uzingativu, n.k.

3. Tahajudi ya mshumaa.

Jinsi ya kuifanya:
Tayarisha mshumaa na kiberiti. Kaa chini au kwenye stuli. Weka mshumaa wako mbele yako kwenye stuli au kitu chochote ili mradi uwe usawa wa macho yako. Uwashe na uanze kuuangalia kwa kuukazia macho bila kupepesa kope. Ukishindwa, pepesa kidogo halafu endelea kuuangalia bila kupepesa tena. Endelea kuuangalia kwa muda usiopungua dakika 10 au 30.

Pia, unaweza kutumia moto huu wa mshumaa kuchoma mambo ambayo uliambiwa huwezi. Mfano, uliambiwa huna akili, hivyo, chukua hili neno na lichome kwenye moto huu wa mshumaa. Kama utakuwa umezingatia sana, utaona moto wa mshumaa ukiongezeka au ukibadilika rangi.

Tahadhari: wakati unachoma, usije ukachoma yale mambo mazuri uliyoambiwa.

4. Tahajudi ya mtoto wa ndani:

Hii ni kwa ajili ya kufuta mambo ambayo uliambiwa huwezi. Huwa tunasema, ongea na mtoto wako wa ndani.

Jinsi ya kufanya: kaa chini, kwenye kiti au lala kitandani (chali). Jenga taswira ya picha yako ulipokuwa mtoto. Jione mahali ulipokuwa kama ni nyumbani au shuleni. Angalia yale maeneo ambayo unayakumbuka na ambayo uliambiwa huwezi. Kila unapofanya chagua eneo moja moja ambalo unakumbuka uliambiwa hufai. Baada ya kutengeneza taswira ya mtoto huyo ambaye ni wewe, rudi kwako sasa ukiwa mtu mzima. Anza kuongea na huyo mtoto ambaye ni wewe pia. Mwambie kwamba, uliambiwa huna akili (kama uliambiwa huna akili) na wewe ukaamini kwa sababu ya utoto, lakini sasa umekua, fahamu ukweli huu kwamba wewe una akili sana sawa na mtu yoyote. Endelea kurudiarudia hayo maneno kwa muda wa dakika tano au zaidi.

Unapoongea na mtoto wako wa ndani mara kwa mara, pamoja na kukupa faida zingine za tahajudi, itakusaidia pia kukuwezesha kujiamini katika hayo maeneo ambayo uliambiwa huwezi au hufai.

5. Tahajudi ya namba:

Hapa, unatakiwa kuhesabu namba kinyumenyume huku ukiwa umefumba macho. Unaweza ukaanzia 100, 99, 98, 97, 96, mpaka 1, au unaweza kuanzia 200, 198, 196, 194, 192, mpaka 2. hakikisha wakati unahesabu namba hizi hukosei, na ikitokea ukakosea namba yoyote hata kama umekaribia kumaliza, itakulazimu kuanza upya. Tahajudi hii ni nzuri sana kwa kurejesha kumbukumbu, ingawa pia ina faida nyingine.
225px-Maharishi_Huntsville_Jan_1978A .JPG


6. Tahajudi ya maua:

Tafuta ua la rangi nyekundu, kijani, njano au nyeupe. Hapa usifumbe macho. Liweke mbele yako na uliangalie kwa kulikazia macho bila kupepesa kope. Hakikisha mawazo, fikra na uzingativu wako wote unaupeleka kwenye ua hilo. Lakini kama una bustani ya maua, unaweza kwenda kukaa bustanini na kuanza kuyaangalia maua hayo kwa kuyakazia macho huku mawazo na uzingativu wako wote ukiwa kwenye ua ulilolichagua.

7. Tahajudi ya rangi:

Hii hutumika kwa ajili ya kujiponya kwani kila rangi inatibu magonjwa fulani kwenye mwili wako kama utaiangalia kwa muda mrefu au kama utavaa nguo ya rangi hiyo. Unaweza ukatumia tunda lenye rangi husika, mfano matunda damu au nyanya kuwakilisha rangi nyekundu.

8. Tahajudi ya sauti:

Hii inahusisha kutaja neno kimoyomoyo ambalo ukishalizoea neno hili itafika mahali huhitaji kulitaja ila utalisikia neno hilo likijitaja lenyewe. Unaruhusiwa kuchagua neno lolote ambalo ndiyo litakuwa nguzo yako ya kujenga uzingativu. Mfano, amani, mungu, furaha n.k.

9. Tahajudi ya kusogea:

Hii huhusisha kuikabili ardhi kama kitovu cha nguvu, huhusisha kusogea kwa aina fulani. Watu wengi hupenda kuifanya usiku.

10. Tahajudi ya kujikagua:

Huhusisha kujikagua baadhi ya maeneo yako ya mwili kwa kutumia macho yako ya akili.

11. Tahajudi ya ukuaji:

Ni tahajudi ambayo imefanyiwa utafiti mwingi sana wa kisayansi na kuthibitishwa kwamba, tahajudi husaidia mwili, akili na hisia, pia ni rahisi kujifunza. Katika tahajudi hii, kila mmoja hupewa neno ambalo hatakiwi kumpa mtu mwingine. Neno unalifanyia kazi ili kujenga uzingativu.

Hizi ni baadhi tu ya tahajudi ambazo huwa zinatumika mara kwa mara. Unachotakiwa ni kuwa mbunifu ili na wewe ubuni tahajudi ya kwako (za kwako) na kuzipa majina yoyote unayotaka. Kwenye maisha hasahasa katika tahajudi, hutakiwi kuwa kasuku wa kutumia tahajudi zilizobuniwa na watu wengine, fanya kila uwezalo kubuni tahajudi yako hata kama ni ndogo kiasi gani ili mradi inakusaidia kukupa uzingativu. Kumbuka kwamba, tahajudi inaweza kufanywa muda wowote na mahali popote.

Usikubali mwili ukutawale kwa kukuambia umechoka na hivyo nenda kalale. Hivi, kuna kitu kinaitwa kuchoka ambako kutakufanya ushindwe kufanya tahajudi? Kama jibu ni ndiyo, jiulize swali hili: umetoka kazini, umechoka sana na unataka kwenda kulala hata kuoga huwezi, halafu kabla hujanyanyuka kwenda kulala, ukamuona nyoka anaingia ndani je, utaendelea kulala au utanyanyuka ili umpige nyoka huyo? Bila shaka, usingizi na uchovu wote utaisha. Unaonaje kama tahajudi itachukua nafasi ya nyoka? Inawezekana! Maelezo haya yanakuonyesha kwamba, hakuna kitu kinachoitwa kuchoka ila wewe unasemaje!

3 hours of Meditation Music




Kwa leo naishi hapa, kama kuna mwenye changamoto, namkaribisha ili tupate kuelimishana.....
Mungu akubarki sana kwa hili darasa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
bigstock-African-American-Woman-Meditat-92821154.jpg

Meditation au taamuli ni kitendo ambacho wengi ambao wamejifunza mambo mengi ya hekima, nguvu ya akili katika maisha ya mwanadamu, sayansi, na Imani mbalimbali, wamekuwa wakivutiwa na kufanya meditation. Mojawapo ya changamoto ya kwanza ambayo wengi wamekuwa wakikutana nayo ni akili kuhama sana kwenye meditation. Kupitia Makala hii, nitajaribu kuelezea njia mbalimbali ambazo unaweza kuzifanya katika kuhakikisha akili inatulia sehemu moja na kuongeza nguvu ya umakini na utambuzi wa hali ya akili yako.

Mwanzo
Meditation au kwa jina la kiswahi Taamuli ni kitendo cha kutazama hali (nature) ya akili na kuongeza utambuzi na umakini. Wengi wanaofanya meditation ni kwa lengo la kuituliza akili kutoka katika stress, msongo wa mawazo, kuongeza hekima, kuongeza umakini na utambuzi juu ya mtu binafsi na jinsi alivyo. Pia wengine hufanya meditation kuachana na addictions na mazoea na kuongeza willi-power. Na wapo wanaofanya meditation kuongeza uwezo wa sheria ya usumaku (law of attraction) na wengine hufanya meditation kuongeza umakini, ubunifu (mfano wachoraji, wanamuziki, wasomi n.k). Kuna sababu nyingi ambazo kila mtu binafsi anaamua kufanya meditation.

Akili ni kitu ambacho ni kitu Tata sana (very complex). Ni sehemu ya mwanadamu ambayo haijagunduliwa vyema jinsi ifanyavyo kazi na hakuna mtu anayeweza kukusaidia kufikiri au kujua jinsi akili yako ifanyavyo kazi. Mara nyingi tumekuwa watumwa wa akili zetu bila kutambua kuwa tunaweza kutawala akili zetu na kuamuru akili iwaze nini, isiwaze chochote au kuamua kuweka umakini katika jambo Fulani kwa jinsi utakavyo wewe. Akili ukiweza kuiongoza utakusaidia lakini ukishindwa utakuwa mtumwa wake utakuwa mtumwa daima. Ndipo utakuta hali kama addictions, mazoea mabaya, umakini, hekima na uvumilivu tunashindwa kuwa navyo kwa sababu hatuwezi kutumia akili zetu ipasavyo.

Tatizo linalosababisha akili kutotulia
Kwa kawaida tangu unapoamka na mpaka unapoenda kulala akili inafanya kazi. Kila wakati utawaza hichi, kisha utawaza kingine, na ukitaka kujua hilo chukua kalamu na karatasi na saa. Andika kwenye karatasi kila kitu au wazo au hisia itakayopita akilini. Mfano ukiwaza kuhusu kazini andika kwenye karatasi “kazini”, ukimuwaza mtu andika jina lake, andika kwa ufupi ili upate muda wa kuandika. Hakikisha umeandika kila kitu na kisha baada ya dakika kumi utaona ni mawazo au hisia nyingi zimepita akili. Huo ni mfano tu kuwa kwa kawaida akili huwa haitulii. Itawaza hichi, itakumbuka ya jana, utakuwa na hisia Fulani, na kila hali inakuja na kupita. Ndivyo tulivyozoea maishani.

Meditation na Akili.
Kwenye meditation unajifunza kuitawala na kuingoza akili kwa dakika Fulani. Mfano meditation ya Samadhi Meditation ambayo unaiweka akili katika umakini mmoja tu; ni kitendo cha kuelekeza akili katika jambo moja au kitu kimoja mfano kwenye pumzi tu. Kila saa na kila dakika tunapumua, lakini hatuweki akili zetu kwenye pumzi kwa sababu haina umuhimu kutazama pumzi kila saa. Hivyo meditation ya kuongoza akili inatumia pumzi kwa sababu ni hali ambayo wakati wote tunayo, haiitaji kuwasha mshumaa au kutazama kitu Fulani. Kuweka akili kwenye pumzi ni cheap/rahisi na haiitaji chochote. Ni mtu tu mwenyewe kutumia pumzi na kujaribu kuiweka akili sehemu moja kwa dakika chache. Unaweza kufanya meditation kwa kuweka akili yako kwenye mshumaa, kutazama bahari, kutazama chochote unachokiamini n.k. Kwa hapa leo nitazungumzia kuitawala akili kwenye pumzi.

Ukiwa unafanya meditation
Ukiwa unafanya meditation unakaa mkao ambao utakuwa huru na utaweza kukaa kwa dakika chache bila kuhama. Unaweza kukaa kwenye kiti lakini usilale kwa sababu unaweza ukasinzia kutokana na uvivu. Pia kama unaweza kukunja miguu kwa muda mrefu pia unaweza kukaa vizuri chini, juu ta mto au kitu ambacho kitaepusha maumivu ukikaa sakafuni.

Ukianza hakikisha hutasumbuliwa na utapata muda wa dakika chache kukaa peke yako. Pia unaweza kufanya meditation na wengine kwa kukaa pamoja na kila mmoja kuangalia upande wake (ili kuwa na concentration/umakini). Kwa wanaoanza tumia dakika 10. Kila wiki unaweza kuongeza dakika 5 mfano 15, halafu wiki ijayo ukajifunza 20 na kisha zoea kutawala akili kwa dakika 20 kila siku ndani ya mwezi mmoja na baadae unaweza kutumia 30 mpaka 40, sio lazima uzidi 40, cha msingi sio dakika ni umakini ndio uongeze. chukua saa au simu ikukumbushe dakika kumi zikifika. Hakikisha umeweka simu silent, na ukiwa kwenye meditation usiangalie zimebaki dakika ngapi, dedicate kuwa na subira mpaka muda utimie.

Ukianza weka akili kwenye pumzi, vuta pumzi taratibu na weka break kisha toa pumzi taratibu. Yaani unavuta pumzi, unakaa kidooogo kisha unaitoa taaratibu huku ukitazama jinsi hewa inavyoingia puani na kifua kikitanuka na hewa ikitoka na kifua kikishuka taaratibu. Ukigundua akili haipo tena kwenye pumzi usijali wala usijilaumu au kuona umekosea, ni kitendo cha kawaida akili kuhama bila kujijua. Cha msingi irudishe tena akili kwenye pumzi kama mwazoni. Endelea hivyo hivyo. Akili ikihama unairudisha kwenye pumzi. Ukiona kama unarelax na unahisi mwili umetulia sana huwa kuna kama raha Fulani unaihisi au umeme/waves Fulani ya relaxation unaiona unakuzunguka achana nayo na usiweke akili kwenye raha inayokujia ukiwa unafanya meditation wewe endelea kuweka akili kwenye pumzi na ile raha itaendelea kuwepo. Ukiiwaza utapotea, ni kama mtego.

Akili ikiwa haitulii.
Samahani kwa kuanza kuelezea mengi kwa sababu hapa ndipo kwenye mada kuu. Nilipenda kutoa introduction kwa ambao hawajui ili wafahamu na tuende sawa.

Akili huwa kwa mara ya kwanza kufanya meditation inahama sana. Sio tatizo ni hali ya kawaida. Ni udhibitisho kuwa akili inahitaji kutulizwa. Kuna njia mbalimbali ambazo unaweza kufanya. Unaweza kuhesabu pumzi inapoingia. Ukahesabu Moja….mbili…tatu na kufika kumi kisha rudi tisa, nane, saba, sita….. mpaka sifuri kisha anza tena moja, mbili…na kuendelea.

Njia nyingine, ukiona akili inahama, mfano unawaza kuhusu jambo Fulani, sema kwa taratibu “akili najua unawaza kuhusu masuala ya kazini, rudi kwenye pumzi”. Kusema hivyo sio kwamba unaongea na akili bali inakupa mazoea ya kujua kinachoendelea akili na kukifanyia maamuzi. Ukiona unawaza kuhusu kitu Fulani mfano pesa zako ulipoziweka sema “akili najua unawaza pesa zangu, rudi kwenye pumzi” kisha endelea kuweka umakini kwenye pumzi.

Baada ya kufanya meditation mara kwa mara utaona kuhama kwa akili kumepungua na unaanza kuona raha kufanya meditation. Pia baada ya meditation utakuwa unahisi Amani na kama ulikuwa umeshusha mzigo mzito akilini. Pia katika maisha utakuwa makini na kinachoendelea akilini mwako na kukusaidia kujitambua vyema.

Asante.


meditate-481700_1280.jpg
Barikiwa sana kiongoz

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Meditation :ni kitendo cha uzingativu wa akili kuwa sehemu moja
Faida za meditation:
1.meditation ina ongeza uwezo wa akili ikiwa inafanywa kila siku
2. Meditation ina ongeza furaha na amani ndani ya nafsi
3.pia meditation endapo ikifanywa kila siku ,inafungua natural power za mtu anaye fanyaa
4. Meditation ina saidia katika mfumo wa upumuaji
5. Meditation ina kupa uwezo wa kuongea na nafsi yako
6.meditation ujianini kuongea mbele za watu ,mfano kwenye mikutano ,siasa,nk.
7. Meditation inakupa nafasi na kuheshimu kila kitu chenye uhai

Mambo ya kuzingatia wakati wa kufanya meditation
1.taafuta sehemu tulivu isiyo na makelele

2.Oga ,vaa nguo nyepesi na zisizo bana,hii inasaidia kuondoa nuwasho kwenye mwili .
3. Imani ya kuwa unaweza kufanya meditation
4. Vuta punzi ndefu na kutoa taratibu hii inakusaidia kuondoa uwoga na kuweza u bongo upate oxygen ya kutosha.
5.Kaa mfumo wa budhaa ,au lala chali,au kaa kwenye stuli hakiki haumii sehemu yoyote 5.legeza misuli na mwili kiujumla
6. Weka akili yako kwenye pumzi inayo ingia na kutoka
7. Hakikisha unafanya meditation ndani muda wa dakika 10 hadi 15
8. Hakikisha usifikilie chochote za ya punziiii
 
Chimbuko/historia ya tahajudi:

Neno tahajudi limetokana na neno la kiingereza linaloitwa 'meditation' likiwa na maana ya kufikiri kwa uzingativu au kwa kujali. Neno meditation, nalo limetokana na neno la kilatini linaloitwa 'meditatio' likiwa na maana ya mazoezi ya mwili na akili.

Asili ya tahajudi ni dini za mashariki. Ilianzia huko Asia zaidi ya miaka 5,000 iliyopita. Kwa sasa tahajudi hufanywa zaidi huko magharibi (Ulaya na Marekani).

Tahajudi ya miaka hii (ya wakati huu), inazungumzia zaidi tahajudi ya kiyoga ambayo asili yake ni huko India.

Kwa ujumla, tahajudi inaelezwa kama njia za uzingativu katika jambo ambalo mawazo yamelinuia. Lakini pia inaweza kuelezwa kama ifuatavyo:

=> Ni hali ya uzingativu na utulivu katika hali halisi ya wakati wa sasa hivi.

=> Ni ile hali wakati mawazo yanapokuwa yameyeyushwa na kufikia mahali ambapo hakuna fikra yenye kuingia tena.

=> Ni ile hali ambayo, uzingativu, kwa makusudi kabisa umeachwa kuelekea kwenye nguvu kubwa zaidi ( Mungu? Nguvu kuu? ).

=> Ni ile hali ya kuweka mawazo na uzingativu katika kitu kimoja, mfano- sanamu ya kidini, pumzi au neno fulani unalotamka (mantra).

=> Wengine wanaielezea tahajudi kwamba, ni sala za usiku wa manane.

CouplePraying.jpg


Tahajudi na dini:

Kila dini ina aina yake ya uzingativu, ingawa ukiutazama kwa undani utagundua kwamba ni tahajudi halisi.

Dini ya kikristo wanatumia rozari, hii huwasaidia kujenga uzingativu. Waislamu wanatumia tasbihi ambayo huwasaidia kujenga uzingativu, lakini pia huwa wanakuwa na sala za usiku wa manane (tahajudi). Wabudha huwa wanafanya tahajudi kila siku kwani ndiyo nguzo yao kuu. Wabahai, hufanya tahajudi kila baada ya sala.

Faida za tahajudi:

Ili uweze kutambua faida za tahajudi, ni muhimu kuifanya kila siku, ikiwezekana asubuhi na jioni. Tahajudi ina faida nyingi sana, faida hizi utaziona tu kama utafanya tahajudi kila siku. Hivyo, tahajudi inahitaji nguvu kubwa sana ya kujituma (wheel power). Ina faida kubwa sana, hivyo ni vizuri ukajenga mazoea ya kuifanya kila siku. Nakushauri, kama huwezi kufanya tahajudi, basi ni afadhali ujifunze upendo ingawa, ni rahisi mara kumi kufanya tahajudi kuliko kuwa na upendo. baadhi ya faida hizo ni kama ifuatavyo:

1. Husaidia kuongeza ubora wetu kiakili, kimwili pamoja na uwezo wetu kwa ujumla. Husaidia kuuburudisha mwili, pia husaidia kupumzisha akili na mwili.

2. Husaidia kujenga uzingativu na kukuwezesha kumudu kupata suluhu ya matatizo kirahisi.

3. Husaidia kuratibu msukumo wa damu pamoja na usafirishwaji wa damu mwilini.

4. Husaidia pumzi pamoja na kurahisisha usagwaji wa chakula mwilini.

5. Husaidia kuimarisha mfumo wa kinga mwilini.

6. Husaidia kuleta furaha ya nafsi.

7. Husaidia kuimarisha nguvu yako ya machale pamoja na nguvu zako za ziada.

8. Husaidia kutibu matatizo mengi ya kisaikolojia kwani hubadili hali ya mfumo wa fahamu na mawazo (endapo itafanywa kila siku).

9. tahajudi pia inaweza kutumika kuomba kitu unachohitaji, kama vile kazi au mahitaji mbalimbali, ingawa inashauriwa uwe mwangalifu badala ya kufanya kazi unaweza ukawa mtegemezi wa tahajudi. Mfano, unaweza ukatumia tahajudi kuomba shilingi laki moja na ukapata bila kufanya kazi yoyote au kwa kufanya kazi kidogo sana ambayo hailingani na malipo ya laki moja.

Je, tahajudi huleta utajiri?

Ni swali gumu kwa sababu, utajiri ni dhana pana sana, inategemea tu unazungumzia utajiri upi, wa kitu gani na wapi. Hata ule utajiri wa kimazoea, nao bado ni mgumu kuuelezea. Mfano, tajiri wa kijijini, akihamia mjini anaonekana ni mtu wa kawaida kabisa kwani kuna matajiri wengi sana wanaomzidi.

Lakini, swali la kujiuliza ni hili, unataka utajiri ili iweje au upate nini? Kama unataka utajiri ili uwe maarufu kwa kuandikwa na magazeti, ukweli ni kwamba, kuna uwezekano mkubwa wa wewe kuandikwa na magazeti ingawa siyo kwa utajiri ila kwa kubaka mtoto. Lakini pia kama unataka utajiri ili ukupe furaha na amani, ukweli utabaki palepale kwamba, hata kama utaupata huo utajiri, furaha au amani haitapatikana kwani utakuwa umevunja kanuni ya maisha kwani hukuja duniani kutafuta utajiri, bali kuishi kwa kufanya kazi unayoipenda sana, inayokupa furaha na amani bila kujali maslahi, heshima au umaarufu kutoka kwenye kazi hiyo.

Kwakuwa kazi hii unaipenda, utaifanya kwa ufanisi mkubwa sana, na ndipo utajiri utakapokuja. Kanuni ya maisha kuhusu utajiri inaanza na kufanya kazi inayokupa furaha na amani na ndipo utajiri unafuata, haianzi na utajiri na ndipo furaha na amani vipatikane. Kama huamini, wachunguze matajiri unaowafahamu, ambao walipata utajiri ili uwape furaha na amani, utagundua kwamba, hawana furaha wala amani. Kwa upande wa pili wa shilingi, wale matajiri ambao, utajiri wao ulikuja kupitia kwa kufanya kazi inayowapa furaha na amani, utagundua kwamba wana furaha na amani kubwa sana.

Swali lililoulizwa hapo juu linasema, je, tahajudi huleta utajiri? Kama utajiri ni kupata furaha na amani ya nafsi, jibu ni ndiyo. Hii ni kwa sababu, tahajudi hukusaidia au kukufundisha namna bora kabisa ya kupumzisha akili na mwili na hivyo kuwa mtu mwenye furaha na amani. Kumbuka, ukishakuwa mwenye furaha na amani, wewe tayari ni tajiri wa mali pia.


Tahajudi ina madhara yoyote?

Kwa watu wenye matatizo ya kifafa, matatizo makubwa ya moyo au wenye matatizo ya akili, tahajudi inaweza kuwaumiza wasipokuwa waangalifu, ingawa kwa upande mwingine, tahajudi ni tiba/dawa kwao. Hivyo, wanashauriwa wachague tahajudi ambayo haitawaletea matatizo.

Ni vizuri wakajaribu aina tofauti tofauti ya tahajudi, halafu wakaangalia ni ipi inawasumbua na ni ipi inawapa nafuu. Wakishapata inayowapa nafuu, ni vizuri wakaendelea kuifanya mara kwa mara. Baada ya muda, watagundua kwamba, matatizo yao ya akili, moyo au kifafa yamepungua kwa kiwango kikubwa sana au yameisha kabisa.

meditation-techniques.jpg


Jinsi ya kufanya tahajudi:

Mbinu za kufanya tahajudi hutofautiana kutokana na kiwango cha uzingativu, uwezo wa kujenga taswira na namna mtu anavyoweza kukabili mawazo yanayomwingilia wakati anafanya tahajudi yake.

Baadhi ya mbinu hizi, humfanya mtu apotelee kwenye kile anachozingatia na kutoingiliwa kabisa na wazo lolote. Mbinu hizi ni rahisi mtu kujifunza mwenyewe, ingawa kuna baadhi zinahitaji awepo mwongozaji.


Hatua zinazotakiwa wakati unajiandaa kufanya tahajudi ni kama ifuatavyo:

1. Tafuta sehemu iliyotulia, isiyo na makelele. Kaa kwenye kiti au chini, au lala kitandani. Hakikisha huumii mahali popote. Legeza mwili wako pamoja na misuli yote ya mwili wako kwa kadri utakavyoweza.

2. Sahau matatizo yako yaliyopita, yaliyopo na yajayo. Sahau matatizo yako ya kazini au nyumbani. Jitahidi usifikirie chochote. kama kuna mawazo yataingia, usigombane nayo, usiyape muda na nafasi, wewe endelea na kile ulichoamua kukizingatia. Hakikisha uzingativu wako ni mkubwa. Pia kione hicho unachokizingatia kwa jicho lako la ndani, kijengee taswira kana kwamba unacho tayari au kana kwamba unakiona (unacho).

3. Ni muhimu sana kujali hisia zako wakati unafanya tahajudi. Kwa mfano, kama unafanya tahajudi ya kujenga nyumba. Hakikisha hiyo nyumba unaiona ilivyo, ingia ndani ya hiyo nyumba, sebuleni, chumbani, chooni, stoo, jikoni na sehemu ya kulia chakula (dining). Kila unapoingia, onyesha hisia zako, jione una furaha ndani mwako na ikiwezekana tabasamu, pia jione una amani ndani mwako. Ukweli ni kwamba, utakapokuja kujenga hiyo nyumba, zile hisia ulizokuwa unazionyesha wakati unafanya tahajudi, zitajitokeza au utaziona. Kama tahajudi yako ulikuwa unaifanya ukiwa na huzuni, hali hiyo itajitokeza baada ya kumaliza kujenga nyumba yako. Inaweza ikatokea baada tu ya kujenga nyumba yako, ndugu zako au wa mkeo wakajaa pale nyumbani, wakawa wanafanya vurugu ambazo zitakuletea huzuni na hivyo kuanza kujuta ni kwa nini umejenga hiyo nyumba.

Ukweli ni kwamba, tatizo siyo ndugu, tatizo ni wewe mwenyewe, ni hisia zako ulizokuwa unazionyesha wakati unafanya tahajudi yako ya kujenga nyumba. Na kama wakati unafanya tahajudi yako ulikuwa na hisia za furaha, hali hiyo pia itajitokeza baada ya kumaliza nyumba yako. Hata kama ndugu wa mkeo au mumeo watajaa pale nyumbani, vicheko, tabasamu na mambo mengine ambayo yatakupa furaha yatatamalaki pale nyumbani. Kwa hiyo, hisia ni muhimu sana wakati unafanya tahajudi.

4. Pumua kwa kuingiza pumzi ya kutosha mapafuni, halafu toa pumzi yote na kufanya kifua kiwe kama kitupu. Weka mawazo yako yote kwenye pumzi zako. Vuta pumzi kwa kina kiasi ili oksijeni iingie nyingi zaidi. Unapotoa pumzi unafanya msuli wa mapafu kujisafisha bila kukwazwa. Ni muhimu kuvuta na kutoa pumzi kwa kina angalau mara tatu kabla ya kuanza kufanya tahajudi yoyote.

5. Kila siku asubuhi baada tu ya kuamka na jioni au usiku baada ya watu wote kulala (au usiku wa manane), tenga dakika kumi na tano au zaidi kwa ajili ya kufanya tahajudi. Kuna wakati utakuta mwili hautaki, lakini jenga utashi mkubwa zaidi ya mwili hadi uzoee. Ukiahidiwa safari ya bure ya kwenda ulaya kutembea na ukaambiwa ndege itaondoka saa kumi usiku, nina uhakika ikifika saa saba utakuwa macho au yamkini unaweza usilale kabisa. Lakini pia ikitokea ukaahidiwa kutiwa au kumtia kila siku saa nane mchana na umpendaye sana, nina uhakika utafika kwenye eneo saa sita au saa saba mchana, hata chakula hutakumbuka. Ninakuomba ujenge utashi wa aina hii kwenye tahajudi.

6. Ukipata muda, kama huna kazi ya kufanya, ukiwa peke yako, ofisini, nyumbani, kwenye basi/daladala, kituoni, jaribu kufanya tahajudi. Mazoezi ya tahajudi hufanyika mahali popote.

7. kama ukifanya vizuri tahajudi, utahisi nafuu fulani kimwili au kiakili ama vyote. Utagundua kwamba, mwili hasa upande wa msukumo wa damu, utakuwa na mabadiliko.


Aina za tahajudi:

1. Tahajudi ya pumzi.

Ni kongwe zaidi. Ilianzia china na India. Ni tahajudi nzuri au muhimu kwa wale wanaoanza kujifunza.

Jinsi ya kuifanya: tafuta sehemu tulivu, kaa chini,kwenye kiti au lala kitandani (chali). Hakikisha mwili wako hauumii mahali popote, legeza misuli na viungo vyako vyote vya mwili, fumba macho yako. Vuta pumzi kwa kina halafu iruhusu itoke taratibu, wakati pumzi inatoka unaweza kutaja neno 'moja' au 'one' au neno lolote ambalo ni rahisi kwako. Usitaje neno hilo kwa mdomo, litaje kwa kulifikiri (kimoyomoyo) na baada ya muda utalizoea, litakuwa linakuja lenyewe.

Faida yake: husaidia kupumzisha mwili na akili.


2. Tahajudi ya mkono:

Hii inakuonyesha ni kwa jinsi gani mawazo yako yana nguvu zaidi kuliko mwili. Lakini pia inakuonyesha uhusiano uliopo kati ya mawazo yako na mwili wako.

Jinsi ya kuifanya: kaa kwenye kiti kisichokuwa na mkono. Miguu ikanyage chini na uweke mikono yako magotini (juu ya mapaja). Fumba macho, tulia, usiwaze kitu chochote, mawazo yakija usishindane nayo, usiyape nafasi wala muda, wewe endelea kutulia.

Ukiwa katika hali ya kupumzika na kufumba macho, chagua kati ya mkono wako wa kulia au kushoto na kupeleka mawazo (ufahamu) wako hapo. Peleka ufahamu wako kwenye mkono uliouchagua (mfano wa kulia). Fahamu kuwa sasa unaufahamu mkono wako wa kulia, yaani unauona kwa macho ya mawazo yako (kumbuka mawazo yetu yana macho, yanaweza kuona kitu hata kama hakipo mbele yetu).

Kwa kutumia macho ya mawazo yako, kitazame kiganja chako cha mkono wa kulia, kifahamu kabisa jinsi kilivyo huku ukiwa umefumba macho. Halafu kwa macho ya mawazo yako, itazame damu inavyozunguka kwenye mkono na kiganja chako, endelea kukitazama kiganja cha mkono huo wa kulia, kitazame kwa mbele na nyuma (ndani na nje). Halafu itazame damu inayotiririka ndani ya kiganja hicho. Wakati unaendelea kukitazama kiganja chako kwa macho ya mawazo yako, kuna mawazo yanapita kwenye ufahamu wako na kukuondoa kwenye uzingatifu wako. Usijaribu kushindana na mawazo hayo, yaache, bali endelea kuweka nguvu yako kwenye kiganja na damu inayotiririka ndani ya kiganja. Endelea kukitazama kiganja chako tena na tena na tena. Sasa hama kwenye kiganja na kitazame kidole gumba cha mkono wako, endelea kukitazama na baada ya muda, hamisha ufahamu wako na kukiona kidole cha pili, cha tatu, cha nne na cha tano yaani cha mwisho. Baada ya hapo, hamisha mawazo yako na kutazama katikati ya paji lako la uso, ni wazi unafahamu vizuri jinsi paji lako la uso lilivyo, endelea kulitazama kwa muda. Jaribu kukadiria umbali uliopo kati ya paji lako la uso na kiganja chako.

Baada ya hapo, endelea kukitazama kiganja chako kwa ndani, ione damu inayotiririka kwenye kiganja chako, tumia muda kidogo kuiangalia. Halafu angalia kiganja chako kwa juu(nje), kione vizuri jinsi kilivyo, peleka ufahamu wako kwenye kidole gumba, kidole kinachofuata, yaani cha pili, cha tatu, cha nne na cha tano. Peleka ufahamu wako kwenye paji lako la uso, endelea na zoezi hili kama ilivyoelezwa hapo juu. Baada ya muda, kama umejenga uzingativu wa kutosha kwa kufuata maelekezo, utaona mkono wako umeanza kupanda wenyewe. Na kama utaendelea kufanya zoezi hili, mkono wako utapanda na kugusa paji lako la uso. Na kama utaendelea kufanya, mkono utashuka wenyewe baada ya kugusa paji lako la uso na kutelemka chini mpaka kwenye paja lako na ukiendelea utapanda tena na kushuka tena.

Faida yake: husaidia kupumzisha mwili na akili, husaidia kutuliza maumivu ya mwili, husaidia kujenga uzingativu, n.k.

3. Tahajudi ya mshumaa.

Jinsi ya kuifanya: Tayarisha mshumaa na kiberiti. Kaa chini au kwenye stuli. Weka mshumaa wako mbele yako kwenye stuli au kitu chochote ili mradi uwe usawa wa macho yako. Uwashe na uanze kuuangalia kwa kuukazia macho bila kupepesa kope. Ukishindwa, pepesa kidogo halafu endelea kuuangalia bila kupepesa tena. Endelea kuuangalia kwa muda usiopungua dakika 10 au 30.

Pia, unaweza kutumia moto huu wa mshumaa kuchoma mambo ambayo uliambiwa huwezi. Mfano, uliambiwa huna akili, hivyo, chukua hili neno na lichome kwenye moto huu wa mshumaa. Kama utakuwa umezingatia sana, utaona moto wa mshumaa ukiongezeka au ukibadilika rangi.

Tahadhari: wakati unachoma, usije ukachoma yale mambo mazuri uliyoambiwa.

4. Tahajudi ya mtoto wa ndani:

Hii ni kwa ajili ya kufuta mambo ambayo uliambiwa huwezi. Huwa tunasema, ongea na mtoto wako wa ndani.

Jinsi ya kufanya: kaa chini, kwenye kiti au lala kitandani (chali). Jenga taswira ya picha yako ulipokuwa mtoto. Jione mahali ulipokuwa kama ni nyumbani au shuleni. Angalia yale maeneo ambayo unayakumbuka na ambayo uliambiwa huwezi. Kila unapofanya chagua eneo moja moja ambalo unakumbuka uliambiwa hufai. Baada ya kutengeneza taswira ya mtoto huyo ambaye ni wewe, rudi kwako sasa ukiwa mtu mzima. Anza kuongea na huyo mtoto ambaye ni wewe pia. Mwambie kwamba, uliambiwa huna akili (kama uliambiwa huna akili) na wewe ukaamini kwa sababu ya utoto, lakini sasa umekua, fahamu ukweli huu kwamba wewe una akili sana sawa na mtu yoyote. Endelea kurudiarudia hayo maneno kwa muda wa dakika tano au zaidi.

Unapoongea na mtoto wako wa ndani mara kwa mara, pamoja na kukupa faida zingine za tahajudi, itakusaidia pia kukuwezesha kujiamini katika hayo maeneo ambayo uliambiwa huwezi au hufai.

5. Tahajudi ya namba:

Hapa, unatakiwa kuhesabu namba kinyumenyume huku ukiwa umefumba macho. Unaweza ukaanzia 100, 99, 98, 97, 96, mpaka 1, au unaweza kuanzia 200, 198, 196, 194, 192, mpaka 2. hakikisha wakati unahesabu namba hizi hukosei, na ikitokea ukakosea namba yoyote hata kama umekaribia kumaliza, itakulazimu kuanza upya. Tahajudi hii ni nzuri sana kwa kurejesha kumbukumbu, ingawa pia ina faida nyingine.
225px-Maharishi_Huntsville_Jan_1978A  .JPG


6. Tahajudi ya maua:

Tafuta ua la rangi nyekundu, kijani, njano au nyeupe. Hapa usifumbe macho. Liweke mbele yako na uliangalie kwa kulikazia macho bila kupepesa kope. Hakikisha mawazo, fikra na uzingativu wako wote unaupeleka kwenye ua hilo. Lakini kama una bustani ya maua, unaweza kwenda kukaa bustanini na kuanza kuyaangalia maua hayo kwa kuyakazia macho huku mawazo na uzingativu wako wote ukiwa kwenye ua ulilolichagua.

7. Tahajudi ya rangi:

Hii hutumika kwa ajili ya kujiponya kwani kila rangi inatibu magonjwa fulani kwenye mwili wako kama utaiangalia kwa muda mrefu au kama utavaa nguo ya rangi hiyo. Unaweza ukatumia tunda lenye rangi husika, mfano matunda damu au nyanya kuwakilisha rangi nyekundu.

8. Tahajudi ya sauti:

Hii inahusisha kutaja neno kimoyomoyo ambalo ukishalizoea neno hili itafika mahali huhitaji kulitaja ila utalisikia neno hilo likijitaja lenyewe. Unaruhusiwa kuchagua neno lolote ambalo ndiyo litakuwa nguzo yako ya kujenga uzingativu. Mfano, amani, mungu, furaha n.k.

9. Tahajudi ya kusogea:

Hii huhusisha kuikabili ardhi kama kitovu cha nguvu, huhusisha kusogea kwa aina fulani. Watu wengi hupenda kuifanya usiku.

10. Tahajudi ya kujikagua:

Huhusisha kujikagua baadhi ya maeneo yako ya mwili kwa kutumia macho yako ya akili.

11. Tahajudi ya ukuaji:

Ni tahajudi ambayo imefanyiwa utafiti mwingi sana wa kisayansi na kuthibitishwa kwamba, tahajudi husaidia mwili, akili na hisia, pia ni rahisi kujifunza. Katika tahajudi hii, kila mmoja hupewa neno ambalo hatakiwi kumpa mtu mwingine. Neno unalifanyia kazi ili kujenga uzingativu.

Hizi ni baadhi tu ya tahajudi ambazo huwa zinatumika mara kwa mara. Unachotakiwa ni kuwa mbunifu ili na wewe ubuni tahajudi ya kwako (za kwako) na kuzipa majina yoyote unayotaka. Kwenye maisha hasahasa katika tahajudi, hutakiwi kuwa kasuku wa kutumia tahajudi zilizobuniwa na watu wengine, fanya kila uwezalo kubuni tahajudi yako hata kama ni ndogo kiasi gani ili mradi inakusaidia kukupa uzingativu. Kumbuka kwamba, tahajudi inaweza kufanywa muda wowote na mahali popote.

Usikubali mwili ukutawale kwa kukuambia umechoka na hivyo nenda kalale. Hivi, kuna kitu kinaitwa kuchoka ambako kutakufanya ushindwe kufanya tahajudi? Kama jibu ni ndiyo, jiulize swali hili: umetoka kazini, umechoka sana na unataka kwenda kulala hata kuoga huwezi, halafu kabla hujanyanyuka kwenda kulala, ukamuona nyoka anaingia ndani je, utaendelea kulala au utanyanyuka ili umpige nyoka huyo? Bila shaka, usingizi na uchovu wote utaisha. Unaonaje kama tahajudi itachukua nafasi ya nyoka? Inawezekana! Maelezo haya yanakuonyesha kwamba, hakuna kitu kinachoitwa kuchoka ila wewe unasemaje!

3 hours of Meditation Music




Kwa leo naishi hapa, kama kuna mwenye changamoto, namkaribisha ili tupate kuelimishana.....


Navutiwa sana na huu Uzi, niliwai kuwaona jamaa pale coco beach Lakin skujua kiundani Leo nmepata picha kwa ukubwa sana
 
Nilisoma kidogo mambo ya Budhism nao hutumia sana hii kitu japo ukiitumia vibaya ni hatari maana ukishazama kwenye maombi haya waweza pata nguvu za ajabu za kufanya jambo fulani ambalo katika hali ya kawaida huwezi kufanya.

Ni nguvu ambayo kila mtu anayo kama alivyowahi kusema Mpwa wangu Pasco na ndio maana kuna wengine wanaonekana kuwa na supernatural powers jao hawana asili ya kuwa nazo....

Asante sana Mpwa wangu Mtambuzi ila utakapoiweka vizuri nitaomba urekebishe pale mwanzoni kuwa tahajudi ni limetokana na neno la kiingereza linaloitwa 'meditation'.

Nafikiri ulilenga kutueleza maana ya neno Tahajudi kwa Kiingereza na sio kuwa limetokana na Neno Meditation. Otherwise, the article is Great!!!
Kwani hata hawa ma-prophet tunaowaona wanazuka siku hizi na kutenda miujiza nawao walipitia huko?
 
Ndiyo left back gunner nilipoona neno tahajjud linatumika hapa nikapata na hofu tunaanza kutaka kutohoa vibaya lugha, isije kuleta tatizo kwa wanalugha wanaochipukia katika kupata mzizi wa maana ya jambo.

Ninadhani tutohoe tu meditation kuwa miditisha... Halafu kwa nini tusitohoe moja kwa moja kutoka kwenye maneno ya kihindi? Hilo neno tahajudi kwa maana ya kiingereza kutajwa ni namna ya 'concetration' basi tuseme ni 'dharaa/dharana'...

Kitu cha kukaziwa fahamu huitwa 'tratak' na bidii ya yake kuitwa dharana-- ilivyo kimaksudio , jitihada ni kubadili uwezo wa akili kupitia kwenye 'jicho la tatu' ambalo ni lensi ya utambuzi iliyo ni tezi ya Pineli ili hiyo kuanza kudaka habari na taarifa hata zilizo nje ya fahamu ya kuona kwa wakati ama hata nje ya mzingo wa uono wa mahala afanyiapo mwenye kufanya hiyo.
Asante mkuu
 
Machale..... ndio maana naona wanaofanya meditation kama wanga.
Kuna jamaa yangu Rodrick Ntepa aliniambia kaanzisha dini yake inaitwa WANAZARAYO. Na yeye ndiye Mungu wa dini hiyo. Akanifundisha ku meditate. Tulimeditate kwa masaa matatu none stop. Yeye akaniambia alishawahi kumeditate hadi akawa kama mfu. Na siku hiyo alikuwa ameenda kwenye mbingu ya saba ambako anakaa Mungu wa Wakristo.
Ikawaje?
 
Tahajudi (Meditation) ni mmoja wa sehemu nane za Patanjali Yog. Pia inajulikana kwa maneno Ashtang Yog. Hizo sehemu nane ni kama ifuatavyo: Yam, Niyam, Asan, Pranayam, Pratyahar, Dharana, Dhyan, Samadhi. Tahajudi ni kama Pratyahar ikiendelea kwenye stages zifuatazo, kufika kwenye stage ya mwisho Samadhi.
 
Tahajudi (Meditation) ni mmoja wa sehemu nane za Patanjali Yog. Pia inajulikana kwa maneno Ashtang Yog. Hizo sehemu nane ni kama ifuatavyo: Yam, Niyam, Asan, Pranayam, Pratyahar, Dharana, Dhyan, Samadhi. Tahajudi ni kama Pratyahar ikiendelea kwenye stages zifuatazo, kufika kwenye stage ya mwisho Samadhi.

Ningependa kujuzwa zaid kuhusiana na hizi zote
 
Tahajudi (Meditation) ni mmoja wa sehemu nane za Patanjali Yog. Pia inajulikana kwa maneno Ashtang Yog. Hizo sehemu nane ni kama ifuatavyo: Yam, Niyam, Asan, Pranayam, Pratyahar, Dharana, Dhyan, Samadhi. Tahajudi ni kama Pratyahar ikiendelea kwenye stages zifuatazo, kufika kwenye stage ya mwisho Samadhi.

Ningependa kujuzwa zaid kuhusiana na hizi zote
 
Unaposema furaha na amani ni utajir,nakataana na ww...utajir ni ukwasi.full stop,hamna tafsir nyngne
 
Tahajudi (Meditation) ni mmoja wa sehemu nane za Patanjali Yog. Pia inajulikana kwa maneno Ashtang Yog. Hizo sehemu nane ni kama ifuatavyo: Yam, Niyam, Asan, Pranayam, Pratyahar, Dharana, Dhyan, Samadhi. Tahajudi ni kama Pratyahar ikiendelea kwenye stages zifuatazo, kufika kwenye stage ya mwisho Samadhi.

Naja pm
 
Tahajudi (Meditation) ni mmoja wa sehemu nane za Patanjali Yog. Pia inajulikana kwa maneno Ashtang Yog. Hizo sehemu nane ni kama ifuatavyo: Yam, Niyam, Asan, Pranayam, Pratyahar, Dharana, Dhyan, Samadhi. Tahajudi ni kama Pratyahar ikiendelea kwenye stages zifuatazo, kufika kwenye stage ya mwisho Samadhi.

Nashindwa kuja pm em naomba uje ili nipate huo wasaa
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom