Tahadhari ya mvua kubwa kwa siku tano kwa mikoa ya Kanda ya Ziwa yatolewa

Influenza

JF-Expert Member
Jul 1, 2018
1,442
3,353
Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini imetoa utabiri wa hali ya hewa hatarishi kwa siku tano ambapo mvua kubwa inatarajiwa katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Mwanza, Geita, Kagera, Mara pamoja na Magharibi mwa mkoa wa Simiyu.

Mamlaka hiyo imesema uwezekano wa kutokea kwa mvua hizo ni wa wastani huku kiwango cha athari kinachoweza kutokea pia ni cha wastani.

Athari zinazoweza kujitokeza ni pamoja na baadhi ya makazi kuzungukwa na maji, ucheleweshwaji wa usafiri na kusimama kwa muda kwa baadhi ua shughuli za kiuchumi na kijamii.


1.jpg
 
Kwahiyo tutakuwa na foleni kwa siku tano? Maana kwa foleni za jana usiku na leo asubuhi hapa Mwanza sio poa kabisa. Utafikiri tupo Dar.
 
Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini imetoa utabiri wa hali ya hewa hatarishi kwa siku tano ambapo mvua kubwa inatarajiwa katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Mwanza, Geita, Kagera, Mara pamoja na Magharibi mwa mkoa wa Simiyu.

Mamlaka hiyo imesema uwezekano wa kutokea kwa mvua hizo ni wa wastani huku kiwango cha athari kinachoweza kutokea pia ni cha wastani.

Athari zinazoweza kujitokeza ni pamoja na baadhi ya makazi kuzungukwa na maji, ucheleweshwaji wa usafiri na kusimama kwa muda kwa baadhi ua shughuli za kiuchumi na kijamii.


View attachment 1248131
Taarifa kama hii ikishatolewa kie kitengo cha Maafa kilitakiwa kiwe na timu ambayo ishajiandaa kwa lolote katika hiyo miko na tusisubiri mpaka iwe ishatokea, pia kuna umuhimu sana watu kupewa elimu juu ya mambo ya majanga kama haya ya Mvua na namna watakavyojinasua, pia kuwe na Collection point ambapo raia wakiona hali ni tete wakimbilie huko mpaka hali itakapotengaa, hii itasaidia sana kupunguza maafa, huu ndio muda muafaka wa kile Kitengo cha Majanga kuwa alert
 
Wanasema hivyo baada ya kuona mwanza leo siku ya3 mvua inamwagika
Hakunaga mamtu maongo kama haya yanayojiita matabiri ya hali ya hewa
 
Mamlaka ya Hali ya Hewa nchini imetoa utabiri wa hali ya hewa hatarishi kwa siku tano ambapo mvua kubwa inatarajiwa katika baadhi ya maeneo ya mikoa ya Mwanza, Geita, Kagera, Mara pamoja na Magharibi mwa mkoa wa Simiyu.

Mamlaka hiyo imesema uwezekano wa kutokea kwa mvua hizo ni wa wastani huku kiwango cha athari kinachoweza kutokea pia ni cha wastani.

Athari zinazoweza kujitokeza ni pamoja na baadhi ya makazi kuzungukwa na maji, ucheleweshwaji wa usafiri na kusimama kwa muda kwa baadhi ua shughuli za kiuchumi na kijamii.


View attachment 1248131
Mamlaka itoe mwongozo wa kuwa tunajiandaa,vipeperushi vya picha nk.
Pongezi kwa kutoa taarifa mapema.
 
Taarifa kama hii ikishatolewa kie kitengo cha Maafa kilitakiwa kiwe na timu ambayo ishajiandaa kwa lolote katika hiyo miko na tusisubiri mpaka iwe ishatokea, pia kuna umuhimu sana watu kupewa elimu juu ya mambo ya majanga kama haya ya Mvua na namna watakavyojinasua, pia kuwe na Collection point ambapo raia wakiona hali ni tete wakimbilie huko mpaka hali itakapotengaa, hii itasaidia sana kupunguza maafa, huu ndio muda muafaka wa kile Kitengo cha Majanga kuwa alert
Point nzuri na ndivyo inapaswa kuwa hivyo ila bahati mbaya kwa nchi yetu hii huwa wanawaachia mamlaka ya hali ya hewa kila kitu ikiwemo kutoa taadhari wakati mamlaka ya hali ya hewa ikishatoa taarifa kila wizara na idara zake zinapaswa kuwa na kitengo cha "early warning" ambapo wanakuwa wanajiandaa na namna ya kupambana na athari zozote zitakazojitokeza mfano watu kama TANROAD na TARURA nao wanaangalia namna gani ya ku-deal na barabara zao, pia watu wa kilimo nao wanajiandaa pia endapo itatokea uharibu wa mashamba na kitengo cha maafa hali kadhalika pamoja na wananchi wote kwa ujumla kuwa tayari
 
Back
Top Bottom