Pyaar
JF-Expert Member
- Feb 11, 2018
- 15,339
- 75,510
Duh!Hadithi yako ni kama yangu.
Nakumbuka mwaka fulani hivi majuzi nilinunua simu ya mkononi.
Ilikua ni Samsung Galaxy s6 edge. Nilinunua kwa sh 370,000.
Nilikaa nayo miezi mitano ndipo nilipofuatwa na askari kuwa ile simu ni ya wizi. Askari hao walikuja pamoja na yule dada aliyeniuzia. Tukaenda mpaka Osterbay kuandika maelezo.
Sikurudishiwa hata cent tano
Nilichogundua ni kuwa yule dada anashirikiana na wale jamaa kutapeli watu.
Yeye anauza alafu baada ya muda wanaifuata simu yao. Kwakua hakuna mauziano halali ya simu za mkononi, basi unakosa cha kujitetea