svc
JF-Expert Member
- Jun 27, 2012
- 429
- 157
Anaitwa "Glenn Roseberry" na anadai ni Mmisionari kutoka Tennessee Marekani na kwa sasa anaishi na kufundisha Arusha, pamoja na kufanya kazi zake nyingine Kenya.
Aliona tangazo langu la pikipiki kwenye internet akawasiliana ili ainunue. Leo kafika nyumbani anadai kutoka Arusha, akasema anaijaribu pikipiki. Akaondoka nayo yeye na jamaa fundi pikipiki anaitwa Shila wa Kawe. Walijaribu kuiiba pikipiki kwa kukimbia nayo wakidai wanai-test.
Hapohapo leo hiihii akaniahidi kwa kunipigia simu na kwa email kuinunua kwa ku-transfer pesa kutoka akaunti yake Tennessee kwenda kwenye akaunti yangu Marekani, na ningezipata baada ya masaa mawili ili nimruhusu aondoke na pikipiki. Kumbe ni uwongo mtupu, lakini cha ajabu sana kila kitu kuanzia jina la mfanyakazi wa benki, namba ya simu ya benki, email, anwani ya benki yake Tennessee na kila kitu nime-confirm ni sahihi. Hadi mfanayakazi wa benki ananipigia simu kunihakikishia kuwa anahamisha pesa, na kunitumia email kwa anwani pepe ya benki halali ya Marekani.
Lakini kumbe yote ni danganya toto. Wanadai wanipe confirmation ya bank wire transfer nimruhusu achukue pikipiki. Lakini confirmation ya wire transfer kamwe siyo ushahidi wa malipo. Ni ajabu sana kwa kweli. Mzungu mzee wa makamo wa Kimarekani anajaribu kuiba pikipiki Dar kwa kutapeli, na hadi kukimbia nayo? Duh! Dunia imekwisha!
Website ya benki: https://www.themetropolitanbank.com/
Glenn Roseberry (na ni mwenyewe huyo mzee kwenye picha, amini usiamini): https://www.google.com/#q=glenn+roseberry
Aliona tangazo langu la pikipiki kwenye internet akawasiliana ili ainunue. Leo kafika nyumbani anadai kutoka Arusha, akasema anaijaribu pikipiki. Akaondoka nayo yeye na jamaa fundi pikipiki anaitwa Shila wa Kawe. Walijaribu kuiiba pikipiki kwa kukimbia nayo wakidai wanai-test.
Hapohapo leo hiihii akaniahidi kwa kunipigia simu na kwa email kuinunua kwa ku-transfer pesa kutoka akaunti yake Tennessee kwenda kwenye akaunti yangu Marekani, na ningezipata baada ya masaa mawili ili nimruhusu aondoke na pikipiki. Kumbe ni uwongo mtupu, lakini cha ajabu sana kila kitu kuanzia jina la mfanyakazi wa benki, namba ya simu ya benki, email, anwani ya benki yake Tennessee na kila kitu nime-confirm ni sahihi. Hadi mfanayakazi wa benki ananipigia simu kunihakikishia kuwa anahamisha pesa, na kunitumia email kwa anwani pepe ya benki halali ya Marekani.
Lakini kumbe yote ni danganya toto. Wanadai wanipe confirmation ya bank wire transfer nimruhusu achukue pikipiki. Lakini confirmation ya wire transfer kamwe siyo ushahidi wa malipo. Ni ajabu sana kwa kweli. Mzungu mzee wa makamo wa Kimarekani anajaribu kuiba pikipiki Dar kwa kutapeli, na hadi kukimbia nayo? Duh! Dunia imekwisha!
Website ya benki: https://www.themetropolitanbank.com/
Glenn Roseberry (na ni mwenyewe huyo mzee kwenye picha, amini usiamini): https://www.google.com/#q=glenn+roseberry