TAHADHARI: Mvua kubwa kunyesha Arusha Kilimanjaro na Manyara

Hivi punde

JF-Expert Member
Apr 1, 2017
2,554
8,552
Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) imesema kuanzia usiku wa leo Machi 1, 2018 hadi kesho Machi 2, 2018 kutakuwa na vipindi vya mvua kubwa katika maeneo mengi ya nyanda za Juu Kaskazini Mashariki.


Taarifa ya TMA iliyotolewa leo imebainisha maeneo hayo kuwa ni mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro ambapo mvua hizo itazidi milimita 50 ndani ya saa 24 huku ilieleza hali hiyo inatokana na kuimarika kwa ukanda wa mvua.


TMA imewashauriwa wakazi wa maeneo husika kuchukua tahadhari stahiki na kuendelea kufuatilia taarifa pamoja na tahadhari zinazotolewa.
 
Mh,,mi naomba tu inyeshe usiku,maana wengine vibarua vyetu nivya nje
 
Back
Top Bottom