Page 94
JF-Expert Member
- Oct 22, 2015
- 5,205
- 15,162
Wasalaam!
Wakati zoezi la kumuaga aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndg John Pombe Magufuli likiendelea mkoani Dar es Salaam ni vema kila anayepanga kwenda kutoa heshima za mwisho achukue tahadhari zifuatazo.
a) Jitahidi uvae barakoa. Inakupasa kufahamu ya kuwa unaenda kwenye msongamano mkubwa wa watu na ukweli ni kuwa gonjwa hatari la COVID-19 lipo. Hivyo, chukua tahadhari kwa kuvaa barakoa yako ili kupunguza uwezekano wa kuambukizwa ama kuwaambukiza wengine..
b) Kama una shinikizo la juu la damu na matatizo mengine ya upumuaji kama Athma, pumu, kifafa, basi nakushauri ubaki nyumbani. Kumuona marehemu amelala inaweza kukusababisha mshtuko na kuzirai. Na huenda ikakusabisha matatizo mengine zaidi. Vema ubakie tu nyumbani kufatilia kwenye luninga.
c) Hakuna sababu yeyote ya kumpeleka mtoto mdogo kwenye shughuli kama hiyo. Kwanza ni kwa ajili ya usalama wake. Hewa ni nzito, jua ni kali na hakuna mantiki yeyote ya kumuonesha marehemu. Taswira ya marehemu hubaki sana kwenye kumbukumbu zao na siyo afya kwa ukuaji wake. Mtoto anaweza pia kukupotea. Ikakusababishia usumbufu zaidi. Watoto wabaki nyumbani.
d) Vaa viatu vya kufunika uendapo huko. Usipendelee kuvaa Sandals. Kuvaa viatu inakupa nafasi ya kutembea kwa uangalifu. Sandals zinaweza kukatika na kusababisha utembee peku. Kwa kuwa watu ni wengi, mnapotembea ni rahisi sana sandals kukanyagwa na kusababisha usumbufu.
e) Tunza vitu vyako kwa umakini. Kuibiwa na kupoteza mali ni jambo la kawaida katika makutano ya watu wengi kiasi hicho. Inaweza kukuletea hasara inayoepukika. Usibebe vitu vyenye ncha kali au vifaa vya moto. Huenda usiwe na nia mbaya lakini ikakugharimu.
f) Fuata maelekezo yote utakayopewa na wana usalama na waongozaji. Njia gani ya kupita, tumia muda mchache kutoa heshima. Ikibidi isizidi sekunde 10. Kama ni ishara ya msalaba, ifanye ukiwa unatembea. Kuchukua muda inasabisha usumbufu na ucheleweshaji.
g) Umalizapo kuaga, rudi nyumbani haraka na kaendelee na majukumu mengine ili kuwapa wengine fursa ya kuaga.. Haina haja ya kuendelea kubaki uwanjani na maeneo jirani.
Mungu atusimamie.
Wakati zoezi la kumuaga aliyekuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Ndg John Pombe Magufuli likiendelea mkoani Dar es Salaam ni vema kila anayepanga kwenda kutoa heshima za mwisho achukue tahadhari zifuatazo.
a) Jitahidi uvae barakoa. Inakupasa kufahamu ya kuwa unaenda kwenye msongamano mkubwa wa watu na ukweli ni kuwa gonjwa hatari la COVID-19 lipo. Hivyo, chukua tahadhari kwa kuvaa barakoa yako ili kupunguza uwezekano wa kuambukizwa ama kuwaambukiza wengine..
b) Kama una shinikizo la juu la damu na matatizo mengine ya upumuaji kama Athma, pumu, kifafa, basi nakushauri ubaki nyumbani. Kumuona marehemu amelala inaweza kukusababisha mshtuko na kuzirai. Na huenda ikakusabisha matatizo mengine zaidi. Vema ubakie tu nyumbani kufatilia kwenye luninga.
c) Hakuna sababu yeyote ya kumpeleka mtoto mdogo kwenye shughuli kama hiyo. Kwanza ni kwa ajili ya usalama wake. Hewa ni nzito, jua ni kali na hakuna mantiki yeyote ya kumuonesha marehemu. Taswira ya marehemu hubaki sana kwenye kumbukumbu zao na siyo afya kwa ukuaji wake. Mtoto anaweza pia kukupotea. Ikakusababishia usumbufu zaidi. Watoto wabaki nyumbani.
d) Vaa viatu vya kufunika uendapo huko. Usipendelee kuvaa Sandals. Kuvaa viatu inakupa nafasi ya kutembea kwa uangalifu. Sandals zinaweza kukatika na kusababisha utembee peku. Kwa kuwa watu ni wengi, mnapotembea ni rahisi sana sandals kukanyagwa na kusababisha usumbufu.
e) Tunza vitu vyako kwa umakini. Kuibiwa na kupoteza mali ni jambo la kawaida katika makutano ya watu wengi kiasi hicho. Inaweza kukuletea hasara inayoepukika. Usibebe vitu vyenye ncha kali au vifaa vya moto. Huenda usiwe na nia mbaya lakini ikakugharimu.
f) Fuata maelekezo yote utakayopewa na wana usalama na waongozaji. Njia gani ya kupita, tumia muda mchache kutoa heshima. Ikibidi isizidi sekunde 10. Kama ni ishara ya msalaba, ifanye ukiwa unatembea. Kuchukua muda inasabisha usumbufu na ucheleweshaji.
g) Umalizapo kuaga, rudi nyumbani haraka na kaendelee na majukumu mengine ili kuwapa wengine fursa ya kuaga.. Haina haja ya kuendelea kubaki uwanjani na maeneo jirani.
Mungu atusimamie.