Tahadhari kwa wamiliki wa magari: Ukiwa kwenye taa au foleni funga vioo, inasemekana kuna Vibaka wenye visu vikali wanapora pesa kimya kimya

Kukabiliana na huyo mtu ni rahisi mno ila:
- lazima uwe na ujuzi wa mapambano hasa ya michezo ya visu kwani nae anaeiba kwa kisu hujui uwezo wake upoje,ukiwa mjuzi kwa jinsi alivyokishika na kukutaiti nacho utajua ukubwa wa hatari wa mpinzani wako.

- wewe unaetaka kumtoa mkeo sadaka sitisha hilo zoezi utaachiwa mzoga hapo toka purukushani za kufungua mlango wa nyuma kumkabili mtu wa nje mjuzi utakuwa umechelewa sana.

Ushauli.

- kama likizo hii ya corona umeamua kudeal na hao watu basi tafuta gari mbili mkeo aendeshe ya mbele kwenye mataa wewe kaa ya nyuma na uwe na bastola akimtait mkeo unaanza kumvunja kiuno then unamalizia kumwaga ubongo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizo nyasi kwenye lami wakati huo utaziona wapi kakutaiti ikumbukwe kisu ni kidogo halafu kikali akigusa kidogo tu huna koromeo!
Au unazani kisu anakibeba begani kama shoka?
Acha UZEMBE wewe khaaa
 
Mimi walishanibananisha kimya kimya na wembe
Siku izi uswahilini Kuna mbinu nyingine imebuniwa ya kukaba wanakutaiti na Bomba la sindano, ukifanya masikhara anakudunga sindano yenye mchanganyiko wa madawa ya kulevya na HIV. Alafu Hao wakabaji wamepitia maswala ya ngumi, sio watoto wa mama kama watu wa bushi wanavyofikiri. Mtu anaekaba full kifua kama mcheza mieleka. Kama mjini watu wanafikiri wakabaji unaweza kupambana toka kijijini alafu uje utembee mida ya usiku sehemu korofi kama Keko, watakuja kutoa ushahidi apa Jamii forum

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hizo nyasi kwenye lami wakati huo utaziona wapi kakutaiti ikumbukwe kisu ni kidogo halafu kikali akigusa kidogo tu huna koromeo!
Au unazani kisu anakibeba begani kama shoka?
Hata kama kingekuwa kikali kuliko kiwembe. Nitamwonyesha cha mtema kuni. Aonee kina mama na wanaume legelege siyo mimi.
 
ONYO
ukiingia kwenye target kuwa mpole
unaweza kukabwa na hospital unakaa wiki
kuwa makini usiingie kwenye target


NB wakabaji. wenyewe wakiingia kwenye target wanakabwa hata wanajeshi wanakabwa
 
Nimesikia kuna Clip inazunguka kwenye mitandao kwamba; Kuna aina mpya ya uporaji Kwa madreva wenye magari madogo wakiwa kwenye foleni au taa!
Mashuhuda wanasimulia kwamba Mwizi anapokuona umeshusha vioo, ukiwa peke ako kwenye foleni au taa (makutano junction)!

Anakuvizia Kama wapitavyo Machinga anajibana kama vile mshikaji huku mikono yake ikiwa ndani tayali anaanza kukutomasa Kwa kisu kikali sana huku akikuomba utoe Pesa zote umpe!

Inadaiwa style ya vibaka hao wanayotumia haiwezi kushitukiwa kirahisi na watu wanaokuzunguka kwasababu anakuja kama mshikaji, na akimaliza kukupora anakwambia "Siku ingine kwenye foleni au taa usiache kioo wazi"

Halafu anapokuaga anakuambia "NITAKUPIGIA TUONGEE VIZURI"
Ili kuwahadaa wanaokuzunguka waone kama no mtu na mshikaji wake!

Wanaume Kwa wanawake wengi wanasimulia kuporwa Kwa style hiyo mpya!
Mmoja anasadikiwa kuwepo maeneo ya taa za mnazi mmoja na pale BigBon

Hawajabahatika kupata PICHA yake lakini inadaiwa ni lijitu jeusi lenye sura ya kikauzu!

WITO;
  1. Polisi hususani Trafiki wanaongoza magari wasiruhusu wafanya biashara (machinga & ombaomba) kutembea kwenye foleni au taa
  2. Madreva wachukue tahadhari wapandishe vioo hasa wakiona wapo wenyewe.
  3. Ile sheria ya faini ya laki mbili Kwa mtu anaempa pesa ombaomba kwenye foleni iongezewe nguvu
NOTE; Sisi wenye ESCUDO Tutafte namna nyingine ya kujihami maana AC zetu ni za MAZABE!

NAMNA YA KUMKATA MTU HUYO

Wanaume Wa Dar; kama mkeo anafaham kuendesha mkabidhi aendeshe, halafu wewe jilaze siti ya nyuma kwenye foleni au taa mwambie mkeo ashushe vioo vya mbele tena kama ikiwezekana mwambie azuge kujipodoa na lips stick ili mwizi asogee, halafu ukisikia mazungumzo toka na panga Kwa mlango Wa nyuma usiulize na umuarest haraka iwekezekanavyo!

Mimi binafsi nimeaza operesheni hii tangu Jana sisubiri hadi Polisi waseme! Nitawapa mrejesho!
Wafanye yote ila wasiue watu wetu
 
Akiniwekea bastola atafanikiwa kunipora lakini siyo kisu. Niko ndani ya gari halafu yeye yuko nje aingize mikono yenye kisu ndani nimpe nilichonacho? Nyasi zitawaka moto!
Acha ngebe wewe. Wewe si jirani yangu uswaz lini ukawa na gari na bastola?

Mmegeuza jf kituo cha kupoozea makali ya maisha
 
hiii ni hatari sana kwani hakuna kitu kigumu kama kupambana na adui usiye mjua màana yy amekuwai lazima utaumia tu
 
Hizo nyasi kwenye lami wakati huo utaziona wapi kakutaiti ikumbukwe kisu ni kidogo halafu kikali akigusa kidogo tu huna koromeo!
Au unazani kisu anakibeba begani kama shoka?
Msela anasema atabeba panga na kujificha siti ya nyuma mkewe akiwa anaendesha mpe tahadhari atakuja kuua machinga!
 

Similar Discussions

15 Reactions
Reply
Back
Top Bottom