Tahadhari kwa BAVICHA kuelekea tarehe 23/07/2016

Salary Slip

JF-Expert Member
Apr 3, 2012
46,986
144,313
Napenda kuwatahadharisha vijana wa BAVICHA wanaopenda kuenda Dodoma(kama kweli dhamira hiyo ipo) kuwa makini na vijana wanaoambatana nao na hata wale watakaowakuta hapa Dodoma.Epukeni kabisa kuambatana na vijana msiowafahamu vizuri au kubeba vijana mradi tu wako teyari kwenda nanyi Dodoma.Bora mkaenda wachache waaminufu kuliko kundi kubwa lenye mamluku ndani yake.

Ninachokusudia kuwaonya vijana hawa wa BAVICHA ni uwezekano wa kujipenyeza mamluki/mapandikizi miongoni mwenu wenye silaha za jadi n.k, kwa lengo la kuonyesha mnapanga kufanya hujuma/uovu tofauti na ahadu yenu ya kutofanya mambo ya aina hiyo.

Mamluki hao wanaweza kabisa kujisalimisha na wakatoa maelezo ya kipropaganda kuwa walitumwa au walielekezwa kwenda Dodoma kufanya moja mbili tatu.Wanaweza hata kuwataja wasiohusika kwa lengo la kuwachafua.

Msisahau hii ni siasa na namalizia kwa kuwakumbusha msemo maarufu unaosema: "kwenye msafara wa mamba,hata kenge wamo."
 
Kitendo cha ukawa kwenda Dodoma kwa kile kinachoitwa kuisaidia polisi kuwakumbusha ccm utii wa sheria ni kipimo tosha cha wananchi kujua kama kweli serikali inakipendelea chama tawala kama ambavyo wapinzani wamekuwa wakidai na kulalamika au la! Haiwezekani tamko la mkuu wa nchi kwa vyama vya kisiasa lipuuzwe na chama kimoja.
 
akili za bavicha. wanashauriana kutenda jinai.

BAVICHA wanachofanya ni kama hiki.Mwisho wa siku haya weee

fearless-officer.jpg
 
Ninachokusudia kuwaonya vijana hawa wa BAVICHA ni uwezekano wa kujipenyeza mamluki/mapandikizi miongoni mwenu wenye silaha za jadi n.k, kwa lengo la kuonyesha mipanga kufanya hujuma/uovu tofauti na ahadu yenu ya kutofanya mambo ya aina hiyo.


Na nyongeza wa epuke kutembea na mabegi makubwa au ikiwezekana wawe na timu ya kisiri ya kusimamia taarifa za usalama wao behind za screen kwa kila maeneo wanayokwenda au kukaa.Dunia ya matumizi ya kisayansi a.k.a tehama/teknolojia ipewe kiupaumbe katika safari hiyo.
 
Napenda kuwashauri ndugu zangu BAVICHA, ni heri mara 100 muda na pesa watakazotumia huko Dodoma wangetumia kwa ajili ya kujiletea maendeleo yao binafsi kwa katika hali hiyo lolote linaweza kutokea. Kumbukeni kuwa pamoja na watu wengine pia atakuwepo huko rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na marais wataafu. Kwa maana hiyo ni kwamba, nguvu zote za kiwango chochote zitatumika ili kulinda usalama wa watu hao muhimu. Pia wakumbuke kuwa kama watavunjwa miguu au mikono au lolote lile litakalotokea itakuwa ni hasara kwao au kwa yule atakayekuwa ameupata mkasa huo.
 
Nawahakikishia kama kweli mtakuwa maeneo yale mtavunjwa miguu kwa risasi za moto na kutiwa ulemavu wa kudumu na akosekane kuwatibu na msiyafanye chochote haya mapolisi ya kibongo kuuwa kuvunja miguu hayaoni shida kama unajipenda kaa mbele ya tv yako siku hiyo kusubiri breaking news
 
Mleta Uzi, "vijana wa Bavicha mnaopenda kwenda Dodoma" na hapo hapo, "vijana mtakaowakuta hapa Dodoma". Akili za kupewa....
 
Intelijensia inasemaje?
Imeshatoa kibali cha mkutano 23/7?

Hamna machafuko?

Mikutano ya kisiasa mpaka 2o20 isharuhusiwa?
 
salary slip uko vzuri!hesabu uliyotoa ikikosewa fomula kdogo tu,basi mambo yataenda halijojo!wajilinde kwanza wao then kwa aman kabsa waendlee na shughul yao.
 
Back
Top Bottom