Tahadhari kuna wezi wapya wanatumia madawa

Kishalu

JF-Expert Member
Nov 1, 2010
1,173
708
Habari ya kweli iliyotokea wiki iliyopita.

Kuna dada mmoja anasoma chuo buguruni na pia ni mfanyakazi hivyo jioni akitoka kazini ndipo huenda shule.Sasa akiwa njiani kuelekea chuo akapigiwa simu na mtu asiyemfahamu akajitambulisha kwamba yeye ni daktari wa lugaro hosp na kumuulizia habari za mwanae ambae alishawahi kwenda kumtibu pale na chakushangaza zaidi akataja mpaka aina na rangi ya nguo aliyovaa siku ile alipokwenda hapo hospitali na yote yalikuwa kweli. Na zaidi akamwambia najua sasa hivi unaelekea chuo buguruni na kweli ilikuwa hivyo, lakini mwishoni akamweleza kwamba kuna mambo anataka kujua kujua kuhusu hicho chuo hivyo nae anaelekea huko hivyo akifika tu atamtafuta. Kwa muda wote huo huyo dada hakuweza kabisa kumkumbuka ila akajipa moyo kwamba yamkini huyo mtu atakuwa anamfahamu vizuri.

Baada ya kutoka chuo akiwa na wenzake watatu akawa anawasimulia habari za huyo mtu ndipo simu yake ikaita,kupokea yule mtu akamwambia nakuona uko na wenzio wawili mnavuka barabara na kumueleza jinsi alivyovaa sasa wenzie wakasema huyo mtu anakufahamu haiwezekani hapa tupo watatu kweli na ameweza kukutambua. Kisha huyo mtu akamwelekeza mahali alipo ambapo haikuwa mbali na barabara.

Lakini alipomtazama hakumfahamu kabisa, basi akampa mkono kumsalimia, baada ya hapo hakujitambua na zaidi alijikuta yuko maeneo ya chuo kikuu cha DSM akiwa hoi. Kuangalia simu na kila kitu chake kilikuwa salama na hakufanyiwa kitu chochote, kwa bahati kulikuwa kuna ndugu yake anasoma chuo hivyo akawasiliana nae ili kupata msaada ikabidi awahishwe mwananyamala hosp lakini ikaonekana sumu iliyotumika ni kali na dawa yake wanayo regency hosp,hivyo akawahishwa regency na kupata matibabu.

Baada ya ufahamu kumrudia akakuta mtu huyo kachukua pesa zote kwenye mpesa,tigo pesa na bank ( NMB na CRDB) kiasi cha milioni 3, hivyo inawezekana walipompa sumu alitaja password pasipo kujijua.

Na bank walipotazama kwenye ATM Camera waliona picha ya huyo mtu na yeye alimkumbuka vizuri, lakini polisi Kijitonyama wakakiri kwamba kesi hizo sasa hivi zimetokea mara nyingi na huo mtandao ni mkubwa, walipoenda kwenye usajili wa simu walikuta ni huyo huyo na jina lake ndilo alilojitambulisha.Ingawa polisi wameshindwa kumkamata.

Akiwa kituo cha polisi mara huyo mtu akampigia simu akimwambia ‘’kumbe wewe ni muoga sana tutakurudishia pesa zako’’. Sasa kumbe wanachofanya wanakuambia’’ tutafutie mtu ambae unahisi ana pesa kuliko hizi halafu tukifanikiwa tutarudisha pesa zako’’ hivyo inawezekana nae kuna mtu anaemjua alifanyiwa hivyo akaamua kumtaja yeye.





 
Habari ya kweli iliyotokea wiki iliyopita.

Kuna dada mmoja anasoma chuo buguruni na pia ni mfanyakazi hivyo jioni akitoka kazini ndipo huenda shule.Sasa akiwa njiani kuelekea chuo akapigiwa simu na mtu asiyemfahamu akajitambulisha kwamba yeye ni daktari wa lugaro hosp na kumuulizia habari za mwanae ambae alishawahi kwenda kumtibu pale na chakushangaza zaidi akataja mpaka aina na rangi ya nguo aliyovaa siku ile alipokwenda hapo hospitali na yote yalikuwa kweli. Na zaidi akamwambia najua sasa hivi unaelekea chuo buguruni na kweli ilikuwa hivyo, lakini mwishoni akamweleza kwamba kuna mambo anataka kujua kujua kuhusu hicho chuo hivyo nae anaelekea huko hivyo akifika tu atamtafuta. Kwa muda wote huo huyo dada hakuweza kabisa kumkumbuka ila akajipa moyo kwamba yamkini huyo mtu atakuwa anamfahamu vizuri.

Baada ya kutoka chuo akiwa na wenzake watatu akawa anawasimulia habari za huyo mtu ndipo simu yake ikaita,kupokea yule mtu akamwambia nakuona uko na wenzio wawili mnavuka barabara na kumueleza jinsi alivyovaa sasa wenzie wakasema huyo mtu anakufahamu haiwezekani hapa tupo watatu kweli na ameweza kukutambua. Kisha huyo mtu akamwelekeza mahali alipo ambapo haikuwa mbali na barabara.

Lakini alipomtazama hakumfahamu kabisa, basi akampa mkono kumsalimia, baada ya hapo hakujitambua na zaidi alijikuta yuko maeneo ya chuo kikuu cha DSM akiwa hoi. Kuangalia simu na kila kitu chake kilikuwa salama na hakufanyiwa kitu chochote, kwa bahati kulikuwa kuna ndugu yake anasoma chuo hivyo akawasiliana nae ili kupata msaada ikabidi awahishwe mwananyamala hosp lakini ikaonekana sumu iliyotumika ni kali na dawa yake wanayo regency hosp,hivyo akawahishwa regency na kupata matibabu.

Baada ya ufahamu kumrudia akakuta mtu huyo kachukua pesa zote kwenye mpesa,tigo pesa na bank ( NMB na CRDB) kiasi cha milioni 3, hivyo inawezekana walipompa sumu alitaja password pasipo kujijua.

Na bank walipotazama kwenye ATM Camera waliona picha ya huyo mtu na yeye alimkumbuka vizuri, lakini polisi Kijitonyama wakakiri kwamba kesi hizo sasa hivi zimetokea mara nyingi na huo mtandao ni mkubwa, walipoenda kwenye usajili wa simu walikuta ni huyo huyo na jina lake ndilo alilojitambulisha.Ingawa polisi wameshindwa kumkamata.

Akiwa kituo cha polisi mara huyo mtu akampigia simu akimwambia ‘’kumbe wewe ni muoga sana tutakurudishia pesa zako’’. Sasa kumbe wanachofanya wanakuambia’’ tutafutie mtu ambae unahisi ana pesa kuliko hizi halafu tukifanikiwa tutarudisha pesa zako’’ hivyo inawezekana nae kuna mtu anaemjua alifanyiwa hivyo akaamua kumtaja yeye.






tujulishe jina la huyo mhusika,bado hujatusaidia
 
Habari ya kweli iliyotokea wiki iliyopita.

Kuna dada mmoja anasoma chuo buguruni na pia ni mfanyakazi hivyo jioni akitoka kazini ndipo huenda shule.Sasa akiwa njiani kuelekea chuo akapigiwa simu na mtu asiyemfahamu akajitambulisha kwamba yeye ni daktari wa lugaro hosp na kumuulizia habari za mwanae ambae alishawahi kwenda kumtibu pale na chakushangaza zaidi akataja mpaka aina na rangi ya nguo aliyovaa siku ile alipokwenda hapo hospitali na yote yalikuwa kweli. Na zaidi akamwambia najua sasa hivi unaelekea chuo buguruni na kweli ilikuwa hivyo, lakini mwishoni akamweleza kwamba kuna mambo anataka kujua kujua kuhusu hicho chuo hivyo nae anaelekea huko hivyo akifika tu atamtafuta. Kwa muda wote huo huyo dada hakuweza kabisa kumkumbuka ila akajipa moyo kwamba yamkini huyo mtu atakuwa anamfahamu vizuri.

Baada ya kutoka chuo akiwa na wenzake watatu akawa anawasimulia habari za huyo mtu ndipo simu yake ikaita,kupokea yule mtu akamwambia nakuona uko na wenzio wawili mnavuka barabara na kumueleza jinsi alivyovaa sasa wenzie wakasema huyo mtu anakufahamu haiwezekani hapa tupo watatu kweli na ameweza kukutambua. Kisha huyo mtu akamwelekeza mahali alipo ambapo haikuwa mbali na barabara.

Lakini alipomtazama hakumfahamu kabisa, basi akampa mkono kumsalimia, baada ya hapo hakujitambua na zaidi alijikuta yuko maeneo ya chuo kikuu cha DSM akiwa hoi. Kuangalia simu na kila kitu chake kilikuwa salama na hakufanyiwa kitu chochote, kwa bahati kulikuwa kuna ndugu yake anasoma chuo hivyo akawasiliana nae ili kupata msaada ikabidi awahishwe mwananyamala hosp lakini ikaonekana sumu iliyotumika ni kali na dawa yake wanayo regency hosp,hivyo akawahishwa regency na kupata matibabu.

Baada ya ufahamu kumrudia akakuta mtu huyo kachukua pesa zote kwenye mpesa,tigo pesa na bank ( NMB na CRDB) kiasi cha milioni 3, hivyo inawezekana walipompa sumu alitaja password pasipo kujijua.

Na bank walipotazama kwenye ATM Camera waliona picha ya huyo mtu na yeye alimkumbuka vizuri, lakini polisi Kijitonyama wakakiri kwamba kesi hizo sasa hivi zimetokea mara nyingi na huo mtandao ni mkubwa, walipoenda kwenye usajili wa simu walikuta ni huyo huyo na jina lake ndilo alilojitambulisha.Ingawa polisi wameshindwa kumkamata.

Akiwa kituo cha polisi mara huyo mtu akampigia simu akimwambia ''kumbe wewe ni muoga sana tutakurudishia pesa zako''. Sasa kumbe wanachofanya wanakuambia'' tutafutie mtu ambae unahisi ana pesa kuliko hizi halafu tukifanikiwa tutarudisha pesa zako'' hivyo inawezekana nae kuna mtu anaemjua alifanyiwa hivyo akaamua kumtaja yeye.






Jamani, hii inaweza ikawa kweli lakini pia inawezekana ikawa ni story ya kutunga. Hebu jiulize inakuwaje huyo mtu kumpa tu mkono tayari akawa amepoteza fahamu kutokana na sumu/chemical alizokuwa nazo huyo mtu. Sasa hizo kemikali zinabagua watu wa kuwadhuru? Kwa nini huyo Bwana yeye hadhuriki? Na kwa nini huyo dada hakwenda na hao wenzake wawili wakati anakwenda kuonana na mtu asiyekuwa na uhakika naye!!!

I am just being curious!!!!!

Tiba
 
Kuna mdada ninamfahamu alipigwa wizi kama huo unaousema wa kuibiwa kwenye ATM pesa zote zikaenda.

Yeye alikutana na kijana Handsome boy akajua ameshajipatia boy friend , kumbe daah tapeli akatolewa out kupewa fanta ya kopo akajikuta yupo kule Tabata ya mwisho mwisho kwenye mapori akaokotwa na kibabu.Kuja kucheki simu imeenda kila kitu na kwenye account akakuta balance kwishne.
 
Siamini hata kidogo eti mtu umpe mkono kisha upotee ghafla hadi ukutwe kichakani. Kama hao wezi wana uwezo huo basi wangeshaacha utapeli huo sababu wana nguvu za ajabu. By the way, kuna matapeli wengi mji huu unakutana na mtu anakuchekea as if mnafahamiana anakuuliza "za siku nyingi Bwana?" ukimuuliza mbona sikufahamu anakuambia tulikuwa wote chuo kikuu lakini ulikuwa umenitangulia kidogo. Mwisho anakuomba biz card ili aanzie hapo kukufahamu!! Jihadhari na watu hao!!
 
Habari ya kweli iliyotokea wiki iliyopita.

Kuna dada mmoja anasoma chuo buguruni na pia ni mfanyakazi hivyo jioni akitoka kazini ndipo huenda shule.Sasa akiwa njiani kuelekea chuo akapigiwa simu na mtu asiyemfahamu akajitambulisha kwamba yeye ni daktari wa lugaro hosp na kumuulizia habari za mwanae ambae alishawahi kwenda kumtibu pale na chakushangaza zaidi akataja mpaka aina na rangi ya nguo aliyovaa siku ile alipokwenda hapo hospitali na yote yalikuwa kweli. Na zaidi akamwambia najua sasa hivi unaelekea chuo buguruni na kweli ilikuwa hivyo, lakini mwishoni akamweleza kwamba kuna mambo anataka kujua kujua kuhusu hicho chuo hivyo nae anaelekea huko hivyo akifika tu atamtafuta. Kwa muda wote huo huyo dada hakuweza kabisa kumkumbuka ila akajipa moyo kwamba yamkini huyo mtu atakuwa anamfahamu vizuri.

Baada ya kutoka chuo akiwa na wenzake watatu akawa anawasimulia habari za huyo mtu ndipo simu yake ikaita,kupokea yule mtu akamwambia nakuona uko na wenzio wawili mnavuka barabara na kumueleza jinsi alivyovaa sasa wenzie wakasema huyo mtu anakufahamu haiwezekani hapa tupo watatu kweli na ameweza kukutambua. Kisha huyo mtu akamwelekeza mahali alipo ambapo haikuwa mbali na barabara.

Lakini alipomtazama hakumfahamu kabisa, basi akampa mkono kumsalimia, baada ya hapo hakujitambua na zaidi alijikuta yuko maeneo ya chuo kikuu cha DSM akiwa hoi. Kuangalia simu na kila kitu chake kilikuwa salama na hakufanyiwa kitu chochote, kwa bahati kulikuwa kuna ndugu yake anasoma chuo hivyo akawasiliana nae ili kupata msaada ikabidi awahishwe mwananyamala hosp lakini ikaonekana sumu iliyotumika ni kali na dawa yake wanayo regency hosp,hivyo akawahishwa regency na kupata matibabu.

Baada ya ufahamu kumrudia akakuta mtu huyo kachukua pesa zote kwenye mpesa,tigo pesa na bank ( NMB na CRDB) kiasi cha milioni 3, hivyo inawezekana walipompa sumu alitaja password pasipo kujijua.

Na bank walipotazama kwenye ATM Camera waliona picha ya huyo mtu na yeye alimkumbuka vizuri, lakini polisi Kijitonyama wakakiri kwamba kesi hizo sasa hivi zimetokea mara nyingi na huo mtandao ni mkubwa, walipoenda kwenye usajili wa simu walikuta ni huyo huyo na jina lake ndilo alilojitambulisha.Ingawa polisi wameshindwa kumkamata.

Akiwa kituo cha polisi mara huyo mtu akampigia simu akimwambia ‘’kumbe wewe ni muoga sana tutakurudishia pesa zako’’. Sasa kumbe wanachofanya wanakuambia’’ tutafutie mtu ambae unahisi ana pesa kuliko hizi halafu tukifanikiwa tutarudisha pesa zako’’ hivyo inawezekana nae kuna mtu anaemjua alifanyiwa hivyo akaamua kumtaja yeye.





sasa huo ni ushirikina au tusemeje?? mkono mtu unapoteza fahamu?
 
Story wacha tupige story tu tustorike jamani mweee.................!:target:
 
Wabongo tuache ukarimu uliopitiliza kwa strangers, binafsi nina utaratibu wa kutojifanya mkarimu kwa mtu yoyote nisiyemfahamu. Wengi huja na gia kama hizo, "Eti hospitali ya kutibu kuvimbiwa ipo wapi?", eboh! kwani mjini nilikuleta mimi.
Juzi kati hapa Morocco kijiwe cha wazee wa Favor, nimekutana na mbulula kama huyo, "E bwana huwa nakuona sana mitaa ya Mkwajuni, hivi huwa unaishi kule eeh"...kwanza nilimkata jicho moja kali, halafu nikamwambia nitatawanya sasa hivi ubongo wako. Yule bwana mkubwa haja kubwa na ndogo zote zilikua zinagonga chupi na makalio kumtetemeka kama kia la kondoo....
 
Jamani, hii inaweza ikawa kweli lakini pia inawezekana ikawa ni story ya kutunga. Hebu jiulize inakuwaje huyo mtu kumpa tu mkono tayari akawa amepoteza fahamu kutokana na sumu/chemical alizokuwa nazo huyo mtu. Sasa hizo kemikali zinabagua watu wa kuwadhuru? Kwa nini huyo Bwana yeye hadhuriki? Na kwa nini huyo dada hakwenda na hao wenzake wawili wakati anakwenda kuonana na mtu asiyekuwa na uhakika naye!!!

I am just being curious!!!!!

Tiba

hata mi naona kuwa hii stori imetungwa kiasi flani..
 
Haya ni kweli yapo huko mijini kwenu .Rafiki yangu anasema- Hata nami niliyakuta Kampala lakini wakashindwa kwani mitandao iligoma na kuna mtu anisaidia baada ya kuwaona. Ila ukivaa Rosari iliyobalikiwa kama wewe ni Mkatoliki nasikia hayakudhuruu, nahisi ukitaja Yesu unafanikiwa
 
Kuna mdada ninamfahamu alipigwa wizi kama huo unaousema wa kuibiwa kwenye ATM pesa zote zikaenda.

Yeye alikutana na kijana Handsome boy akajua ameshajipatia boy friend , kumbe daah tapeli akatolewa out kupewa fanta ya kopo akajikuta yupo kule Tabata ya mwisho mwisho kwenye mapori akaokotwa na kibabu.Kuja kucheki simu imeenda kila kitu na kwenye account akakuta balance kwishne.

tobaa yahilah......nimekwisha mie.....uwiiiii.......
 
Haya ni kweli yapo huko mijini kwenu .Rafiki yangu anasema- Hata nami niliyakuta Kampala lakini wakashindwa kwani mitandao iligoma na kuna mtu anisaidia baada ya kuwaona. Ila ukivaa Rosari iliyobalikiwa kama wewe ni Mkatoliki nasikia hayakudhuruu, nahisi ukitaja Yesu unafanikiwa

ungetufafanulia basi mkasa wako ulikuaje mana inawezekana tunasema jamaa stori katunga kumbe kweli yanatokea!!
halafu inabidi utujuze mana inawezekana ni wezi hao hao wa k'la ndio wamehamia huku baada ya njama zao kushtukiwa huko kwao.
 
jamani story sio ya kutunga, kuna watu wawili mmoja nafanya nae kazi na mwingine ndugu yangu wameibiwa kwa style iyo iyo. Na ukienda police pia wanajifanya hawaamini style uliyoibiwa but its happening. just be careful with strangers.
 
Hadithi hii inatufundisha kwamba tusizoeane zoeane kwa harakaharaka na watu tusiowafahamu vizuri. Yapo na kweli yanatokea mambo kama haya. Penda kukaa bars au mitaa ya Kinondoni na Sinza siku moja utayaona au yatakukuta haya!
 
Jamani kuna wizi umeibuka hivi sasa unaofanana na huo, mimi mdogo wangu amekuta benki hana hata shilingi baada ya wizi kuchukua hela zote kwenye akaunti yake bila yeye kufahamu, ameenda benki anaambiwa amechukua yeye mwenyewe. Ila baadaye wamefanya uchunguzi wakakuta mfanyakazi wa benki anahusika.
 
ungetufafanulia basi mkasa wako ulikuaje mana inawezekana tunasema jamaa stori katunga kumbe kweli yanatokea!!
halafu inabidi utujuze mana inawezekana ni wezi hao hao wa k'la ndio wamehamia huku baada ya njama zao kushtukiwa huko kwao.

anavyosema: Yeye walimwita wakamgusa na wakamwambia unajua unashida sana na pesa akasema ndiyo , basi sis tumekuona una shida sana na tukaona tukusaidie. Unatoka Tz ,kayanga na umekuja kununua vitu hapa. utupe pesa zako zote ili tuzidishie mara 10. Akasema sina hapa bali twende Bank, wakamwambia paki gari lako alafu tupande Tax(daladala za uganda uitwa tax) twende bank. akapaki gari wakaenda Bank ,wao wakakaa mbali kidogo akaenda kuchukua hela ,network ikagoma. Wakati anahangaika akaja mtu akamgusa akamuuliza unafanya nini hapa ,ndo akaanza kushangaa na watu wakatimka, basi akaeleza mkasa wake hivyo. Wakamwambia uhuni huu hapa upo sana na anayekuchomekea anapewa naye mzigo, akaenda hospital bahati nzuri hakuwa amewekewa sumu japo alichanjwa kidogo na kiwembe
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom