Tahadhari: Kuna tatizo la 'Heart Failure' kwa wanawake wanaojifungua tuwe makini

Tingitane

Senior Member
Apr 18, 2012
116
130
Habari wakuu,

Kuna tatizo la heart failure kwa wanawake wanaojifungua nafikiri tatizo hili linasababisha vifo vya kina mama wengi sana lakini sijui kama mimi ndio nilikuwa silijua au wengi pia hatulifahamu na kwanini elimu juu ya tatizo hili haitolewi wakati wa clinic kwa kinamama.

Iko hivi mwishoni mwa mwezi January kuna rafiki yetu alijaaliwa mtoto sasa tukaamua kwa pamoja tukamtembelee na kumpa hongera kwa kujaaliwa mtoto, hivyo tulienda kama kikundi cha washikaji kwa umoja wetu.

Wakati mazungumzo yanaendelea ndio rafiki zetu waliamua kutuweka wazi kuhusu tatizo lililompata mama wakati anajifungua kuwa kuna maji huwa yanaingia kwenye mapafu pamoja na moyo jambo ambalo lilipelekea moyo kushindwa kufanya kazi vizuri na kujisIkia mchovu sana na kushindwa kupumua akawa anahisi ni uchovu tu wa kujifungua lakini kadri muda ulivyozidi kwenda hali ikazidi kuwa mbaya ndipo alipolazimika kuchukua hatua ya kumpigia Daktari pale Aga Khan kwani ndpko alipojifungulia alipomuelezea Daktari kuhusu hali anayojisikia akamjibu hebu acha unachokifanya uje hapa hospital mara moja.

Dr. hakutaka kumshtua sana lakini baada ya kupata ahueni ndipo alipomwambia ukweli kuwa hali aliyokuwa nayo ni hatari sana na mapigo ya moyo yakishafika chini ya 50 hata moyo wasingeweza kuupump tena ndio ingekuwa mwisho wake.

Washukuriwe Madaktari wa Aga Khan kwa kufaulu kuokoa maisha ya rafiki yetu ijapokuwa amepewa masharti mengi sana ikiwa hakuna kuzaa tena, akafunge tu kizazi na hakuna kutumia uzazi wa mpango wa aina yoyote na hakuna kunyonyesha mtoto (Na tatizo lilitokea ndani ya siku mbili baada ya kujifungua).

Sasa sababu kubwa sana ya mimi kuja hapa katika hili jukwaa ni kutaka watu wengi zaidi wafahamu kuhusu "heart failure during delivery" kwani nimegundua wengi sana wanapoteza maisha pasipo kujua na naomba kama kwenye hili jukwaa kuna Daktari ambaye anaweza kuelezea hili tatizo kwa upana zaidi atusaidie na kama pia kuna uwezekano wa kushare huu ujumbe kwa namna yoyote ili wengi wafahamu naamini wengi wataokolewa.

Ahsante.
 
Sitaki ata kukumbuka hili tatizo, ni chozi tu ndilo linalonitoka kila nikikumbuka. Mama angu mdg alivyofariki sbb ya tatizo hili.
 
Sitaki ata kukumbuka hili tatizo, ni chozi tu ndilo linalonitoka kila nikikumbuka. Mama angu mdg alivyofariki sbb ya tatizo hili.
[/QUOTE

Pole sana mkuu, nitatizo kubwa sana hili lakini elimu bado ni ndogo sana na watu wengi sana wanapoteza maisha pasipo kujua kwani inavyoonekana ukishachelewa tu kufika hospitali madr. hawakuambii lakin wanakuwa wanajua kuwa utakufa, kwani inasemekana mapigo ya moyo yakiwa juu ya hamsini wanaweza kupump moyo na ukatibiwa ukapona lakin ikiwa chini ya hamsini inakuwa "too late".
 
Mwanamke akiwa mjamzito damu(plasma) huongezeka wingi, kuongezeka kwa wingi hupelekea kuupa moyo kazi zaidi.

Lakini kuanzia wiki ya 40 ya ujauzito na mpaka kujifungua na kuendelea damu hurudi kwenye kiwango chake cha kawaida.

Sasa ukiona mama kapata tatizo la moyo baada ya kujifungua ina maana inawezekana moyo umeshindwa ku-cope na mabadiliko yaliyotokea kipindi cha ujauzito.

Hili ni tatizo serious ambalo tunasema kwa kimombo "life threatening", ina maana usipopata aggressive management unaondoka kimasihara hivihivi.

Kwa nchi zilizooendelea huwa wanamonitor vitu vingi sana baada ya mama kujifungua, lkn kibongo bongo ni mwendo wa bora liende.

Lkn nashangaa huyo dada kujifungulia Aga Khan na hawakuligundua mpaka wanamruhusu wakati ni hospitali yenye standard za kimataifa.

Unforgetable
 
Mwanamke akiwa mjamzito damu(plasma) huongezeka wingi, kuongezeka kwa wingi hupelekea kuupa moyo kazi zaidi.

Lakini kuanzia wiki ya 40 ya ujauzito na mpaka kujifungua na kuendelea damu hurudi kwenye kiwango chake cha kawaida.

Sasa ukiona mama kapata tatizo la moyo baada ya kujifungua ina maana inawezekana moyo umeshindwa ku-cope na mabadiliko yaliyotokea kipindi cha ujauzito.

Hili ni tatizo serious ambalo tunasema kwa kimombo "life threatening", ina maana usipopata aggressive management unaondoka kimasihara hivihivi.

Kwa nchi zilizooendelea huwa wanamonitor vitu vingi sana baada ya mama kujifungua, lkn kibongo bongo ni mwendo wa bora liende.

Lkn nashangaa huyo dada kujifungulia Aga Khan na hawakuligundua mpaka wanamruhusu wakati ni hospitali yenye standard za kimataifa.

Unforgetable
Kuna mambo mengi sana hao pengine alikuwa hana bima baada ya kujifungua aliomba kuondoka kwa sababu ya gharama lakin pia wao ndio walimuokoa baada ya kupiga simu na kuelezea hiyo hali walimshauri arudi hospital na bahati nzuri aliwahi kabla hali haijakuwa mbaya zaidi.

Ushauri wangu ni wengi sana wanajiskia hivyo baada ya kujifungua wanafikiri ni hali ya kawaida na mwishowe wanapoteza maisha ni vyema mtu akiskia dalili za namna hiyo awahi kwa dr. haraka iwezekanavyo.
 
Asante sn mkuu. Yani moyo unashindwa kupumua, na likaongezeka na mapafu kujaa maji. Ikazd kusbabsh kifo chake
 
Mwanamke akiwa mjamzito damu(plasma) huongezeka wingi, kuongezeka kwa wingi hupelekea kuupa moyo kazi zaidi.

Lakini kuanzia wiki ya 40 ya ujauzito na mpaka kujifungua na kuendelea damu hurudi kwenye kiwango chake cha kawaida.

Sasa ukiona mama kapata tatizo la moyo baada ya kujifungua ina maana inawezekana moyo umeshindwa ku-cope na mabadiliko yaliyotokea kipindi cha ujauzito.

Hili ni tatizo serious ambalo tunasema kwa kimombo "life threatening", ina maana usipopata aggressive management unaondoka kimasihara hivihivi.

Kwa nchi zilizooendelea huwa wanamonitor vitu vingi sana baada ya mama kujifungua, lkn kibongo bongo ni mwendo wa bora liende.

Lkn nashangaa huyo dada kujifungulia Aga Khan na hawakuligundua mpaka wanamruhusu wakati ni hospitali yenye standard za kimataifa.

Unforgetable

Habari,
Uliyoyaeleza ni kweli kuhusu mabadiliko yanayotokea wakati wa wa ujauzito.
Lakini pia tukumbuke si mabadiliki yote hufuata utaratibu ulioueleza hapo.
Mabadiliko mengine ya ujazo na msukumo wa damu hutokea baada baada ya kujifungua.

Kwa mama mjamzito, tunasema ni nusu mgonjwa kwa kipindi chote cha ujauzito na ni nusu mgonjwa kipindi chote cha siku arobaini baada ya kujifungua.

Toa taarifa za chochote ambacho unajisikia hauko sawa kwa vipindi hi viwili.

Si rahisi kufanya vipimo vyote ili kuhakiki kila mgonjwa ameathiliwa vipi na kwa kiwango gapi kila baada ya kujifungua, ila pindi daktari anapoona utofauti wa hali ya mgonjwa/ mteja anaweza kuomba vipimo zaidi.

Cha mhimu tusichukulie kawaidi dalili zozote ambazo si njema.

Tatizo husika lipo na linagarimu maisha ya wapendwa wetu wengi.

Ahsante
 
Ntarudi kuchangia
Habari wakuu,

Kuna tatizo la heart failure kwa wanawake wanaojifungua nafikiri tatizo hili linasababisha vifo vya kina mama wengi sana lakin sijui kama mimi ndio nilikuwa silijua au wengi pia hatulifahamu na kwanini elimu juu ya tatizo hili haitolewi wakati wa clinic kwa kinamama.

Iko hivi mwishoni mwa mwezi january kuna rafiki yetu alijaaliwa mtoto sasa tukaamua kwa pamoja tukamtembelee na kumpa hongera kwa kujaaliwa mtoto, hivyo tulienda kama kikundi cha washikaji kwa umoja wetu.

Wakati mazungumzo yanaendelea ndio rafiki zetu waliamua kutuweka wazi kuhusu tatizo lililompata mama wakati anajifungua kuwa kuna maji huwa yanaingia kwenye mapafu pamoja na moyo jambo ambalo lilipelekea moyo kushindwa kufanya kazi vizuri na kujiskia mchovu sana na kushindwa kupumua akawa anahisi ni uchovu tu wa kujifungua lakini kadri muda ulivyozidi kwenda hali ikazidi kuwa mbaya ndipo alipolazimika kuchukua hatua ya kumpigia Daktari pale Aga khan kwani ndiko alipojifungulia alipomuelezea Daktari kuhusu hali anayojisikia akamjibu hebu acha unachokifanya uje hapa hospital mara moja.

Dr. hakutaka kumstua sana lakini baada ya kupata ahueni ndipo alipo mwambia ukweli kuwa hali aliyokuwa nayo ni hatari sana na mapigo ya moyo yakishafika chini ya 50 hata moyo wasingeweza kuupump tena ndio ingekuwa mwisho wake.

Washukuriwe Madaktari. wa Aga khan kwa kufaulu kuokoa maisha ya rafiki yetu ijapokuwa amepewa masharti mengi sana ikiwa hakuna kuzaa tena, akafunge tu kizazi na hakuna kutumia uzazi wa mpango wa aina yoyote na hakuna kunyonyesha mtoto (Na tatizo lilitokea ndani ya siku mbili baada ya kujifungua).

Sasa sababu kubwa sana ya mimi kuja hapa katika hili jukwaa ni kutaka watu wengi zaidi wafahamu kuhusu "heart failure during delivery" kwani nimegundua wengi sana wanapoteza maisha pasipo kujua na naomba kama kwenye hili jukwaa kuna Daktari ambaye anaweza kuelezea hili tatizo kwa upana zaidi atusaidie na kama pia kuna uwezekano wa kushare huu ujumbe kwa namna yoyote ili wengi wafahamu naamini wengi wataokolewa.

Ahsante.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom