TAHADHARI: Kuna matapeli! Fuata taratibu hizi...

Wakuu,

Penye wengi, pana mengi pia. Jukwaa hili pamoja na kuwa na matangazo mengi, lakini wengine ni matapeli wakubwa sana. Tafadhali, tulishatoa angalizo na tunasisitiza tena: Mnapoamua kufanya biashara yoyote nje au ndani ya JF bila kutushirikisha msiilaumu JF.

Tunafahamu kuna ambao mmeshalizwa, tafadhali tufahamisheni ili tuweze kuwaanika (tutaanzisha thread maalum kwa ajili ya hili).

Nisisitize, IWENI MAKINI NA MATAPELI!

kuna jamaa anaitwa gmabumbe yupo humu ndani anauza vifaa vibovu ukishampa pesa anatokomea kabisa.....i think something should be done
 
wakuu,

penye wengi, pana mengi pia. Jukwaa hili pamoja na kuwa na matangazo mengi, lakini wengine ni matapeli wakubwa sana. Tafadhali, tulishatoa angalizo na tunasisitiza tena: Mnapoamua kufanya biashara yoyote nje au ndani ya jf bila kutushirikisha msiilaumu jf.

Tunafahamu kuna ambao mmeshalizwa, tafadhali tufahamisheni ili tuweze kuwaanika (tutaanzisha thread maalum kwa ajili ya hili).

Nisisitize, iweni makini na matapeli!
avatar yako imeniacha hoi!!!
 
Ni kweli kabisa kuna member humu ndani si waaminifu kabisa.Kuna mmoja januari mwaka huu aliniahidi kunipatia gari kwa Tsh. 3.5 m hadi leo sijaipata na fedha nilishampatia zaidi ya Tsh.3.8 m.Nimefadhaishwa sana na nasikitika sana na nimemwachia Mungu,maana nimepata tayari Gari lingine.Nina hakika haitamsaidia zaidi ya kumwongezea mateso na dhiki kuu ili ajue Mungu hajaribiwi.

Taja ID yake tumjue,humu ndani tapeli maarufu ni Kitomari2 aka culboy huyo jamaa ni hatari yani ni sheeeda kifupi ni waalade.
 
Last edited by a moderator:
king kong nmeshasema MIMI SIO KITOMARI, em jaribu kupitia post zote za kitomari2 na za kwangu halafu utagundua kwamba kuna ki2 kilitokea somewhere.
 
huyu mtu anajiita ukwelikitugani ashawahi kuniliza hela zangu! Pia alimdhulumu huyu dada sweetbaby.

ukwelikitugani, nimekusamehe ila naomba nikutaje kwa faida ya wanaJF wengine wasijedhulumiwa na wewe.
 
Last edited by a moderator:
Naunga mkono hoja. Kweli humu JF kuna matapeli ingawa siyo wote. Mimi nimenunua sana kupitia JF na karibu mara zote nimeuziwa vitu genuine, kasoro mara moja. Nilinunua the so called universal solar charger for laptops and mobile phones. Muuzaji alimwaga sifa kibao mpaka nikaingia laini. Cha ajabu ni kwamba siyo charger hata kidogo bali ni kama universal battery ya laptops. Baada ya kumweleza matatizo yake muuzaji kakata mawasiliano, ingawa bado yumo JF.

Tujihadhari!!!

huyo tapel,mtaje tuuuuu
 
kama imethibitika ni tapeli, ifungwe akaunti yake, na ndo dawa pekee!

Mkuu mbona hiyo haitamcost sana mtuhumiwa coz si lazima atabadilisha ID tuu na ataendelea na utapeli wake km kawa dawa yao watangazwe tu id zao na washughulikiwe ipasavyo
 
Habari wakuu, jf inasaidia sana ukiwa unataka kununua ama kuuza kitu. Nimeshawahi kununua mara nyingi na kuuza pia bila tatizo lolote ila moja tu ambalo limenifika.
Niliuziwa ipad 2 na huyu MWALUPALE 0652834080 kumbe ilikuwa mbovu yani baada ya siku mbili tu mpaka leo haiwaki kila mjuzi wa ipad nikimpelekea anasema mbovu na pia ishawahi kufunguliwa. Najuta maana nilimnunulia mzee wangu mpaka sasa sijui ananionaje. Nilijaribu kuwasiliana naye akasema nimfate morogoro mara yupo ifakara mara ilikuwa sio yake, kwenye uuzaji huo aliambulia 40,000 tu na sasa hapokei wala hajibu msg. Sawa nimekubali nimemuachia mungu. Lakini kuweni waangalifu.
 
Mbona mnakuza mambo! Jf ni free online forum iwe kwa siasa biashara mpnzi au umbea etc!!! Sasa kazi kwako unapoingia kwenye reality world kwenda kuona bidhaa live! Hata madukani watu utapeliwa au sokoni sio jf tu! Akili yako tu
 
Na unanunuaje kitu bila guarantee! Mi sioni kama issue! Ila ikithibitika umetapeliwa na si uzembe wako aanikwe! Kumbuka hapa ni Mjini
 
kuna jamaa m1 yupo humu nmemsahau jina ila katika avata yake anabonge la bichwa, kwa kweli huyo jamaa ni tapeli sana.
 
Back
Top Bottom