TAHADHARI: Kuna matapeli! Fuata taratibu hizi...

na mm nimenunua samsung s6 online kutoka dar ikanifikia vzur kitendo cha kuingiza email yangu tu simu ikajiloki ikawa mwisho wa maelezo na ikawa mwisho wa kununua bidhaa online
 
Siku kadhaa zilizopita niliweka Uzi nauza simu S3 ,
Nikapata mteja akanitumia SMS ila Ile simu tayari nilishauza.
Nikaona nimtafutie simu kwa mtu mwingine.
Wakati anapelekewa simu akaione kumbe ameshaandaa wezi wake tayari, wakamkaba Yule aliyepeleka simu wakamuibia Ile simu .
Huyu mteja alidai yuko Sinza darajani baada ya tukio akadai yuko Kimara. Na akakana kutaja Sinza.

Mwizi wangu najua humo humu na namba yangu umeichukua humu na umefanya nasambazwa Whatsap Kama mwizi wa simu ila nitakupata tu. Halafu mbaya zaidi ni Mtandao wenye wanaume na wanawake.
Tahadhari ukipata mteja muite aje eneo ambalo ni salama.
Pole sana, ila avator yako inavutia mbaya.
 
Hata kelvin Isaya ni mwizi ameiba pesa nyingi sana. Niliwapa watu taadhari mapema wakasema nina wivu na biashara yake.
 
"Mwizi wangu najua humo humu"
Faiza Foxy akiwakoromea kuhusu matumizi sahihi ya lugha mnamwanzishia thread. Haya sasa tatizo sugu la kuchanganya irabu za Kiswahili na kikanushi (h-) limebadili kabisa maana ya ulichotaka kukisema (japo pengine watu wamekuelewa). Tunaporekebishwa na huyu mama mtaalamu wa lugha tukubali kujifunza na tubadilike. Binafsi, ukiachilia mbali lugha za kitoto kama xaxa, uxije..., hakuna kitu kinachonikera kama huu mkanganyiko wa h- na irabu za Kiswahili.

===> By the way - pole kwa kuibiwa. Ndiyo mambo ya mtandaoni haya. Wengine wamepoteza mpaka maisha. Wengine wamebakwa...Tuwe waangalifu sana na haya mambo!
 
Maneno Mengi pointi ya msingi haionekani.
Faiza Foxy akiwakoromea kuhusu matumizi sahihi ya lugha mnamwanzishia thread. Haya sasa tatizo sugu la kuchanganya irabu za Kiswahili na kikanushi (h-) limebadili kabisa maana ya ulichotaka kukisema (japo pengine watu wamekuelewa). Tunaporekebishwa na huyu mama mtaalamu wa lugha tukubali kujifunza na tubadilike. Binafsi, ukiachilia mbali lugha za kitoto kama xaxa, uxije..., hakuna kitu kinachonikera kama huu mkanganyiko wa h- na irabu za Kiswahili.

===> By the way - pole kwa kuibiwa. Ndiyo mambo ya mtandaoni haya. Wengine wamepoteza mpaka maisha. Wengine wamebakwa...Tuwe waangalifu sana na haya mambo!
 
kwann usimtaje huyo tao
Naunga mkono hoja. Kweli humu JF kuna matapeli ingawa siyo wote. Mimi nimenunua sana kupitia JF na karibu mara zote nimeuziwa vitu genuine, kasoro mara moja. Nilinunua the so called universal solar charger for laptops and mobile phones. Muuzaji alimwaga sifa kibao mpaka nikaingia laini. Cha ajabu ni kwamba siyo charger hata kidogo bali ni kama universal battery ya laptops. Baada ya kumweleza matatizo yake muuzaji kakata mawasiliano, ingawa bado yumo JF.

Tujihadhari!!!
kwann usimtaje huyo tapeli naye ajitetee humu humu
 
tunaomba jf mtengeneze utaratibu kwa wanaofanya biashara humu kwamba wajitambulishe kwanza kwenu wajenge trust kwenu ili sisi tukiwaamini basi nyie mshakuwa mmejiridhisha na akitapeli basi nyinyi mnadili nae
 
80 Reactions
Reply
Back
Top Bottom