tajirijasiri
JF-Expert Member
- Oct 13, 2012
- 2,864
- 3,851
Kila mtu anakumbuka jinsi fedha za Walipa kodi zilivyokwapuliwa toka Escrow Account pale BOT. Hebu tujiulize haya:-
1. Ni kiasi gani cha fedha kinazalishwa kwa kuweka fedha BOT, zaidi ya kile kinachozalishwa kwa kuweka fedha kwenye Commercial Banks Fixed Deposit Accounts?
2. Je, deposits za Commercial Banks zinakuzwa vipi, ili baadae deposits hizo zitumike kuwakopesha Wakulima, Wafanyakazi na Wafanyabiashara, na baadae kusisimua (Stimulate) shughuli za kiuchumi, kukuza soko la ajira na Serikali kukusanya kodi?
3. Je, ni kwa kiasi gani mapato ya Commercial Banks yataathirika, na kupelekea kupunguza wafanyakazi na kulipa kodi kiduchu?
4. Je, kuna ushahidi usio shaka juu ya kiasi gani cha fedha na kilichotwa na nani, kutoka Fixed Deposit Accounts za hizo Commercial Banks?
5. Je, BOT kuna malaika wasio na tamaa ya kuchukua fedha, na kama wapo, utatuhakikishia vipi kama hii sio mbinu ya wakubwa kuzisogeza fedha karibu ili wazipige kama walivyofanya kwenye Escrow Account?
Haya Maswali yakijibiwa, yatahalalisha uamuzi huo. Vinginevyo kutakuwa na shaka ya kuleta Escrow Season II, ambapo kwenye Season I watu walijibebea fedha kwenye sandarusi, Rambo, lumbesa, mabegi n.k. toka pale pale BOT.
Hayo tu kwa leo.
1. Ni kiasi gani cha fedha kinazalishwa kwa kuweka fedha BOT, zaidi ya kile kinachozalishwa kwa kuweka fedha kwenye Commercial Banks Fixed Deposit Accounts?
2. Je, deposits za Commercial Banks zinakuzwa vipi, ili baadae deposits hizo zitumike kuwakopesha Wakulima, Wafanyakazi na Wafanyabiashara, na baadae kusisimua (Stimulate) shughuli za kiuchumi, kukuza soko la ajira na Serikali kukusanya kodi?
3. Je, ni kwa kiasi gani mapato ya Commercial Banks yataathirika, na kupelekea kupunguza wafanyakazi na kulipa kodi kiduchu?
4. Je, kuna ushahidi usio shaka juu ya kiasi gani cha fedha na kilichotwa na nani, kutoka Fixed Deposit Accounts za hizo Commercial Banks?
5. Je, BOT kuna malaika wasio na tamaa ya kuchukua fedha, na kama wapo, utatuhakikishia vipi kama hii sio mbinu ya wakubwa kuzisogeza fedha karibu ili wazipige kama walivyofanya kwenye Escrow Account?
Haya Maswali yakijibiwa, yatahalalisha uamuzi huo. Vinginevyo kutakuwa na shaka ya kuleta Escrow Season II, ambapo kwenye Season I watu walijibebea fedha kwenye sandarusi, Rambo, lumbesa, mabegi n.k. toka pale pale BOT.
Hayo tu kwa leo.