TAHADHARI: Angalizo kwa wanaoingia na magari Uwanja wa Ndege wa Dar(JNIA)

Kanye2016

JF-Expert Member
Jun 4, 2016
2,466
2,440
Nimeona sio vibaya nikatoa tahadhari au angalizo kwa ndugu zangu wenye usafiri binafsi ambao wanapenda kwenda nao Airport ya Julius Nyerere International Airport either kusindikiza ndugu jamaa na marafiki au kupokea wasafiri.

Katika hali ya serikali kuongeza mapato kumetokea na ongezeko la faini nyingi pale JNIA, mfano wiki iliyopita na wiki hii iliyoanza leo nimejionea watu wakitozwa faini kwa makosa ambayo kawaida hayakuwa yakitozwa.

Mfano wa makosa hayo ni kama;-

1) Ukiegesha gari lako katika parking iliyowekwa na matairi ya gari lako yakikanyaga mstari mmoja au yote ujue gari litawekwa minyororo na utatakiwa ulipe faini. Unachotakiwa ukipaki gari lako hakikisha lipo ndani ya mistari miwili ile iliyopo, kabla ya kuondoka hakikisha unakagua maana itakutoka si chini ya mwekundu.

2) Ukisahau kufunga dirisha au ukafunga lakini pakawa na nafasi ya mtu kuingiza hata mkono ujue utapigwa faini tu, gari litawekwa minyororo ile na haitoki lazima utoe chao kwanza.

3) Hakikisha ukifika airport egesha gari lako na wewe utoke ndani ya gari, kama ni dereva nenda kule arrival au departure ukasubiri kule maana ukikaa ndani kwenye gari lililoegeshwa ni kosa pia wakikukuta wenye njaa zao utalipa faini tu na risiti utapewa.

4) Halikadharika, pakiwa na mlango wa gari umesahau kuufunga utalipishwa faini tu.

N.B: Kuna watu wamepewa kazi hiyo ya kukagua gari baada ya gari yaliyokuwa yameegeshwa pale wakisaidiana na askari polisi wanaozungunga pale; so muwe makini na vyombo vyenu.

Na hayo ni baadhi tu ya makosa ambayo nimeyaona binafsi na watu wakalipishwa faini, hivyo kuweni makini.
 
Hivi siku hizi mbona TRA hawatutangazii kwa mbwe mbwe kuvuka malengo ya ukusanyaji wa kodi!!!
 
Asante. Ila namba 2 haieleweki
Hyo nimeiona leo kuna jamaa alisahau kufunga dirisha la gari (kioo cha nyuma siti ya abiria kilikuwa kipo nusu haikufungwa chote mpaka juu), kuna dada akapita alivyoliona akawaita wenzake wakaja na minyororo likafungiwa ikambidi atoe faini ndo wakamuachia.
 
Hyo nimeiona leo kuna jamaa alisahau kufunga dirisha la gari (kioo cha nyuma siti ya abiria kilikuwa kipo nusu haikufungwa chote mpaka juu), kuna dada akapita alivyoliona akawaita wenzake wakaja na minyororo likafungiwa ikambidi atoe faini ndo wakamuachia.
Hukuuliza kwanini ukisahau kioo unapigwa faini? Sioni mantiki,gari langu nina uhuru wa kuamua nifunge au nisifunge dirisha.
 
Hyo nimeiona leo kuna jamaa alisahau kufunga dirisha la gari (kioo cha nyuma siti ya abiria kilikuwa kipo nusu haikufungwa chote mpaka juu), kuna dada akapita alivyoliona akawaita wenzake wakaja na minyororo likafungiwa ikambidi atoe faini ndo wakamuachia.
Wamewakuta wajinga wajinga aseee
 
Sasa nimelikumbuka neno la mkuu wa kaya; "Hao wenye magari ni matajiri". Hapa ninaamini kuwa Tz kuwa na gari ni utajiri mkubwa. Fikiri, umejikakamua ununue mafuta kuweka kwenye gari ili uje kumpokea mgeni wako. Ukakausha pochi, ukifika pale JNIA ukapaki vibaya, ukasahau kuufunga mlango kwa kumkimbilia mgeni, ukasahau kupandisha kioo Je hiyo fine utaweza kuilipa?? Ndo mwanzo wa kulia kilio mbele za watu kuomba tu udhalilike ili uuondoe huo mkweche wako. Hakika namba itasomeka tu.
 
Sasa nimelikumbuka neno la mkuu wa kaya; "Hao wenye magari ni matajiri". Hapa ninaamini kuwa Tz kuwa na gari ni utajiri mkubwa. Fikiri, umejikakamua ununue mafuta kuweka kwenye gari ili uje kumpokea mgeni wako. Ukakausha pochi, ukifika pale JNIA ukapaki vibaya, ukasahau kuufunga mlango kwa kumkimbilia mgeni, ukasahau kupandisha kioo Je hiyo fine utaweza kuilipa?? Ndo mwanzo wa kulia kilio mbele za watu kuomba tu udhalilike ili uuondoe huo mkweche wako. Hakika namba itasomeka tu.
Bora mimi nimejiamulia kuwa dereva wa Uber. Ubishoo tupa kule. Njaa sooo
 
Hukuuliza kwanini ukisahau kioo unapigwa faini? Sioni mantiki,gari langu nina uhuru wa kuamua nifunge au nisifunge dirisha.
Jamaa aliuliza akajibiwa na wale askari polisi kuwa kuna kesi nyingi zinapelekwa kwa mabosi wao kuwa watu wanaibiwa vitu vyao wakiwa wameegesha magari yao pale. Sasa wao kama askari wanaotakiwa walinde maeneo yale wanaonekana na mabosi zao kama hawafanyi kazi vizuri so now wameanza kufatilia makosa kama hayo ili watu wasijisahau au wasiweke vitamanisho vikapelekea mtu akawaibia.
 
Nimeona sio vibaya nikatoa tahadhari au angalizo kwa ndugu zangu wenye usafiri binafsi ambao wanapenda kwenda nao Airport ya Julius Nyerere International Airport either kusindikiza ndugu jamaa na marafiki au kupokea wasafiri.

Katika hali ya serikali kuongeza mapato kumetokea na ongezeko la faini nyingi pale JNIA, mfano wiki iliyopita na wiki hii iliyoanza leo nimejionea watu wakitozwa faini kwa makosa ambayo kawaida hayakuwa yakitozwa.

Mfano wa makosa hayo ni kama;-

1)Ukiegesha gari lako katika parking iliyowekwa na matairi ya gari lako yakikanyaga mstari mmoja au yote ujue gari litawekwa minyororo na utatakiwa ulipe faini. Unachotakiwa ukipaki gari lako hakikisha lipo ndani ya mistari miwili ile iliyopo, kabla ya kuondoka hakikisha unakagua maana itakutoka si chini ya mwekundu.

2)Ukisahau kufunga dirisha au ukafunga lakini pakawa na nafasi ya mtu kuingiza hata mkono ujue utapigwa faini tu, gari litawekwa minyororo ile na haitoki lazima utoe chao kwanza.

3)Hakikisha ukifika airport egesha gari lako na wewe utoke ndani ya gari, kama ni dereva nenda kule arrival au departure ukasubiri kule maana ukikaa ndani kwenye gari lililoegeshwa ni kosa pia wakikukuta wenye njaa zao utalipa faini tu na risiti utapewa.

4) Halikadharika pakiwa na mlango umesahau kufunga utalipishwa faini tu.

N.B kuna watu wamepewa kazi hyo ya kukagua gari baada ya gari yaliyokuwa yameegeshwa pale wakisaidiana na askari polisi wanaozungunga pale so muwe makini na vyombo vyenu. Na hayo ni baadhi tu ya makosa ambayo nimeyaona binafsi na watu wakalipishwa faini, so kuweni makini.
hao wanaokagua na kushika magari ya watu nitawatofautishaje na waharifu
 
29 Reactions
Reply
Back
Top Bottom