duda
Senior Member
- Mar 23, 2011
- 113
- 25
Habari wana JF, napenda kuwatahadhalisha hasa wanawake na handbags zetu, kuna wizi umezuka hasa maeneo ya kuanzia kijitonyama mpaka mwenge, wanaoiba wanatumia pikipiki, yn anakua dereva na mtu mmoja nyuma then dereva anakumulika taa then anasimama karibu kabisa na wewe, halafu yule mtu wa nyuma anakwapua pochi yako na dereva mara anaondoa pikipiki, imemtokea mdada mmoja juzi pale Bamaga japo alijitahidi kuing'ang'ania pochi yake alichoambulia ni kuburuzwa na kuchunika maana dereva tayari alishaondoa pikipiki hivyo ikabidi aiachie ili asiendelee kuumia.
Tahadhali jamani, tuweni makini na mikoba yetu!!!
nawasilisha
Tahadhali jamani, tuweni makini na mikoba yetu!!!
nawasilisha