Tafsiri ya Mwongozo wa Spika kuhusu hoja ya Kumwondoa Waziri Mkuu

Kiranja

JF-Expert Member
May 19, 2007
751
336
Kwa kuwa spika kaamua kwa makusudi kupindisha katiba na kanuni za Bunge na akiwa na lengo moja tuu la kuuhadaa umma wa watanzania walioko nje kuwa kinachofanyika hakina mantiki, ila ni jambo tuu ambalo linafanywa na watu ambao hawana au hawajui utaratibu , ni mwongozo wa ajabu sana kuwahi kutolewa na Spika yeyote yule.

Katiba inachosema ni kuwa ili kuweza kumwondoa Waziri mkuu lazima hoja iwasilishwe kwa maandishi na iwe imeungwa mkono na wabunge asilimia 20 ya wabunge wote .Sasa jambo la ajabu la kwanza ni kuwa Spika hajapelekewa hoja mezani kwake na katika mazingira ya ajabu kabisa anatoa uamuzi wa jambo ambalo halijawasilishwa kwake kwani anapaswa alipokee kwa maandishi.

Mbili, alichofanya Zitto jana na kutoa tangazo kwa wabunge ambao wako tayari kupiga kura ya kumwondoa PM na hoja yake ilipaswa kuungwa mkono na wabunge kwa kusaini kuwa wanaunga mkono hoja ya kupiga kura ya kukosa imani na waziri mkuu. Sasa huyu Mama anaamua kutoa hukumu kwenye jambo ambalo halipo ni uamuzi wa ajabu kabisa na linaonyesha uwezo wake ulivyo mdogo katika kutazama mambo na kuweza kuyaamulia .

Tatu, hakuna Mbunge ambaye amesema kuwa kesho ndio PM anaondolewa , ila kwenye kanuni za bunge wameandika kwenye kifungu cha 133 (3) "hoja ya kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu haitajadiliwa na Bunge isipokuwa tuu kama ;
(a) "taarifa ya maandishi iliyowekwa saini na kuungwa mkono na wabunge wasiopungua asilimia ishirini ya wabunge wote itatolewa kwa Spika,siku zisizopungua kumi na nne kabla ya siku inayokusudiwa kuwasilishwa Bungeni";

sasa kiherehere cha spika kutoa uamuzi wakati hoja haijawasilishwa kwake nini maana yake?

Kifungu cha (4) "Hoja inayotolewa chini ya kanuni hii na iliyotimiza masharti ya katiba,itawasilishwa Bungeni mapema iwezekanavyo na itaamuliwa kwa kura za siri"

sasa hapa kifungu hiki ndio naona kinamfanya mama kiti kisiweze kuenea kwani anatakiwa kuiwasilisha mapema iwezekanavyo na kama ataona kuwa mapema ni Bunge lijalo ama atapaswa kuitisha Bunge hapo ntawaachia magwiji wa sheria waweze kuliongelea maana , kama hatafanya hivyo, hivi PM ambaye wabunge hawana imani naye atapaswa kupisha mpaka kura iamue ama ataendelea kukalia kiti? Hapa ndipo penye presha kwa mama na wabunge wa CCM.

Huu ni sehemu ya ushahidi mkubwa kuwa Spika wa Bunge huwa hafuati kanuni katika kufanya maamuzi yake , na hivyo anapaswa na yeye kufanyiwa kazi kwa mujibu wa kanuni za bunge kifungu cha 134 ambacho hakihitaji hata saini za wabunge ila ni mbunge mmoja kuwasilisha taarifa hiyo na hatimaye atapigiwa kura na theluthi mbili ya wabunge.

Nafikiri, kuna haja sasa kwa wananchi wetu kila mmoja akawa anawaelewesha kuhusiana na kanuni na sheria mbalimbali ili pindi wanapopotosha basi wakutane na wananchi ambao wanaelewa
 
Nimesema CDM watumie hii list na ile ripoti ya CAG na nyingine ili iwamalize tu. After all wao waendelee kulindana na CDM wanaendelea kuvua kanda ya ZIWA!! Kazi ipo.
 
Janja ya nyani itawatokea puani soon or later...

Wananchi tuko macho sana
 
Ilikuwa utashi na kwa maslahi ya waliomweka huyo mama kwenye kiti kuwa apatikane mwenye uwezo kama wa huyu mama ili aendeshwe remotely.
 
asante kwa ufafanuzi! ila wakati anatoa huu muongozo nilitarajia gwiji la sheria na kanuni za bunge kamanda Tundu asimame nae aombe muongozo! lakini kimya sijui kama yupo bungeni!!
 
Janja ya nyani itawatokea puani soon or later...

Wananchi tuko macho sana

Hofu kubwa kwa wabunge wa CCM inatokana na ukweli kuwa kura hizi ni za siri ,sasa zikipigwa atapona? na msishangae kanuni zikabadilishwa kuwa ili uweze kupeleka hoja lazima uungwe mkono na asilimia hamsini ya wabunge wote , subiri mtaona .

Nchi hii iko karibu sana na kupata ukombozi na hakuna wa kuweza kuzuia ukombozi kupatikana kwani ni suala la madakika tuu ndio limebakia .
 
Tatizo kubwa ninaloliona hapo ni mgongano wa kiutawala na kichama zaidi. Spika wa Bunge ni mwanachama wa CCM na ana vyeo ndani ya chama chake (CCM). Ikiwezekana nafasi ya Uspika na uchama utenganishwe kwenye Katiba mpya. Pengine hii inaweza kuondoa migongano ya kiutawala na kuisaidia nchi yetu isonge mbele zaidi.
 
Hata mimi nimeshangaa kuona Spika bi kiriboto kutolea mwongozo kusudio ambalo halijawasilishwam kweli magamba sasa wanafunika tu kombe mwanaharamu apite. Wenye akili w ameshang'amua
 
Kwa kuwa spika kaamua kwa makusudi kupindisha katiba na kanuni za Bunge na akiwa na lengo moja tuu la kuuhadaa umma wa watanzania walioko nje kuwa kinachofanyika hakina mantiki, ila ni jambo tuu ambalo linafanywa na watu ambao hawana au hawajui utaratibu , ni mwongozo wa ajabu sana kuwahi kutolewa na Spika yeyote yule.

Katiba inachosema ni kuwa ili kuweza kumwondoa Waziri mkuu lazima hoja iwasilishwe kwa maandishi na iwe imeungwa mkono na wabunge asilimia 20 ya wabunge wote .Sasa jambo la ajabu la kwanza ni kuwa Spika hajapelekewa hoja mezani kwake na katika mazingira ya ajabu kabisa anatoa uamuzi wa jambo ambalo halijawasilishwa kwake kwani anapaswa alipokee kwa maandishi.

Mbili, alichofanya Zitto jana na kutoa tangazo kwa wabunge ambao wako tayari kupiga kura ya kumwondoa PM na hoja yake ilipaswa kuungwa mkono na wabunge kwa kusaini kuwa wanaunga mkono hoja ya kupiga kura ya kukosa imani na waziri mkuu. Sasa huyu Mama anaamua kutoa hukumu kwenye jambo ambalo halipo ni uamuzi wa ajabu kabisa na linaonyesha uwezo wake ulivyo mdogo katika kutazama mambo na kuweza kuyaamulia .

Tatu, hakuna Mbunge ambaye amesema kuwa kesho ndio PM anaondolewa , ila kwenye kanuni za bunge wameandika kwenye kifungu cha 133 (3) "hoja ya kura ya kutokuwa na imani na waziri mkuu haitajadiliwa na Bunge isipokuwa tuu kama ;
(a) "taarifa ya maandishi iliyowekwa saini na kuungwa mkono na wabunge wasiopungua asilimia ishirini ya wabunge wote itatolewa kwa Spika,siku zisizopungua kumi na nne kabla ya siku inayokusudiwa kuwasilishwa Bungeni";

sasa kiherehere cha spika kutoa uamuzi wakati hoja haijawasilishwa kwake nini maana yake?

Kifungu cha (4) "Hoja inayotolewa chini ya kanuni hii na iliyotimiza masharti ya katiba,itawasilishwa Bungeni mapema iwezekanavyo na itaamuliwa kwa kura za siri"

sasa hapa kifungu hiki ndio naona kinamfanya mama kiti kisiweze kuenea kwani anatakiwa kuiwasilisha mapema iwezekanavyo na kama ataona kuwa mapema ni Bunge lijalo ama atapaswa kuitisha Bunge hapo ntawaachia magwiji wa sheria waweze kuliongelea maana , kama hatafanya hivyo, hivi PM ambaye wabunge hawana imani naye atapaswa kupisha mpaka kura iamue ama ataendelea kukalia kiti? Hapa ndipo penye presha kwa mama na wabunge wa CCM.

Huu ni sehemu ya ushahidi mkubwa kuwa Spika wa Bunge huwa hafuati kanuni katika kufanya maamuzi yake , na hivyo anapaswa na yeye kufanyiwa kazi kwa mujibu wa kanuni za bunge kifungu cha 134 ambacho hakihitaji hata saini za wabunge ila ni mbunge mmoja kuwasilisha taarifa hiyo na hatimaye atapigiwa kura na theluthi mbili ya wabunge.

Nafikiri, kuna haja sasa kwa wananchi wetu kila mmoja akawa anawaelewesha kuhusiana na kanuni na sheria mbalimbali ili pindi wanapopotosha basi wakutane na wananchi ambao wanaelewa

Kamanda nakubaliana na wewe hasa hapo kwenye RED. najua akina Zitto wanapitia hoja hizi.
 
Hoja ya Mh. Zitto haijapigwa chini per se coz mpaka bunge lijalo kigezo cha siku 14 kitakuwa kimetimia, swala liliopigwa chini ni kuwasilisha hoja iyo jumatatu kwani zitakuwa zimetimia siku 4 tu, hivyo basi nafasi ya hoja hii bado ipo hai.
 
Bi mkora at work. Spika hovyo kabisa kati ya maspika wote waliopata kutokea. Na hii imetokana na: -
1. Uongozi mbovu kabisa wa CCM kupaata kutokea
2. Rais dhaifu zaidi kupata kutawala TZ
3. Waziri mkuu mnyonge zaidi kuwahi kutokea
4. Bunge lililokusanya wabunge wa CCM, wa hovyo kabisa (wakiongozwa na Lusinde) kuliko bunge lolote lililopita
5. Na matokeo lazima yawe Spika taka........taka, hafai hata kuliwa na kunguru mla mizoga. Labda awe chakula ya kitimoto.
 
Hao watu wajimboni kwa huyo mwanamke waliompigia kura na wanaoendelea kumuamini ndo wanaotuzorotesha,kwani dawa ni kutokumchagua mama huyu.
 
Wadau naomba kila mmoja wetu ajiulize hivii.
Inawezekanaje kutolea mwongozo kusudio???????
Nawasillisha
 
Hivi ANNE, kapata mume??! Yule ni changu tu yule. 2015 atafute kichaka cha kujificha
 
Safi Kiranja..., Mi ninaomba na huyu mama atafutiwa kura za kukosa nae imani (sababu mimi sina wala sijawahi kuwa na imani nae), Tena huyu am sure hata kura ya Sitta na kundi lake mtazipata (nadhani anawaza ugumu wa maisha Dodoma)
 
Hoja ya Mh. Zitto haijapigwa chini per se coz mpaka bunge lijalo kigezo cha siku 14 kitakuwa kimetimia, swala liliopigwa chini ni kuwasilisha hoja iyo jumatatu kwani zitakuwa zimetimia siku 4 tu, hivyo basi nafasi ya hoja hii bado ipo hai.
Ingawa wewe ni gwanda, hapo umetoa pointi.
 
mvua inyeshe ama jua liwake ukombozi ni lazima, wanavyozidi kujichanganya ndivyo wanavyozidi onesha udhaifu wa kila upande. hawa ni viongozi wa mihimili wako hivyo hao mawaziri, wakuu wa mikoa na ma-DC ndio usiseme. hata walie viboko lazima wapate.
 
NAAMINI MUNGU YU PAMOJA NASI! Kamwe hila za magamba na shetani wao wa ufisadi hawawezi kushinda!! MUNGU IBARIKI TANZANIA, MUNGU MLINDE ZITTO KABWE
 
Spika anajirudi kwa muongozo wake , anajisahihisha kama ambavyo nimesema hapo juu.
 
asante kwa ufafanuzi! ila wakati anatoa huu muongozo nilitarajia gwiji la sheria na kanuni za bunge kamanda Tundu asimame nae aombe muongozo! lakini kimya sijui kama yupo bungeni!!

Lazima ataomba mwongozo
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom