Tafsiri Ya Mahakama Kuu Kenya Kutangaza Uchaguzi Mkuu Kenya Ni Batili..

maggid

JF-Expert Member
Dec 3, 2006
1,084
1,246
Ndugu zangu,

Tafsiri yake; Kilichoangaliwa na Majaji si matokeo , bali mchakato wa uchaguzi. Kwamba mchakato ulikuwa batili. Na ilivyo, mchakato unaweza kuathiri matokeo.

Kenya imethibitisha kuwa Mahakama ni kimbilio la mnyonge na mwenye nguvu. Ndivyo inavyotakiwa iwe. Raila Odinga alionekana kichekesho na wale waliokuwa wakiamini kuwa Afrika mgombea aliye madarakani akishinda ni kujisumbua kwenda mahakamani. Hongera Sana Kenya kwa kuionyesha dunia kuwa Afrika uhuru wa Mahakama upo, na kwamba anayeshindwa uchaguzi kama anaona hakutendewa haki aende mahakamani, na si kuandamana na kufanya vurugu.

Maggid,

Iringa.
 
Ingekuwa kwetu baada ya watu kuibiwa kura badala ya mtu aliyeibiwa kutakiwa kwenda mahakamani kudai haki yake,vyombo vya dola vingekuwa vinafanya mazoezi mitaani kumtisha aliyeibiwa kura asiendelee kupiga kelele.
 
Ndugu zangu,

Tafsiri yake; Kilichoangaliwa na Majaji si matokeo , bali mchakato wa uchaguzi. Kwamba mchakato ulikuwa batili. Na ilivyo, mchakato unaweza kuathiri matokeo.

Kenya imethibitisha kuwa Mahakama ni kimbilio la mnyonge na mwenye nguvu. Ndivyo inavyotakiwa iwe. Raila Odinga alionekana kichekesho na wale waliokuwa wakiamini kuwa Afrika mgombea aliye madarakani akishinda ni kujisumbua kwenda mahakamani. Hongera Sana Kenya kwa kuionyesha dunia kuwa Afrika uhuru wa Mahakama upo, na kwamba anayeshindwa uchaguzi kama anaona hakutendewa haki aende mahakamani, na si kuandamana na kufanya vurugu.

Maggid,

Iringa.
Afrika au Kenya?Tz kwetu vipi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu zangu,

Tafsiri yake; Kilichoangaliwa na Majaji si matokeo , bali mchakato wa uchaguzi. Kwamba mchakato ulikuwa batili. Na ilivyo, mchakato unaweza kuathiri matokeo.

Kenya imethibitisha kuwa Mahakama ni kimbilio la mnyonge na mwenye nguvu. Ndivyo inavyotakiwa iwe. Raila Odinga alionekana kichekesho na wale waliokuwa wakiamini kuwa Afrika mgombea aliye madarakani akishinda ni kujisumbua kwenda mahakamani. Hongera Sana Kenya kwa kuionyesha dunia kuwa Afrika uhuru wa Mahakama upo, na kwamba anayeshindwa uchaguzi kama anaona hakutendewa haki aende mahakamani, na si kuandamana na kufanya vurugu.

Maggid,

Iringa.
Maggid wewe ni mnafiki Sana, hakuna mtu mnafiki Kama wewe.
Kwa hiyo ulimaanisha kuwa na siye Tanzania tuwe tunaenda mahakamani na tusiandamane?
Matokeo ya urais Tanzania hayaruhusiwi kuhojiwa mahakamani kwa katiba mbovu ya ma ccm , ndo maana huwa tunaandamana.
Wewe umeandika kinafiki kutunanga wapinzani acha unafiki Maggid.
 
Wapenda mabadiliko ya kweli tukomae na katiba mpya itayoleta mapinduzi ya msingi. Upinzani wanatuzingua na siasa zao za matukio ..
 
Kiukweli Kwa ishu ya demokrasia Kenya wametuzidi sana! Hata huyu Kenyata anaonekana ni mtu wa kuheshimu katiba! Mungu awape busara hawa ccm na wao waruhusu demokrasia kama hii tunayoiona Kenya! Hakika tunalo la kujifunza hapa!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom