Tafsiri ya Kitanzania ya Ugaidi, uchochezi na kuvuruga amani na umoja wa kitaifa

Hamatan

JF-Expert Member
Nov 10, 2020
3,183
7,645
Kuna msemo unasema matendo huongea zaidi kuliko maneno.

Sasa hivi, kila kona ya nchi ni kesi ya ugaidi dhidi ya Mbowe. Wapo wanaosema kuwa kesi hiyo ya ugaidi dhidi ya Mbowe na Makomandoo wetu, ni ya kuwabambikizia. Wanasema hivi kutokana na mazingira ya hawa watu kupewa hiyo kesi, kukosekana kwa kiashiria chochote mpaka sasa cha kuashiria mipango na maandalizi ya ugaidi:

1) kwenye mipango - hakuna shahidi hata mmoja wa upande wa Serikali aliyethibitisha kulikuwa na vikao vya kupanga ugaidi namna utakavyotekeleza

2) kwenye maandalizi - hakuna shahidi yeyote aliyeonesha au aliyeleta zana zilizoandaliwa kutekeleza ugaidi.

Lakini hawa wote wanaosema kuwa kesi hii ya ugaidi ni ya kubambikiza, wanalalia kwenye maana ya ugaidi kama ilivyotafsiriwa kimataifa.

Lakini kwa tafsiri ya kimatendo ya Polisi, Serikali, CCM, na Rais wa Tanzania, maana ya ugaidi, uchochezi, na kuvuruga amani, vina tafsiri tofauti kabisa.

1) Ugaidi - kwa kuzingatia kauli za mara kwa mara za Polisi, na kauli ya Samia, bila shaka, gaidi ni mtu yeyote ambaye anapingana na kauli ya Rais. Yena Samia alifafanua vizuri sana maana ya ugaidi kwa tafsri ya Kitanzania, pale alipokuwa akijibu ombi la Zito, aliposema kuwa Mbowe hakumheshimu. Kwa hiyo kutomheshimu yeye Samia, ni ugaidi. Rais alisema kwamba suala la katiba mpya lisubiri. Mbowe akasema hatuwezi kusubiri. Kwa sababu Mbowe alipinga kauli ya Rais, hivyo ni gaidi.

2) Uchochezi - CCM imekuwa ikifurahia ujinga wa Watanzania. CCM inawaambia Watanzania ni matajiri, lakini wakati huo huo wapo wanaoshindwa kupata hata milo mitatu iliyo bora. Mtanzania yeyote anaweza kuwekwa ndani na DC masaa 48, halafu akakuachia. Huna hata pa kuhoji. Ukiwaambia wananchi kuwa hiyo siyo haki, wewe ni mchochezi kwa sababu watanzania wanatakiwa wabakie kwenye ujinga, kwa nini wewe unataka waondoke kwenye ujinga? Hilo ni kosa la uchochezi.

3) Kuvuruga Amani - kwa tafsiri ya kimatendo, kwa Tanzania, kuvuruga amani ni kuuweka ukweli mahali peupe. Ukweli unaohusiana na uchafu wa muundo mbaya wa utawala unatakiwa kufichwa. Ukisema kwamba mihimili miwili, yaani Bunge na Mahakama, ipo tu kinadharia, lakini kiuhalisia ipo kwenye kwapa za Rais kwa sababu Jaji mkuu anateuliwa na Rais, majaji wanateuliwa na Rais, viongozi wote wa mahakama huteuliwa na Rais, na huko Bungeni, Rais asipomtaka spika au mbunge yeyote atamfukuza kama alivyofanyiwa Ndugai au Tundu Lisu, wewe unahatarisha amani ya nchi. Kwa nini unayaweka mambo ya kweli hadharani, wakati kila mtanzania jukumu lake kuu alilolipewa kwa njia ya kificho ni kumsifia na kumwabudu Rais?

4) kuharibu Umoja wa Kitaifa - kwa tafsiri ya kimatendo ya CCM, Serikali, Polisi na Rais, umoja wa kitaifa, unakuwepo kama wote mkikubaliana kuishi katika ujinga na kuruhusu mtu mmoja tu kufikiri. Angalia umoja ulioopo ndani ya CCM. CCM, kwa utafiti wa TWAWEZA ndiyo chama kinachopendwa zaidi na wajinga. Na kutokana na kuwa na wajinga wengi, mshikamano wao ni mkubwa, na huo ndio umoja wa kitaifa unaotakiwa kuwepo. Sasa ukitaka wewe kufikiri badala ya kumsifu Rais na kuitikia tu NDIYOOOO, unahatarisha Umoja wa Kitaifa.

Kwa hiyo kwa tafsiri ya kimatendo ya CCM, Serikali, Polisi na Rais, Mbowe ni gaidi.

Kwa tafsiri ya kimatendo ya CCM, serikali, Polisi na Rais, wanaofikiri na kuhoji, wote hao wanahatarisha amani, umoja wa kitaifa, na ni wachochezi. Hivyo ni wahalifu.

Kuna machaguo mawili tú - moja ni kuukana utu wetu ili tusiwe magaidi, wachochezi, wavurugaji wa amani na umoja wa kitaifa; na ya pili ni kutii dhamira na utu wetu kama binadamu, dhamira zetu zinazoishi katika ukweli unaotambua kuwa:

1) kuwa Rais haimaanishi mtu ana akili na maarifa kuwazidi watanzania wote. Jukumu lake Rais ni kutengeneza tu mazingira ili karama, vipaji, maarifa na ujuzi wa watu mbalimbali, viweze kustawi na kutumika kwa manufaa ya nchi (mwili ni mmoja, viungo ni vingi).

2) polisi ni mlinzi wa raia. Polisi ni mwajiriwa wa raia, siyo mkubwa kuliko mwajiri wake. Mwajiriwa mjinga, muuaji, mbambikiaji kesi, mwongo, mporaji, anatakiwa kufukuzwa mara moja, iwe kwa hiari au kwa nguvu.

3) mwenye mamlaka ya kuweka mipaka ya mihimili ni mwananchi, na siyo Rais. Wananchi, kwa kupitia katiba, ndio wenye mamlaka ya kuweka ukomo wa kiutendaji na kiutawala wa Rais, Serikali, Bunge, Mahakama, DPP, DCI, Polisi, na ofisi nyingine zote. Mamlaka haya ni ya umma, siyo ya Rais. Anayekiuka au kuvuka mipaka ya katiba, bila ya kujali kama ni Rais, Jaji Mkuu au Spika, anatakiwa kufukuzwa mara moja.
 
Uko sahihi asilimia Zote lakini nilichokuja kugundua hapa nchini kwetu viongozi wengi tulionao zaidi ya 80% Wana akili ndogo Sana kiasi kwamba vyeo walivyonavyo vinawazidi uwezo in short ni useless.

Hawaoni mbele na hawajui nchi baada ya miaka kadhaa inatakiwa iwe wapi kiuchumi wanachofanya ni Bora liende .Ndo Mana viongozi wengi tulionao Kila wakiamka wanawaza waibeje Mali ya uma na sio kubuni njian za kukuza uchumi wa Nchi na Wananchi wake.

Sasa Hapa tunafanyaje njia ni moja tu Wananchi kwa ujmla wetu tukatae Huu uhuni kwa njia za amani hasa kishinikiza kwa nguvu Zote tuwe na katiba mpya.
 
Kuna msemo unasema matendo huongea zaidi kuliko maneno.

Sasa hivi, kila kona ya nchi ni kesi ya ugaidi dhidi ya Mbowe. Wapo wanaosema kuwa kesi hiyo ya ugaidi dhidi ya Mbowe na Makomandoo wetu, ni ya kuwabambikizia...
Mkuu jiandae kwa kejeli na dhihaka toka kwa wazalendo wa CCM.Umesema yote vema lakini utawasikia waimba mapambio watakavyofoka.Utaambiwa wewe siyo Raia wa Tanzania maana kwa mujibu wa CCM Watanzania ni wajinga wasioweza kuhoji na kunena ukweli.

Tunahitaji Katiba mpya haraka ili tuponywe dhidi ya udhalimu.
 
Kinachotakiwa kukifanya km watanzania ni kumuombea mh rais ili kimkute kama kilichomkuta jiwe ili na yeye tuka mdampo kwao zenjibaa
 
nilichokuja kugundua hapa nchini kwetu viongozi wengi tulionao zaidi ya 80% Wana akili ndogo Sana kiasi kwamba vyeo walivyonavyo vinawazidi uwezo in short ni useless. Hawaoni mbele na hawajui nchi baada ya miaka kadhaa inatakiwa iwe wapi kiuchumi wanachofanya ni Bora liende
imagine Samia anatokea mbele ya chombo cha kimataifa anaiambia dunia wana ushahidi Mbowe ni gaidi,huku kesi ikiwa mahakamani.halafu huyo Rais ☹☹☹
 
Prof.Assad kasha liona hili muda mrefu Sana "60% ya:viongozi waliopo serikalini wanauwezo mdogo" na mbaya zaidi wanajifanya kuvaa viatu ambavyo haviwatoshi yale yale ya Mwal.JKN na "kaptula la Marx"
 
Mkuu jiandae kwa kejeli na dhihaka toka kwa wazalendo wa CCM.Umesema yote vema lakini utawasikia waimba mapambio watakavyofoka.Utaambiwa wewe siyo Raia wa Tanzania maana kwa mujibu wa CCM Watanzania ni wajinga wasioweza kuhoji na kunena ukweli.
Tunahitaji Katiba mpya haraka ili tuponywe dhidi ya udhalimu.
Haishangazi maana waziri mzima, wakati watu wanahoji kuhusu tozo, anawaambia wanaohoji wahamie Burundi. Unajiuliza, yeye ni nani hata awaambie watu wanapohoji mambo yanayowahusu, wahame nchi! Kwa nini yeye aliye kinyume cha wengi, asiende huko Burundi?
 
Kuna msemo unasema matendo huongea zaidi kuliko maneno.

Sasa hivi, kila kona ya nchi ni kesi ya ugaidi dhidi ya Mbowe. Wapo wanaosema kuwa kesi hiyo ya ugaidi dhidi ya Mbowe na Makomandoo wetu, ni ya kuwabambikizia. Wanasema hivi kutokana na mazingira ya hawa watu kupewa hiyo kesi, kukosekana kwa kiashiria chochote mpaka sasa cha kuashiria mipango na maandalizi ya ugaidi:

1) kwenye mipango - hakuna shahidi hata mmoja wa upande wa Serikali aliyethibitisha kulikuwa na vikao vya kupanga ugaidi namna utakavyotekeleza

2) kwenye maandalizi - hakuna shahidi yeyote aliyeonesha au aliyeleta zana zilizoandaliwa kutekeleza ugaidi.

Lakini hawa wote wanaosema kuwa kesi hii ya ugaidi ni ya kubambikiza, wanalalia kwenye maana ya ugaidi kama ilivyotafsiriwa kimataifa.

Lakini kwa tafsiri ya kimatendo ya Polisi, Serikali, CCM, na Rais wa Tanzania, maana ya ugaidi, uchochezi, na kuvuruga amani, vina tafsiri tofauti kabisa.

1) Ugaidi - kwa kuzingatia kauli za mara kwa mara za Polisi, na kauli ya Samia, bila shaka, gaidi ni mtu yeyote ambaye anapingana na kauli ya Rais. Yena Samia alifafanua vizuri sana maana ya ugaidi kwa tafsri ya Kitanzania, pale alipokuwa akijibu ombi la Zito, aliposema kuwa Mbowe hakumheshimu. Kwa hiyo kutomheshimu yeye Samia, ni ugaidi. Rais alisema kwamba suala la katiba mpya lisubiri. Mbowe akasema hatuwezi kusubiri. Kwa sababu Mbowe alipinga kauli ya Rais, hivyo ni gaidi.

2) Uchochezi - CCM imekuwa ikifurahia ujinga wa Watanzania. CCM inawaambia Watanzania ni matajiri, lakini wakati huo huo wapo wanaoshindwa kupata hata milo mitatu iliyo bora. Mtanzania yeyote anaweza kuwekwa ndani na DC masaa 48, halafu akakuachia. Huna hata pa kuhoji. Ukiwaambia wananchi kuwa hiyo siyo haki, wewe ni mchochezi kwa sababu watanzania wanatakiwa wabakie kwenye ujinga, kwa nini wewe unataka waondoke kwenye ujinga? Hilo ni kosa la uchochezi.

3) Kuvuruga Amani - kwa tafsiri ya kimatendo, kwa Tanzania, kuvuruga amani ni kuuweka ukweli mahali peupe. Ukweli unaohusiana na uchafu wa muundo mbaya wa utawala unatakiwa kufichwa. Ukisema kwamba mihimili miwili, yaani Bunge na Mahakama, ipo tu kinadharia, lakini kiuhalisia ipo kwenye kwapa za Rais kwa sababu Jaji mkuu anateuliwa na Rais, majaji wanateuliwa na Rais, viongozi wote wa mahakama huteuliwa na Rais, na huko Bungeni, Rais asipomtaka spika au mbunge yeyote atamfukuza kama alivyofanyiwa Ndugai au Tundu Lisu, wewe unahatarisha amani ya nchi. Kwa nini unayaweka mambo ya kweli hadharani, wakati kila mtanzania jukumu lake kuu alilolipewa kwa njia ya kificho ni kumsifia na kumwabudu Rais?

4) kuharibu Umoja wa Kitaifa - kwa tafsiri ya kimatendo ya CCM, Serikali, Polisi na Rais, umoja wa kitaifa, unakuwepo kama wote mkikubaliana kuishi katika ujinga na kuruhusu mtu mmoja tu kufikiri. Angalia umoja ulioopo ndani ya CCM. CCM, kwa utafiti wa TWAWEZA ndiyo chama kinachopendwa zaidi na wajinga. Na kutokana na kuwa na wajinga wengi, mshikamano wao ni mkubwa, na huo ndio umoja wa kitaifa unaotakiwa kuwepo. Sasa ukitaka wewe kufikiri badala ya kumsifu Rais na kuitikia tu NDIYOOOO, unahatarisha Umoja wa Kitaifa.

Kwa hiyo kwa tafsiri ya kimatendo ya CCM, Serikali, Polisi na Rais, Mbowe ni gaidi.

Kwa tafsiri ya kimatendo ya CCM, serikali, Polisi na Rais, wanaofikiri na kuhoji, wote hao wanahatarisha amani, umoja wa kitaifa, na ni wachochezi. Hivyo ni wahalifu.

Kuna machaguo mawili tú - moja ni kuukana utu wetu ili tusiwe magaidi, wachochezi, wavurugaji wa amani na umoja wa kitaifa; na ya pili ni kutii dhamira na utu wetu kama binadamu, dhamira zetu zinazoishi katika ukweli unaotambua kuwa:

1) kuwa Rais haimaanishi mtu ana akili na maarifa kuwazidi watanzania wote. Jukumu lake Rais ni kutengeneza tu mazingira ili karama, vipaji, maarifa na ujuzi wa watu mbalimbali, viweze kustawi na kutumika kwa manufaa ya nchi (mwili ni mmoja, viungo ni vingi).

2) polisi ni mlinzi wa raia. Polisi ni mwajiriwa wa raia, siyo mkubwa kuliko mwajiri wake. Mwajiriwa mjinga, muuaji, mbambikiaji kesi, mwongo, mporaji, anatakiwa kufukuzwa mara moja, iwe kwa hiari au kwa nguvu.

3) mwenye mamlaka ya kuweka mipaka ya mihimili ni mwananchi, na siyo Rais. Wananchi, kwa kupitia katiba, ndio wenye mamlaka ya kuweka ukomo wa kiutendaji na kiutawala wa Rais, Serikali, Bunge, Mahakama, DPP, DCI, Polisi, na ofisi nyingine zote. Mamlaka haya ni ya umma, siyo ya Rais. Anayekiuka au kuvuka mipaka ya katiba, bila ya kujali kama ni Rais, Jaji Mkuu au Spika, anatakiwa kufukuzwa mara moja.
Kwa andiko hili wewe pia kwa tafsiri yetu ya ki-Tanzania hatutashangaa utakapoitwa gaidi, maana unaleta taharuki na unaweza sababisha tukaandamana bila kikomo.
 
Uko sahihi asilimia Zote lakini nilichokuja kugundua hapa nchini kwetu viongozi wengi tulionao zaidi ya 80% Wana akili ndogo Sana kiasi kwamba vyeo walivyonavyo vinawazidi uwezo in short ni useless. Hawaoni mbele na hawajui nchi baada ya miaka kadhaa inatakiwa iwe wapi kiuchumi wanachofanya ni Bora liende .Ndo Mana viongozi wengi tulionao Kila wakiamka wanawaza waibeje Mali ya uma na sio kubuni njian za kukuza uchumi wa Nchi na Wananchi wake .
Sasa Hapa tunafanyaje njia ni moja tu Wananchi kwa ujmla wetu tukatae Huu uhuni kwa njia za amani hasa kishinikiza kwa nguvu Zote tuwe na katiba mpya.
Kusema Wana akili ndogo nakukatalia. Kwa sababu akili wanayoitumia kuwafanya watanzania kua wajinga ni kubwa mno. Ila kinachowafanya viongozi kua hivi ni kwa sababu tayari walishajiingiza kwenye mfumo wa ukandamizaji, kuua, kupora Mali za umma nk. Ko ni ngumu sana kuona watu hao kuacha matendo mabaya kwa sababu mfumo unamlazimisha. Mfano watu wanasema IGP Siro hajiuzuli kwa sababu ya kuwajibika, ilo hawezi kulifanya kwa sababu naye yuko kwenye huo mfumo. Labda mfumo uamue kumtoa sadaka ili kufunika kombe mwanaharamu apite. Hata Kama yeye ataamua kutubu lakini hatakua na uwezo wa kufanya lolote kwa wenzie kwenye huo mfumo wao wanamjua akimwaga mboga watamwaga ugali na yeye ndo atatolewa sadaka.
Ili kuushinda huu mfumo ni kupata katiba mpya. CCM wanalijua hilo ndio maana wako tayari hata kuua kila atakayesema kuhusu katiba mpya kwa sababu Wana ccm wote wako kwenye huo mfumo. Mi Kuna wakati nilimuona JK kua mzalendo sana alipambana angalau tupate katiba Ila mfumo uliamua kugoma. Na upinzani kipindi kile haukupiga hesabu za mbele kwa sababu Kama sijasahau mchakato uliharibika kwenye serikali tatu. Kitu ambacho hakikua na uhimu sana kuliko ya kuuvunja mfumo. Wangeliacha hili lipite. Hata Kama yasingepatikana yote unakuta nusu yangepatikana. Kwa sababu uwezi kuuvunja huu mfumo kwa Mara moja.
 
Back
Top Bottom