Mshana Jr
Platinum Member
- Aug 19, 2012
- 269,633
- 697,782
Katika utawala wa kirumi ilikuwa ni kawaida sana kufanya GWARIDE katika mitaa mbalimbali siku ya kuwapa MEDANI MAJENERALI wa KIJESHI wanaokuwa wamefanya mambo MAKUBWA na ya KISHUJAA katika nchi.
.
Baada ya gwaride kuisha, jukumu la kumvisha TAJI (crown) jenerali aliyekuwa anapewa heshima lilikuwa ni la MTUMWA mmoja anayechaguliwa ambaye maarufu alikuwa anaitwa jina la “Auriga”.
.
Kazi kubwa ya “Auriga” haikuwa KUVISHA taji bali haswa MANENO ambayo alitakiwa kuongea anapomvisha taji jenerali wa jeshi. Alitakiwa kusema kwa KUMNONG’ONEZA “Memento Homo’(Kumbuka wewe ni mwanadamu tu)(Remember, you are only a human).
.
Maneno haya ambayo ilikuwa lazima yasemwe yalilenga KUMKUMBUSHA kila jenerali kuwa bila kujali USHINDI aliopata, UWEZO aliouonyesha au SIFA anazomiminiwa,ASIRUHUSU hayo yote yakampa KIBURI na AANZE kujiona AMESHAFIKA.
.
Ni rahisi sana KUJISAHAU na mtu ukajiona HAKUNA kama WEWE, ni rahisi KIBURI kukuvamia kwa sababu ya SIFA zinazomiminwa kwako,ni rahisi sana KUDHARAU wengine kwa sababu ya CHEO au PESA ulizonazo.Usipokuwa makini unaweza kujikuta unajiona kama wewe ni “mungu mtu”.Kumbuka,wewe ni mwanadamu tu.
.
Inawezekana hauna mtu wa kukunong’oneza,hauna AURIGA pembeni yako, amua kujikumbusha mwenyewe hata leo na jiambie- “MEMENTO, HOMO”. Ukimuona rafiki yako,kiongozi wako,msanii au bosi wako anayejisahau kujikumbusha, kama unampenda usisahau kumnong’oneza leo-“MEMENTO, HOMO”. Bila Mungu, Bila Unyenyekevu hakuna anayeweza kufika mbali.
.
See You At The Top
.
@joelnanauka_
.
TIMIZAMALENGOYAKO
Jr
.
Baada ya gwaride kuisha, jukumu la kumvisha TAJI (crown) jenerali aliyekuwa anapewa heshima lilikuwa ni la MTUMWA mmoja anayechaguliwa ambaye maarufu alikuwa anaitwa jina la “Auriga”.
.
Kazi kubwa ya “Auriga” haikuwa KUVISHA taji bali haswa MANENO ambayo alitakiwa kuongea anapomvisha taji jenerali wa jeshi. Alitakiwa kusema kwa KUMNONG’ONEZA “Memento Homo’(Kumbuka wewe ni mwanadamu tu)(Remember, you are only a human).
.
Maneno haya ambayo ilikuwa lazima yasemwe yalilenga KUMKUMBUSHA kila jenerali kuwa bila kujali USHINDI aliopata, UWEZO aliouonyesha au SIFA anazomiminiwa,ASIRUHUSU hayo yote yakampa KIBURI na AANZE kujiona AMESHAFIKA.
.
Ni rahisi sana KUJISAHAU na mtu ukajiona HAKUNA kama WEWE, ni rahisi KIBURI kukuvamia kwa sababu ya SIFA zinazomiminwa kwako,ni rahisi sana KUDHARAU wengine kwa sababu ya CHEO au PESA ulizonazo.Usipokuwa makini unaweza kujikuta unajiona kama wewe ni “mungu mtu”.Kumbuka,wewe ni mwanadamu tu.
.
Inawezekana hauna mtu wa kukunong’oneza,hauna AURIGA pembeni yako, amua kujikumbusha mwenyewe hata leo na jiambie- “MEMENTO, HOMO”. Ukimuona rafiki yako,kiongozi wako,msanii au bosi wako anayejisahau kujikumbusha, kama unampenda usisahau kumnong’oneza leo-“MEMENTO, HOMO”. Bila Mungu, Bila Unyenyekevu hakuna anayeweza kufika mbali.
.
See You At The Top
.
@joelnanauka_
.
TIMIZAMALENGOYAKO
Jr