Tafakuri ya tasnia ya filamu tanzania

Da vincci

Member
Aug 9, 2009
61
9
[h=6]Salaam wanabodi,

Kama inavyofahamika kwa wengi kiini cha filamu bora siku zote huanza na muswada bora wa filamu ambao ni zao la hadithi iliyotimilika katika nyanja zote za fasihi.Siku zote nimekua nikiamini muswada wa filamu ni kama ramani au mchoro wa nyumba na mchoraji wa ramani ya nyumba ni kama mwandishi wa filamu! Wote hawa hufikirisha akili zao na kuwasilisha mawazo yao katika Makaratasi,lakini mara nyingi watu hawa hukosa ama taaluma ya kutosha au uwezo wa kutosha kuweza kuyatoa mawazo yao kutoka kwenye makaratasi na kuyaweka katika hali ya uhalisia zaidi (jengo/filamu) ambayo uma au hadhira huvutiwa nayo na kunufaishwa kwa namna moja au nyingine.Ikitokea mchoraji wa ramani ya jengo (architect) akawa na taaluma ya uhandisi (engineering) kimaadili ya taaluma ni ruksa akaendelea na ujenzi vivyo hivyo basi ikatokea mwandishi wa muswada wa filamu akawa na taaluma ya uongozaji wa filamu ni ruksa pia akaendelea na mchakato huo wa utayarishaji wa filamu husika.Lakini ijulikane wazi ya kuwa kila kazi ina miiko yake na walioleta mgawanyiko wa kazi hawakua majuha.

Ndugu zangu leo hii ukimuacha mwandishi wa muswada wa filamu akawa muongozaji hata kama ana taaluma zote mbili kuna hatari kubwa ya kuzuia wigo wa ubunifu ambao ungeweza kuongezwa kwa kuwagawanyia majukumu watu hawa. Mfano huu unakwenda sambamba na maamuzi ya kumuacha mchora ramani ya jengo akawa mhandisi! Kwa mantiki hii katu hautotegemea kupata jipya habadani.

Wandugu,kukosekana huku kwa 'a clear demarcation line of responsibilities' (mstari angavu wa mpishano au mpaka wa majukumu) baina ya pande hizi mbili ambazo kimsingi ndio mihimili ya tasnia nzima ya filamu umepelekea kuwa na zao la 'bora filamu' nyingi zisizo na mguso kwa jamii.
Wengi watakuja na kueleza matatizo mengine lakini mgogoro mkuu utabaki huku chini! Tukitibu huku kwenye shina huko juu itatuwia rahisi,lakini tukiendelea kushupalia huko juu wakati huku chini kumetushinda hatutafanikiwa kamwe!
Watu wanalalamikia maswala ya location (muktadha),casting (ushiriki) n.k vyote hivi ni rahisi ukavirekebisha endapo utakua na msingi mzuri wa waandishi na waongozaji kama mhimili mkuu wa tasnia nzima ya filamu.

Nimekua nikisema mara nyingi ya kwamba uandishi mzuri wa filamu huanza na kipaji kikifuatiwa na mafunzo lakini uongozaji wa filamu huitaji mafunzo ya kitaalamu zaidi kabla ya kipaji binafsi.
Wandugu,ningependa kuwaasa wadau wa tasnia hii kutosingizia mitaji midogo ya kufadhili utayarishaji wa filamu kama chanzo cha kujipachika vyeo siyo tu wasivyoviweza bali wasivyostahili kwa minajili ya uzao wa kazi za mikono na fikra zao (tumeziona)!

Wandugu,wenzetu wa magharibi wana taasisi na wakala za uwezeshaji fedha wa filamu (film financing agencies and institutions), mwandishi unapeleka muswada wa filamu ,afisa mikopo na baraza lake wanaupitia na kama una tija mnaingia mkataba wa kufadhili filamu kuanzia mwanzo mpaka mwisho wa hatua ya usambazaji.
Lakini haya yote hayatawezekana endapo hakutakua na miswada bora ya filamu yenye uwezo wa kumvutia mwekezaji kama hii tuliyokua nayo sasa.

Wandugu uwezo tunao na nafasi husika tunazo mfano Tanzania Investment Bank,benki za kibiashara kama NBC, CRDB ,NMB, donors (wahisani) n.k.Nina uhakika kama tutakua na mipango sahihi na ushawishi wa kutosha tutaweza kuyakabili makundi tajwa hapo juu na kuweza kufinance filamu zetu kuelekea kwenye ubora tunaouona kwa wenzetu na kuuota huku tukitamani ungekua wa kwetu.

Tumechoka kuwa na filamu za bajeti ndogo zisizozidi milioni kumi huku tukitegemea kazi zenye viwango bora. Nawaomba Wadau wenye njia mbadala na mitizamo jengefu na watujuze tukajuzike ili tupate kujua tunatokaje hapa na kuendelea mbele kwani tulipotoka twapajua.
Natumai wachangiaji watatoa maoni huru kulingana na utashi na weledi wao na siyo mapenzi binafsi wala kuegemea mrengo fulani.

Ahsanteni na poleni kwa kusoma waraka huu na majukumu mengine yanayowakabili.
Nawasilisha.
[/h]
 
Mimi naanzia kwenye subtitles aisee huwa zinanitia kichefuchefu, wanaharibu tu lugha ya watu na kuishia kuandika vitu vya ajabu kama vipi sio lazima kuweka subtitles kama hawana watu wanaoweza kutranslate vizuri, ni aibu tu
 
Da vincci..!
Nashukuru kwa andiko lako, katika namna fulani umeandika kama ni mdau halisi kabisa wa sanaa hii.
Ni mda sasa kuwa na mjadala hai wa tasnia hii....

Kama nimekusoma sawa sawa umelenga zaidi kwenye swala la muswada na umuhimu wake katika tasnia,
nakubaliana sana na wewe.
Kuna siku tuliwahi kujadiliana kidogo na Bishop Ihuka (nadhani atajumuika nasi punde), ye Bishop amekuwa ni muhubiri mzuri sana wa hii dhana, ila mi nilimkatisha kidogo.

Nilitoa mfano kuwa tasnia ni kama mwili wa binadamu kuwa hamna kiungo ambacho ni muhimu kuliko kingine hata kama, hata kama ni kidole cha shada.

Katika namna ya pekee leo umezungumzia "film financing agencies and institutions" hichi ni kitu cha maana sana hasa katika uchumi wa sasa wa pesa ambapo filamu ni uwekezaji na ni biashara kubwa.

Mi binafsi linapokuja suala la sanaa kwa ujumla iwe music au filamu, ninaamini bila intervention ya serikali katika mambo haya hamna tutakachofanya kikubwa, tutazunguka tu hapahapa.
Pamoja na yote uliyoyasema mkuu D-C mwisho wa siku kazi bora (kama tunavyopigania) imetoka imeenda sokoni, soko hili lenye matundu hivi??

Jamani hali ya kwenye soko ni mbaya sana wakuu, hawa "steps" na wadosi wengine wanafanya wanvyotaka na wamezingira kila upande.
Ukijaribu kwenda kinyume nao, ni unapotezwa kabisa, haupati promo wala.

Tubadili namna ya kusimamia BASATA, iwe kama AGENCY (marekebisho ya sheria)... wakuu wake wabadilishwe apatikane mkurugenzi mwenye uelewa wa sanaa na asipatikane kwa fitina au dili chafu za wakina Ruge (Mtu nisiyempenda kuliko wote kwenye sanaa ya bongo ie kweli ni kirusi namba moja kwenye sanaa ya bongo).
Iangaliwe namna makini ya kumpata mtu huyo ie Mkurugenzi wa AGENCY hiyo!

Then, AGENCY hii mpya kwa kushirikiana na TRA ziangalie ni namna ya ku-secure soko la kazi za sanaa na usimamizi wake, kuna mbinu nyingi sana hapa tutazipata kutoka TRA.
Hapo tunatengeneza mapato ya serikali na tasnia kwa ujumla wake.

Hii haimaanishi kwamba maeneo mengine ya filamu yatakuwa yamelala tu, no!
Tasnia lazima iendelee na maboresho enderevu kama hayo ya kurekebisha "crew" na kupiga msasa ikiruhusu weledi zaidi ya vipaji tu.

Marekebisho ya kwenye soko ndio yatakayotoa uhakika wa hali halisi ya sokoni hivyo kulirasimisha soko na hivyo kuwa rahisi kupata mkopo toka hawa watu "film financing agencies and institutions".

Kwa hali ilivyo sasan ni ngumu kupata mkopo toka kwa hayo mashirika ya fedha, pia soko limezungukwa na risk nyingi sana ndio maana hata matajiri bongo wanaopenda filamu hawawezi kuingia huku kwenye filamu.
 
Salaam wanabodi,

Kama inavyofahamika kwa wengi kiini cha filamu bora siku zote huanza na muswada bora wa filamu ambao ni zao la hadithi iliyotimilika...

Wandugu,wenzetu wa magharibi wana taasisi na wakala za uwezeshaji fedha wa filamu (film financing agencies and institutions), mwandishi unapeleka muswada wa filamu ,afisa mikopo na baraza lake wanaupitia na kama una tija mnaingia mkataba wa kufadhili filamu kuanzia mwanzo mpaka mwisho wa hatua ya usambazaji.

Wandugu uwezo tunao na nafasi husika tunazo mfano Tanzania Investment Bank,benki za kibiashara kama NBC, CRDB ,NMB, donors (wahisani) n.k...

Nawasilisha.

Da vincci,
Kuna mambo nakubaliana na wewe katika kile ulichokiandika kuhusiana na scipt bora
na mengineyo ingawa ni marudio ya yale ambayo nimeshayaandika kwenye makala zangu
zilizotoka gazeti la KULIKONI na yapo kwenye blog na website yangu.

Kwanza sisi kujifananisha na nchi za Magharibi si sahihi hata kidogo. Serikali za Magharibi
huichukulia sekta ya filamu seriously politically na wana political consensus wakiwa na ajenda
kuu ya kuhakikisha sekta inakua, kisiasa na kiuchumi. Pia nchi za Magharibi, mfano Hollywood,
tasnia ya filamu inashikilia na watu matajiri wakubwa mno, ndiyo maana inashika nafasi ya pili
(kwa mapato) nchini Marekani na ya tatu duniani.

Kwanza tunahitaji kubadili mtazamo uliojengeka miongoni mwetu kuwa sanaa ya filamu
ni kimbilio la wasiojiweza kiuchumi. Tunapaswa kutambua kuwa sanaa hii ni kazi kama
kazi zingine ambayo inahitaji ubunifu, akili, maarifa na ni muhimu katika kuinua pato la
mtu husika na taifa kwa ujumla kwani inatoa fursa mbalimbali kama vile: Ajira na kuendeleza
biashara ndani na nje ya nchi na kukuza pato la taifa kwa ujumla.

Nakubaliana na wewe kuwa tuna changamoto ya kukosa fursa za kupata mikopo kwenye asasi
za kifedha. Lakini hii si changamoto pekee, zipo nyingine kama: kukosa sera zinazosimama katika
misingi ya utendaji, kukosa elimu, ubinafsi na kutokuwa na malengo.

Pia suala la masoko na usambazaji kwa ajili ya filamu ambazo ni kwa maslahi kwa watazamaji
wa Tanzania ni tatizo kubwa. Soko ni pamoja na kuzitangaza kazi za Tanzania kwenye matamasha
ya filamu ya kimataifa na masoko ya filamu na watazamaji wa ndani walio katika maeneo ambayo
uwezo wa vyombo vya habari kupenya ni mdogo.

Unapoyaongelea mabenki uelewe kuwa hakuna anayeweza kuwekeza katika biashara isiyo
rasmi na ya mashaka. Benki yoyote inahitaji kupata majibu ya maswali haya kabla haijajitumbukiza
katika kusaidia sekta ya filamu nchini:

• Tasnia ya filamu nchini ina thamani kiasi gani kwa sasa?
• Je, gharama kiasi gani inatosha kuzalisha filamu nzuri?
• Je, nini wastani wa mauzo ya kila mwaka ya uzalishaji wa filamu?
• Je, makampuni ya filamu katika sekta ya filamu yana dhamana gani kwa ajili ya kupata mikopo?
• Je, hesabu za makampuni ya filamu katika tasnia ya filamu zinafanyiwa ukaguzi?
• Je, makampuni ya filamu katika tasnia yana miundo rasmi?


Kumbuka, hakuna tafiti zozote zinazofanywa na serikali wala data zinazowekwa kutusaidia katika
kutambua thamani halisi ya tasnia na soko la filamu nchini. Kwa maana hiyo tusitake kujifananisha
na nchi za Magharibi hata kidogo, huu ni wendawazimu! Katika mataifa ya Magharibi wasanii wapo
rasmi ndiyo maana wameweza kuvuma na kupaa kiuchumi.

Tasnia ya filamu nchini bado si rasmi. Sifa za kuwa rasmi ni kusajiliwa kwa kazi zao, kuwa na
jina la biashara, zenye ubia, zikifanywa kikampuni, zenye leseni ya biashara, zenye eneo/mahali
maalum pa kufanyia kazi, zilizo kwenye kumbukumbu inayoeleweka, zinazotofautisha mali ya
biashara na binafsi. Nadhani nimeeleweka.

Hakuna 'excuse' yoyote ambapo wasanii wanaweza kukuza pato lao, kuondokana na umaskini
na hata kushindana kimataifa kama hawataingizwa kwenye mfumo rasmi ambao utawafanya
watambulike ndani na nje ya nchi ili kujenga mazingira ya wao kuweza kukopesheka, kupata
fursa za kikazi na kukuza kazi wanazozifanya.

Pia mabenki kwa kawaida hayawezi kuwa na uhusiano wa kibenki na makampuni au wasanii
kama hawatakuwa rasmi na wanaotambulika kisheria. Sekta ya filamu Tanzania inapaswa
kuboreshwa zaidi, na kuanza kudumisha kumbukumbu sahihi na akaunti, kushiriki huduma ya
wakaguzi na kuwa na miundo rasmi ya shirika.

Ukweli ni kwamba, sinema ikiwezeshwa huwa na lifetime property, huku benki ikimiliki asilimia
30 ya hisa na kushikilia copyright ya sinema hiyo hadi mkopo uliotolewa utakapolipwa.

Kuna kipindi nilibahatika kukutana na kiongozi mwandamizi wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA),
katika kikao rasmi alipokuwa akijaribu kuangalia uwezekano wa kukusanya mapato kupitia tasnia
ya burudani, hasa muziki na filamu baada ya kupewa agizo hilo na Rais.

Nilimweleza wazi kuwa hadi pale nchi hii itakapoacha kuishi katika nadharia zaidi, kwani matamko
yoyote yanayotolewa na viongozi huwa hayafanyiwi kazi, hata kama kinachoongelewa kina tija.

Nakubaliana kabisa na malalamiko ya wasanii kukosa fursa za kupata mikopo kwenye asasi za kifedha,
mianya ya kufanya kazi mbalimbali za serikali, na hata kama kazi zao za sanaa zinakua lakini
hazithaminiwi ipasavyo kutokana na wao kutokuwa rasmi.

Pengine walioanzilisha Mkurabita walikuwa na lengo zuri wakitaraji mafanikio mbalimbali yatokane
na mpango huo, lakini bado kuna changamoto nyingi katika kufanikiwa kwake. Changamoto hizo
ni pamoja na uelewa mdogo wa baadhi ya watendaji serikalini unaopelekea wananchi kukosa
uelewa pia, urasimu uliopo kwenye wizara na Idara mbalimbali serikalini, uwepo wa sheria zenye
mkanganyiko kama ile ya manunuzi (Procurement Act) na kadhalika.

Urasimishaji wa Biashara yoyote ni jambo lisiloepukika kama tunataka kuendelea, ili wasanii
waweze kuwa na maendeleo na kukua kiuchumi hawana budi kurasimishwa ikiwa ni pamoja na
kazi wanazozifanya.

Siku nikipata muda nitaelezea kuhusu nchi tunayopaswa kuiga maendeleo yake ya Afrika Kusini
ambao wana chombo maalum “Film and Video Promotions Board”, chombo kama hiki kinapaswa
kuwepo nchini. ambacho kina idara tano:
- Idara ya utoaji wa taarifa za upatikanaji wa pesa (funding information) na kutoa fursa kwa
watengeneza sinema.
- Idara ya kuandaa takwimu za kina na kutoa fursa ya kuzitangaza kazi zetu katika masoko
mengine ya Afrika, na duniani na hivyo kuongeza uwezekano wa kuuza kazi zetu kimataifa na
kuigiza pesa za kigeni.
- Idara inayosimamia na kuwalazimisha wasanii na watendaji wengine katika sekta ya filamu
kupata mafunzo ya weledi (professionalism).
- Idara inayosimamia revenue generation itokanayo na filamu.
- Idara inayosimamia kwa ukamilifu sheria za piracy kwa kazi za sanaa na hivyo kuwafanya
watengenezaji wa kazi hizi kutokuwa na hofu ya kupoteza mapato (economic reward) yatokanayo
na kazi zao.

Utengenezaji wa filamu hapa Tanzania kwa soko la Tanzania unatafsiriwa kuwa sawa na biashara
ya barafu (block of ice) inayoweza kumyeyukia aliyenayo mikononi wakati wowote, hii huwafanya
watengeneza filamu wa Kitanzania wajikute wakiingia mikataba haraka ya kupata pesa japo kiduchu
kabla barafu haijawayeyukia na kugeuka maji.

Huu ndo mtazamo wangu...
 
Da vincci..!
Nashukuru kwa andiko lako, katika namna fulani umeandika kama ni mdau halisi kabisa wa sanaa hii.
Ni mda sasa kuwa na mjadala hai wa tasnia hii....

Kama nimekusoma sawa sawa umelenga zaidi kwenye swala la muswada na umuhimu wake katika tasnia,
nakubaliana sana na wewe.
Kuna siku tuliwahi kujadiliana kidogo na Bishop Ihuka (nadhani atajumuika nasi punde), ye Bishop amekuwa ni muhubiri mzuri sana wa hii dhana, ila mi nilimkatisha kidogo...

Mkuu, nashukuru kwa kutambua mchango wangu ingawa umekosea jina langu.
Ni Hiluka si Ihuka. Hata hivyo tupo pamoja...
 
Mkuu, nashukuru kwa kutambua mchango wangu ingawa umekosea jina langu.
Ni Hiluka si Ihuka. Hata hivyo tupo pamoja...

My apology Bishop...
Nashukuru kwa post yako #4...

Nisaidie kidogo maswali haya...!

Hivi makampuni ya filamu hapa bongo ni yepi??

Steps na wenzake ni kampuni ya filamu??

Upi ni mkangtanyiko wa katika PPA katika mfumo wa filamu tunaoutaka??

Na je unazungumzia PPA ipi? 2004 au 2011??

NB: PPA= Public Procurement Act.

Nasubiria kwa hamu sana udadavuzi wako kuhusu "Film and Video Promotions Board"...

Na jinsi tutakavyoweza kuitekeleza hapa kwetu.

Kila la kheri.
Tupo pamoja.
 
My apology Bishop...
Nashukuru kwa post yako #4...

Nisaidie kidogo maswali haya...!

Hivi makampuni ya filamu hapa bongo ni yepi??

Steps na wenzake ni kampuni ya filamu??

Upi ni mkanganyiko wa katika PPA katika mfumo wa filamu tunaoutaka??

Na je unazungumzia PPA ipi? 2004 au 2011??

NB: PPA= Public Procurement Act.

Nasubiria kwa hamu sana udadavuzi wako kuhusu “Film and Video Promotions Board”...

Na jinsi tutakavyoweza kuitekeleza hapa kwetu.

Kila la kheri.
Tupo pamoja.

Mkuu,
Makampuni ya filamu yapo ya aina mbili: kuna yaliyosajiriwa
kama makampuni ya production kwa msajiri wa makampuni
Brela, haya ni kama Benchmark Production, Abantu Vision,
Afrikan Image, nk. ambayo yapo formal na yanakaguliwa na
ndiyo maana imekuwa rahisi kwao kukopesheka. Tatizo la
makampuni haya ni kwamba haya-deal na commercial movie
ambazo zinalenga soko la filamu la Tanzania moja kwa moja
bali yamejikita kutengeneza documentary au artistic films
(filamu za miradi kama Ukimwi, malaria, nk.), na makampuni
mengine yaliyo mengi ambayo yamejikita moja kwa moja
katika kutengeneza commercial movies ni yale ya wasanii
wetu; kina Kanumba (Kanumba the Great Production), Ray
(RJ Production), nk. ambayo hayajasajiriwa kwa msajiri bali
wamesajiri jina tu na kupewa TIN, kitu kinachowanyima fursa
ya kukopesheka. Haya ndiyo makampuni ninayoyaongelea.
Steps na Wahindi wenzie ni makampuni ya distribution japo
hawazuiwi kuandaa movie...
Kuhusu PPA nitakuja na mjadala mpana kama nilivyoahidi
kwenye FVPB ya South Africa. Napenda sana hoja zako kwani
humfanya mtu aaumize sana kichwa katika kuzitafakari...
 
Back
Top Bottom