Ng'wanangwa
JF-Expert Member
- Aug 28, 2010
- 10,827
- 4,172
Ni shukrani za pongezi alizopewa mkurugenzi wa Vodacom bwana Rene meza kwa kampuni yake kuchangia dollar 450,000/ kwa mradi wa mbwa mwitu tena ni kutoka kwa Rais Kikwete hii ni hata jamani!si bora wangeangalia miradi mingine jamani ss hili la mbwa kweli wakati ndugu zetu wengi tu hata maji safi hawana,na barabara?
hii ni kufuru kubwa!!!!!!
Voda ni wawekezaji na kwa tz,mwekezaji anachotaka ni kumfurahisha alieko madarakani na si jamii ili misaada ya kodi izidi kutolewa! Hata kama wangetoa £1,000,000 kwa mradi wa kuwinda njiwa pori pongezi zingetolewa pamoja na press conference juu! Anyway,days are numbered....!
Nusu ya watumiaji wote wa simu Tanzania ni wateja wa Vodacom, lakini kodi hakuna! Leo hii rais anakaa na mkurugenzi kuomba USD 450,000? Something is not right here.
Front page ya Majira inasema kuwa mbwa mwitu waliohamishwa (toka Mara) ni 11. Yaani USD 450,000 kuhamisha mbwa mwitu 11 from what distance?! Na hii initiative ya kuhamisha hao mbwa mwitu iko chini ya serikali/wizara? Vodacom waliingiaje kwenye huu mradi?