Tafakuri ya Faizafoxy 5: Mtego wa panya, Rushwa, Ufisadi, Siasa, Uchumi, vimenasa vyote?

FaizaFoxy

Platinum Member
Apr 13, 2011
92,820
109,108
Kwetu Mkuranga, kuna mitego ya panya maarufu sana. Hutengenezwa kama dema la samaki na wengine hadi leo hii huiita "dema la panya". Mitego hii ni mizuri sana lakini kila kizuri huwa na changamoto zake. Mtego huo ukitegwa hunasa panya na vinginevyo.

Tanzania kabla ya hapo, Tanganyika, tunajitawala wenyewe kwa miaka 58 sasa, toka tulipokabidhiwa nchi, sifahamu na Umoja wa Mataifa au Uingereza.

Huwa najiuliza, kwanini miaka 58 bado tunategemea hata bajeti yetu kujalizwa na nchi za nje?

Uhuru tunaojivunia ulikuwa ni
"dema la panya?

Tanzania tuna reli ya Mjerumani na tuna reli ya Mchina na sasa tunaongeza reli ya tatu, ya Mturuki. Swali, tumeshindwa nini kuziendeleza reli za Mjerumani na Mchina hadi tuanze alifu kwa kijiti na reli ya Mturuki? Jee, siyo dema hili?

Reli mpya siyo dema litakalo unasa na uchumi wetu?

Vipi? Najaribu kufikiria magari mangapi makubwa ya mizigo yatakosa kazi kwa kuundwa reli hii, najaribu kufikiria vituo vingapi vya haya magari makubwa ya mizigo vitakosa biashara kuanzia Dar hadi mpakani? Maelfu (kama si malaki) ya Watanzania watakosa ajira za moja kwa moja (direct employment) na wangapi watakosa ajira na vipato vya "indirect"? Siyo dema hili?

Ndege:
Tunafanya la maana sana kuwa na ndege zetu wenyewe lakini nalo siyo dema? Maana ni muda mchache toka tuanzishe tena kuwa na ndege zetu wenyewe, kwa muda huu mchache
tumeshashuhudia ndege hizo watu wakianza ubadhirifu hata kwenye kuzichora nembo tu! Pia tumeshuhudia zikishikwa sasa mara ya tatu na watu wenye madai yao. Siyo dema hili?

Viwanda.
Nachelea kuuliza ya viwanda kwani nafahamu mfumo wetu wa sasa wa kuwekeza kwenye viwanda ni tofauti na ule tulioshindwa kabisa kuuendesha, wa awamu ya kwanza. Ule ulikuwa mfumo wa mali za umma, sasa tunawataka wawekezaji wawekeze kwenye viwanda. Hiyo ndiyo tofauti.

Lakini jee, likija suala la kukorofishana na wawekezaji hivi viwanda havitakosa vipuli na baadhi ya mahitaji ya nje ya kuviendesha? Siyo dema hili?

Nachelea zaidi kuongelea umeme wetu mpya kwa kuyatafakari hayo hayo ya kuwa labda tunaingizwa kwenye dema huku tunajiona mahodari?

Vipi? Tunasoma kuwa dunia ya leo inajikita katika teknolojia ya kuufanya umeme uwe (localized) kwa kuanza kubuni na kuijaribu teknolojia ya kuendesha umeme wa nyumba kwa nyumba, jumba kwa jumba, kiwanda kwa kiwanda badala ya kuwa na umeme wa kizamani wa kufuliwa sehemu moja (kama tufanyavyo) na kutawanywa. Siyo dema hili?

Tafakuri yangu inanipelekea kuona kuwa siasa, uchumi, rushwa na ufisadi vyote vinaweza kutumiwa na wasuka dema kutunasa tuliokuwemo na tusiokuwemo.

Cha kufanya? Tujadili.

"Damned if you do, damned if you don't".
 
Ati tumeshindwa nini kuendeleza reli ya mjerumani na reli ya mchina

Niliposoma hiyo mistari tu nikajua kuna kitu unakosa kichwani kuhusu miundo mbinu ya reli
Kichwani mwangu kunakosa vingi sana ambavyo wewe unavyo. Hilo si tatizo lako wala siyo mada iliyopo.

Au nikikosa kitu kichwani mwangu tatizo ni lako wewe?

Shule za kusomea ujinga zinafahamika haraka sana.
 
Ni mara ya pili nikipenda nyuzi zako, una akili wewe mdada sema tu kijani kinakuharibia.
Niko Mkuranga natamani nikusalimie mwenyeji wangu
Kichwani mwangu kunakosa vingi sana ambavyo wewe unavyo. Hilo si tatizo lako wala siyo mada iliyopo.

Au nikikosa kitu kichwani mwangu tatizo ni lako wewe?

Shule za kusomea ujinga zinafahamika haraka sana.
 
Kichwani mwangu kunakosa vingi sana ambavyo wewe unavyo. Hilo si tatizo lako wala siyo mada iliyopo.

Au nikikosa kitu kichwani mwangu tatizo ni lako wewe?

Shule za kusomea ujinga zinafahamika haraka sana.
Dada umeninyooshea Siku...kula tano! Huyu Kawe NI zaidi ya Shule ya kusomea ujinga...NI kundi ambalo ni wajinga na waneamua kujitia ujinga kwa kuabudu!
 
Na hapa ndipo namkumbuka CAG mstaafu,

Tunahitaji Taasisi imara ,Si kuongoza Nchi kwa akili za Mtu mmoja,

Hii mada inafikirisha sana ,Kuna hatari ya kupoteza yote haya tukiendelea kusifu bila kuwa na frikra kama hizi..

Nimeshangaa Majuzi Dada amejisitiri vizuri nikajua anafahamu vizuri imani yake lakini akasifu mpaka kumpigia magoti Magu duh!!
 
Kichwani mwangu kunakosa vingi sana ambavyo wewe unavyo. Hilo si tatizo lako wala siyo mada iliyopo.

Au nikikosa kitu kichwani mwangu tatizo ni lako wewe?

Shule za kusomea ujinga zinafahamika haraka sana.

Katika Mara chache ninazokubaliana nawe hii ni moja wapo, na inaweza kuongoza zingine kwa ubora.
Umeujibu kiweledi sana huo "mzigo wa ujinga" ingawa pengine ndio umeuchanganya zaidi badala ya kuuponya.
 
Na hapa ndipo namkumbuka CAG mstaafu,

Tunahitaji Taasisi imara ,Si kuongoza Nchi kwa akili za Mtu mmoja,

Hii mada inafikirisha sana ,Kuna hatari ya kupoteza yote haya tukiendelea kusifu bila kuwa na frikra kama hizi..

Nimeshangaa Majuzi Dada amejisitiri vizuri nikajua anafahamu vizuri imani yake lakini akasifu mpaka kumpigia magoti Magu duh!!
Ni kweli kabisa, tunahitaji "taasisi imara". Hilo halina ubishi.
 
Nchi zote zilizoendea duniani ata Africa zina reli za kisasa so reli ya kisasa haikwepeki kama tunataka kwenda kwenye uchumi wa kati katika vitu ninavyoweza kumpongeza Magufuli basi ni hii reli na bwawa la umeme ila angalizo tuanze na treni za mizigo kuliko abiria maana hakuna faida kwenye abiria kama kwenye mizigo.

Ajira za magari haziwezi kuisha leo ikifika Morogoro tunaweka bandari kavu magari yanayoenda zambia na Congo yataanzia apo ajira zitapotea vipi? wakati 60% ya magari upita njia ya tunduma?

Nilitegemea ungekuja na wazo kwamba tukajifunze Marekani, Ujerumani, Urusi, China, South Africa au Ethiopia wao baada ya reli walifanya nini kwenye swala la ajira? maana izo nchi zote zina reli ya kisasa na tatizo la ajira kwao huwezi kulinganisha na sisi.

Unasema reli zipo mbili wakati huo huo unasema kwanini tujenge nyingine wakati zipo mbili sasa kama unajua zipo mbili mbona hazijamaliza ajira za aya magari uko nyuma?
 
Mkuu umejitaid kuzieleza hisia zako bila kuzingatia itifaki, je binafsi wewe katika maisha yako unaishi ukiwa huru (bila changamoto) kama zipo basi rejea kwa uzi wako then u-conclude kua changamoto ndo huongoza njia ya mafanikio hivo kuzikabili ndo ushindi wenyewe na si kuzikwepa.
 
FAIZA ASW. Nimekusoma na nimekuelewa. Ila tatizo linabakia pale pale. Watanzania tunaogopa ukweli kuliko hata tnavyoiogopa jehanamu. Mfano mzuri ni huyo Kawe Alumn. Kama Watanzania tutaukubali ukweli na kushirikishana pamoja kumuamua kuwa na taasisi imara na sio vimiungu watu tulivyonavyo Nchi itaenda. Ila kwasasa tunatengeza dema kubwa zaidi.
 
Nchi zote zilizoendea duniani ata africa zina reli Za kisasa so reli ya kisasa haikwepeki kama tunataka kwenda kwenye uchumi wa kati katika vitu ninavyoweza kumpongeza Magufuli basi ni hii reli na bwawa la umeme ila angalizo tuanze na treni za mizigo kuriko abiria maana hakuna faida kwenye abiria kama kwenye mizigo.

= kuliko

Hilo la kumpongeza si tatizo wala si suala lililopo. Rudia kipande hiki kinachohusiana na reli, kisha ujibu maswali yaliyopo...

Tanzania tuna reli ya Mjerumani na tuna reli ya Mchina na sasa tunaongeza reli ya tatu, ya Mturuki. Swali, tumeshindwa nini kuziendeleza reli za Mjerumani na Mchina hadi tuanze alifu kwa kijiti na reli ya Mturuki? Jee, siyo dema hili?

Reli mpya siyo dema litakalo unasa na uchumi wetu?

Vipi? Najaribu kufikiria magari mangapi makubwa ya mizigo yatakosa kazi kwa kuundwa reli hii, najaribu kufikiria vituo vingapi vya haya magari makubwa ya mizigo vitakosa biashara kuanzia Dar hadi mpakani? Maelfu (kama si malaki) ya Watanzania watakosa ajira za moja kwa moja (direct employment) na wangapi watakosa ajira na vipato vya "indirect"? Siyo dema hili?
 
Ati tumeshindwa nini kuendeleza reli ya mjerumani na reli ya mchina

Niliposoma hiyo mistari tu nikajua kuna kitu unakosa kichwani kuhusu miundo mbinu ya reli


Sijaribu kukubadilisha mtazamo wako japo unaonekana dunia imekuacha mbali mno kifkra

Tumewahi kusema sana humu, kama ni reli mpya ilipaswa kupelekwa kusini kisha ihudumie mikoa hiyo, huku kwingine zifufuliwe na kuboreshwa reli zilizopo.
 
Mkuu umejitaid kuzieleza hisia zako bila kuzingatia itifaki, je binafsi wewe ktk maisha yako unaishi ukiwa huru (bila changamoto) kama zipo basi rejea kwa uzi wako then u-conclude kua changamoto ndo huongoza njia ya mafanikio hivo kuzikabili ndo ushindi wenyewe na si kuzikwepa
Changamoto ni ndugu wa damu na Maisha.

Nisome vizuri kisha "tujadili", ndicho nilichomalizia hapo juu.

Sasa changamoto zangu binafsi tukianza kuzijadili tutapoteza muelekeo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom