Tafakuri Tunduizi ya Uongozi: Mhe Mwanri na saikolojia ya anawaongoza

eliesikia

JF-Expert Member
Oct 29, 2010
787
755
Kwanza angalia na sikiliza vizuri hii video. Dawa ya Asubuhi.



Utaona ni jinsi gani Mhe Mwanri anatumia saikolojia ya uongozi kuteka nyoyo na hisia za anaowaongoza. Katika hili anaongea na bodaboda ambao wako kwenye ugomvi na polisi. Nitafanya tafakuri tunduizi katika mambo machache

1. Mavazi na hadhira yako
Huku akijua fikra yeye ni kiongozi na polisi wako chini yake aliamua kuvaa mavazi ambayo yanapendwa sana na makondakta pamoja na bodaboda. Pia akaamua kuvaa kofia ambayo ni nadra sana kwa viongozi na wakuu wanaweza kuvaa. Hii kofia hutumika sehemu zenye baridi lakini kwa Tanzania ni mavazi ya watu wa chini sana. Wenye kipato au wadhifa huwa hawavai za namna hiyo labda sehemu iwe na baridi sana.
Mavazi yake yanamfanya awe mmojawapo wa bodaboda ambao ndio nia yake kuwaelimisha. Bodaboda wanajisikia vizuri kumuona RC kavaa kama kondakta au Mchumia jua.

2. Hoja za kukubaliana
Anawasilisha hoja zake kama maswali ambayo anahitaji pande mbili wakubaliane, yaani polisi na bodaboda. Akiwasilisha anawauliza Bodaboda kama anachosema hakifai basi waseme huku kaweka adabulugha yakini yenye kusisimua na kuchekesha ili kumteka msikilizaji. Mhe angeweza kuweka vitisho na kuwaambia bodaboda kama hawataki atawanyoosha lakini badala yake anaongea nao kama marafiki ambao anahitaji sana wabadili tabia.

3. Mapumziko kwenye maelezo
Huku akionekana mtu mwenye unyenyekevu sana anakuwa anazipishanisha hoja zake kwa mapumziko ya vichekesho kabla hajahamia kwingine. Nakumbuka shuleni mwalimu mwenye kipindi cha muda mrefu kuna wakati anasema simameni kidogo kisha rukaruka kidogo. Ni kuamsha tuu ari ya kusikiliza na kuchakata maelezo.

4. Mifano ya kumuelewesha mtu wa kawaida
Rais Magufuli alishawahi kumwambia yule dada wa SSRA kuwa yuko "too academic" ndio maana haeleweki na wengi. Mhe Mwanri akiwa kama kiongozi wa siku nyingi anafahamu jambo hili vizuri ndio maana kila hoja yake anaisindikiza na mifano mirahisi kabisa ili walengwa ambao ni BodaBoda wakubaliane nae na wabadili mienendo. Kwenye Movie Slumdog Millionaire, yule muhusika mkuu anaonyesha jinsi gani "experience" ya matukio hueleweka. Hata biblia na vitabu vingine vya dini hutumia "parables" ili kuweka uelewa wa hadhira mezani.

5. Uongozi unaoacha alama
Kama kiongozi, Mhe Mwanri, anataka kuacha alama ya upendo na uongozi bora. Huku akijitapa kuwa bodaboda wakifuata sheria za barabarani vizuri basi ajali zitapungua kwa sababu mkoa wake ni kama TORONTO. Huku akisema ulishawahi kuona Toronto wanavunja sheria? Kimsingi anawajengea watu wake hisia kwamba ukifuata sheria basi maisha yako yanakuwa "civilized" kwa kuwa unaishi mkoa ambao ni "civilized". Kimsingi anataka kila anaemsikiliza akiondoka aende akafanye mabadiliko ya tabia zake barabarani. Lakini kuna uwezekano akitoka hapo anaenda kuwaambia polisi wakamate wanaovunja sheria wakiwa kikaoni lakini JUKWAANI ameamua kuwa mnyenyekevu ili bodaboda nao wafanye kwa unyenyekevu. Uongozi unaocha alama hujikita katika kutoa UHURU kwa watu na kuwaheshimu. Haujikiti katika majivuno na mashindano. Hulka ya binadamu au Temperament yake hutulia endapo itapepewa.

Nawasilisha wadau.
 
Ni sahihi usemayo! Ni kiongozi wa mfano kwa viongozi wengine. Kila asemalo linatekelezeka kwa kila kada inaweza. Tofauti na Darisalama yetu hapa.
Kwanza angalia na sikiliza vizuri hii video. Dawa ya Asubuhi.



Utaona ni jinsi gani Mhe Mwanri anatumia saikolojia ya uongozi kuteka nyoyo na hisia za anawaongoza. Katika hili anaongea na bodaboda ambao wako kwenye ugomvi na polisi. Nitafanya tafakuri tunduizi katika mambo machache

1. Mavazi na hadhira yako
Huku akijua fikra yeye ni kiongozi na polisi wako chini yake aliamua kuvaa mavazi ambayo yanapendwa sana na makondakta pamoja na bodaboda. Pia akaamua kuvaa kofia ambayo ni nadra sana kwa viongozi na wakuu wanaweza kuvaa. Hii kofia hutimika sehemu zenye baridi lakini kwa Tanzania ni mavazi ya watu wa chini sana. Wenye kipato au wadhifa huwa hawavai za namna hiyo labda sehemu iwe na baridi sana.
Mavazi yake yanamfanya awe mmojawapo wa bodaboda ambao ndio nia yake kuwaelimisha. Bodaboda wanajisikia vizuri kumuona RC kavaa kama kondakta au Mchumia jua.

2. Hoja za kukubaliana
Anawasilisha hoja zake kama maswali ambayo anahitaji pande mbili wakubaliane, yaani polisi na bodaboda. Akiwasilisha anawauliza Bodaboda kama anachosema hakifai basi waseme huku kaweka adabulugha yakini yenye kusisimua na kuchekesha ili kumteka msikilizaji. Mhe angeweza kuweka vitisho na kuwaambia bodaboda kama hawataki atawanyoosha lakini badala yake anaongea nao kama marafiki ambao anahitaji sana wabadili tabia.

3. Mapumziko kwenye maelezo
Huku akionekana mtu mwenye unyenyekevu sana anakuwa anazipishanisha hoja zake kwa mapumziko ya vichekesho kabla hajahamia kukwingine

4. Mifano ya kumuelewesha mtu wa kawaida
Rais Magufuli alishawahi kumwambia yule dada wa SSRA kuwa yuko "too academic" ndo maana haeleweki. Mhe Mwanri akiwa kama kiongozi wa siku nyingi anafahamu jambo hili vizuri ndio maana kila hoja yake anaisindikiza na mifano mirahisi kabisa ili walengwa ambao ni BodaBoda wakubaliane nae na wabadili mienendo.

5. Uongozi unaocha alama
Kama kiongozi, Mhe Mwanri, anataka kuacha alama ya upendo na uongozi bora. Huku akijitapa kuwa bodaboda wakifuata sheria za barabarani vizuri basi ajali zitapungua kwa sababu mkoa wake ni kama TORONTO. Huku akisema ulishawahi kuona Toronto wanavunja sheria? Kimsingi anawajengea watu wake hisia kwamba ukifuata sheria basi maisha yako yanakuwa "civilized" kwa kuwa unaishi mkoa ambao ni "civilized". Kimsingi anataka kila anaemsikiliza akiondoka aende akafanye mabadiliko ya tabia zake barabarani. Lakini kuna uwezekano akitoka hapo anaenda kuwaambia polisi wakamate wanaovunja sheria wakiwa kikaoni lakini JUKWAANI ameamua kuwa mnyenyekevu ili bodaboda nao wafanye kwa unyenyekevu. Uongozi unaocha alama hujikita katika kutoa UHURU kwa watu na kuwaheshimu. Haujikiti katika majivuno na mashindano. Hulka ya binadamu au Temperament yake hutulia endapo itapepewa.

Nawasilisha wadau.
 
Unayosema yana ukweli kiasi Fulani,,lakini anachemka anapojiweka kwenye nafasi ya kila mtaalamu. Yaani akiongea na wananchi yeye ni Afisa kilimo, ni daktari, ni Mwalimu, ni Polisi ni Afisa uvuvi, ni...!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata mimi namkubari sana huyu jamaa. Tabora washindwe wenyewe kusogea hatua moja mbele
 
Unayosema yana ukweli kiasi Fulani,,lakini anachemka anapojiweka kwenye nafasi ya kila mtaalamu. Yaani akiongea na wananchi yeye ni Afisa kilimo, ni daktari, ni Mwalimu, ni Polisi ni Afisa uvuvi, ni...!

Sent using Jamii Forums mobile app

Ngoja nikwambie kitu. Nafasi yake kama RC basi shughuli za mkoa anakuwa "facilitator". Kwa msingi huo anapofanya ugani kama kuonyesha wananchi ni jinsi gani unafanya fertigation au pesticide application ni katika kuwaonyesha "watu wake" au wanaugani namna ya kuongea na wananchi.
Kuna video utaona amepanga makopo chini na kuonyesha njia bora ya kupanda, kupanda kwa mstari na kumwagia sumu ya wadudu. Hizi zote tunaita Kazi mfano kwa wananchi na watu wa ugani. Anawaonyesha namna ya ku"communicate effectively" na wananchi wa chini. Maana yeye anafanya pale tuu lakini wale jamaa wa ugani wanaenda vijiji vyote kufanya ugani.

Basi vivyo hivyo kwenye kada zingine kama za udaktari, ualimu, uhandisi na kadhalika. Ndo maana kama kitu hakiko sawa anasema kabisa nitatuma wataalamu waje. Rejea ili ishu ya nondo kuwa chache kwenye Beam ya jengo. Idadi ya nondo na mchoro wa consultancy ulitofautiana. Lakini pia alitumia lugha ya kistaarabu na kumwambia yule mhandisi asiogope RC akipata wasiwasi. Ana haki ya kuwa na wasiwasi. Kama yuko sawa basi wataalamu watakuja na kumuelewesha RC. Huku akiongea adabulugha astilahi yenye kumtoa wasiwasi yule mkandarasi.
 
Hahaha hamna kaka.. Nafanya tafiti zangu hapa nikaona kwa nini wadau wa humu jamvini nisiwape kipande cha andiko langu kidogo?
Hulka ya binadamu au Temperament yake hutulia endapo itapepewa.

Kongole kwa mkuu wa mkoa..na kwako pia mkuu kwa andiko zuri..karibu tena kwa vipande vingine..nimesoma na kuelewa na kuangalia video iliyonifundisha na kunichekesha pia..Tanzania tunaihitaji viongozi wanyenyekevu na wenye hofu ya Mungu..nimefurahi pia ulivyomalizia bandiko lako..Ni kweli kabisa uongozi sio kutisha au kukoromea wale walio chini yako..Ongea na watu kwa upole na unyenyekevu watakuelewa tu..
 
Kwanza angalia na sikiliza vizuri hii video. Dawa ya Asubuhi.



Utaona ni jinsi gani Mhe Mwanri anatumia saikolojia ya uongozi kuteka nyoyo na hisia za anaowaongoza. Katika hili anaongea na bodaboda ambao wako kwenye ugomvi na polisi. Nitafanya tafakuri tunduizi katika mambo machache

1. Mavazi na hadhira yako
Huku akijua fikra yeye ni kiongozi na polisi wako chini yake aliamua kuvaa mavazi ambayo yanapendwa sana na makondakta pamoja na bodaboda. Pia akaamua kuvaa kofia ambayo ni nadra sana kwa viongozi na wakuu wanaweza kuvaa. Hii kofia hutumika sehemu zenye baridi lakini kwa Tanzania ni mavazi ya watu wa chini sana. Wenye kipato au wadhifa huwa hawavai za namna hiyo labda sehemu iwe na baridi sana.
Mavazi yake yanamfanya awe mmojawapo wa bodaboda ambao ndio nia yake kuwaelimisha. Bodaboda wanajisikia vizuri kumuona RC kavaa kama kondakta au Mchumia jua.

2. Hoja za kukubaliana
Anawasilisha hoja zake kama maswali ambayo anahitaji pande mbili wakubaliane, yaani polisi na bodaboda. Akiwasilisha anawauliza Bodaboda kama anachosema hakifai basi waseme huku kaweka adabulugha yakini yenye kusisimua na kuchekesha ili kumteka msikilizaji. Mhe angeweza kuweka vitisho na kuwaambia bodaboda kama hawataki atawanyoosha lakini badala yake anaongea nao kama marafiki ambao anahitaji sana wabadili tabia.

3. Mapumziko kwenye maelezo
Huku akionekana mtu mwenye unyenyekevu sana anakuwa anazipishanisha hoja zake kwa mapumziko ya vichekesho kabla hajahamia kwingine. Nakumbuka shuleni mwalimu mwenye kipindi cha muda mrefu kuna wakati anasema simameni kidogo kisha rukaruka kidogo. Ni kuamsha tuu ari ya kusikiliza na kuchakata maelezo.

4. Mifano ya kumuelewesha mtu wa kawaida
Rais Magufuli alishawahi kumwambia yule dada wa SSRA kuwa yuko "too academic" ndio maana haeleweki na wengi. Mhe Mwanri akiwa kama kiongozi wa siku nyingi anafahamu jambo hili vizuri ndio maana kila hoja yake anaisindikiza na mifano mirahisi kabisa ili walengwa ambao ni BodaBoda wakubaliane nae na wabadili mienendo. Kwenye Movie Slumdog Millionaire, yule muhusika mkuu anaonyesha jinsi gani "experience" ya matukio hueleweka. Hata biblia na vitabu vingine vya dini hutumia "parables" ili kuweka uelewa wa hadhira mezani.

5. Uongozi unaoacha alama
Kama kiongozi, Mhe Mwanri, anataka kuacha alama ya upendo na uongozi bora. Huku akijitapa kuwa bodaboda wakifuata sheria za barabarani vizuri basi ajali zitapungua kwa sababu mkoa wake ni kama TORONTO. Huku akisema ulishawahi kuona Toronto wanavunja sheria? Kimsingi anawajengea watu wake hisia kwamba ukifuata sheria basi maisha yako yanakuwa "civilized" kwa kuwa unaishi mkoa ambao ni "civilized". Kimsingi anataka kila anaemsikiliza akiondoka aende akafanye mabadiliko ya tabia zake barabarani. Lakini kuna uwezekano akitoka hapo anaenda kuwaambia polisi wakamate wanaovunja sheria wakiwa kikaoni lakini JUKWAANI ameamua kuwa mnyenyekevu ili bodaboda nao wafanye kwa unyenyekevu. Uongozi unaocha alama hujikita katika kutoa UHURU kwa watu na kuwaheshimu. Haujikiti katika majivuno na mashindano. Hulka ya binadamu au Temperament yake hutulia endapo itapepewa.

Nawasilisha wadau.

Kwa training Mwanri ni Mwalimu.
Anajua sana ku communicate, hivyo mambo magumu kwa jamii ayanaelezea kirahisi.
Hivyo kukubalika sana na wana Tabora na sasa nchi nzima.
 
Back
Top Bottom