Tony Gwanco
JF-Expert Member
- Jan 22, 2013
- 5,913
- 1,208
wale vijana wa buku 7 sidhani kama watapata mda wakufikiri, wanachowaza wao ni buku 7 tu, baasi.
kama rose kamili slaa alihongwa ubunge itakuwa tabu yeye kuhonga hongo ni jadi ya chadema
wale vijana wa buku 7 sidhani kama watapata mda wakufikiri, wanachowaza wao ni buku 7 tu, baasi.
wabunge wa viti maalum chadema wamepata kwa kutoa rushwa za aina mbalimbali. bila rushwa chadema haiwezekani
Hivi CHADEMA mlipomkamata yule mama DC kule Igunga akiwa kwenye kikao cha ndani na kumdhalilisha ilikuwa ni sawa lakini CCM kumkamata mbunge wenu mnaanza kulia lia!
Haya mambo ya kukamata watu mlianzisha wenyewe na sasa mchezo umewageukia.
CCM wanapanga kwa kutumia vichwa vya chini badala ya vichwa vya juu
Mods:
Kwa heshima na taadhima nawaomba msiunganishe thread hii bali muiache tujadili kwa hoja na tafakuri tunduizi kwa wale ambao watakuwa tayari kuumiza vichwa vyao na kushusha nonda za uhakika
Kwanza nikiri kuwa sina uhakika kuwa Rose Kamili katoa rushwa kama alivyotuhumiwa na wana CCM kwenye tukio la jana usiku kule Kalenga, lakini kama ni kweli iliyo kweli tupu bila chembe ya shaka naomba tutafakari pamoja kwa kutumia tafakuri tunduizi kwa kujiuliza maswali kadhaa.
1. Kama CCM wana greenguard ya kuzuia rushwa kama ni kweli kama wanavyosema, ipo kwa ajili ya kuwazuia wapinzani tu? Kwa nini wasitumie greenguard hiyohiyo kumsaidia Mzee Mangula aliyewapa siku 90 viongozi wa NEC walio chaguliwa kwa rushwa wajisalimishe kwake?! Siku 90 zilisha isha kwa nini wasisaidie?! kumbuka pia jk alisha wahi kusema rushwa itaiua ccm, kwa nini wasisaide kusimamia kauli ya mwenyekiti wao ili chama kisizidi kuwa kichaka cha rushwa?
2. Kama Mama rosekamili alikuwa anagawa rushwa kwa nini wasiwaite maafisa wa Takukuru na matokeo yake walienda naye kwenye ofisi ya chama chao na sio Polisi?! Kama waliweza kwenda nae kwenye ofisi ya chama kwa nini isiwe Polisi? Kwa nini wawaite Polisi wamchukulie kwenye ofisi yao ya chama wakati walikuwa na gari waliyokuwa na uwezo wa kuikimbiza Polisi au Takukuru moja kwa moja?
3. Kama kosa liko kwa Mtoa na Mpokea rushwa kama sheria zinavyo elekeza, mbona waliokuwa wanapokea hizo rushwa hawajakamatwa na kikosi cha greenguard cha kuzuia na kupambana na rushwa kule Kalenga? Wao hawakuwa na kosa?! Dhamira ya kumkamata Rose Kamili pekee na kuwaacha wengine ni safi na haiibui mashaka hujma kwa mtu makini?!
4. Je tukio hilo lilikuwa la kupangwa au limetokea kwa bahati mbaya?! Bahati mbaya kwa maana ya kumkamata na kumpeleka ofisi za ccm nasi Polisi au kuwaita maofisa wa Takukuru waje eneo la tukio?
5. Tuna uhakika CCM huwa hawashirikiani na vyombo vya dola kukandamiza upinzani na kuwabambikiza kesi?! Kama jibu ni "HAPANA" Kwa nini mwenyekiti wa CCM taifa ambaye ni rais aliwahi kuwaambia CCM "...Na nyinyi acheni kuwategemea polisi kupambana na upinzani.." alikuwa ana maana gani?! Je inaweza kuwa CCM na Polisi hawakumsikia ndio tunashuhudia haya ya rose kamili?!
6. Je CCM waliomkamata Rose Kamili wanaweza kuaminika mbele ya Macho ya watu makini wanapomtuhumu Mpinzani wao kisiasa kuwa ni mtoa rushwa?! Ni dhana zipi tunaweza kuzitumia kuwa amini? Je tutawaamini?
7. Je zinaweza kuwa Propaganda za kisiasa na kuzitumia kwa kasi kwenye vyombo vya habari ili wananchi waone CCM na CHADEMA ni walewale na hivyo wananchi hawana haja wala hoja ya kufanya mabadiliko maana heri zimwi likujualo hali kuli likakwisha?!
Majibu ya maswali hayo yakikuridhisha bila chembe ya shaka changanya na zako na uanze kufungau ukurasa mpya wa kujifunza kutafakari kwa kina na mapana na marefu.
Tafakari ukiwa sober
mama rose alikuwa anahonga wapigakura ,hilo.liko wazi. hizi nyingine ni bla bla tu. huu uchaguzi chadema hawatoki. wanakalenga wamewakataa...
Hakuna cha kujadili hapa,Mkuu.
usiingie kichwa kichwa! ninacho kiongelea hapa ni msingi wa kawaida kabisa unapo mkamata mtoa na mpokea rushwa! je, unampeleka ofisi kwako au unaita/kupeleka kwenye vyombo vinavyohusika? je unamkamata mtoa rushwa tu na kumuacha mpokea rushwa?
Na hili ndilo CCM walilotakiwa kulisema kuwa tumefanya hivi kwa ajili ya kulipiza kisasi wengeweza kueleweka kidogo kuliko kuleta propaganda zao zisizo kuwa na ukweli wowope.
Mbona haya ndio matamanio yako?Mods ningeomba msimamie weledi wenu wa kazi na msikubali kuendeshwa na matamanio ya members humu ndani.
Kama ni kweli mlijiwekea majukwaa wenyewe humu JF na mijadala yote ufanywa kwenye jukwaa lake husika. Kwanini hii mada isipelekwe kule "jukwaa la chaguzi ndogo" maana ndio mahala pake? Naomba hatua zichukuliwe.
Invisible, Moderator
Kuhusu Rose Kamili: Hapa hakuna cha tafakuri tundizi wala lisuizi, huyo mwanamama hiyo tabia ya kutoa hongo si ngeni kwake, inasemekana hata huo ubunge wa viti maalumu alitoa hongo mbalimbali, leo iwe uchaguzi wa ubunge tena wa rafiki yake?
Tuiache TAKUKURU ifanye kazi yake. CHADEMA acheni kupepesuka, shughuli ndio kwanza imeanza.
mama rose alikuwa anahonga wapigakura ,hilo.liko wazi. hizi nyingine ni bla bla tu. huu uchaguzi chadema hawatoki. wanakalenga wamewakataa...
Hakuna cha kujadili hapa,
Kasome kifungu cha 16 na 14(a-h) cha Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya jinai Sura ya 20 utapata majibu yako.
rushwa mtoe nyie ccm tumefikaje hapo