Watanzania wote tupoe kwa msiba wa Mzee wetu huyu muhimu katika Taifa letu. Mapenzi ya mungu hayana makosa.
Nikirudi kwenye mada, katika wiki hii ya maombelezo, kuna mengi yanaendelea kujadiliwa kumuhusu Mzee wetu. yameelezwa mazuri mengi na mapungufu vile vile.
Mimi tafakuri yangu imefupisha eneo la Mapungufu au maeneo aliyoharibu.
Wakati najaribu kutoa maelezo yangu sijasahau mafanikio ya Mzee kwenye kuasisi mifumo, kuijenga Tanzania kidiplomasia, Msingi wa uchumi wa kujitegemea, Kujiamini kama kiongozi, kuacha alama nyingi na kuitangaza Tanzania na Afrika.
Kwenye eneo nililokusudia la madhaifu nimeyaweka kwenye makundi matatu.
1. Madhaifu mtambuka: Yale yote yanayotajwa kama madhaifu yakiwemo lugha kavu, kuwadharau waandishi na kudhibiti vyombo vya habari, kutaifisha mashirika ya umma n.k.
2. Kosa la kihistoria: Hili ni kosa ambalo mwenyewe amekiri kwenye kitabu chake cha "My life, My purpose" kuhusu mauaji ya Wazanzibari wa Pemba yaliyotokea kwenye utawala wake mwaka 2001 Januari, 27. Kama kiongozi amekiri kutia doa utawala wake.
3. Kosa la kushindwa kuondoa doa: Hili ndilo kosa kuu alilofanya Mzee wetu. Licha ya kuandika kitabu na kukiri alishindwa kuomba radhi. Hapo ndipo alifanya kosa zaidi.
Niishie hapo kwa muhtasari.
Naambatanisha na shairi la Mshairi. Malenga wa VISIWANI "Nenda baba yetu nenda, pumziko upatiwe".
Kishada
Nikirudi kwenye mada, katika wiki hii ya maombelezo, kuna mengi yanaendelea kujadiliwa kumuhusu Mzee wetu. yameelezwa mazuri mengi na mapungufu vile vile.
Mimi tafakuri yangu imefupisha eneo la Mapungufu au maeneo aliyoharibu.
Wakati najaribu kutoa maelezo yangu sijasahau mafanikio ya Mzee kwenye kuasisi mifumo, kuijenga Tanzania kidiplomasia, Msingi wa uchumi wa kujitegemea, Kujiamini kama kiongozi, kuacha alama nyingi na kuitangaza Tanzania na Afrika.
Kwenye eneo nililokusudia la madhaifu nimeyaweka kwenye makundi matatu.
1. Madhaifu mtambuka: Yale yote yanayotajwa kama madhaifu yakiwemo lugha kavu, kuwadharau waandishi na kudhibiti vyombo vya habari, kutaifisha mashirika ya umma n.k.
2. Kosa la kihistoria: Hili ni kosa ambalo mwenyewe amekiri kwenye kitabu chake cha "My life, My purpose" kuhusu mauaji ya Wazanzibari wa Pemba yaliyotokea kwenye utawala wake mwaka 2001 Januari, 27. Kama kiongozi amekiri kutia doa utawala wake.
3. Kosa la kushindwa kuondoa doa: Hili ndilo kosa kuu alilofanya Mzee wetu. Licha ya kuandika kitabu na kukiri alishindwa kuomba radhi. Hapo ndipo alifanya kosa zaidi.
Niishie hapo kwa muhtasari.
Naambatanisha na shairi la Mshairi. Malenga wa VISIWANI "Nenda baba yetu nenda, pumziko upatiwe".
Kishada