figganigga
JF-Expert Member
- Oct 17, 2010
- 25,483
- 54,853
Heshima kwenu wakuu,
Leo tujaribu kuangalia matukio ya Ukandamizaji kupitia vyombo vya dola, Je inatusaidia kama Taifa? Nini kifanyike kuondoka kwenye huuu mkwamo?
Naomba tutumie nafasi hii kushauri nini kifanyike ili kudumisha umoja wa Kitaifa ikizingatia sisi sote ni wamoja.
Chuki zimeanza zamani kidogo, Nakumbuka huko zazibar watu walikuwa hawazikani kwa sababu za kisiasa. Hivi sasa imefika hadi Tanganyika, watu hawazikani kisa Siasa, inaonekana Chuki ya Wazi mfano mdogo Kifo cha Mzee Ndesamburo.
Sasa hivi mtaani hakukaliki, mtu wa Upinzani anapofanya kosa hapelekwi mahakamani, Viongozi wa kisiasa wanatumia Mamlaka yao kuhukumu. Mfano Uharibifu wa Shamba la Mbowe.
Hivi juzi Serikali imeamua kukaa na Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuwakanya ili Wafuate Sheria bila shaka wamesikia.
Sasa kwenye hili Swala, Wewe kama Mwananchi wa Kawaida, nini Mchango wako ili tujikwamue hapa tulipo.
Ninachoamini, Serikali haiwezi kuwatuma wanasiasa wabaguane au wanyanyasane kwa vyeo vyao.
Hapa chini nmeweka picha za Shamba la Freeman Mbowe mwenyekiti wa CHADEMA liloharibiwa kwa Kigezo kwamba kalima sehemu oevu, Kumba haya ni mashamba ya Familia yapo miaka nenda rudi. Je Angeshitakiwa sheria zingechukua mkondo wake? Kwanini Hakishitakiwa?
Je unaweza vaa Viatu vya moyo wa huyu baba aliyramrisha waharibu shamba? Unafikiri alishawahi kulima?
Unadhani anazo fedha za kulipa kama akishindwa kesi au watatumia kodi zetu kulipa fidia?
Unaamini kama alisifiwa baada ya tukio hili?
Usiku alilala usingizi mzuri?
Tufanyeje kuokoa kizazi kijacho dhidi ya hizi chuki?
Karibuni.
Leo tujaribu kuangalia matukio ya Ukandamizaji kupitia vyombo vya dola, Je inatusaidia kama Taifa? Nini kifanyike kuondoka kwenye huuu mkwamo?
Naomba tutumie nafasi hii kushauri nini kifanyike ili kudumisha umoja wa Kitaifa ikizingatia sisi sote ni wamoja.
Chuki zimeanza zamani kidogo, Nakumbuka huko zazibar watu walikuwa hawazikani kwa sababu za kisiasa. Hivi sasa imefika hadi Tanganyika, watu hawazikani kisa Siasa, inaonekana Chuki ya Wazi mfano mdogo Kifo cha Mzee Ndesamburo.
Sasa hivi mtaani hakukaliki, mtu wa Upinzani anapofanya kosa hapelekwi mahakamani, Viongozi wa kisiasa wanatumia Mamlaka yao kuhukumu. Mfano Uharibifu wa Shamba la Mbowe.
Hivi juzi Serikali imeamua kukaa na Wakuu wa Mikoa na Wilaya kuwakanya ili Wafuate Sheria bila shaka wamesikia.
Sasa kwenye hili Swala, Wewe kama Mwananchi wa Kawaida, nini Mchango wako ili tujikwamue hapa tulipo.
Ninachoamini, Serikali haiwezi kuwatuma wanasiasa wabaguane au wanyanyasane kwa vyeo vyao.
Hapa chini nmeweka picha za Shamba la Freeman Mbowe mwenyekiti wa CHADEMA liloharibiwa kwa Kigezo kwamba kalima sehemu oevu, Kumba haya ni mashamba ya Familia yapo miaka nenda rudi. Je Angeshitakiwa sheria zingechukua mkondo wake? Kwanini Hakishitakiwa?
Je unaweza vaa Viatu vya moyo wa huyu baba aliyramrisha waharibu shamba? Unafikiri alishawahi kulima?
Unadhani anazo fedha za kulipa kama akishindwa kesi au watatumia kodi zetu kulipa fidia?
Unaamini kama alisifiwa baada ya tukio hili?
Usiku alilala usingizi mzuri?
Tufanyeje kuokoa kizazi kijacho dhidi ya hizi chuki?
Karibuni.