Tafakari ya Pasaka: Tunaonyeshwa kuwa Magufuli hakuyaishi maono yake na kama aliyaishi hayakuwa maono sahihi?

SANCTUS ANACLETUS

JF-Expert Member
Mar 5, 2016
3,337
4,664
Wanajamvi:

Kwa wale Wakristu, wanafahamu matukio muhimu yaliyojiri baada ya Yesu Kristu Kufa Msalabani. Kwanza, Dunia ilitetemeka kuonyesha kuwa yule aliyekuwa msalabani ni Mungu anayetawala maumbile. Pili, Pazia la Hekalu la wayahudi kupasuka vipande Viwili kutoka juu mpaka chini. Wafu waliokuwa wamekwisha kufa na kuzikwa kama ambavyo tumemzika Marehemu Raisi Magufuli kufufuka na baada ya Yesu Kristu kufufuka wakaingia Mji Mtakatifu na watu wakawaona na kuwatambua! Kubwa Zaidi, Wayahudi wenyewe waliokuwa wanamuona Yesu kabla ya kifo chake kama mhuni fulani hivi (rejea kauli ya kuwa wewe tunakujua ni Mwana wa Seremala tu), aliyekuja kuwaharibia maisha yao na watoto wao kufikia kukiri kwa midomo yao kuwa kwa hakika Yesu aliyekufa alikuwa ni Mwana wa Mungu.

Napenda kutumia kauli hii Ungamo ya wayahudi ambayo mimi naipa sura mbili: moja kama toba dhidi ya ukweli waliokuwa hawajaukubali lakini kama majuto kwa ujinga waliokuwa wameubeba na kuwapofusha kiasi kile ili kuangazia utawala wa juu wa Nchi yetu.

Katika kufanya hivyo, Ninajiuliza hivi kumbe: Raisi Magufuli hakuwa mwenye maono sahihi kama tulivyokuwa tunaimbiwa na kuaminishwa na sisi kuamini hivyo na hatimaye tumemtuza Sifa hiyo wakati wa kumsindikiza katika safari yake ya maisha mapya Mbinguni? Ninauliza Raisi Magufuli hakuwa Kiongozi mwenye maono na rajua iliyoeleweka? Nimesikia na kuona kauli na vitendo vya Kiongozi Mrithi kama vile vinasema Magufuli hakuwa hivyo kama tulivyomtazama! Tofauti na wayahudi, baada ya kifo cha Yesu wao kuungama kwamba Yesu alikuwa “Mwamba”, Uongozi wa juu wa Nchi na pengine wapambe wake wanatuonyesha movie nyingine tofauti kabisa tunavyofahamu. Ninaomba kutumia Mifano michache ili tuelewane maana watu wengi bila mifano ni kama Kenge mpaka damu itoke masikioni:

1. Kauli “hii ni Serikali ya Awamu ya Sita”.

Mimi sio mjuzi wa Sheria na Katiba ya Jamhuri ya Muungano. Hivi siku zote tunaposema hii ni awamu Fulani, tunakuwa tunaongozwa na uchaguzi Mkuu ambao unaweka Madiwani, Wabunge na Raisi Madarakani au kundi lolote tu kati ya hapo linatosha kuita Awamu fulani?

Tumemaliza Uchaguzi Mwaka jana na kupata Serikali ya Awamu ya tano. Inakuwaje leo kuwa Warithi wa Kiti cha marehemu wajitanabaishe wanaongoza Awamu ya Sita bila kujali kuwa wao ni mwendelezo tu wa serikali ambayo imetoka kuchaguliwa mwaka jana? Hivi Ilani ya uchaguzi nayo imeshabadilishwa na kusomeka Awamu ya Sita ili kuakisi hicho Kivumishi? Mbona sote tunajua ninyi warithi mlikuwa wasaidizi wa marehemu na mambo yote hayo mlikuwa mnatuambia kuwa mlikuwa mnafanya pamoja? Sababu za kujiita Awamu ya Sita ni zipi? Ni kitu gani cha kipekee na mahsusi ambacho hakiko katika Ilani ya chama ambacho mnakusudia kuwatendea watanzania na ambacho marehemu hakunuia kukifanya?

2. Kubadilisha Baraza la Mawaziri na Viongozi waandamizi.

Tunakumbuka ngwe ya mwisho ya Serikali ya awamu ya tano (5) toka imeundwa haina miezi sita. Na tunakumbuka marehemu Magufuli alipata kutueleza kuwa mlichukua miezi kibao ili kujipa nafasi ya kuunda Serikali madhubuti baada ya uchaguzi wa Mwaka 2020 na kwamba sawia mlikuwa mumeweka akiba (pool) ya viongozi ili kama kukitokea Ombwe au mwendo wa Jongoo replacement ifanyike. Tunajiuliza ikiwa ilikuwa ni lazima kupangua Baraza la Mawaziri kwa sababu ya Mhe. Waziri Mipango kutoa pengo kwa kupewa wadhifa Mkuu zaidi, upanguaji wa Makatibu Wakuu,Manaibu Makatibu Wakuu na Wizara Mpya, Wakuu wa Mikoa na Wilaya pamoja na Wakuu wa Taasisi zingine za Serikali ulazima wake unatoka wapi? Ile Wizara ya mambo ya uwekezaji ambayo marehemu alikuwa ameamua kuitoa ofisi ya Waziri Mkuu na kuipeleka Ofisi yake imeonekana na mapungufu gani mpaka kutolewa tena? Hamkushauriana wakati wa kufanya hayo maamuzi?

Hivi ni Meseji gani unatupatia kuhusu mtu uliyekuwa mnasadiana kazi? Tuelewe kuwa ulikuwa unaburuzwa kiimaamuzi? Tuelewe kuwa wasadizi wa karibu hivi walikuwa wanabariki tu maamuzi ya marehemu?

3. Kuvutia wawekezaji na Kutoa misamaha ya kodi.

Nina Imani Marehemu Raisi Magufuli alipokuwa anasema Nchi hii ilikuwa imefanywa shamba la Bibi, alimaanisha wawekezaji wezi na waporaji ndio waliokuwa wanahamisha utajiri wa Nchi na kwenda kuusondeka kwao. Hivi hawa wawekezaji tunaoambiwa sasa kuwa walikimbia na sasa wanaomba warudi ina maana tuelewe kuwa kumbe Raisi aliyepita alikuwa muonevu? Hivi ni wawekezaji gani serious ambao walikuwa wanaelewa na waliokuwa wanatimiza muono wa Win-win situation waliokimbia na kodi kiasi gani walikuwa wanachangia kwa Nchi yetu?


Hivi, tunayo hiyo orodha ya wawekezaji na idadi ya ajira walizokuwa wametengeneza hapa Nchini? Hivi tunaweza kwa ajili ya kuufanya mjadala huu uwe wenye tija kwa Nchi yetu, mitaji ya kiasi gani kwa ujumla wao walikuwa wamewekeza hao wawekazaji waliokimbia? Hivi kwa takwimu, tunaweza kusema ni pesa kiasi gani waliporwa hao wawekezaji na mamlaka ya kukusanya kodi? Hivi kweli kama kuna mwekezaji anasitasita kulipa kodi yetu halali tumsamehe ili pengnine asiondoke kwa sababu sisi ndio wenye shida? Hivi kumbe kwenye uwekezaji, kuna wenye shida na wasio wenye shida?

Hivi, wawekezaji wameibiwa, kudhulumiwa na kuonewa?

Hivi watu kama Barrick ambao Raisi wao alifika Ikulu kuja kuungama hadharani kuwa ni kweli walikuwa wanatuibia ikitokea wakikabwa walipe kile wasistaili kulipa na hawakulipa, inakuwa ni kufukuza wawekezaji? Hivi tuna idadi kiasi gani cha wawekezaji tunawahitaji ili Nchi hii iendelee kutokana na kukusanya Kodi na kupata ajira?Ni lazima tuwe na mamilioni ya wawekezaji au wawekezaji wachache serious wanaojua kuwa wanahitaji rasilimali zetu na sisi tunahitaji kunufaika na hizo rasimali? Ina maana kwa kauli hizi, tunaambiana kuwa tulikuwa tunaidanganya Dunia kwa tafiti za kisomi kama za akina Prof. Osoro?

Rasilimali madini na Shida zetu: Nimejiuliza kusikia kauli kuwa tusikaze sana mambo kwa sababu sisi ndio wenye shida! Sisi tuna shida ila wawekezaji hawana shida? Nimejiuliza sana kusikia kuwa eti yale madini ya Uranium kule Hifadhini hayaliwi na Tembo mpaka tutunishe misuli ya kutochimbwa haraka! Hivi kumbe hata Mwalimu aliyekuwa amesema kuwa Madini sio Kabichi kuwa yataoza na hivi yanaweza kusubiria mpaka watanzania watakapojitambua alikuwa anawafukuza wawekezaji?

Mimi ni maamuma wa mambo ya uwekezaji na mitaji lakini kichwa changu kinayo maswali mengi sana juu ya kauli za “sisi ndio wenye shida”. Akina Rostam Azizi na akina Bakheressa wao walitoa nini mpaka hawakuwa wamenyang’anywa pesa zao au kuonewa au wao hawakuwa na pa kukimbilia kupeleka investments zao?

Suala la Vibali vya kazi: Najiuliza hivi vibali vya kazi kwa wageni tunavyoambiwa vitolewe ili wawekezaji waweze kufanya kazi na watu wanaowaamini, tunapewa Elimu gani mpya? Hivi, tunayo mifano ya wawekezaji wengine duniani ambao hawakuweka ndugu zao na marafiki zao na watu wa rangi zao kwenye biashara zao ambao walifisika?

Tuambizane: tunayo mifano isiyoacha shaka ya wawekezaji ambao walipoamua kuweka maswahiba zao kwenye uwekezaji walipata faida kubwa na hawakuibiwa? Tunataka kurudisha enzi za wageni kuwamwagia watanzania maji ya mitaroni na kuwatemea mate usoni?

Tunataka kurudia enzi za wawekezaji wa mashine za Bahati Nasibu kukusanya sarafu na kuzihifadhi kwenye Magunia ndani ya Nyumba? Ni wageni wangapi wenye sifa ambao wamesumbuliwa kupata vibali? Hivi tunajua kuwa baadhi ya hao wageni hata kwa nafasi zinazokubalika kisheria bado wanapika competence zao? Mimi nina mfano mzuri na tena mbichi: kuna wachina wako hapa wengine wakiwa wamekuja kama Makapteni wa Meli za uvuvi na wengine mainjia, wameomba vibali vya kazi kupitia wakala Fulani lakini vyeti vyao ni vya kutilia shaka. Wasifu wao(CV) umebumbwa.Nitashangaa sana baada ya kauli kama hii wakipewa vibali. Kazi hawajui na wanafundishwa na wazawa hawahawa.


4. Mimi ni “Raisi Mwanamke”.

Wengi walishangilia na kusifia kauli hiyo. Binafsi iliniachia maswali. Toka Nchi hii tupate uhuru hakujawahi kupata Kiongozi anayeaminisha anawaongoza juu ya uwezo wake kwa kubainisha jinsia yake badala ya kufafanua maono, Sera na Mikakati na kuchukua hatua mara moja pale inapostahiki.

Watu walipouliza kama ni kweli unafaa hawakuuliza kwa sababu ya ujinsia. Baba wa Taifa alipohoji uwezo wa akina Malecela mwaka 1995 hakuongozwa na jinsia zao. Alijua ni wanaume lakini alikuwa anahoji Sifa zao za Ziada za kiuongozi. Mwalimu alipata kutuvujishia siri jinsi Ikulu kulivyo kugumu na kutahadharisha kuwa sio mahali pa watu kwenda kwa tambotambo na majigambo. Marehemu Magufuli naye alirudia jambo hilo hilo kuwa kama angalijua mambo yako vile Ikulu asingalikubali kuingiza jina lake. Tunajiuliza: mambo ni mepesi hata tuelezwe kuwa tofauti yangu na mtangulizi wangu ni jinsia tu? Ni kweli kwamba jinsia tu inaweza kuchora utofauti yeyoye na mtangulizi Raisi Magufuli na sio sifa za ziada za kiuongozi?


5. Kauli Mbiu ya “Jamhuri ya Muungano wa Tanzania: Kazi iendelee”

Tunafahamu pamoja na marehemu mlikuwa na kauli Mbiu ya “Hapa kazi tu”. Kwa kaulimbiu hii mpya inadokezwa kuwa ile ya “hapa kazi tu” ilikuwa na mapungufu pamoja na kwamba mlikuwa mkiitumia pamoja tu?

Juzi kwa mara ya kwanza, niliposikia salaamu yako hiyo nilishangaa ni salaamu gani isiyo na kiitikio? Nadhani wenye uelewa wamefikisha ujumbe na pengine ndio kisa sasa tumesikia kiitikio.

Pamoja na Kiitikio kupatikana bado tuna maswali: Ni kazi ipi itaendelea ilhali yaonekana kama kazi iliyokuwa inafanyika ina shida na dosari? Ikiwa kazi ilikuwa yatendeka vyema, haya mabadiliko ya haraka haraka kuanzia Baraza mpaka Wakurugenzi kama inavyokusudiwa yanaashia nini? Hivi, haionekani kwa kupanguapangua hivi (kiongozi mwenzenu mliyepita naye katika kampeini miezi michache tu iliyopita) kabla hata hajamaliza mwezi kaburini itawajengea picha kwa watanzania kuwa hamkuwa mkienda pamoja naye? Hivi, mwenzenu hajamaliza hata mwezi kaburini mumekuja na mabadiliko kama haya, inaashiria nini? Hivi, kweli kauli mbiu tu yatosha kufanikisha mipango, sera na maono kufikiwa?


Hitimisho: Watu tuna maswali mengi sana vichwani kwa kipindi hiki kifupi cha Uongozi. Ninaomba kurejea swali langu hapo juu? Mabadiliko haya yana mrengo wa kutueeleza kuwa watanzania tunaomlilia Marehemu Magufuli kama “Mwana wa Mungu” (Kiongozi shupavu sana na wa kuigwa) tunakosea na badala yake tunapewa picha kama ile waliyokuwa nayo wayahudi kabla ya Yesu hajateswa na kuuawa?


Ni ushauri tu kuwa ikiwa mumeshauriwa muwe makini sana kwa sababu wengine tunaona hizi zinaweza kuja kuwa sababu za kuthibitisha kuwa humutoshi kuvaa viatu ya marehemu. Na la kama ni mawazo na maono yako binafsi, basi humtendei haki kiongozi mwenzio mliyekuwa pamoja Ofisini kwa Zaidi ya miaka 5 na hakupata kukunanga hadharani. Shida iko wapi? Kama kulikuwa na tatizo mbona hukujitenga naye ikiwa ni ishara ya kuonyesha uongozi wa kuigwa? Karibuni tujadiliane.
 
Wanajamvi:

Kwa wale Wakristu, wanafahamu matukio muhimu yaliyojiri baada ya Yesu Kristu Kufa Msalabani. Kwanza, Dunia ilitetemeka kuonyesha kuwa yule aliyekuwa msalabani ni Mungu anayetawala maumbile. Pili, Pazia la Hekalu la wayahudi kupasuka vipande Viwili kutoka juu mpaka chini. Wafu waliokuwa wamekwisha kufa na kuzikwa kama ambavyo tumemzika Marehemu Raisi Magufuli kufufuka na baada ya Yesu Kristu kufufuka wakaingia Mji Mtakatifu na watu wakawaona na kuwatambua! Kubwa Zaidi, Wayahudi wenyewe waliokuwa wanamuona Yesu kabla ya kifo chake kama mhuni fulani hivi (rejea kauli ya kuwa wewe tunakujua ni Mwana wa Seremala tu), aliyekuja kuwaharibia maisha yao na watoto wao kufikia kukiri kwa midomo yao kuwa kwa hakika Yesu aliyekufa alikuwa ni Mwana wa Mungu.

Napenda kutumia kauli hii Ungamo ya wayahudi ambayo mimi naipa sura mbili: moja kama toba dhidi ya ukweli waliokuwa hawajaukubali lakini kama majuto kwa ujinga waliokuwa wameubeba na kuwapofusha kiasi kile ili kuangazia utawala wa juu wa Nchi yetu.

Katika kufanya hivyo, Ninajiuliza hivi kumbe: Raisi Magufuli hakuwa mwenye maono sahihi kama tulivyokuwa tunaimbiwa na kuaminishwa na sisi kuamini hivyo na hatimaye tumemtuza Sifa hiyo wakati wa kumsindikiza katika safari yake ya maisha mapya Mbinguni? Ninauliza Raisi Magufuli hakuwa Kiongozi mwenye maono na rajua iliyoeleweka? Nimesikia na kuona kauli na vitendo vya Kiongozi Mrithi kama vile vinasema Magufuli hakuwa hivyo kama tulivyomtazama! Tofauti na wayahudi, baada ya kifo cha Yesu wao kuungama kwamba Yesu alikuwa “Mwamba”, Uongozi wa juu wa Nchi na pengine wapambe wake wanatuonyesha movie nyingine tofauti kabisa tunavyofahamu. Ninaomba kutumia Mifano michache ili tuelewane maana watu wengi bila mifano ni kama Kenge mpaka damu itoke masikioni:

1. Kauli “hii ni Serikali ya Awamu ya Sita”.

Mimi sio mjuzi wa Sheria na Katiba ya Jamhuri ya Muungano. Hivi siku zote tunaposema hii ni awamu Fulani, tunakuwa tunaongozwa na uchaguzi Mkuu ambao unaweka Madiwani, Wabunge na Raisi Madarakani au kundi lolote tu kati ya hapo linatosha kuita Awamu fulani?

Tumemaliza Uchaguzi Mwaka jana na kupata Serikali ya Awamu ya tano. Inakuwaje leo kuwa Warithi wa Kiti cha marehemu wajitanabaishe wanaongoza Awamu ya Sita bila kujali kuwa wao ni mwendelezo tu wa serikali ambayo imetoka kuchaguliwa mwaka jana? Hivi Ilani ya uchaguzi nayo imeshabadilishwa na kusomeka Awamu ya Sita ili kuakisi hicho Kivumishi? Mbona sote tunajua ninyi warithi mlikuwa wasaidizi wa marehemu na mambo yote hayo mlikuwa mnatuambia kuwa mlikuwa mnafanya pamoja? Sababu za kujiita Awamu ya Sita ni zipi? Ni kitu gani cha kipekee na mahsusi ambacho hakiko katika Ilani ya chama ambacho mnakusudia kuwatendea watanzania na ambacho marehemu hakunuia kukifanya?

2. Kubadilisha Baraza la Mawaziri na Viongozi waandamizi.

Tunakumbuka ngwe ya mwisho ya Serikali ya awamu ya tano (5) toka imeundwa haina miezi sita. Na tunakumbuka marehemu Magufuli alipata kutueleza kuwa mlichukua miezi kibao ili kujipa nafasi ya kuunda Serikali madhubuti baada ya uchaguzi wa Mwaka 2020 na kwamba sawia mlikuwa mumeweka akiba (pool) ya viongozi ili kama kukitokea Ombwe au mwendo wa Jongoo replacement ifanyike. Tunajiuliza ikiwa ilikuwa ni lazima kupangua Baraza la Mawaziri kwa sababu ya Mhe. Waziri Mipango kutoa pengo kwa kupewa wadhifa Mkuu zaidi, upanguaji wa Makatibu Wakuu,Manaibu Makatibu Wakuu na Wizara Mpya, Wakuu wa Mikoa na Wilaya pamoja na Wakuu wa Taasisi zingine za Serikali ulazima wake unatoka wapi? Ile Wizara ya mambo ya uwekezaji ambayo marehemu alikuwa ameamua kuitoa ofisi ya Waziri Mkuu na kuipeleka Ofisi yake imeonekana na mapungufu gani mpaka kutolewa tena? Hamkushauriana wakati wa kufanya hayo maamuzi?

Hivi ni Meseji gani unatupatia kuhusu mtu uliyekuwa mnasadiana kazi? Tuelewe kuwa ulikuwa unaburuzwa kiimaamuzi? Tuelewe kuwa wasadizi wa karibu hivi walikuwa wanabariki tu maamuzi ya marehemu?

3. Kuvutia wawekezaji na Kutoa misamaha ya kodi.

Nina Imani Marehemu Raisi Magufuli alipokuwa anasema Nchi hii ilikuwa imefanywa shamba la Bibi, alimaanisha wawekezaji wezi na waporaji ndio waliokuwa wanahamisha utajiri wa Nchi na kwenda kuusondeka kwao. Hivi hawa wawekezaji tunaoambiwa sasa kuwa walikimbia na sasa wanaomba warudi ina maana tuelewe kuwa kumbe Raisi aliyepita alikuwa muonevu? Hivi ni wawekezaji gani serious ambao walikuwa wanaelewa na waliokuwa wanatimiza muono wa Win-win situation waliokimbia na kodi kiasi gani walikuwa wanachangia kwa Nchi yetu?


Hivi, tunayo hiyo orodha ya wawekezaji na idadi ya ajira walizokuwa wametengeneza hapa Nchini? Hivi tunaweza kwa ajili ya kuufanya mjadala huu uwe wenye tija kwa Nchi yetu, mitaji ya kiasi gani kwa ujumla wao walikuwa wamewekeza hao wawekazaji waliokimbia? Hivi kwa takwimu, tunaweza kusema ni pesa kiasi gani waliporwa hao wawekezaji na mamlaka ya kukusanya kodi? Hivi kweli kama kuna mwekezaji anasitasita kulipa kodi yetu halali tumsamehe ili pengnine asiondoke kwa sababu sisi ndio wenye shida? Hivi kumbe kwenye uwekezaji, kuna wenye shida na wasio wenye shida?

Hivi, wawekezaji wameibiwa, kudhulumiwa na kuonewa?

Hivi watu kama Barrick ambao Raisi wao alifika Ikulu kuja kuungama hadharani kuwa ni kweli walikuwa wanatuibia ikitokea wakikabwa walipe kile wasistaili kulipa na hawakulipa, inakuwa ni kufukuza wawekezaji? Hivi tuna idadi kiasi gani cha wawekezaji tunawahitaji ili Nchi hii iendelee kutokana na kukusanya Kodi na kupata ajira?Ni lazima tuwe na mamilioni ya wawekezaji au wawekezaji wachache serious wanaojua kuwa wanahitaji rasilimali zetu na sisi tunahitaji kunufaika na hizo rasimali? Ina maana kwa kauli hizi, tunaambiana kuwa tulikuwa tunaidanganya Dunia kwa tafiti za kisomi kama za akina Prof. Osoro?

Rasilimali madini na Shida zetu: Nimejiuliza kusikia kauli kuwa tusikaze sana mambo kwa sababu sisi ndio wenye shida! Sisi tuna shida ila wawekezaji hawana shida? Nimejiuliza sana kusikia kuwa eti yale madini ya Uranium kule Hifadhini hayaliwi na Tembo mpaka tutunishe misuli ya kutochimbwa haraka! Hivi kumbe hata Mwalimu aliyekuwa amesema kuwa Madini sio Kabichi kuwa yataoza na hivi yanaweza kusubiria mpaka watanzania watakapojitambua alikuwa anawafukuza wawekezaji?

Mimi ni maamuma wa mambo ya uwekezaji na mitaji lakini kichwa changu kinayo maswali mengi sana juu ya kauli za “sisi ndio wenye shida”. Akina Rostam Azizi na akina Bakheressa wao walitoa nini mpaka hawakuwa wamenyang’anywa pesa zao au kuonewa au wao hawakuwa na pa kukimbilia kupeleka investments zao?

Suala la Vibali vya kazi: Najiuliza hivi vibali vya kazi kwa wageni tunavyoambiwa vitolewe ili wawekezaji waweze kufanya kazi na watu wanaowaamini, tunapewa Elimu gani mpya? Hivi, tunayo mifano ya wawekezaji wengine duniani ambao hawakuweka ndugu zao na marafiki zao na watu wa rangi zao kwenye biashara zao ambao walifisika?

Tuambizane: tunayo mifano isiyoacha shaka ya wawekezaji ambao walipoamua kuweka maswahiba zao kwenye uwekezaji walipata faida kubwa na hawakuibiwa? Tunataka kurudisha enzi za wageni kuwamwagia watanzania maji ya mitaroni na kuwatemea mate usoni?

Tunataka kurudia enzi za wawekezaji wa mashine za Bahati Nasibu kukusanya sarafu na kuzihifadhi kwenye Magunia ndani ya Nyumba? Ni wageni wangapi wenye sifa ambao wamesumbuliwa kupata vibali? Hivi tunajua kuwa baadhi ya hao wageni hata kwa nafasi zinazokubalika kisheria bado wanapika competence zao? Mimi nina mfano mzuri na tena mbichi: kuna wachina wako hapa wengine wakiwa wamekuja kama Makapteni wa Meli za uvuvi na wengine mainjia, wameomba vibali vya kazi kupitia wakala Fulani lakini vyeti vyao ni vya kutilia shaka. Wasifu wao(CV) umebumbwa.Nitashangaa sana baada ya kauli kama hii wakipewa vibali. Kazi hawajui na wanafundishwa na wazawa hawahawa.


4. Mimi ni “Raisi Mwanamke”.

Wengi walishangilia na kusifia kauli hiyo. Binafsi iliniachia maswali. Toka Nchi hii tupate uhuru hakujawahi kupata Kiongozi anayeaminisha anawaongoza juu ya uwezo wake kwa kubainisha jinsia yake badala ya kufafanua maono, Sera na Mikakati na kuchukua hatua mara moja pale inapostahiki.

Watu walipouliza kama ni kweli unafaa hawakuuliza kwa sababu ya ujinsia. Baba wa Taifa alipohoji uwezo wa akina Malecela mwaka 1995 hakuongozwa na jinsia zao. Alijua ni wanaume lakini alikuwa anahoji Sifa zao za Ziada za kiuongozi. Mwalimu alipata kutuvujishia siri jinsi Ikulu kulivyo kugumu na kutahadharisha kuwa sio mahali pa watu kwenda kwa tambotambo na majigambo. Marehemu Magufuli naye alirudia jambo hilo hilo kuwa kama angalijua mambo yako vile Ikulu asingalikubali kuingiza jina lake. Tunajiuliza: mambo ni mepesi hata tuelezwe kuwa tofauti yangu na mtangulizi wangu ni jinsia tu? Ni kweli kwamba jinsia tu inaweza kuchora utofauti yeyoye na mtangulizi Raisi Magufuli na sio sifa za ziada za kiuongozi?


5. Kauli Mbiu ya “Jamhuri ya Muungano wa Tanzania: Kazi iendelee”

Tunafahamu pamoja na marehemu mlikuwa na kauli Mbiu ya “Hapa kazi tu”. Kwa kaulimbiu hii mpya inadokezwa kuwa ile ya “hapa kazi tu” ilikuwa na mapungufu pamoja na kwamba mlikuwa mkiitumia pamoja tu?

Juzi kwa mara ya kwanza, niliposikia salaamu yako hiyo nilishangaa ni salaamu gani isiyo na kiitikio? Nadhani wenye uelewa wamefikisha ujumbe na pengine ndio kisa sasa tumesikia kiitikio.

Pamoja na Kiitikio kupatikana bado tuna maswali: Ni kazi ipi itaendelea ilhali yaonekana kama kazi iliyokuwa inafanyika ina shida na dosari? Ikiwa kazi ilikuwa yatendeka vyema, haya mabadiliko ya haraka haraka kuanzia Baraza mpaka Wakurugenzi kama inavyokusudiwa yanaashia nini? Hivi, haionekani kwa kupanguapangua hivi (kiongozi mwenzenu mliyepita naye katika kampeini miezi michache tu iliyopita) kabla hata hajamaliza mwezi kaburini itawajengea picha kwa watanzania kuwa hamkuwa mkienda pamoja naye? Hivi, mwenzenu hajamaliza hata mwezi kaburini mumekuja na mabadiliko kama haya, inaashiria nini? Hivi, kweli kauli mbiu tu yatosha kufanikisha mipango, sera na maono kufikiwa?


Hitimisho: Watu tuna maswali mengi sana vichwani kwa kipindi hiki kifupi cha Uongozi. Ninaomba kurejea swali langu hapo juu? Mabadiliko haya yana mrengo wa kutueeleza kuwa watanzania tunaomlilia Marehemu Magufuli kama “Mwana wa Mungu” (Kiongozi shupavu sana na wa kuigwa) tunakosea na badala yake tunapewa picha kama ile waliyokuwa nayo wayahudi kabla ya Yesu hajateswa na kuuawa?


Ni ushauri tu kuwa ikiwa mumeshauriwa muwe makini sana kwa sababu wengine tunaona hizi zinaweza kuja kuwa sababu za kuthibitisha kuwa humutoshi kuvaa viatu ya marehemu. Na la kama ni mawazo na maono yako binafsi, basi humtendei haki kiongozi mwenzio mliyekuwa pamoja Ofisini kwa Zaidi ya miaka 5 na hakupata kukunanga hadharani. Shida iko wapi? Kama kulikuwa na tatizo mbona hukujitenga naye ikiwa ni ishara ya kuonyesha uongozi wa kuigwa? Karibuni tujadiliane.
Kiongozi pole kwa misiba mikubwa ya Baba Mosinyori na Baba Askofu

Je unazungumzia vipi pressure kubwa anazozitoa Mh. Samia kwa wizara za muungano kuhusu Zanzibar?!?.....mfano wizara ya fedha 'hazina' kutenga na kupeleka mafungu Zanzibar
 
Ndugu mwandishi,

Swala la kuiita "AWAMU YA KWANZA, AWAMU YA PILI, AWAMU YA TATU, AWAMU YA NNE, AWAMU YA TANO, AWAMU YA SITA" ni kwasababu tu ya kutofautisha utawala wa uongozi uliopo/uliokuwepo madarakani. Halipo hilo swala kikatiba, ni swala la kufanya wepesi kwenye reference ya utawala fulani.

Mfano, mtu ukimwambia Awamu Ya Pili, basi moja kwa moja anajua utawala ulikua wa Mzee Mwinyi, ukimwambia Awamu Ya Tano anajua moja kwa moja utawala ulikua wa Marehemu Magufuli, na hata baada ya miaka 100 mtu ukimwambia Awamu Ya Sita atajua moja kwa moja utawala ulikua ni wa Rais Mama Samia (Kipenzi cha wananchi) baada ya Marehemu Magufuli kufariki madarakani.

Pili, yote yaliofanyika katika uteuzi na ubadilishwaji wa Mawaziri na Makatibu ni kwa kufuata katiba na sheria za nchi. Rais anapokula kiapo, hawajibiki kisheria wala kikatiba kwa ulazima wa kufuata Baraza la Mawaziri au watendaji wowote wa serikali waliochaguliwa na Rais aliopita.

Katiba Ya Jamhuri Ya Muungano Wa Tanzania, inasema;

Ibara Ya 36 (1): - Rais atakua na mamlaka ya "KUANZISHA na KUFUTA" nafasi za madaraka ya namna mbali mbali katika utumishi wa serikali ya jamhuri ya muungano wa Tanzania.

Ibara Ya 37 (1): - Rais atakua "HURU na HATALAZIMIKA" kufuata ushauri atakaopewa na mtu yoyote, isipokua tu pale anapotakiwa na Katiba.

NOTE: Hata wewe mwandishi wa uzi huu, Rais halazimiki kisheria kufuata ushauri wako ng'o.
 
Kiongozi pole kwa misiba mikubwa ya Baba Mosinyori na Baba Askofu

Je unazungumzia vipi pressure kubwa anazozitoa Mh. Samia kwa wizara za muungano kuhusu Zanzibar?!?.....mfano wizara ya fedha 'hazina' kutenga na kupeleka mafungu Zanzibar
Huyu mazaa anataka awe anakata mapande anapeleka zenji...
 
Dikteta Magufuli alikuwa na maoni? Yepi hayo? Ya kupandikiza mbegu za chuki ya kutisha na mauaji!?
Kwa wale Wakristu, wanafahamu matukio muhimu yaliyojiri baada ya Yesu Kristu Kufa Msalabani. Kwanza, Dunia ilitetemeka kuonyesha kuwa yule aliyekuwa msalabani ni Mungu anayetawala maumbile. Pili, Pazia la Hekalu la wayahudi kupasuka vipande Viwili kutoka juu mpaka chini. Wafu waliokuwa wamekwisha kufa na kuzikwa kama ambavyo tumemzika Marehemu Raisi Magufuli kufufuka na baada ya Yesu Kristu kufufuka wakaingia Mji Mtakatifu na watu wakawaona na kuwatambua! Kubwa Zaidi, Wayahudi wenyewe waliokuwa wanamuona Yesu kabla ya kifo chake kama mhuni fulani hivi (rejea kauli ya kuwa wewe tunakujua ni Mwana wa Seremala tu), aliyekuja kuwaharibia maisha yao na watoto wao kufikia kukiri kwa midomo yao kuwa kwa hakika Yesu aliyekufa alikuwa ni Mwana wa Mungu.

Napenda kutumia kauli hii Ungamo ya wayahudi ambayo mimi naipa sura mbili: moja kama toba dhidi ya ukweli waliokuwa hawajaukubali lakini kama majuto kwa ujinga waliokuwa wameubeba na kuwapofusha kiasi kile ili kuangazia utawala wa juu wa Nchi yetu.

Katika kufanya hivyo, Ninajiuliza hivi kumbe: Raisi Magufuli hakuwa mwenye maono sahihi kama tulivyokuwa tunaimbiwa na kuaminishwa na sisi kuamini hivyo na hatimaye tumemtuza Sifa hiyo wakati wa kumsindikiza katika safari yake ya maisha mapya Mbinguni? Ninauliza Raisi Magufuli hakuwa Kiongozi mwenye maono na rajua iliyoeleweka? Nimesikia na kuona kauli na vitendo vya Kiongozi Mrithi kama vile vinasema Magufuli hakuwa hivyo kama tulivyomtazama! Tofauti na wayahudi, baada ya kifo cha Yesu wao kuungama kwamba Yesu alikuwa “Mwamba”, Uongozi wa juu wa Nchi na pengine wapambe wake wanatuonyesha movie nyingine tofauti kabisa tunavyofahamu. Ninaomba kutumia Mifano michache ili tuelewane maana watu wengi bila mifano ni kama Kenge mpaka damu itoke masikioni:

1. Kauli “hii ni Serikali ya Awamu ya Sita”.

Mimi sio mjuzi wa Sheria na Katiba ya Jamhuri ya Muungano. Hivi siku zote tunaposema hii ni awamu Fulani, tunakuwa tunaongozwa na uchaguzi Mkuu ambao unaweka Madiwani, Wabunge na Raisi Madarakani au kundi lolote tu kati ya hapo linatosha kuita Awamu fulani?

Tumemaliza Uchaguzi Mwaka jana na kupata Serikali ya Awamu ya tano. Inakuwaje leo kuwa Warithi wa Kiti cha marehemu wajitanabaishe wanaongoza Awamu ya Sita bila kujali kuwa wao ni mwendelezo tu wa serikali ambayo imetoka kuchaguliwa mwaka jana? Hivi Ilani ya uchaguzi nayo imeshabadilishwa na kusomeka Awamu ya Sita ili kuakisi hicho Kivumishi? Mbona sote tunajua ninyi warithi mlikuwa wasaidizi wa marehemu na mambo yote hayo mlikuwa mnatuambia kuwa mlikuwa mnafanya pamoja? Sababu za kujiita Awamu ya Sita ni zipi? Ni kitu gani cha kipekee na mahsusi ambacho hakiko katika Ilani ya chama ambacho mnakusudia kuwatendea watanzania na ambacho marehemu hakunuia kukifanya?

2. Kubadilisha Baraza la Mawaziri na Viongozi waandamizi.

Tunakumbuka ngwe ya mwisho ya Serikali ya awamu ya tano (5) toka imeundwa haina miezi sita. Na tunakumbuka marehemu Magufuli alipata kutueleza kuwa mlichukua miezi kibao ili kujipa nafasi ya kuunda Serikali madhubuti baada ya uchaguzi wa Mwaka 2020 na kwamba sawia mlikuwa mumeweka akiba (pool) ya viongozi ili kama kukitokea Ombwe au mwendo wa Jongoo replacement ifanyike. Tunajiuliza ikiwa ilikuwa ni lazima kupangua Baraza la Mawaziri kwa sababu ya Mhe. Waziri Mipango kutoa pengo kwa kupewa wadhifa Mkuu zaidi, upanguaji wa Makatibu Wakuu,Manaibu Makatibu Wakuu na Wizara Mpya, Wakuu wa Mikoa na Wilaya pamoja na Wakuu wa Taasisi zingine za Serikali ulazima wake unatoka wapi? Ile Wizara ya mambo ya uwekezaji ambayo marehemu alikuwa ameamua kuitoa ofisi ya Waziri Mkuu na kuipeleka Ofisi yake imeonekana na mapungufu gani mpaka kutolewa tena? Hamkushauriana wakati wa kufanya hayo maamuzi?

Hivi ni Meseji gani unatupatia kuhusu mtu uliyekuwa mnasadiana kazi? Tuelewe kuwa ulikuwa unaburuzwa kiimaamuzi? Tuelewe kuwa wasadizi wa karibu hivi walikuwa wanabariki tu maamuzi ya marehemu?

3. Kuvutia wawekezaji na Kutoa misamaha ya kodi.

Nina Imani Marehemu Raisi Magufuli alipokuwa anasema Nchi hii ilikuwa imefanywa shamba la Bibi, alimaanisha wawekezaji wezi na waporaji ndio waliokuwa wanahamisha utajiri wa Nchi na kwenda kuusondeka kwao. Hivi hawa wawekezaji tunaoambiwa sasa kuwa walikimbia na sasa wanaomba warudi ina maana tuelewe kuwa kumbe Raisi aliyepita alikuwa muonevu? Hivi ni wawekezaji gani serious ambao walikuwa wanaelewa na waliokuwa wanatimiza muono wa Win-win situation waliokimbia na kodi kiasi gani walikuwa wanachangia kwa Nchi yetu?


Hivi, tunayo hiyo orodha ya wawekezaji na idadi ya ajira walizokuwa wametengeneza hapa Nchini? Hivi tunaweza kwa ajili ya kuufanya mjadala huu uwe wenye tija kwa Nchi yetu, mitaji ya kiasi gani kwa ujumla wao walikuwa wamewekeza hao wawekazaji waliokimbia? Hivi kwa takwimu, tunaweza kusema ni pesa kiasi gani waliporwa hao wawekezaji na mamlaka ya kukusanya kodi? Hivi kweli kama kuna mwekezaji anasitasita kulipa kodi yetu halali tumsamehe ili pengnine asiondoke kwa sababu sisi ndio wenye shida? Hivi kumbe kwenye uwekezaji, kuna wenye shida na wasio wenye shida?

Hivi, wawekezaji wameibiwa, kudhulumiwa na kuonewa?

Hivi watu kama Barrick ambao Raisi wao alifika Ikulu kuja kuungama hadharani kuwa ni kweli walikuwa wanatuibia ikitokea wakikabwa walipe kile wasistaili kulipa na hawakulipa, inakuwa ni kufukuza wawekezaji? Hivi tuna idadi kiasi gani cha wawekezaji tunawahitaji ili Nchi hii iendelee kutokana na kukusanya Kodi na kupata ajira?Ni lazima tuwe na mamilioni ya wawekezaji au wawekezaji wachache serious wanaojua kuwa wanahitaji rasilimali zetu na sisi tunahitaji kunufaika na hizo rasimali? Ina maana kwa kauli hizi, tunaambiana kuwa tulikuwa tunaidanganya Dunia kwa tafiti za kisomi kama za akina Prof. Osoro?

Rasilimali madini na Shida zetu: Nimejiuliza kusikia kauli kuwa tusikaze sana mambo kwa sababu sisi ndio wenye shida! Sisi tuna shida ila wawekezaji hawana shida? Nimejiuliza sana kusikia kuwa eti yale madini ya Uranium kule Hifadhini hayaliwi na Tembo mpaka tutunishe misuli ya kutochimbwa haraka! Hivi kumbe hata Mwalimu aliyekuwa amesema kuwa Madini sio Kabichi kuwa yataoza na hivi yanaweza kusubiria mpaka watanzania watakapojitambua alikuwa anawafukuza wawekezaji?

Mimi ni maamuma wa mambo ya uwekezaji na mitaji lakini kichwa changu kinayo maswali mengi sana juu ya kauli za “sisi ndio wenye shida”. Akina Rostam Azizi na akina Bakheressa wao walitoa nini mpaka hawakuwa wamenyang’anywa pesa zao au kuonewa au wao hawakuwa na pa kukimbilia kupeleka investments zao?

Suala la Vibali vya kazi: Najiuliza hivi vibali vya kazi kwa wageni tunavyoambiwa vitolewe ili wawekezaji waweze kufanya kazi na watu wanaowaamini, tunapewa Elimu gani mpya? Hivi, tunayo mifano ya wawekezaji wengine duniani ambao hawakuweka ndugu zao na marafiki zao na watu wa rangi zao kwenye biashara zao ambao walifisika?

Tuambizane: tunayo mifano isiyoacha shaka ya wawekezaji ambao walipoamua kuweka maswahiba zao kwenye uwekezaji walipata faida kubwa na hawakuibiwa? Tunataka kurudisha enzi za wageni kuwamwagia watanzania maji ya mitaroni na kuwatemea mate usoni?

Tunataka kurudia enzi za wawekezaji wa mashine za Bahati Nasibu kukusanya sarafu na kuzihifadhi kwenye Magunia ndani ya Nyumba? Ni wageni wangapi wenye sifa ambao wamesumbuliwa kupata vibali? Hivi tunajua kuwa baadhi ya hao wageni hata kwa nafasi zinazokubalika kisheria bado wanapika competence zao? Mimi nina mfano mzuri na tena mbichi: kuna wachina wako hapa wengine wakiwa wamekuja kama Makapteni wa Meli za uvuvi na wengine mainjia, wameomba vibali vya kazi kupitia wakala Fulani lakini vyeti vyao ni vya kutilia shaka. Wasifu wao(CV) umebumbwa.Nitashangaa sana baada ya kauli kama hii wakipewa vibali. Kazi hawajui na wanafundishwa na wazawa hawahawa.


4. Mimi ni “Raisi Mwanamke”.

Wengi walishangilia na kusifia kauli hiyo. Binafsi iliniachia maswali. Toka Nchi hii tupate uhuru hakujawahi kupata Kiongozi anayeaminisha anawaongoza juu ya uwezo wake kwa kubainisha jinsia yake badala ya kufafanua maono, Sera na Mikakati na kuchukua hatua mara moja pale inapostahiki.

Watu walipouliza kama ni kweli unafaa hawakuuliza kwa sababu ya ujinsia. Baba wa Taifa alipohoji uwezo wa akina Malecela mwaka 1995 hakuongozwa na jinsia zao. Alijua ni wanaume lakini alikuwa anahoji Sifa zao za Ziada za kiuongozi. Mwalimu alipata kutuvujishia siri jinsi Ikulu kulivyo kugumu na kutahadharisha kuwa sio mahali pa watu kwenda kwa tambotambo na majigambo. Marehemu Magufuli naye alirudia jambo hilo hilo kuwa kama angalijua mambo yako vile Ikulu asingalikubali kuingiza jina lake. Tunajiuliza: mambo ni mepesi hata tuelezwe kuwa tofauti yangu na mtangulizi wangu ni jinsia tu? Ni kweli kwamba jinsia tu inaweza kuchora utofauti yeyoye na mtangulizi Raisi Magufuli na sio sifa za ziada za kiuongozi?


5. Kauli Mbiu ya “Jamhuri ya Muungano wa Tanzania: Kazi iendelee”

Tunafahamu pamoja na marehemu mlikuwa na kauli Mbiu ya “Hapa kazi tu”. Kwa kaulimbiu hii mpya inadokezwa kuwa ile ya “hapa kazi tu” ilikuwa na mapungufu pamoja na kwamba mlikuwa mkiitumia pamoja tu?

Juzi kwa mara ya kwanza, niliposikia salaamu yako hiyo nilishangaa ni salaamu gani isiyo na kiitikio? Nadhani wenye uelewa wamefikisha ujumbe na pengine ndio kisa sasa tumesikia kiitikio.

Pamoja na Kiitikio kupatikana bado tuna maswali: Ni kazi ipi itaendelea ilhali yaonekana kama kazi iliyokuwa inafanyika ina shida na dosari? Ikiwa kazi ilikuwa yatendeka vyema, haya mabadiliko ya haraka haraka kuanzia Baraza mpaka Wakurugenzi kama inavyokusudiwa yanaashia nini? Hivi, haionekani kwa kupanguapangua hivi (kiongozi mwenzenu mliyepita naye katika kampeini miezi michache tu iliyopita) kabla hata hajamaliza mwezi kaburini itawajengea picha kwa watanzania kuwa hamkuwa mkienda pamoja naye? Hivi, mwenzenu hajamaliza hata mwezi kaburini mumekuja na mabadiliko kama haya, inaashiria nini? Hivi, kweli kauli mbiu tu yatosha kufanikisha mipango, sera na maono kufikiwa?


Hitimisho: Watu tuna maswali mengi sana vichwani kwa kipindi hiki kifupi cha Uongozi. Ninaomba kurejea swali langu hapo juu? Mabadiliko haya yana mrengo wa kutueeleza kuwa watanzania tunaomlilia Marehemu Magufuli kama “Mwana wa Mungu” (Kiongozi shupavu sana na wa kuigwa) tunakosea na badala yake tunapewa picha kama ile waliyokuwa nayo wayahudi kabla ya Yesu hajateswa na kuuawa?


Ni ushauri tu kuwa ikiwa mumeshauriwa muwe makini sana kwa sababu wengine tunaona hizi zinaweza kuja kuwa sababu za kuthibitisha kuwa humutoshi kuvaa viatu ya marehemu. Na la kama ni mawazo na maono yako binafsi, basi humtendei haki kiongozi mwenzio mliyekuwa pamoja Ofisini kwa Zaidi ya miaka 5 na hakupata kukunanga hadharani. Shida iko wapi? Kama kulikuwa na tatizo mbona hukujitenga naye ikiwa ni ishara ya kuonyesha uongozi wa kuigwa? Karibuni tujadiliane.
 
Jiwe alikuwa mkono wa chuma. Unafikiri Mama angefanya nini. Kwahiyo Tulia watu tupumue kidogo sawa
 
Stori uliyosimuliwa hapo kale ilikuwa feki,unayoyaona sasa ndio uhalisia wenyewe.
 
Kiongozi pole kwa misiba mikubwa ya Baba Mosinyori na Baba Askofu

Je unazungumzia vipi pressure kubwa anazozitoa Mh. Samia kwa wizara za muungano kuhusu Zanzibar?!?.....mfano wizara ya fedha 'hazina' kutenga na kupeleka mafungu Zanzibar

Asante sana. Pole Nawe pia. Pamoja na misiba ya wapendwa wetu ila pia leo nimepata Askofu mpya wa Jimbo la Bunda. Mintarafu suala la ZN, hilo naona anaongea kinadharia. Tunayo mambo ya Muungano, Na kama anaongea juu ya hayo ni sawa ila kama anataka kila Wizara ifanye hivyo alete Katiba Mpya ili tuwe na Serikali Moja.
 
Wanajamvi:

Kwa wale Wakristu, wanafahamu matukio muhimu yaliyojiri baada ya Yesu Kristu Kufa Msalabani. Kwanza, Dunia ilitetemeka kuonyesha kuwa yule aliyekuwa msalabani ni Mungu anayetawala maumbile. Pili, Pazia la Hekalu la wayahudi kupasuka vipande Viwili kutoka juu mpaka chini. Wafu waliokuwa wamekwisha kufa na kuzikwa kama ambavyo tumemzika Marehemu Raisi Magufuli kufufuka na baada ya Yesu Kristu kufufuka wakaingia Mji Mtakatifu na watu wakawaona na kuwatambua! Kubwa Zaidi, Wayahudi wenyewe waliokuwa wanamuona Yesu kabla ya kifo chake kama mhuni fulani hivi (rejea kauli ya kuwa wewe tunakujua ni Mwana wa Seremala tu), aliyekuja kuwaharibia maisha yao na watoto wao kufikia kukiri kwa midomo yao kuwa kwa hakika Yesu aliyekufa alikuwa ni Mwana wa Mungu.

Napenda kutumia kauli hii Ungamo ya wayahudi ambayo mimi naipa sura mbili: moja kama toba dhidi ya ukweli waliokuwa hawajaukubali lakini kama majuto kwa ujinga waliokuwa wameubeba na kuwapofusha kiasi kile ili kuangazia utawala wa juu wa Nchi yetu.

Katika kufanya hivyo, Ninajiuliza hivi kumbe: Raisi Magufuli hakuwa mwenye maono sahihi kama tulivyokuwa tunaimbiwa na kuaminishwa na sisi kuamini hivyo na hatimaye tumemtuza Sifa hiyo wakati wa kumsindikiza katika safari yake ya maisha mapya Mbinguni? Ninauliza Raisi Magufuli hakuwa Kiongozi mwenye maono na rajua iliyoeleweka? Nimesikia na kuona kauli na vitendo vya Kiongozi Mrithi kama vile vinasema Magufuli hakuwa hivyo kama tulivyomtazama! Tofauti na wayahudi, baada ya kifo cha Yesu wao kuungama kwamba Yesu alikuwa “Mwamba”, Uongozi wa juu wa Nchi na pengine wapambe wake wanatuonyesha movie nyingine tofauti kabisa tunavyofahamu. Ninaomba kutumia Mifano michache ili tuelewane maana watu wengi bila mifano ni kama Kenge mpaka damu itoke masikioni:

1. Kauli “hii ni Serikali ya Awamu ya Sita”.

Mimi sio mjuzi wa Sheria na Katiba ya Jamhuri ya Muungano. Hivi siku zote tunaposema hii ni awamu Fulani, tunakuwa tunaongozwa na uchaguzi Mkuu ambao unaweka Madiwani, Wabunge na Raisi Madarakani au kundi lolote tu kati ya hapo linatosha kuita Awamu fulani?

Tumemaliza Uchaguzi Mwaka jana na kupata Serikali ya Awamu ya tano. Inakuwaje leo kuwa Warithi wa Kiti cha marehemu wajitanabaishe wanaongoza Awamu ya Sita bila kujali kuwa wao ni mwendelezo tu wa serikali ambayo imetoka kuchaguliwa mwaka jana? Hivi Ilani ya uchaguzi nayo imeshabadilishwa na kusomeka Awamu ya Sita ili kuakisi hicho Kivumishi? Mbona sote tunajua ninyi warithi mlikuwa wasaidizi wa marehemu na mambo yote hayo mlikuwa mnatuambia kuwa mlikuwa mnafanya pamoja? Sababu za kujiita Awamu ya Sita ni zipi? Ni kitu gani cha kipekee na mahsusi ambacho hakiko katika Ilani ya chama ambacho mnakusudia kuwatendea watanzania na ambacho marehemu hakunuia kukifanya?

2. Kubadilisha Baraza la Mawaziri na Viongozi waandamizi.

Tunakumbuka ngwe ya mwisho ya Serikali ya awamu ya tano (5) toka imeundwa haina miezi sita. Na tunakumbuka marehemu Magufuli alipata kutueleza kuwa mlichukua miezi kibao ili kujipa nafasi ya kuunda Serikali madhubuti baada ya uchaguzi wa Mwaka 2020 na kwamba sawia mlikuwa mumeweka akiba (pool) ya viongozi ili kama kukitokea Ombwe au mwendo wa Jongoo replacement ifanyike. Tunajiuliza ikiwa ilikuwa ni lazima kupangua Baraza la Mawaziri kwa sababu ya Mhe. Waziri Mipango kutoa pengo kwa kupewa wadhifa Mkuu zaidi, upanguaji wa Makatibu Wakuu,Manaibu Makatibu Wakuu na Wizara Mpya, Wakuu wa Mikoa na Wilaya pamoja na Wakuu wa Taasisi zingine za Serikali ulazima wake unatoka wapi? Ile Wizara ya mambo ya uwekezaji ambayo marehemu alikuwa ameamua kuitoa ofisi ya Waziri Mkuu na kuipeleka Ofisi yake imeonekana na mapungufu gani mpaka kutolewa tena? Hamkushauriana wakati wa kufanya hayo maamuzi?

Hivi ni Meseji gani unatupatia kuhusu mtu uliyekuwa mnasadiana kazi? Tuelewe kuwa ulikuwa unaburuzwa kiimaamuzi? Tuelewe kuwa wasadizi wa karibu hivi walikuwa wanabariki tu maamuzi ya marehemu?

3. Kuvutia wawekezaji na Kutoa misamaha ya kodi.

Nina Imani Marehemu Raisi Magufuli alipokuwa anasema Nchi hii ilikuwa imefanywa shamba la Bibi, alimaanisha wawekezaji wezi na waporaji ndio waliokuwa wanahamisha utajiri wa Nchi na kwenda kuusondeka kwao. Hivi hawa wawekezaji tunaoambiwa sasa kuwa walikimbia na sasa wanaomba warudi ina maana tuelewe kuwa kumbe Raisi aliyepita alikuwa muonevu? Hivi ni wawekezaji gani serious ambao walikuwa wanaelewa na waliokuwa wanatimiza muono wa Win-win situation waliokimbia na kodi kiasi gani walikuwa wanachangia kwa Nchi yetu?


Hivi, tunayo hiyo orodha ya wawekezaji na idadi ya ajira walizokuwa wametengeneza hapa Nchini? Hivi tunaweza kwa ajili ya kuufanya mjadala huu uwe wenye tija kwa Nchi yetu, mitaji ya kiasi gani kwa ujumla wao walikuwa wamewekeza hao wawekazaji waliokimbia? Hivi kwa takwimu, tunaweza kusema ni pesa kiasi gani waliporwa hao wawekezaji na mamlaka ya kukusanya kodi? Hivi kweli kama kuna mwekezaji anasitasita kulipa kodi yetu halali tumsamehe ili pengnine asiondoke kwa sababu sisi ndio wenye shida? Hivi kumbe kwenye uwekezaji, kuna wenye shida na wasio wenye shida?

Hivi, wawekezaji wameibiwa, kudhulumiwa na kuonewa?

Hivi watu kama Barrick ambao Raisi wao alifika Ikulu kuja kuungama hadharani kuwa ni kweli walikuwa wanatuibia ikitokea wakikabwa walipe kile wasistaili kulipa na hawakulipa, inakuwa ni kufukuza wawekezaji? Hivi tuna idadi kiasi gani cha wawekezaji tunawahitaji ili Nchi hii iendelee kutokana na kukusanya Kodi na kupata ajira?Ni lazima tuwe na mamilioni ya wawekezaji au wawekezaji wachache serious wanaojua kuwa wanahitaji rasilimali zetu na sisi tunahitaji kunufaika na hizo rasimali? Ina maana kwa kauli hizi, tunaambiana kuwa tulikuwa tunaidanganya Dunia kwa tafiti za kisomi kama za akina Prof. Osoro?

Rasilimali madini na Shida zetu: Nimejiuliza kusikia kauli kuwa tusikaze sana mambo kwa sababu sisi ndio wenye shida! Sisi tuna shida ila wawekezaji hawana shida? Nimejiuliza sana kusikia kuwa eti yale madini ya Uranium kule Hifadhini hayaliwi na Tembo mpaka tutunishe misuli ya kutochimbwa haraka! Hivi kumbe hata Mwalimu aliyekuwa amesema kuwa Madini sio Kabichi kuwa yataoza na hivi yanaweza kusubiria mpaka watanzania watakapojitambua alikuwa anawafukuza wawekezaji?

Mimi ni maamuma wa mambo ya uwekezaji na mitaji lakini kichwa changu kinayo maswali mengi sana juu ya kauli za “sisi ndio wenye shida”. Akina Rostam Azizi na akina Bakheressa wao walitoa nini mpaka hawakuwa wamenyang’anywa pesa zao au kuonewa au wao hawakuwa na pa kukimbilia kupeleka investments zao?

Suala la Vibali vya kazi: Najiuliza hivi vibali vya kazi kwa wageni tunavyoambiwa vitolewe ili wawekezaji waweze kufanya kazi na watu wanaowaamini, tunapewa Elimu gani mpya? Hivi, tunayo mifano ya wawekezaji wengine duniani ambao hawakuweka ndugu zao na marafiki zao na watu wa rangi zao kwenye biashara zao ambao walifisika?

Tuambizane: tunayo mifano isiyoacha shaka ya wawekezaji ambao walipoamua kuweka maswahiba zao kwenye uwekezaji walipata faida kubwa na hawakuibiwa? Tunataka kurudisha enzi za wageni kuwamwagia watanzania maji ya mitaroni na kuwatemea mate usoni?

Tunataka kurudia enzi za wawekezaji wa mashine za Bahati Nasibu kukusanya sarafu na kuzihifadhi kwenye Magunia ndani ya Nyumba? Ni wageni wangapi wenye sifa ambao wamesumbuliwa kupata vibali? Hivi tunajua kuwa baadhi ya hao wageni hata kwa nafasi zinazokubalika kisheria bado wanapika competence zao? Mimi nina mfano mzuri na tena mbichi: kuna wachina wako hapa wengine wakiwa wamekuja kama Makapteni wa Meli za uvuvi na wengine mainjia, wameomba vibali vya kazi kupitia wakala Fulani lakini vyeti vyao ni vya kutilia shaka. Wasifu wao(CV) umebumbwa.Nitashangaa sana baada ya kauli kama hii wakipewa vibali. Kazi hawajui na wanafundishwa na wazawa hawahawa.


4. Mimi ni “Raisi Mwanamke”.

Wengi walishangilia na kusifia kauli hiyo. Binafsi iliniachia maswali. Toka Nchi hii tupate uhuru hakujawahi kupata Kiongozi anayeaminisha anawaongoza juu ya uwezo wake kwa kubainisha jinsia yake badala ya kufafanua maono, Sera na Mikakati na kuchukua hatua mara moja pale inapostahiki.

Watu walipouliza kama ni kweli unafaa hawakuuliza kwa sababu ya ujinsia. Baba wa Taifa alipohoji uwezo wa akina Malecela mwaka 1995 hakuongozwa na jinsia zao. Alijua ni wanaume lakini alikuwa anahoji Sifa zao za Ziada za kiuongozi. Mwalimu alipata kutuvujishia siri jinsi Ikulu kulivyo kugumu na kutahadharisha kuwa sio mahali pa watu kwenda kwa tambotambo na majigambo. Marehemu Magufuli naye alirudia jambo hilo hilo kuwa kama angalijua mambo yako vile Ikulu asingalikubali kuingiza jina lake. Tunajiuliza: mambo ni mepesi hata tuelezwe kuwa tofauti yangu na mtangulizi wangu ni jinsia tu? Ni kweli kwamba jinsia tu inaweza kuchora utofauti yeyoye na mtangulizi Raisi Magufuli na sio sifa za ziada za kiuongozi?


5. Kauli Mbiu ya “Jamhuri ya Muungano wa Tanzania: Kazi iendelee”

Tunafahamu pamoja na marehemu mlikuwa na kauli Mbiu ya “Hapa kazi tu”. Kwa kaulimbiu hii mpya inadokezwa kuwa ile ya “hapa kazi tu” ilikuwa na mapungufu pamoja na kwamba mlikuwa mkiitumia pamoja tu?

Juzi kwa mara ya kwanza, niliposikia salaamu yako hiyo nilishangaa ni salaamu gani isiyo na kiitikio? Nadhani wenye uelewa wamefikisha ujumbe na pengine ndio kisa sasa tumesikia kiitikio.

Pamoja na Kiitikio kupatikana bado tuna maswali: Ni kazi ipi itaendelea ilhali yaonekana kama kazi iliyokuwa inafanyika ina shida na dosari? Ikiwa kazi ilikuwa yatendeka vyema, haya mabadiliko ya haraka haraka kuanzia Baraza mpaka Wakurugenzi kama inavyokusudiwa yanaashia nini? Hivi, haionekani kwa kupanguapangua hivi (kiongozi mwenzenu mliyepita naye katika kampeini miezi michache tu iliyopita) kabla hata hajamaliza mwezi kaburini itawajengea picha kwa watanzania kuwa hamkuwa mkienda pamoja naye? Hivi, mwenzenu hajamaliza hata mwezi kaburini mumekuja na mabadiliko kama haya, inaashiria nini? Hivi, kweli kauli mbiu tu yatosha kufanikisha mipango, sera na maono kufikiwa?


Hitimisho: Watu tuna maswali mengi sana vichwani kwa kipindi hiki kifupi cha Uongozi. Ninaomba kurejea swali langu hapo juu? Mabadiliko haya yana mrengo wa kutueeleza kuwa watanzania tunaomlilia Marehemu Magufuli kama “Mwana wa Mungu” (Kiongozi shupavu sana na wa kuigwa) tunakosea na badala yake tunapewa picha kama ile waliyokuwa nayo wayahudi kabla ya Yesu hajateswa na kuuawa?


Ni ushauri tu kuwa ikiwa mumeshauriwa muwe makini sana kwa sababu wengine tunaona hizi zinaweza kuja kuwa sababu za kuthibitisha kuwa humutoshi kuvaa viatu ya marehemu. Na la kama ni mawazo na maono yako binafsi, basi humtendei haki kiongozi mwenzio mliyekuwa pamoja Ofisini kwa Zaidi ya miaka 5 na hakupata kukunanga hadharani. Shida iko wapi? Kama kulikuwa na tatizo mbona hukujitenga naye ikiwa ni ishara ya kuonyesha uongozi wa kuigwa? Karibuni tujadiliane.
Google kwa nje utaiona ni kampuni search engine tu, lakini kwa ndani ni advertising surveillance company.

Ni sawa na Magu kwa nje mpigania wanyonge, mpinga ufisadi, ila kiuhalisia kwa ndani
👇👇👇👇👇👇
Magufuli hakuwahi kuamini katika kuboresha maisha ya watu.

Kila siku alikuwa akilala anaamka akiwaza amtese nani ili awe na furaha.

Genge lake limeiba, limepora, limetishia maisha, limedhalikisha, limefisadi, limegonga propaganda za nguvu huku likijitajirisha kupindukia. Hakuna mtu akiyeko genge la Magu ambaye ni masikini.
 
5 Reactions
Reply
Back
Top Bottom