Uchaguzi 2020 Tafakari ya Kina: Tundu Lissu akifuta kodi ataendeshaje nchi?

Masokotz

JF-Expert Member
Nov 26, 2018
3,493
5,528
Naendelea na mada zangu za Kumuunga mkono Ndugu Tundu Antipasi Mughai Lissu kwa nafasi ya Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania bali kwa sababu namuelewa. Ili kuweka kumbukumbu sawa mimi sio mwanachama wa CHADEMA wala CCM na wala mimi siamini katika ITIKADI za chama cha CHADEMA. Tofauti yangu ya kiitikadi utaipata kupitia jibu la swali hili.

JE, UKILALA NA NJAA KWA SABABU YA KUKOSA CHAKULA JE SERIKALI INASTAHILI KULAUMIWA? KAMA JIBU LAKO NI NDIO BASI TUKO KATIKA ITIKADI MOJA ILA KAM JIBU LAKO NI HAPANA BASI ITIKADI ZETU NI TOFAUTI. Sasa Tuendelee. Kodi nini?

Kodi ni Mchango wa Hiyari ya Lazima unaotolewa na wananchi na wakazi wa nchi kuchangia uendeshaji wa shuguli za serikali.Ni hiyari kwa sababu lazima wanachi wakubaliane kulipa mchango huo kupitia vyombo vya maamuzi na ni lazima kwa sababu ikishapitishwa usipolipa ni kosa.

Kwa misingi hio basi KODI ndio chanzo kikuu cha mapati ya serikali yoyote duniani. Katika malipo ya Kodi kuna aina mbili za kodi pamoja na nyingine nyingi humo ndani nazo ni KODI za MOJA KWA MOJA(DIRECT TAXES) na Kodi ambazo sio za moja kwa moja (INDIRECT TAX)

Katika mifumo hii miwili ya kodi msingi wa ukusanyaji na utoaji wa taarifa za kodi unazingatia vigezo mbalimbali ikiwamo vyanzo ya mapato na urahisi wa ukusanyaji kwa upande wa serikali na kwa upande wa mlipaji. Kwa kawaida gharama ya kulipa au kukusanya kodi inapaswa kuwa ndogo ili iwe na tija. Ni upumbavu wa kiwango cha lami kutumia Bilioni moja kukusanya kodi yenye thamani ya BIlioni moja. Kama unajua hesabu unaelewa huu ujinga unafanyika wapi.

Lakini pia katika mfumo wa ukusanyaji wa kodi kuna kodi zinatozwa wakati wa kupata kipato na kodi zinatozwa wakati kutumia kipato. Zote ni kodi ili kuna yofauti kubwa sana kati ya kodi hizi mbili na ufanisi wake.

Kwa mujibu wa uzoefu, KODI BORA kuliko zote ni kodi zilizounganishwa na huduma(Kwa mfano Kodi ya kusafisha mazingira na ukaona watu wanasafisha mazingira, Kodi ya Huduma za afya na ukapewa huduma ya afya, Kodi ya huduma ya elimu na ukaona huduma ya elimu, kodi ya matumiz ya huduma kama vile bandari, barabara, etc) Hizi kodi mlipaji anazifurahia wakati wa kuzilipa na ni rahisi kukusanya.

Kuna hizi kodi za kuwindana na kutafutana huku mtaani na makofuli eti sijui huna leseni tunakufungia Biashara.Hizi ni kodi kero na ni ama zifutwe au zibadilishiwe utaratibu wa kukusanya. Kwa mfano-Kusajili Biashara kuwe ni Bure halafu ada ya leseni iwe compounded kwenye system with penaltie kama ukcihelewa kulipa with options ya kulipa installments etc. Hakuna haja ya kufungia watu biashara.

Mkaguzi wa Kodi akija akikuta una deni kubwa akiweka kofuli kwenye biashara yako maana yake anakufilisi duka linakuwa Public Property. Kuna ugumu gani hapo?

Sasa niwaeleze vizuri kuhusu TUNDU LISSU
Akiwa Rais wetu huyu BWANA ndivyo atakavyofanya. Hutasumbuliwa Barabarani kuhusu leseni au kodi. Utapata TEX kwenye SIMU yako inakwambia unadaiwa leseni ya MIAKA 3 jumla deni lako ni Milioni 100, Iwapo unafikiri kuna makosa basi piga simu halmashauri/ofisi ya kodi/leseni upate msaada zaidi. Hii inaitwa kuendesha nchi kisasa.

Unaposajili Biashara yako unapewa mafunzo na fursa mbalimbali. Unawekwa katika orodha ya suppliers wa halamashauri husika ili kukiwa nakazi basi na wewe unaweza kuomba kuwa supplier kwa sababu una leseni na kodi unalipa. HAYO NDIO MAENDELEO YA WATU

Tuache kudanganywa na watu ambao hawajui hata wnachofanya. TUMCHAGUA TUNDU LISSU AWE RAIS WETU TUONE MAENDELEO YA KWELI

Nimeandika haya nikiwa katika UFUKWE Kimbiji,Kigamboni Jijini Dar es Salaama

Kizito S.
 
Ndugu yangu uko sawa kabisa mfa maji haishi kutapa tapa lissu anahangaika ili kuwafurahisha watu.aonekana mwema lkn misingi ya nchi yoyote dunia ni kodi sasa yeye anataka kutuletea wafadhili hapa ili tuwe kama nairobi sasa hiv wanahaha kukabilina na amri za bwana trumb
 
Hayo yote baadae kwa sasa mziki ni mmoja tu, kuiondoa CCM madarakani ili tupate uhuru ulio na Uhuru.

Yaani kila mkoa kila wilaya kutakuwa na kijiwe ,vitavyoruhusiwa kusema chochote kile juu ya nchi yako kama inaendeshwa vibaya vizuri vijiwe au viwanja hivyo vitakuwepo kisheria kabisa, utakalosema hapo huwezi kushitakiwa wala kuguswa, tutaviita viwanja vya demokrasia kwa ajili ya siasa za nchi yetu, wananchi kutoa joto lao dhidi ya serikali iliyopo madarakani.
 
ndugu yangu uko sawa kabisa mfa maji haishi kutapa tapa lissu anahangaika ili kuwafurahisha watu.aonekana mwema lkn misingi ya nchi yoyote dunia ni kodi sasa yeye anataka kutuletea wafadhili hapa ili tuwe kama nairobi sasa hiv wanahaha kukabilina na amri za bwana trumb
Hivi umeelewa kilichoamdikwa kwel? Au umesoma kichwa cha habar ukakimbilia kutoa maoni, hii ndo shida ya Lumumba
 
Nyinyi mbona wapumbavu

Amewaambia anafuta kodi? Au ataboresha makusanyo ya kodi kwa haki.

Hebu weka ushahidi pasi na mashaka kuthibitisha hii hoja yako.
Nawe soma acha uvivu, mbona unakuwa kama lumumba? Ama kwel kwenye safina hata mapepo yaliingia
 
Ishu ni kodi onevu.

Kwa sababu ya kupenda shortcut tumijikita kwenye maeneo ambayo ni rahisi kuwabana watu. Mfano kodi yetu kubwa inatokana na mizigo inayoingia au kutoka kwenye bandari kuu.

Kuna sehemu nyingi tu unaweza kupata vyanzo vya mapato.

Pia baadhi ya nchi huzifutia kodi kampuni kubwa zinazoajiri wafanyakazi wengi. Badala yake inaiambia ile kampuni kuwekeza zaidi ndani ya nchi na kuongeza ajira.

Kikubwa kinachohitajika ni mchunguko wa pesa kwa wananchi.
 
Hakika inasikitisha saana, watz hatupendi kujadili masuala tunapenda ushabiki!!!, nani kasema kodi itafutwa?!!!?, mantiki yake ni mfumo wa kukusanya kodi utaboreshwa na ukiboreshwa mlipa kodi atalipa kodi kwa furaha. ndugu yangu fanya biashara kwa sasa uone watoza ushuru hawa walivyo na karaha!!
 
Nchi hii ni tajiri sana,kuna nchi haxina kodi na wanaendesha maisha kama kawaida..
 
Watu watahamasishwa tu waone kulipa Kodi ni haki yao ya lazima km kuvuta hewa! kula chakula ili uishi, ni lazima. watajipeleka wenyewe, kazi hii ya uhamasishaji ifanywe na vijana wapole wazuri wa sura, ke'' kwa me'' wanao ongea kwa lafudhi tamu na rafiki. nasema vijana sababu kundi hili ndiyo zuri kwa biashara yeyote, km Bar, Ndege, Hotel nk!

watoe ushauri na msaada kwa wafanya biashara, siyo km sasa wanatembea na Mgambo, Police km ugomvi, kufunga maduka ya dawa. mtu akiona Mgambo tu hana amani moyoni.

Kodi ni gharama za maendeleo ya huduma ninayo patiwa mimi mwananchi. Badilini neno kuendesha huduma za serikali, sijui kodi ya kichwa no! ni maneno ambayo si rafiki! sema ''Afya yako mwanana yaja malangoni pako leo'' na kweli umpe hiyo Afya uzuri.

Kifupi watu wenyewe watamani yale sirikali inayowafanyia faster na kwa ufanisi, hata akikwama kuipata hiyo huduma usimzodoe ongea nae taatibu aseme alipo kwama!!!

watu Million 67 siyo wengi kuwapa huduma mpaka mlangoni. hata ukiwaambia nitakuwa nakuoshea viatu vyako kila siku, atatoa hela hiyo! siyo ukajenge uwanja wa ndege chato kibabe! walahi lazima wakuibie na wewe utumie nguvu kuwapata.
 
Back
Top Bottom