Kiranja Mkuu
JF-Expert Member
- Feb 18, 2010
- 4,066
- 4,085
Neno la leo linatoka katika kitabu Kitakatifu kilichoandikwa na nabii Yeremia 17: 5-8, nalo lasema hivi:-
5. Bwana asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha Bwana.
6. Maana atakuwa kama fukara nyikani, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jangwani palipo ukame, Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.
7. Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake.
8. Maana atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji, Uenezao mizizi yake karibu na mto; Hautaona hofu wakati wa hari ujapo, Bali jani lake litakuwa bichi; Wala hautahangaika mwaka wa uchache wa mvua, Wala hautaacha kuzaa matunda
Mungu atubariki sana, tumtegemee yeye pekee. Tuwasahau waganga na waganguzi, wachawi, hirizi na vile vyote mwanadamu anavyovitegemea kwa nguvu zake mwenyewe.
5. Bwana asema hivi, Amelaaniwa mtu yule amtegemeaye mwanadamu, Amfanyaye mwanadamu kuwa kinga yake Na moyoni mwake amemwacha Bwana.
6. Maana atakuwa kama fukara nyikani, Hataona yatakapotokea mema; Bali atakaa jangwani palipo ukame, Katika nchi ya chumvi isiyokaliwa na watu.
7. Amebarikiwa mtu yule anayemtegemea Bwana, Ambaye Bwana ni tumaini lake.
8. Maana atakuwa kama mti uliopandwa kando ya maji, Uenezao mizizi yake karibu na mto; Hautaona hofu wakati wa hari ujapo, Bali jani lake litakuwa bichi; Wala hautahangaika mwaka wa uchache wa mvua, Wala hautaacha kuzaa matunda
Mungu atubariki sana, tumtegemee yeye pekee. Tuwasahau waganga na waganguzi, wachawi, hirizi na vile vyote mwanadamu anavyovitegemea kwa nguvu zake mwenyewe.