Meitinyiku L. Robinson
JF-Expert Member
- Aug 29, 2011
- 412
- 90
Tumaini langu ni kwamba member wote mmeamka salama. Na naomba tusaidiane hili;
Kumbukumbu zangu zinaonesha kuwa Nchi yetu mpaka hapa ilipofikia ilishwahi kuwa na Mawaziri Wakuu 9 toka tupate Uhuru na ili kuweka kumbukumbuku sawa nitaomba niwataje na kama kuna nitakapokwenda tofauti nipo tayari kurekebishwa
Mhe. NYERERE Julius Kambarage
Mhe. MORINGE Edward Sokoine
Mhe. MSUYA Cleopa David
Mhe. SALIM Ahmed Salim
Mhe. WARIOBA Sinde Joseph
Mhe. MALECELA John
Mhe. TULUWAY Sumai Frederick
Mhe. LOWASSA Ngoyai Edward na huyu tumtazamiaye
Mhe. PINDA Mizengo Kayanza Peter
Sasa kama wasemavyo Kiutaratibu watu hawa wakishastaafu huendelea kulipwa na Serikali (Kodi za Wananchi) na hata wanpokufa familia zao bado huendelea kufaidi ama kuneemeka kwa kodi za Wananchi tu kwa sababu ya nafasi walizowahi kuwa nazo katika Taifa hili ikiwa na maana kwamba watajwa hapo juu mpaka ninapoandika hapa ni kwamba wao bado wanalipwa na wataendelea kulipwa labda mpaka Kristo arudi.
Hili siwezi kulijengea hoja nimelichukulia kama utangulizi manake ni utaratibu ambao ulikwisha pitishwa hivyo hata kuujadili ni sawa na kujaza maji gunia labda kwa ushauri Katiba mpya tunayoitazamia hili litizamwe kwa jicho lingine. Kinachonigusa zaidi ni swala la "kama" Waziri Mkuu aliyepo ama atajiuzulu au kutolewa na Mkuu wake je kuna haja kweli ya kuteua Waziri Mkuu mpya kuliongoza Taifa hili?? Hii ni kwa kuzingatia utangulizi huo hapo juu na ikizingatiwa kuwa Mrisho Kikwete toka aingie madarakani amekwisha kuwa na Mawaziri Wakuu wawili hivyo kama atateua mwingine basi atakamilisha jumla ya Mawaziri Wakuu watatu katika kipindi chake.
Mawaziri Wakuu ambao watalipwa na kuendelea kulipwa fedha za walipa kodi katika maisha yao yote wao pamoja na familia yao. Mkapa alikwishawahi kuulizwa ni kwa nini hakumbadilisha Frederick Sumai na badala yake akamteua tena kwa kipindi kingine jibu lake lilikuwa fupi alisema naona huruma fedha za Watanzania kuendelea kumlipia Waziri Mkuu mwingine nitakaye mteua. Kama alimaanisha ama kama hakumaanisha hilo siwezi fanya mada ila binafsi niliguswa na majibu yake manake kama kweli angeteua mwingine basi idadi yao ingeongezeka.
Hivyo mimi nadhani tuendelee kujiuliza na kushauriana je Nchi yetu hapa ilipofikia tukizingatia kutafunwa kwake kote, tukizingatia uzembe wa watendaji na wakuu wake, tukizingatia matatizo yaliyopo katika taasisi mbalimbali za Serikali na nyinginezo, tukizingatia umasikini na shida tulizonazo Watanzani ambayo kwayo wao ni "maisha bora", tukizingatia hitaji letu kama Taifa na kubwa zaidi tukizingatia kwamba sisi ndio wahusika wakuu na walipaji halali wa mishahara na mahitaji mengine ya huyo Waziri Mkuu akiwa katika nafasi yake na hata atakapostaafu, akiwa hai na hata atakapotwaliwa.
MWISHO laiti ningekuwa JK ningedhihirisha kiwango cha busara nilicho nacho kwa kuamua kuweka kando swala la makundi, na kuamua kujishusha na kuamua kulitanguliza Taifa mbele hivyo kuamini pasipo shaka kuwa katika majina ya wasstafu tajwa hapo juu mbali na wale waliokwisha tangulia katika haki (Mungu awalaze pema peponi) bado wapo si wenye nguvu tu bali wazalendo pia; hivyo ili kulisaidia Taifa na Wananchi wangu ningekaa chini na kuamua kuchagua mmoja kati ya hao ili kumrithi huyu tumtazamiaye.
Mungu Ibariki Tanzania.
MEITINYIKU L. Robinson.
Kumbukumbu zangu zinaonesha kuwa Nchi yetu mpaka hapa ilipofikia ilishwahi kuwa na Mawaziri Wakuu 9 toka tupate Uhuru na ili kuweka kumbukumbuku sawa nitaomba niwataje na kama kuna nitakapokwenda tofauti nipo tayari kurekebishwa
Mhe. NYERERE Julius Kambarage
Mhe. MORINGE Edward Sokoine
Mhe. MSUYA Cleopa David
Mhe. SALIM Ahmed Salim
Mhe. WARIOBA Sinde Joseph
Mhe. MALECELA John
Mhe. TULUWAY Sumai Frederick
Mhe. LOWASSA Ngoyai Edward na huyu tumtazamiaye
Mhe. PINDA Mizengo Kayanza Peter
Sasa kama wasemavyo Kiutaratibu watu hawa wakishastaafu huendelea kulipwa na Serikali (Kodi za Wananchi) na hata wanpokufa familia zao bado huendelea kufaidi ama kuneemeka kwa kodi za Wananchi tu kwa sababu ya nafasi walizowahi kuwa nazo katika Taifa hili ikiwa na maana kwamba watajwa hapo juu mpaka ninapoandika hapa ni kwamba wao bado wanalipwa na wataendelea kulipwa labda mpaka Kristo arudi.
Hili siwezi kulijengea hoja nimelichukulia kama utangulizi manake ni utaratibu ambao ulikwisha pitishwa hivyo hata kuujadili ni sawa na kujaza maji gunia labda kwa ushauri Katiba mpya tunayoitazamia hili litizamwe kwa jicho lingine. Kinachonigusa zaidi ni swala la "kama" Waziri Mkuu aliyepo ama atajiuzulu au kutolewa na Mkuu wake je kuna haja kweli ya kuteua Waziri Mkuu mpya kuliongoza Taifa hili?? Hii ni kwa kuzingatia utangulizi huo hapo juu na ikizingatiwa kuwa Mrisho Kikwete toka aingie madarakani amekwisha kuwa na Mawaziri Wakuu wawili hivyo kama atateua mwingine basi atakamilisha jumla ya Mawaziri Wakuu watatu katika kipindi chake.
Mawaziri Wakuu ambao watalipwa na kuendelea kulipwa fedha za walipa kodi katika maisha yao yote wao pamoja na familia yao. Mkapa alikwishawahi kuulizwa ni kwa nini hakumbadilisha Frederick Sumai na badala yake akamteua tena kwa kipindi kingine jibu lake lilikuwa fupi alisema naona huruma fedha za Watanzania kuendelea kumlipia Waziri Mkuu mwingine nitakaye mteua. Kama alimaanisha ama kama hakumaanisha hilo siwezi fanya mada ila binafsi niliguswa na majibu yake manake kama kweli angeteua mwingine basi idadi yao ingeongezeka.
Hivyo mimi nadhani tuendelee kujiuliza na kushauriana je Nchi yetu hapa ilipofikia tukizingatia kutafunwa kwake kote, tukizingatia uzembe wa watendaji na wakuu wake, tukizingatia matatizo yaliyopo katika taasisi mbalimbali za Serikali na nyinginezo, tukizingatia umasikini na shida tulizonazo Watanzani ambayo kwayo wao ni "maisha bora", tukizingatia hitaji letu kama Taifa na kubwa zaidi tukizingatia kwamba sisi ndio wahusika wakuu na walipaji halali wa mishahara na mahitaji mengine ya huyo Waziri Mkuu akiwa katika nafasi yake na hata atakapostaafu, akiwa hai na hata atakapotwaliwa.
MWISHO laiti ningekuwa JK ningedhihirisha kiwango cha busara nilicho nacho kwa kuamua kuweka kando swala la makundi, na kuamua kujishusha na kuamua kulitanguliza Taifa mbele hivyo kuamini pasipo shaka kuwa katika majina ya wasstafu tajwa hapo juu mbali na wale waliokwisha tangulia katika haki (Mungu awalaze pema peponi) bado wapo si wenye nguvu tu bali wazalendo pia; hivyo ili kulisaidia Taifa na Wananchi wangu ningekaa chini na kuamua kuchagua mmoja kati ya hao ili kumrithi huyu tumtazamiaye.
Mungu Ibariki Tanzania.
MEITINYIKU L. Robinson.