Tafakari Binafsi: JK Kupokea Kombe la Dunia Jijini Mwanza

Tanganyika50

Member
Dec 8, 2011
97
19
Wana jamvi,
Labda ni haya makengeza yangu.Ila nimejikuta nikitafakari mambo kadha wa kadha yanayoendelea humu kayani kwetu.
La kwanza ni taarifa niliyo isikia kwenye radio kuhusu Mh.Jakaya Kikwete,Rais wa Jamhuri yetu ambaye inaripotiwa ameonesha flexibility kwa kukubali kurusha ndege (Nadhani!) kutoka Mkoa mpya wa Simiyu mpaka Jijini mwanza ili kupokea kikombe cha soka cha Dunia katika hadhara kubwa hapo uwanja wa CCM Kirumba.
Sasa najua soka lina shamra shamra zake!Lakini nikatafakari hii gharama ya safari hii na tija inayotokana na matumizi haya ya fedha ambazo ni jasho la mimi na nyinyi wengine mnao lipa kodi halali.
Ningeelewa zaidi kama tungelikuwa tunaipokea Twiga stars yetu,au Serengeti yetu au Taifa stars yetu walau na kajikombe ka Kagame au CHAN hivi....Ningefarijika.Hilo lingekuwa na maana kwa vile tungekuwa tunasherehekea mafanikio ya soka letu.....walau kwa kiwango hicho cha afrika mashariki yetu.....!
Lakini hapa mantiki iko wapi hasa?!Yaani ni kitu gani hasa tunachoadhimisha au kusherehekea hapa?!
Au kwa vile hatuna hata ndoto za kushinda hilo kombe la dunia tunajifariji kulishika tu na kuliona?!Kiasi cha mkuu wa kaya kuacha mambo mengine ya msingi na kufunga safari kabisa kwenda kuongoza umati wa majuha sisi kulistaajabia kombe la dunia tusilo ota kulishinda karne hizi za karibuni?!
Inaniuma kwa kweli pale mkuu wa kaya anapotumia kodi yangu kwa mambo kama haya yasiyo na tija kwa Taifa letu.
Lingine ni hili la umeme......
Lingine ni hili la mishahara......
Naendelea na tafakuri......
 
Peleka kwenye jukwaa la michezo watakusaidie pengine niseme kidogo tu jk ni mwanamichezo namba moja tanzania,nisehemu ya watanzania sijui ulitaka mjomba wako akalipokea au nani.
 
Peleka kwenye jukwaa la michezo watakusaidie pengine niseme kidogo tu jk ni mwanamichezo namba moja tanzania,nisehemu ya watanzania sijui ulitaka mjomba wako akalipokea au nani.

Nadhani kuna msukumo wa kisiasa katika hili na ndio maana nikalileta huku kwa vile siasa zisizo na tija ni hasara kwa Taifa.
JK Nyerere alikuwa mwanamichezo pia.....mchezaji mzuri wa mchezo wa bao lakini sikuwahi kusikia akionesha "flexibility" kama hii!
Ni mtizamo tu.
 
Ni hivi FIFA inautaratibu, mwaka kuelekea mashindano ya kombe la dunia huwa lazima kombe lirudishwe kule litaposhindaniwa, sasa fifa hiyohiyo huchagua baadhi ya inchi wanachama kulipokea kombe hilo na kulishangaa kidogo wakati linarudi kule litakaposhindaniwa, pia katika inchi hizo zilizochaguliwa basi ni rais wa inchi peke yake anaruhusiwa kulishika, kwa kuwa kombe baada ya kutoka Nairobi kuja TZ lingeanzia Mwanza ni wazi kabisa mkuu wa inchi ilimbidi aende huko kulipokea. Hii ni kanuni ya fifa,so JK kwanda mwanza kulipokea kombe was inevitable.
 
Maelezo mazuri ebaeban.lakini bado nina maswali...hiki kikombe si kitakuwepo hapo uwanja wa taifa kesho?au hii ya taifa imeahirishwa?besides hii promotion ya coca cola imeshafanyika hapa kwetu 2006 na 2009!kwa maelezo ya msemaji wa wizara yenye dhamana siku tatu nyuma wala ratiba ya mwanza haikuwepo!haikuzungumziwa kabisa.kunani hapa?!
 
Back
Top Bottom