Tafadhali ndugu zetu wasipinge kuondolewa kwa Mangu

Mzee Mwanakijiji

Platinum Member
Mar 10, 2006
33,475
39,991
Najua ni rahisi kuona kuwa kwa kumuondoa Ernest Mangu Magufuli atakuwa amekurupuka; inawezekana watu wanaweza kuona kwa kumuondoa bila kumpa nafasi ya kujieleza basi Rais amemnyima Mangu "haki ya asili ya kusikilizwa kabla ya kuhukumiwa".

Inawezekana wapo ambao wanaweza kuona kuwa Magu amemuonea Mangu na hivyo ikasababisha uchungu kwa baadhi ya watu. Kwani wanaweza kusema kuwa "hawajaona makosa yoyote"

Na wengine wanaweza - na nimeona dalili tayari - kuwa Kamanda Sirro amepewa u-IGP kwa sababu amekuwa karibu na Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam Paul Makonda ambaye wapo wanaomuona kuwa ni kipenzi cha Rais. Wengine wanasema kwa vile "alikaa karibu na waridi, akanukia" na hivyo kuona kuwa kweli Makonda ana nguvu sana.

Katika haya yote wapo ambao wanaweza kuingiwa na jaribu lile lile ambalo inaonekana hawalikwepo la kupinga na kukataa. Katika kufanya haya yote wanaweza kabisa kusahau yale yote ambayo jeshi la polisi lilifanya dhidi yao wakati wote wa Mangu akiwa ni IGP.

Hivyo ombi langu, ni wanaotaka kupinga kuondolewa kwa Mangu wafikirie sana; wasije wakawa wanaendelea kugongelea misumari kwenye vidole vyao wenyewe...
 
Najua ni rahisi kuona kuwa kwa kumuondoa Ernest Mangu Magufuli atakuwa amekurupuka; inawezekana watu wanaweza kuona kwa kumuondoa bila kumpa nafasi ya kujieleza basi Rais amemnyima Mangu "haki ya asili ya kusikilizwa kabla ya kuhukumiwa". Inawezekana wapo ambao wanaweza kuona kuwa Magu amemuonea Mangu na hivyo ikasababisha uchungu kwa baadhi ya watu. Kwani wanaweza kusema kuwa "hawajaona makosa yoyote"

Na wengine wanaweza - na nimeona dalili tayari - kuwa Kamanda Sirro amepewa UIGP kwa sababu amekuwa karibu na Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam Paul Makonda ambaye wapo wanaomuona kuwa ni kipenzi cha Rais. Wengine wanasema kwa vile "alikaa karibu na waridi, akanukia" na hivyo kuona kuwa kweli Makonda ana nguvu sana.

Katika haya yote wapo ambao wanaweza kuingiwa na jaribu lile lile ambalo inaonekana hawalikwepo la kupinga na kukataa. Katika kufanya haya yote wanaweza kabisa kusahau yale yote ambayo jeshi la polisi lilifanya dhidi yao wakati wote wa Mangu akiwa ni IGP.

Hivyo ombi langu, ni wanaotaka kupinga kuondolewa kwa Mangu wafikirie sana; wasije wakawa wanaendelea kugongelea misumari kwenye vidole vyao wenyewe...
Wote ni hao hao! Nchi hii ni ya mtu mmoja tu!
 
Hao wameishaamua kufanya siasa zao kinyume nyume na anachokifanya Rais Magufuli.

Rais akiogelea wanadai anawatimulia vumbi.

Rais Magufuli akisimama, wao wanakaa. Akikaa wao wanasimama.

Rais akisema huyu ni fisadi, wao wanasema hapana, huyu sio fisadi pamoja na kwamba sio muda mrefu walikuwa wakisema ni fisadi.

Kinachonishangaza zaidi ni kuwa hawa jamaa hawana hata aibu katika hoja zao.
 
Najua ni rahisi kuona kuwa kwa kumuondoa Ernest Mangu Magufuli atakuwa amekurupuka; inawezekana watu wanaweza kuona kwa kumuondoa bila kumpa nafasi ya kujieleza basi Rais amemnyima Mangu "haki ya asili ya kusikilizwa kabla ya kuhukumiwa". Inawezekana wapo ambao wanaweza kuona kuwa Magu amemuonea Mangu na hivyo ikasababisha uchungu kwa baadhi ya watu. Kwani wanaweza kusema kuwa "hawajaona makosa yoyote"

Na wengine wanaweza - na nimeona dalili tayari - kuwa Kamanda Sirro amepewa UIGP kwa sababu amekuwa karibu na Mkuu wa Mkoa wa Dar-es-Salaam Paul Makonda ambaye wapo wanaomuona kuwa ni kipenzi cha Rais. Wengine wanasema kwa vile "alikaa karibu na waridi, akanukia" na hivyo kuona kuwa kweli Makonda ana nguvu sana.

Katika haya yote wapo ambao wanaweza kuingiwa na jaribu lile lile ambalo inaonekana hawalikwepo la kupinga na kukataa. Katika kufanya haya yote wanaweza kabisa kusahau yale yote ambayo jeshi la polisi lilifanya dhidi yao wakati wote wa Mangu akiwa ni IGP.

Hivyo ombi langu, ni wanaotaka kupinga kuondolewa kwa Mangu wafikirie sana; wasije wakawa wanaendelea kugongelea misumari kwenye vidole vyao wenyewe...
Hivi ni lazima kuanzisha thread?
 
Urais ni kazi ngumu sana.

Hivyo hata Magu afanyeje [au asifanyeje] wapo wataompinga tu.

Watu walimpinga na kumlaani Magu wakati ule Ney wa Mitego alipokamatwa.

Alipoachiliwa kwa kile kilichosemwa kuwa ni kwa influence ya Magu, napo wakampinga na kumlaani eti anaingilia mamlaka yasiyo yake.

It comes and goes with the territory. He is damned either way.

Sad!
 
Wanapinga kwani kuteua na kutengua ni kazi ya nani? Uache kupinga vilivyo chini ya maamuzi yako ukapinge anayofanya rais tena kwa kupewa na katiba, ...so what? Hatuwezi sote kuongoza nchi kila mtu kwa utashi wake, nchi inaendeshwa na taasisi husika.
 
siku zote mbulula hufuata upepo unakoelekea
Juzi tu watu walisema mangu kashindwa kazi!
Haya leo MAGU kawasikia mnalalama nini?

[nasikia SIRRO ni kiboko ya JAMAA WALEEE!
Acha waisome
 
Kwahiyo ameondolewa kwa sababu ya mambo ambayo " Jeshi la polisi limefanya dhidi yao(Wapinzani) Mangu akiwa IGP"? Well, ndilo unalojaribu kusema?
Nadhani Sirro is very good at operational and Media works.... Mangu was complacent , he wasn't that much fit to the stress brought by the position..

Hayo yako ya kutaka kila kitu kiimbiwe nyimbo za sifa nadhani kimepitwa na wakati...

Wacha "wachimba chumvi" wateme nyongo, kama ulivokuwa unatema nyongo mbichi 2005-2015

Sirro alistahili hii nafasi.
 
Magufuli kazi yake ni kuwabadilishia tu cd, Matokeo yake Chadema wanacheza hadi taarifa ya habari.

Hawajui washike lipi waache lipi.!
Ww kweli,hujielewi ngoja uone faida ya haya na mengine ulitaka chadema wafanye nn?
 
Back
Top Bottom