Tafadhali naomba msaada wa hili wana JF

colin_morgan

JF-Expert Member
Jun 8, 2015
2,443
2,894
Habari za muda huu wakuu,

Kama kichwa cha habar hapo juu ninaomba msaada wa kimawazo juu ya course gani asomee yenye market kubwa na chuo gani kitakuwa bora kutokana na ufaulu wake.

Matokeo ni kama ifuatavyo:
Civics D
History D
English D
PhysicsD
Biology C
Math F
Geog F

Natumai nitapata msaada wa mawazo kwa hili
Mbarikiwe wote...

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mtu kafeli hivyo bado unaulizia chuo kizuri na course yenye marketi, we mzee vipi? Mwambie atafute kozi za kuzibua vyoo
 
Yeye kwani hajui anahitaji nini maana mambo ya soko hayatabiriki mkuu kwa huo ufaulu wake!!!...

Mimi nikipewa nafasi ya kumshauri mtu nitaangalia uwezo wake, anachopenda na kumpa options za course ambazo mtu anaweza kujiajiri na kuajiriwa (Hapa course za IT, ICT na business in exclusion ya uhasibu naweza mshauri). Hii ni kwa experience yangu ndogo na soko linapoelekea japo Tz ya sasa haitabiriki haswa kwa business sector
 
Utakuta lengo kuu ni kujaribu kuchekesha, sifa za kijinga au kupata umaarufu ni ulimbukeni tu wa utumiaji mitandao
Hapo nimesema ukweli tu, mpumbavu hupenda Maneno mazuri yenye kufurahisha lakini mwerevu hupenda ukweli hata Kama unauma
 
ungekaa kimya ungepungukiwa nini
Ameomba ushauri, ushauri upo wa aina mbili, upo wa kuambiwa ukweli mkavu au wa Maneno mazuri lakini ya uongo, sasa achague mwenyewe, wewe acha kiherehere, toa ushauri wako Kama mtoa mada alivyoomba
 
Community Health haina deal kabisa ingawa angeweza pata. Siamini kama anapenda afya kutoka moyoni. Atakuwa anapenda kisa anasikia kuna nafasi nzuri ya kupata ajira. Nashauri jua anaelekea kuweza nini then mpeleke chuo chenye tija. Ukishindwa kupata chuo chukua ADA mwanzishie BIASHARA. Najua inauma lakini ni maradufu kuliko kwenda kozi za kichawi kujitia umasikini.
 
Back
Top Bottom