Tabora wamwambia Ditto kalale, yeye ajibu waambieni wake zenu!

BroJay4

JF-Expert Member
Aug 27, 2007
236
16
Sheikh Ponda awaponda mawaziri wa Kikwete

na Moses Mabula, Tabora

ALIYEWAHI kuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Ukiwaona Ditopile Mzuzuri, jana aliingia matatani baada ya kukwaruzana na wananchi katika mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Dk. Batilda Burian.

Matata hayo yalijitokeza wakati Ditopile alipoomba kipaza sauti, ili kumsaidia Dk. Burian kujibu shutuma kali zilizotolewa na kiongozi mmoja wa kidini, dhidi ya mawaziri wa Serikali ya Awamu ya Nne.

Sheikh Ponda Alli Ponda, wa madhehebu ya Shia, alitoa shutuma hizo muda mfupi baada ya waziri huyo kumaliza kuwahutubia wananchi na kuwataka waulize maswali au kueleza kero zao.

Sheikh huyo alimtuhumu Dk. Burian kuwa miongoni mwa mawaziri wanaokwamisha maendeleo ya Serikali ya Awamu ya Nne.

Dk. Burian alikuwa katika mkutano wa hadhara, ambapo baada ya kuhutumbia kuhusu ubora wa bajeti ya serikali ya mwaka wa fedha 2007/08, alitoa fursa kwa wananchi kuuliza maswali na kueleza kero zinazowakabili.

Huku akishangiliwa na wananchi, Sheikh Ponda alimtaka Rais Jakaya Kikwete, kutowalaumu viongozi wa upinzani kwa kitendo chao cha kuzunguka nchi nzima kuwajengea chuki kwa wananchi, kwa kuwa mawaziri wake ni mafisadi na wala rushwa.

Ponda alisema uamuzi wa wapinzani unaonyesha namna walivyo na uchungu na rasilimali za nchi yao na kwamba wao ndio wakombozi wa wanyonge walio wengi.

"Ninyi mawaziri ndio mnamsaliti Rais Kikwete, lazima niseme ukweli, nasema hivyo kwa sababu nchi yetu ina amani… sioni ubaya wa rais, bali ninyi mawaziri ndio wabaya, kamwambieni rais wetu asiwalaumu wapinzani, awalaumu mawaziri wake.

"Sisi kamwe hatuwezi kupuuzia kauli za kina (Freeman) Mbowe na Kabwe) Zitto kama ulivyotuambia, wale ni mashujaa wetu… ni wakombozi wa wananchi maskini kama sisi," alisema Ponda.

Aidha, kiongozi huyo wa kidini alisema kuwa Rais Kikwete, alipokuwa akiomba ridhaa ya wananchi wakati wa kampeni mkoani hapa, alitoa ahadi mbalimbali, ikiwemo maisha bora kwa kila Mtanzania, kupitia upya mikataba ya madini, kupambana na rushwa na kujenga barabara kwa kiwango cha lami ili kuunganisha mikoa ya Tabora, Kigoma, Rukwa na Mbeya, lakini ameshindwa kutekeleza ahadi hizo hadi sasa.

Aidha, alihoji ulazima wa serikali kutumia fedha nyingi za umma kuwasambaza mawaziri na manaibu wao mikoani kufanya kazi inayostahili kufanywa na wabunge wa maeneo husika.

Kutokana na kauli hiyo, aliyekuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Ukiwaona Ditopile Mzuzuri, aliinuka na kuomba kipaza sauti ili kumsaidia Dk. Buriani kujibu shutuma hizo, hali ambayo naye ilimtia matatani baada ya kutakiwa na baadhi ya wananchi waliohudhuria mkutano huo kwenda kulala.

Wananchi hao walimweleza Ditopile kuwa kwa sasa hana lake ndani ya serikali, hivyo ni bora ajikite zaidi kwenye biashara yake ya asali na asijiingize kwenye masuala mazito ya serikali.

Baada ya kauli hizo, Ditopile alihamaki na kuwajibu wananchi hao kwamba wakawaambie wake zao walale na si yeye, huku akionyesha kuchukizwa.


Awali, katika mkutano huo uliofanyika kwenye viwanja vya sanamu ya Mwalimu Nyerere mjini hapa, waziri Burian, aliwaeleza wananchi hao kuwa maisha bora kwa kila Mtanzania kama yalivyoahidiwa, hayawezi kuja kwa kushushwa na mnyororo kutoka kwa Mwenyezi Mungu.

Wakati huo huo, Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana, Dk. Emmanuel Nchimbi, amemtaka Mbunge wa Karatu (CHADEMA) Dk. Willibrod Slaa, na viongozi wengine wa upinzani kuacha kuipaka matope serikali, kwa kuwa mwisho wake watajipaka wenyewe.

Nchimbi, alitoa kauli hiyo jana mjini Monduli wakati akizungumza na watendaji wa halmashauri, madiwani na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika mkutano wa ndani akiwafafanulia kuhusu uzuri wa bajeti ya mwaka huu na mikakati ya kusimamia utekelezaji wake.

Alisema wapinzani wataendelea kupiga kelele huku serikali ikipata mafanikio kwa kasi na ifikapo mwaka 2010 wataona aibu kwa kukosa hoja za kuombea kura.

"Nawaambia mzushi yeyote katika nchi hii hivi sasa anaitwa Slaa na nimesoma katika gazeti moja la kila siku anadai eti anakwenda Marekani kueleza ufisadi wa serikali, ili nchi inyimwe misaada wakati hajui hata njia ya kuelekea katika Bunge la Congres," alisema naibu waziri huyo kijana.

Alisema wapinzani wamekuwa wakilalamika kuhusu ziara za rais nje ya nchi ambazo zinatoa mafanikio kwa nchi wakitaka abaki ikulu kulinda njiwa, ili nchi isipate maendeleo na wapinzani wapate hoja za kuzungumza wakati wa uchaguzi.

"Wapinzani hivi sasa wanaingiwa kiwewe kuona kasi ya maendeleo ya elimu na ujenzi wa barabara, hivyo wanaanza kuwapaka matope viongozi bila sababu yoyote lakini mwisho wa wao umefika na mzushi Slaa atabainika," alisema.

Alisema, wao kama mawaziri wataendelea kuzunguka nchi nzima kuongelea masuala ya bajeti na mbinu za maendeleo bila woga kwani tayari wanayo ridhaa ya wananchi kutekeleza waliyotumwa.


Source: Tanzania Daima.

Hapo patamu sana,Wananchi komaa huu ndio muda wa changes.
 
Kweli CCM jalala la takataka yaani wanakubali kuongozana na Ditopile?

Ingelikuwa nchi za wenzetu hilo lingewatokea puani. Wanaongozana na muuaji?

Sasa mahakama kweli itatenda haki huku huyu muuaji anaongozana na maafisa wa juu serikalini?
 
Kweli CCM jalala la takataka yaani wanakubali kuongozana na Ditopile?

Ingelikuwa nchi za wenzetu hilo lingewatokea puani. Wanaongozana na muuaji?

Sasa mahakama kweli itatenda haki huku huyu muuaji anaongozana na maafisa wa juu serikalini?

Mtanzania,
CCM mbali na kuongozana na muuaji Ditto,anapewa nafasi kujibu malalamiko ya wananchi,atajibu nini wakati muda wote huu alikua ana
kesi hajui kinachoendelea,au anataka apewe cheo tena?
 
CCM ni Maiti kilichobakia ni kupumzishwa.
lakini tusiwadharau tuangalie sheria gani inamdhibiti Ditto kujibu hoja za wananchi ili isije tokea akawaua tena japo najua safari hii akithubutu raia watamchinjilia mbali.
 
haman cha kuangalia hoja wala point gani huyo jamaaa ni muuaji na nashangaa kwa nini hajahukumiwa mpaka leo kwanza ile tu kubadilishiwa tuu kesi eti imekua ya kuua bila kukusudia tuu ilikua ni janja ya nyani na kutupiga changa la macho wa tz...huyo braza ni muuaji tuuu
 
na Moses Mabula, Tabora

ALIYEWAHI kuwa Mkuu wa Mkoa wa Tabora, Ukiwaona Ditopile Mzuzuri, jana aliingia matatani baada ya kukwaruzana na wananchi katika mkutano wa hadhara uliohutubiwa na Waziri katika Ofisi ya Waziri Mkuu, Dk. Batilda Burian.

Wananchi hao walimweleza Ditopile kuwa kwa sasa hana lake ndani ya serikali, hivyo ni bora ajikite zaidi kwenye biashara yake ya asali na asijiingize kwenye masuala mazito ya serikali.

Baada ya kauli hizo, Ditopile alihamaki na kuwajibu wananchi hao kwamba wakawaambie wake zao walale na si yeye, huku akionyesha kuchukizwa.

Source:Tanzania Daima.

Hapo patamu sana,Wananchi komaa huu ndio muda wa changes.

Mnh, kwa mtaji huu I hope huyu 'Babu' keshanyanganywa leseni yake ya kumiliki silaha!
 
What a stupid As****. He should wait for his time in jail.
 
Nchimbi, alitoa kauli hiyo jana mjini Monduli wakati akizungumza na watendaji wa halmashauri, madiwani na viongozi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika mkutano wa ndani akiwafafanulia kuhusu uzuri wa bajeti ya mwaka huu na mikakati ya kusimamia utekelezaji wake.

Mh...yangu macho, kila stahili ya kuitangaza budget.
Hawa sisiem labda wangetumia kauli mbiu nyingine ya kutokea na si uzuri wa budget,
mwananchi gani asiyeona gharama ya maisha inavyopanda kila kukicha?
Ni nani asiyejua wafanyakazi waliitisha maandamano kulilia waongezewe mshahara ili ilingane na gharama halisi za maisha?

Sisiem haina mwenyewe kwa sasa, kila mtu anajali tumbo lake.
 
Hilo jibu alilotoa ni la kihuni na utovu wa nidhamu kwa wakazi wa Tabora. kweli aliyesema "You can take a man out of the bush but not the bush out of a man" hakukosea bado anafikiria yuko Saigon nini?
 
Yaaani mahabusu na mtuhumiwa wa mauaji ya kutumia bastola mbele ya public, ambaye yuko nje kwa dhamana, anafuatana na viongozi wa chama tawala kwenda kuwaelezea wananchi kuhusu bajeti, kwenye public ile ile iliyomuona akifyatua bastola na kumuuua a helpless masikini ya Mungu dereva wa dala dala,

amepewa dhamana baada ya miezi mitatu tu "Rumande/Hospitali", huku akiwaacha wananchi watuhumiwa wenye kesi kama zake wakisota for the next 10 years bila kesi kusomwa mahakamani, maana uchunguzi bado unaendelea, Leo the man has some gutts ya kujaribu kukaripia wananchi publicly,

Kama mkataba wa Buzwagi, Only in Tanzania!
 
Yaaani mahabusu na mtuhumiwa wa mauaji ya kutumia bastola mbele ya public, ambaye yuko nje kwa dhamana, anafuatana na viongozi wa chama tawala kwenda kuwaelezea wananchi kuhusu bajeti, kwenye public ile ile iliyomuona akifyatua bastola na kumuuua a helpless masikini ya Mungu dereva wa dala dala,

amepewa dhamana baada ya miezi mitatu tu "Rumande/Hospitali", huku akiwaacha wananchi watuhumiwa wenye kesi kama zake wakisota for the next 10 years bila kesi kusomwa mahakamani, maana uchunguzi bado unaendelea, Leo the man has some gutts ya kujaribu kukaripia wananchi publicly,

Kama mkataba wa Buzwagi, Only in Tanzania!

Mkuu FM ES, heshima mbele mkuu, huyu mtuhumiwa wa mauaji sio tuu kafuatana na viongozi wa CCM bali amefuatana na waziri wa serikali na anamsaidia hata kujibu hoja, Je kwa mtaji huu mahakama itatenda haki? familia ya marehemu itatendewa haki wakati muuaji wa ndugu yao anaongozana na msafara wa serikali unaogharimiwa na kodi za wananchi? Kweli tanzania tumetupiwa nini au ni laana gani ipo tanzania?

Wananch kibao wako wanasota rumande kwa kei za kusingiziwa sasa huyu muuaji aliyeua mbele ya public bado anapewa kipaza sauti kujibu hoja za wananchi kwa niaba ya serikali? Hivi yeye Ditto alikuwa anawakilisha nani hasa?
 
Yaaani mahabusu na mtuhumiwa wa mauaji ya kutumia bastola mbele ya public, ambaye yuko nje kwa dhamana, anafuatana na viongozi wa chama tawala kwenda kuwaelezea wananchi kuhusu bajeti, kwenye public ile ile iliyomuona akifyatua bastola na kumuuua a helpless masikini ya Mungu dereva wa dala dala,

amepewa dhamana baada ya miezi mitatu tu "Rumande/Hospitali", huku akiwaacha wananchi watuhumiwa wenye kesi kama zake wakisota for the next 10 years bila kesi kusomwa mahakamani, maana uchunguzi bado unaendelea, Leo the man has some gutts ya kujaribu kukaripia wananchi publicly,

Kama mkataba wa Buzwagi, Only in Tanzania!

Mkuu FM ES, heshima mbele mkuu, huyu mtuhumiwa wa mauaji sio tuu kafuatana na viongozi wa CCM bali amefuatana na waziri wa serikali na anamsaidia hata kujibu hoja, ...

...heshima mbele wakuu FMES na Mtoto wa Mkulima. Kesi hii (kwa maoni yangu) ilishamalizika! Hebu rejeeni hii habari;

Ditopile aliua 'Bila kukusudia'
Written by Maxence M. Melo
Tuesday, 13 February 2007
♣Jalada labainika kuwa na upungufu
♣Atinga mahakamani akiwa na pama
♣Abadilishiwa shitaka, sasa ni kuua bila kukusudia
♣DPP asema kesi haziendeshwi kama enzi za Pilato

Kwa mujibu wa DPP, Lawrence Kaduma, msingi wa mashitaka hayo mapya unatokana na ushahidi uliokusanywa kwa watu walioshuhudia tukio hilo.Akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake jana, Kaduma alisema ushahidi unaotolewa wakati wa upelelezi ndiyo unaomfanya abadili shitaka.

Kaduma alisema alifikia uamuzi wa kubadili shitaka kwa kuwa mashahidi wote walitoa ushahidi unaofanana, kwa maelezo kulikuwa na malumbano kati ya Ditopile na dereva na pia Ditopile alitukanwa.

Alisema anashangazwa na baadhi ya watu kuhoji uamuzi wa kubadili shitaka na kwamba hafanyi kazi kwa shinikizo au kusikiliza maneno ya watu, bali anachofuata ni sheria.

Kaduma alisema upelelezi unaonyesha Ditopile alitukanwa na katika hali ya kawaida ya kibinaadamu, hakuna mtu ambaye anapenda kutukanwa hivyo alipandwa na hasira na kupelekea kufanya kosa hilo.
"Unajua watu hawajui sheria, kama angeamka na kutembea na bastola kuanzia asubuhi na kusema lazima auwe hapo sawa. Hiyo moja kwa moja ni shitaka la mauaji, lakini yule siyo 'chizi' atoe bastola na 'kushuti', kulikuwa na majibizano, alitukanwa akapandisha hasira, na kwa misingi ya kisheria hakukusudia kwa sababu hakupanga kufanya hivyo, "alisema Kaduma.

"Hatuwezi kuendesha kesi kama pilato, eti watu wakisema kaua basi iwe hivyo, lazima tufuate sheria na ushahidi na vielelezo husika, Yesu aliuawa bila kosa kwa uoga wa Pilato kwa kuwaridhisha wale watu, sasa sisi hatufanyi hivyo," alisema DPP.

VYANZO: Majira + Uhuru

http://jambotanzania.net/v2/content/view/1039/2/

...Mimi 'nachoshabikia' anyang'anywe leseni ya kumiliki silaha tu, maana huyu braza 'katika hali ya kawaida ya kibinadamu akikasirika' anaweza kuua tena!
 
Mwaka huu tutashuhudia vituko vingi mno. hii inatuonyesha incompetence ya mawaziri wetu. tukirejea matamshi ya Dr. Buriani mengi yana Utata. hana diplomacy ktk kujibu maswali. pengine Ditto aliliona hilo, akaona jahazi linazama, akasahau kwamba yeye hayumo tena serikalini akataka kumsaidia waziri.

Mawaziri wametumwa mikoani huku hawakujiandaa kujibu maswali ya wananchi, pengine hawakujua maswali gani wananchi watauliza. walidhani bado tuko 2005. sasa nimeamini akina Zitto wametia sumu. alipowaambia anaenda kutia sumu kwenye majimbo yao walidhani ni ndoto za alinacha. sasa wamepata somo. wengine wameamua kujifungia ndani na makada wao ili kukwepa kuzomewa, kwa maana nyingine wanataka mabalozi wa nyumba kumi kumi wengi wao wasio na elimu yoyote ndiyo wakaelimishe bajeti wananchi, ndiyo wakajibu maswali ya Buzwagi, ndiyo wakajibu hoja za maisha bora n.k

Huu ni uigizaji mwingine akina Nchimbi wanataka kutuletea. wafa maji hawaishi kutapatapa.
 
Nchimbi Alisema wapinzani wamekuwa wakilalamika kuhusu ziara za rais nje ya nchi ambazo zinatoa mafanikio kwa nchi wakitaka abaki ikulu kulinda njiwa, ili nchi isipate maendeleo na wapinzani wapate hoja za kuzungumza wakati wa uchaguzi.

"Wapinzani hivi sasa wanaingiwa kiwewe kuona kasi ya maendeleo ya elimu na ujenzi wa barabara, hivyo wanaanza kuwapaka matope viongozi bila sababu yoyote lakini mwisho wa wao umefika na mzushi Slaa atabainika," alisema..

1. Tulisema ziara za raisi zipunguzwe ili kuokoa gharama, sio kwamba zisitishwe kabisa. CAG alionyesha gharama halisi ambazo raisi angeweza ku save kama angepunguza safari hizi. Sasa kwa nini huyu Nchimbi anakuwa nunda wa kushindwa kuelewa suala la mantiki ndogo kama hili? Huyu ni Dk kweli?

2. Nilikuwa sijajua kuwa Kikwete huwa akiwa Ikulu "analinda Njiwa". Nchimbi kanifumbua macho! Sie wadanganyika tunashinda mashambani yeye anashinda ikulu kulinda njiwa? Kwa nini asiungane na sie katika kuchimba mitaro ya kunyweshea mashamba yetu? Ama Nchimbi hapa aliropoka? Naomba jibu wanakijiji!

3. Kasi ya maendeleo anayoiongelea Nchimbi ni ipi? Kama ni ndege haijapaa na wala hata uwanjani haipo! Hizi shule za kata anazozisema tumejenga sisi wavuja jasho kwa nguvu zatu na michango yetu. Na shule hizi bado hazina walimu wa kutosha, hazina maabara za kisasa, hazina vitabu vya kutosha, na nyingine madarasa hayajakamilika. Tuwasifu wao kwa lipi? Hapa napo kachemsha!

4. Barabara anazozisema Nchimbi zilianza ujenzi wake awamu ya tatu enzi za Magufuli, ujenzi ukasuasua baada ya awamu ya nne kuingia madarakani. Kwa nini? Kama barabara ya Sam Nujoma tu iliyo Dar es Salaam, yenye kilometa zisizozidi sita inachukua karibu mikaka miwili kukamilika, na zile za mikoani zenye mamia ya kilometa anatarajia zitakamilika? Kwa nini wananchi wa Mwanza na Bukoba hulazimika kupita nchi jirani ili kwenda mikoani kwao, kama barabara anazozisema ziko njema? Kwa nini Rukwa haijaunganishwa kwa lami na mikoa jirani yake hadi leo, kama barabara zinajengwa kwa kasi anayoisema?
Wakati mwingine kama hana cha kuongea no bora akakaa kimya, kuliko kuropoka.

5. Tumesema, na tunarudia kusema kuwa, kama wao sisiemu wanasema Slaa ni mzushi, basi watupatie takwimu za hali ya uchumi ambazo ni sahihi, na watuonyeshe mikataba yote ili tuamini kuwa anachosema Slaa sio sahihi. Kwa nini wao wanaona hili gumu? Eti mikataba ni mali ya sirikali. Aibu!
Tunamsubiri Nchimbi afike kwetu aone atakavyozomewa.
Mungu Ibariki Tanzania.
 
2. Nilikuwa sijajua kuwa Kikwete huwa akiwa Ikulu "analinda Njiwa". Nchimbi kanifumbua macho! Sie wadanganyika tunashinda mashambani yeye anashinda ikulu kulinda njiwa? Kwa nini asiungane na sie katika kuchimba mitaro ya kunyweshea mashamba yetu? Ama Nchimbi hapa aliropoka? Naomba jibu wanakijiji!


kwikwikwikwi! Warioba yupo wapi aje aseme alama ya taifa letu "Raisi" kazi yake ni kulinda njiwa? Hii ni kali ya mwaka
 
mnashangaa hii ..? alipohost ujumbe wa wafanyabiashara na viongozi wa serikali mjini tabora ...si tuliwaletea taarifa hapa??..........kwa kifupi kesi hakuna..
 
Mapambano haya ya kifikra, CCM haina budi kutumia silaha zote ilizonazo.. sasa hivi bado wanajaribu kutumia nguvu za hoja, lakini kwa kadiri wanavyokataliwa ndivyo wanavyosukumwa kuanza kutumia hoja kwa nguvu! Tuko tayari?
 
..Ditopile anapata nafasi ya kuzungumza ktk mkutano wa hadhara wa CCM!!!

..Kweli hawa wamekosa heshima kwa wananchi. Wamelewa madaraka hawa.
 
It is only in Tanzania a FELON can assume executive privileges.. This is sick, outrageous & shameful... Shame to everybody who allowed this kind of garbage!!!
 
0 Reactions
Reply
Back
Top Bottom