Miss Zomboko
JF-Expert Member
- May 18, 2014
- 4,480
- 9,241
Mwanri ametoa kauli hiyo akiwa wilayani Kaliua alipokuwa akizungumza katika mkutano wa hadhara akiwataka ili kupata uhalali wa kuendelea kufanya shughuli za ujasiliamali ni lazima wakate vitambulisho ambavyo kila mjasiliamali atakilipia shilingi elfu ishirini huku akiwanyooshea kidole watendaji watakaoshindwa kutoa vitambulisho hvyo kwa wakati.
Kwa mwaka huu Halmashauri ya wilaya ya Kaliua imepokea jumla ya Vitambulisho elfu sita pungufu ya vile vilivyotolewa mwaka jana ambapo mwaka jana jumla ya vitambulisho elfu nane.
Upatikanaji kwa vitambulisho kwa wajasiliamali wadogo kumesaidia kupunguza usumbufu waliokuwa wakiupata hapo awali.