mshale21
JF-Expert Member
- Apr 8, 2021
- 2,049
- 4,904
Patrick Mtahungwa (60) anatafutwa na Jeshi la Polisi kwa tuhuma za kumbaka mwanafunzi wa darasa la tano mwenye umri wa miaka 13 baada ya kumpa pipi, soda na miwa.
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Safia Jongo amesema mtuhumiwa huyo amekimbia baada ya familia ya mwanafunzi huyo anayesoma Shule ya Msingi Muhulidede kutoa taarifa kituo cha Polisi Shitage kilichopo wilayani Uyui.
Jongo amesema wanamsaka popote alipo ili afikishwe kwenye vyombo vya dola.
Kwa mujibu wa kamanda huyo, mtuhumiwa baada ya kumpa miwa na pipi ndio alimfanyia ukatili huo akiwa ametegea mama wa mwanafunzi huyo akiwa safarini na mwanafunzi huyo alipoulizwa alikiri kufanyiwa vitendo hivyo mara tano.
Ofisa mtabibu wa zahanati ya Shitage Wilaya ya Uyui, Joseph Bundala amesema mwanafunzi huyo alipimwa VVU na mimba na hakukutwa na chochote.
Mama mzazi wa mwanafunzi huyo amesema, "Namuona mzazi kama mimi sasa kuwafanyia watoto kitendo hicho ni uchungu mkubwa na sikutegemea."
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Safia Jongo amesema mtuhumiwa huyo amekimbia baada ya familia ya mwanafunzi huyo anayesoma Shule ya Msingi Muhulidede kutoa taarifa kituo cha Polisi Shitage kilichopo wilayani Uyui.
Jongo amesema wanamsaka popote alipo ili afikishwe kwenye vyombo vya dola.
Kwa mujibu wa kamanda huyo, mtuhumiwa baada ya kumpa miwa na pipi ndio alimfanyia ukatili huo akiwa ametegea mama wa mwanafunzi huyo akiwa safarini na mwanafunzi huyo alipoulizwa alikiri kufanyiwa vitendo hivyo mara tano.
Ofisa mtabibu wa zahanati ya Shitage Wilaya ya Uyui, Joseph Bundala amesema mwanafunzi huyo alipimwa VVU na mimba na hakukutwa na chochote.
Mama mzazi wa mwanafunzi huyo amesema, "Namuona mzazi kama mimi sasa kuwafanyia watoto kitendo hicho ni uchungu mkubwa na sikutegemea."