Analogia Malenga
JF-Expert Member
- Feb 24, 2012
- 5,010
- 9,874
Michael Paschal mwenye umri wa miaka 33, mkazi wa Uhemeli Ndala, Nzega, mkoa wa Tabora, afariki baada ya kuporwa hirizi zake na polisi akifanyiwa upekuzi.
Kijana huyo ambaye ni bodaboda alifikishwa kituoni mara baada ya kumkaba na kumchania sare CPL Lucas aliyekuwa katika majukumu ya usalama barabarani.
Askari (Lucas) alipomsimamisha Michael akiwa anaendesha pikipiki yenye usajili MC.246 BXH kwa ukaguzi, Michael alifanya fujo kwa kumkaba polisi na kumchania sare zake.
Askari alifungua mashtaka ya kuzuiwa kufanya majukumu yake, kijana Michael alikamatwa na kufikishwa kituoni alipokuwa akifanyiwa upekuzi alikutwa na hirizi mbalimbali sehemu ya mwili wake.
Mtuhumiwa akaomba asitolewe hirizi zake kwani zikitolewa atakufa, kulingana na sheria za upekuzi kwa mtuhumiwa anayewekwa mahabusu walizitoa hirizi hizo.
Baada ya kuzitoa hirizi hali yake ikaanza kubadilika kwa kuishiwa nguvu na kuzilai alipelekwa zahanati ya Kashishi kwa matibabu ilipofika saa 3.00 usiku akafariki dunia. Mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Tabora.
Kijana huyo ambaye ni bodaboda alifikishwa kituoni mara baada ya kumkaba na kumchania sare CPL Lucas aliyekuwa katika majukumu ya usalama barabarani.
Askari (Lucas) alipomsimamisha Michael akiwa anaendesha pikipiki yenye usajili MC.246 BXH kwa ukaguzi, Michael alifanya fujo kwa kumkaba polisi na kumchania sare zake.
Askari alifungua mashtaka ya kuzuiwa kufanya majukumu yake, kijana Michael alikamatwa na kufikishwa kituoni alipokuwa akifanyiwa upekuzi alikutwa na hirizi mbalimbali sehemu ya mwili wake.
Mtuhumiwa akaomba asitolewe hirizi zake kwani zikitolewa atakufa, kulingana na sheria za upekuzi kwa mtuhumiwa anayewekwa mahabusu walizitoa hirizi hizo.
Baada ya kuzitoa hirizi hali yake ikaanza kubadilika kwa kuishiwa nguvu na kuzilai alipelekwa zahanati ya Kashishi kwa matibabu ilipofika saa 3.00 usiku akafariki dunia. Mwili wake umehifadhiwa katika Hospitali ya Rufaa ya mkoa wa Tabora.